JWTZ inatarajia kufanya mazoezi mawili ya kijeshi hivyo imewataka wananchi kutokuwa na hofu

JWTZ inatarajia kufanya mazoezi mawili ya kijeshi hivyo imewataka wananchi kutokuwa na hofu

Wangekuja huku tabora,huku kuna uwazi mkubwa na maeneo tengefu mengi hivyo kusingeleta hofu wala wasiwasi kwa wananchi,isitoshe sisi huku tumezoea kuona misafara ya magari ya kijeshi na vifaru vya kijeshi hivyo wangekuja huku tungeburudika na wangepata uwanda mpana kwa ajiri ya mafunzo hayo.
Hakuna bahari huko.
 
Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) limesema kuwa linaendelea na Maandalizi ya Mazoezi mawili ya Kijeshi yatakayofanyika hapa nchini ambapo Wananchi wametaarifiwa kutokuwa na taharuki kwa kuwa katika Mazoezi hayo kutakuwa na ongezeko la matumizi ya Ndege Vita na Meli Vita.

Taarifa ya Kaimu Mkurugenzi wa Habari na Uhusiano wa JWTZ, Kanali Gaudentius Gervas Ilonda imeeleza kuwa JWTZ mazoezi hayo yanajulikana kama Justified Accord’ na ‘Cutlass Express’ yatakayoshirikisha Jeshi la Marekani na Majeshi mengine ya nchi 12 ikiwa ni muendelezo wa ukishiriki wake katika Mazoezi mbalimbali ya Kijeshi ya pamoja baina yake na Majeshi mengine ya nchi rafiki Duniani.

Taarifa hiyo imeendelea kueleza kuwa zoezi la kijeshi ‘Justifield Accord’ ni zoezi la nchi Kavu linalotarajiwa kufanyika eneo la Msata wilaya ya Chalinze Mkoa wa Pwani na Nanyuki nchini Kenya kuanzia tarehe 10 Februari 2025 kwa ushirikiano kati ya Tanzania na nchi ya Marekani.

Zoezi hilo litazinduliwa rasmi tarehe 10 Februari 2025 na linatarajiwa kufungwa tarehe 21 Februari 2025 na kubainisha kwamba kufanyika kwa zoezi hilo kutatoa fursa kwa vikundi shiriki kuongeza weledi na uelewa wa pamoja wa kupambana na matishio mbalimbali ya kiusalama kama vile matishio ya ugaidi.

Zoezi lingine la ‘Cutlass Express’ ni zoezi litakalofanyika kwa lengo la kujenga uelewa wa pamoja na ushirikiano katika kukabiliana na matishio ya Ulinzi na Usalama katika maeneo yetu ya uwajibikaji baharini ikiwa ni pamoja na kuzuia usafirishaji wa madawa ya kulevya.

Zoezi hilo ni la Jeshi la Wanamaji linalotarajiwa kufanyika katika nchi za Tanzania, Madagascar na Ushelisheli kuanzia tarehe 10 Februari 2025 na kufungwa tarehe 21 Februari 2025 ambapo kwa Tanzania litafanyika katika Jiji la Tanga.

Zoezi hilo litashirikisha nchi kumi na nne (14) ikiwemo Marekani ambayo inashirikiana na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania katika Maandalizi ya Mazoezi hayo hapa nchini.

Nchi waalikwa katika zoezi hilo ni pamoja na Kenya, Madagascar, Shelisheli, Djibout, Comoro, Georgia, Msumbiji, Malawi, Mauritius, Tunisia, Somalia na Senegal.
Bon, na boyi te, mais pourquoi basala ba exercices oyo te awa na Goma pona M23? Lisusu, esengeli ba soldats misusu ba sukola ba balabala ya Goma ndenge ba soldats ba sukolaka na tango ya ba protestations ya CHADEMA na Tanzanie?

Sawa sijakataa lakini ni kwa nini haya mazoezi wasije kuyafanyia hapa jijini Goma kwa M23? Pia wanajeshi wengine wafanye usafi kwenye barabara za mji wa Goma kama vile wanajeshi wanavyofanya usafi wakati wa maandamano ya CHADEMA kule Tanzania?
 
Kuna hatari moja kubwa sana naiona inakuja Tanzania.

Rwanda na Uganda zinajiimarisha sana kwenye maeneo ya Teknolojia ya kivita na Intelejensia.

Hivi karibuni Rwanda amesaini mkataba wa mashirikiano katika masuala ya Ulinzi na Uturuki. Nchi inayosifika kwa kutengeneza vifaa bora kabisa vya teknolojia mpya za kiulinzi mfano Drones na Makombora mbalimbali. Inasemwa vifaa hivi vimekisaidia sana Jeshi la Rwanda na M23 katika kuziteka Goma na Bukavu huko Congo.

Pia ameingia makubaliano ya Ethiopia katika masuala ya Ulinzi na hivi Karibuni Ethiopia kupitia Uwekezaji wa Kampuni za Ulinzi za Ubelgiji wameanza kutengeneza vifaa bora vya kijeshi vya teknolojia mpya ikiwemo Drones.

kwa utafiti wangu, nchi pekee zinazotengeneza silaha nzuri na za kisasa zinazoweza kupambana na silaha zinazotengenezwa na Mataifa haya ni Israel, Marekani na Uingereza.

Lord denning ninaamini miaka si zaidi ya 30 inayokuja, yanayotokea Congo Mashariki yataanza kutokea mpaka wa Magharibi wa Tanzania hasa mikoa ya Kagera, Kigoma hadi Geita na Shinyanga.

Lord Denning naamini kwa namna mifumo yetu ya kiulinzi na usalama ilivyokuwa compromised na siasa na mapandikizi haitakuwa rahisi sana kwa Tanzania kuweza kupambana na hiyo hatari.

Hivyo ni ushauri wangu kuwa;

1. Kuanzia sasa tuachane na siasa uchwara na kuwaunga mkono Palestina na Iran na tujikite kutengeneza mahusiano mazuri ikiwemo ya mafunzo ya kiulinzi na usalama na Mataifa ya Israel, Marekani na Uingereza

2. Tuwekeze sana kununua teknolojia za kisasa za kivita kutoka Mataifa haya na mafunzo ya umahiri kwa wanajeshi wetu katika teknolojia hizo

3. Tuwekeze sana kuimarisha kamand Iya Wanamaji hasa katika Maziwa ya Tanganyika, Victoria na Nyasa bila kusahau Bahari ya Hindi. Vifaa vya Kisasa kabisa vinavoendana na teknolojia mpya vinunuliwe na kuwekwa maeneo hayo. Kambi za kisasa za kijeshi zifunguliwe maeneo hayo.

Tujifunze sasa kutokana na aibu tuliyopata Congo baada ya Jeshi letu kushindwa vibaya na vikosi vya Rwanda na M23.

Mwisho ni ushauri wangu kuwa;
1. Jeshi likatae kuingiliwa na Wanasiasa na lijiweke kando na Siasa.

2. TISS ifumuliwe na kuunda upya. Baada ya Mchakato wa Katiba Mpya utakaowaondoa Wanasiasa kwenye ku control Watendaji na Mifumo ya Utendaji.

20250314_124453.png
20250314_124433.jpg
 
we jamaa unafurahisha wakati mwingine, kutwa unamponda mnyarwanda halafu unaongelea tanzagiza kujihusisha na Israeli?hivi unaelewa unachokiandika? rwanda ndiyo Israeli ya afrika kama ulikuwa haujui, mnyarwanda ni only african leader ambaye ni US military trained, labda useme tanzagiza waanzie kwa kujikomba kwa rwanda ndo wawapigie kifua huko kwa Christians, au unafikiri ubabe wote na kanchi kadogo rwanda anaupata wapi ?
 
we jamaa unafurahisha wakati mwingine, kutwa unamponda P.Kagame halafu unaongelea tanzagiza kujihusisha na Israel? hivi unaelewa unachokiandika? rwanda ndiyo Israeli ya afrika kama ulikuwa haujui, P.Kagame ni only african leader ambaye ni US military trained, labda useme tanzagiza waanzie kwa kujikomba kwa rwanda ndo wawapigie kifua huko kwa Christians …
Kagame hakumaliza training zake kwenye Chuo cha Kijeshi cha Marekani.

Alikatisha masomo na kurudi Uganga kuwa Head of Intelligence Agency.

Bahati mbaya hakuna mwenye akili huko CCM na Serikalini wanaoweza kuwaza haya. Wanachowaza sasa ni kushinda uchaguzi na kupiga hela kupitia deals.

Tutimize wajibu wetu kwa kuwa Wazalendo na kuwashauri ipasavyo. Wasipochukua ushauri shauri zao. Tuepuke dhambi ya kutochukua hatua anahimiza hili kila siku Tundu Antipass Lissu.
 
Kagame hakumaliza training zake kwenye Chuo cha Kijeshi cha Marekani.

Alikatisha masomo na kurudi Uganga kuwa Head of Intelligence Agency.

Bahati mbaya hakuna mwenye akili huko CCM na Serikalini wanaoweza kuwaza haya. Wanachowaza sasa ni kushinda uchaguzi na kupiga hela kupitia deals.

Tutimize wajibu wetu kwa kuwa Wazalendo na kuwashauri ipasavyo. Wasipochukua ushauri shauri zao. Tuepuke dhambi ya kutochukua hatua anahimiza hili kila siku Tundu Antipass Lissu.

kwa hiyo inabdailisha nini? isitoshe kwanza tanzagiza ni islamic na communist …
 
Wazungu hawana rafiki kabisa, wanasaidia Taifa na wakiona kuna maslahi wanataka basi huanzisha ugaidi kwa kisingizio cha watu fulani

Tukubali tukatae Trump ametufundisha mengi sana
Na hao ndio wafadhili wakubwa kwa kuivuruga dunia

Unaweza ukakuta unaoshauri wapo na Slim na huku wapo
Kila kitu kinawezekana ila tuna watu wasiozidi laki 5 ndio wanatufanya watu 60 something million tuwe mazuzu
Wengine wanapambana kupata hela zao za ndani ila sisi bado ni ombaomba tu

Kumbuka umasikini ni Laana
Screenshot_20250314_094651_Instagram~2.png
 
Nakubaliana na wewe kuhusu wazungu. Ni bahati mbaya sana wao ndo wenye teknolojia.

Huku kwenye mazao tukiwa na uongozi imara tutazalisha tu na kuuza nje.
Wazungu hawana rafiki kabisa, wanasaidia Taifa na wakiona kuna maslahi wanataka basi huanzisha ugaidi kwa kisingizio cha watu fulani

Tukubali tukatae Trump ametufundisha mengi sana
Na hao ndio wafadhili wakubwa kwa kuivuruga dunia

Unaweza ukakuta unaoshauri wapo na Slim na huku wapo
Kila kitu kinawezekana ila tuna watu wasiozidi laki 5 ndio wanatufanya watu 60 something million tuwe mazuzu
Wengine wanapambana kupata hela zao za ndani ila sisi bado ni ombaomba tu

Kumbuka umasikini ni Laana View attachment 3270079
 
Nakubaliana na wewe kuhusu wazungu. Ni bahati mbaya sana wao ndo wenye teknolojia.

Huku kwenye mazao tukiwa na uongozi imara tutazalisha tu na kuuza nje.
Ni kweli pia tukiwa na nguvu ki uchumi zaidi basi hata hiyo technology tutaipata na kujifunza mengi na kupata silaha sehemu nyingi tu
Na ni kweli hawa wazungu hawaaminiki
Kuna mjadala mwezi uliopita uliwashtua watu wasiojua ila wengi tunalijua hilo kuwa terror organization zinafadhiliwa na wao
USAID ilikuwa inatuma $40m kila week kwa Taliban na kuna vikundi vingi vya kigaidi wao ndio wanafadhili
Sasa ni kuangalia je nani anatufaa hata kinafiki mradi tunaangalia maslahi

Mataifa kama China walituma vijana wao wengi America na nji zingine za magharibi ili kujifunza kila sekta hata ushushu wa kiuchumi na leo wqmefanikiwa pakubwa sana

Nyerere alituma vijana Cuba kujifunza mengi
Kwanini tusiendeleze vijana wengi wakasome huko hata namna ya kutengeneza biological weapons kama inavyosemekana kwa majirani?

Tukiuza sana nje hakika tutapata vya kurudi pia
 
Ni kweli pia tukiwa na nguvu ki uchumi zaidi basi hata hiyo technology tutaipata na kujifunza mengi na kupata silaha sehemu nyingi tu
Na ni kweli hawa wazungu hawaaminiki
Kuna mjadala mwezi uliopita uliwashtua watu wasiojua ila wengi tunalijua hilo kuwa terror organization zinafadhiliwa na wao
USAID ilikuwa inatuma $40m kila week kwa Taliban na kuna vikundi vingi vya kigaidi wao ndio wanafadhili
Sasa ni kuangalia je nani anatufaa hata kinafiki mradi tunaangalia maslahi

Mataifa kama China walituma vijana wao wengi America na nji zingine za magharibi ili kujifunza kila sekta hata ushushu wa kiuchumi na leo wqmefanikiwa pakubwa sana

Nyerere alituma vijana Cuba kujifunza mengi
Kwanini tusiendeleze vijana wengi wakasome huko hata namna ya kutengeneza biological weapons kama inavyosemekana kwa majirani?

Tukiuza sana nje hakika tutapata vya kurudi pia
Cuba atalufundisha nini katik dunia hii ya sayansi na teknolojia? Ana teknolojia gani? Cuba labda madaktari tu
 
Ni kweli pia tukiwa na nguvu ki uchumi zaidi basi hata hiyo technology tutaipata na kujifunza mengi na kupata silaha sehemu nyingi tu
Na ni kweli hawa wazungu hawaaminiki
Kuna mjadala mwezi uliopita uliwashtua watu wasiojua ila wengi tunalijua hilo kuwa terror organization zinafadhiliwa na wao
USAID ilikuwa inatuma $40m kila week kwa Taliban na kuna vikundi vingi vya kigaidi wao ndio wanafadhili
Sasa ni kuangalia je nani anatufaa hata kinafiki mradi tunaangalia maslahi

Mataifa kama China walituma vijana wao wengi America na nji zingine za magharibi ili kujifunza kila sekta hata ushushu wa kiuchumi na leo wqmefanikiwa pakubwa sana

Nyerere alituma vijana Cuba kujifunza mengi
Kwanini tusiendeleze vijana wengi wakasome huko hata namna ya kutengeneza biological weapons kama inavyosemekana kwa majirani?

Tukiuza sana nje hakika tutapata vya kurudi pia
Sisi technolojia yetu ni kuwa na chawa
 
Kuna hatari moja kubwa sana naiona inakuja Tanzania.

Rwanda na Uganda zinajiimarisha sana kwenye maeneo ya Teknolojia ya kivita na Intelejensia.

Hivi karibuni Rwanda amesaini mkataba wa mashirikiano katika masuala ya Ulinzi na Uturuki. Nchi inayosifika kwa kutengeneza vifaa bora kabisa vya teknolojia mpya za kiulinzi mfano Drones na Makombora mbalimbali. Inasemwa vifaa hivi vimekisaidia sana Jeshi la Rwanda na M23 katika kuziteka Goma na Bukavu huko Congo.

Pia ameingia makubaliano ya Ethiopia katika masuala ya Ulinzi na hivi Karibuni Ethiopia kupitia Uwekezaji wa Kampuni za Ulinzi za Ubelgiji wameanza kutengeneza vifaa bora vya kijeshi vya teknolojia mpya ikiwemo Drones.

kwa utafiti wangu, nchi pekee zinazotengeneza silaha nzuri na za kisasa zinazoweza kupambana na silaha zinazotengenezwa na Mataifa haya ni Israel, Marekani na Uingereza.

Lord denning ninaamini miaka si zaidi ya 30 inayokuja, yanayotokea Congo Mashariki yataanza kutokea mpaka wa Magharibi wa Tanzania hasa mikoa ya Kagera, Kigoma hadi Geita na Shinyanga.

Lord Denning naamini kwa namna mifumo yetu ya kiulinzi na usalama ilivyokuwa compromised na siasa na mapandikizi haitakuwa rahisi sana kwa Tanzania kuweza kupambana na hiyo hatari.

Hivyo ni ushauri wangu kuwa;

1. Kuanzia sasa tuachane na siasa uchwara na kuwaunga mkono Palestina na Iran na tujikite kutengeneza mahusiano mazuri ikiwemo ya mafunzo ya kiulinzi na usalama na Mataifa ya Israel, Marekani na Uingereza

2. Tuwekeze sana kununua teknolojia za kisasa za kivita kutoka Mataifa haya na mafunzo ya umahiri kwa wanajeshi wetu katika teknolojia hizo

3. Tuwekeze sana kuimarisha kamand Iya Wanamaji hasa katika Maziwa ya Tanganyika, Victoria na Nyasa bila kusahau Bahari ya Hindi. Vifaa vya Kisasa kabisa vinavoendana na teknolojia mpya vinunuliwe na kuwekwa maeneo hayo. Kambi za kisasa za kijeshi zifunguliwe maeneo hayo.

Tujifunze sasa kutokana na aibu tuliyopata Congo baada ya Jeshi letu kushindwa vibaya na vikosi vya Rwanda na M23.

Mwisho ni ushauri wangu kuwa;
1. Jeshi likatae kuingiliwa na Wanasiasa na lijiweke kando na Siasa.

2. TISS ifumuliwe na kuunda upya. Baada ya Mchakato wa Katiba Mpya utakaowaondoa Wanasiasa kwenye ku control Watendaji na Mifumo ya Utendaji.

View attachment 3270062View attachment 3270063
Hakuna mwenye habari na hayo,ni uchawa na siasa uchwara TU!
 
hakika mtoa uzi umeandika vitu vya msingi sna, tunatakiwa kuchukua hatua sna kwenye security ya nchi yetu maana amani ya mashariki ya kongo inaipact sna kwenye usalama wa nchi yetu
 
Back
Top Bottom