JWTZ msifanye makosa DRC, haya ndio yatakuwa madhara yake

Kwenye Mkutano wa viongozi wa East africa commander in Chief Samia kasema mambo ya historia yabaki historia tujadili ya sasa,Kagame kabweka yote na kumponda sana Rais wa Africa kusini na majeshi yake kajaribu sana kuavoid neno Tanzania na Jeshi lake.
Ki msingi na Sisi katutukana sababu kikosi cha Tanzania kiko chini ya south Africa that's y tunataka ashughulikiwe
 
Huu ni mtihan mwegine
Kikubwa machawa wakae mbali katika swala hili
Waache ushauri wa Jeshi letu ufanye kazi
 
Kwa akili kubwa za Kagame na rasilimali nyingi zilizopo Kivu haki vile Rwanda inaenda kukua kiuchumi na kijeshi.

Miaka ya mbeleni huko hii jamii ya kitusi itakuja kumega maeneo ya Kagera na Uganda iundwe nchi mpya.
 
Waende tu hao Bongo movie watarudishwa kwa aibu kama wale mercenaries wa Kifaransa na Kiromania, jeshi letu linapaswa kusukwa liwe kama lile la enzi za Nyerere kuanzia kwenye drills, discipline na patriotism.
Kwa sasa hatuna soldiers wa kukabiliana na wale wahuni.
Hiyo geopolitical military influence tumeutoa wapi au unazungumzia enzi za Mchonga? Hivi tuna influence Kenya au Uganda au Zambia au wapi labda mimi ndiyo niko gizani?
Acha jeshi na intelijensia yake waendelee kulinda CCM dhidi ya vyama vya upinzani kwani huko ndiyo tuna uhakika hawategemei kuaibishwa na wala kuliaibisha taifa kwa ujumla wake.
Vyombo vyetu vyote vya ulinzi na usalama wamejikita kwenye siasa zaidi na confidence uchwara eti tulimpiga Nduli Idd Amin Dada(history).
 
Na hiyo UN inaongozwa na USA
 
Wameamua kukodi mercenaries waliodhaminiwa na France kwa kuwa wanaamini France wana personal hatred against Kagame so they'll do whatever it takes kumuondoa madarakani.
Kagame kawatukana sana Wafaransa, hata sasa ndiyo taifa la Wazungu linalo piga kelele na kuwahusisha direct na hivyo vita zaidi ya taifa jingine lolote.
Acha seregere liendelee tuone nani atakubali kushindwa.
 
Yapo makosa kidogo yamefanywa siku za hivi karibuni ku link jeshi la wananchi na siasa, kimsingi Kwa namba Fulani credibility imepungua
Lakini hatuwezi kubeza jeshi letu Kwa kuwa miaka kadhaa nyuma tumefanya operation nyingi tuu na zote zimefanikiwa
 
Kwa akili kubwa za Kagame na rasilimali nyingi zilizopo Kivu haki vile Rwanda inaenda kukua kiuchumi na kijeshi.

Miaka ya mbeleni huko hii jamii ya kitusi itakuja kumega maeneo ya Kagera na Uganda iundwe nchi mpya.
Ndio mana tunawasihi Tanzania kuingilia Kati ili Ku regulate ukuaji WA uchumi na kijeshi wa Rwanda
Natumahi Wazee wanatusikia
 
Hapa ndipo ulipokosea ndugu
 
Ndio mana tunawasihi Tanzania kuingilia Kati ili Ku regulate ukuaji WA uchumi na kijeshi wa Rwanda
Natumahi Wazee wanatusikia
Kwa hii nchi yenu ni ngumu.Ulichosema kilitakiwa kiwe kimefanyika miaka mingi nyuma.Kwa nchi za maziwa makuu tz ilitakiwa iwe proud kiuchumi,kijeshi na ushawishi mkubwa kwa nchi jirani,lakini kwa sasa ni mavi matupu hata Burundi hatusikilizi wala hatuogopi.
 
Hapana JWTZ isiingie mashariki ya Kongo, wajikite tu kulinda mipaka yetu kwa nguvu kubwa. Viongozi wetu wasiongee chochote kuhusu huo mzozo wa DRC. Tuwe neutral kama Switzerland, ikiwezekana hata kwenye mazungumzo ya amani sijui nini tusijihusishe au tuwe washiriki tu but no comment. Tuhakikishe tu nchi yetu ni salama alafu fokasi yetu iwe kuajiri walimu mahiri kwenye mashule yetu ili kutengeneza kizazi cha wataalamu baadae.

Elimu ndio itatutoa kwa habari ya maendeleo ya kiuchumi, kiteknolojia, kijamii hata kisiasa. Si mmeuona mtaala mpya, hiyo ni step ya kwanza, angalia syllabus ya computer science kuanzia form one mpaka six, imagine tukiajiri walimu mahiri wakafundisha kwa umahiri na kujitoa kabisa, kuwe na exhibitions na maonyesho ya wanafunzi na mashindano baina ya shule na shule. Shule za private zitasaidia sana kwenye hili, hasa hasa hizi shule kali kali hapa Dar es Salaam na sehemu mbalimbali hapa nchini. Shule za private zikipata walimu wazuri ziwalinde, ziache kuwaondoa kwa upumbavu, ujeuri na ujinga hatuna mda wa kupoteza we have a generation to build.

Wahitimu wetu wa BSc Computer Science, IT, IT systems, ICT with business, na wale wa BSc with Education kwenye hayo mambo ya IT wakafundishe wasione soo hamna kuwaza mshahara wa ualimu mdogo ela kitu gani tujenge kizazi kijacho imara. Mbali na kufundisha wapoteze mda wao mwingi Github, Stack Overflow wakazane sana kusoma the Bootstrap documentation, Oracle documentation na kujifunza modern frameworks kama vile angular javascript n.k

Najua wengine watasema hatuhitaji walimu tunahitaji wajasiriamali, ooh! sijui jiajiri jiajiri jiajiri. Hapana walimu ni muhimu sana sana sana kuliko wajasiriamali. Ikiwezakana watu wenye uwezo wagawe au wauze maduka yao wakafundishe. Ualimu, ualimu ualimu. Ikiwezekana kila mtu atake kuwa mwalimu siyo kwasababu inalipa bali kwasababu itaikomboa Tanzania yetu kwenye ishu za maendeleo kiuchumi, kijamaa n.k

Wazee waache kuwafanyia vijana mauzauza yaani mtu ukipiga stori za kisiasa siku moja ukamkosoa kiongozi wa kisiasa siku moja basi unafuatiliiiiwaaaa mauzauza mauzauza mauzauza, ina maana haturuhusiwi tena kuzungumza habari za nchi yetu.

Ndivyo hivyo aisee kwenda Rwanda sijui Kongo hakutusaidii chochote, hata kama Rwanda anataka Kongo iwe koloni lake muacheni si inatuhusu nini bana. Kitakachotusaidia ni kuwekeza kwenye elimu.

Sijawahi mtukana rais naweza taja jina langu. mm ni mwalimu Robert Mdee namba zangu ni
0685967259 - airtel
0655980538 - tigo

Moja wapo ya kazi zangu ni hii hapa Mdee Academy nisaidie tafadhali kupromote kazi yangu, kwa bahati mbaya vijana wetu wako bize kumuangalia Kagame badala ya kuangalia vitu vya maana. Kagame Kagame, Kagame bongo mm mwenyewe ni mrefu na mwembamba vilevile.
 
Na physics pia ifundishwe vizuri zaidi siyo kukaririsha watoto. Tukifanya hivyo tutatoboa
 
Hawezi kutoa taarifa nyeti za kiusalama Kwa maelezo hayo, hui sio mada ya uchawa Kwanza nakushitumu kama pandikizi
Umekosea Sana na jeshi letu haliwezi kutoa nafasi Kwa watu wapuuzi kama ww
Sawa wewe wasema lakini ukweli ndio huo hata uende wapi mambo haya hayawezekani kwa mwili bali kwa Roho. We are all connected ndio maana imeandikwa Bwana hasipolinda mji....
 
Unafikiri Tanzania inaweza kwenda peke yake na kutia suluhisho la kudumu?

Kuna Wanyarwanda waliozaliwa DRC, walikuwepo kwenye utawala na jeshi la Kabila Senior baadaye wakafukuzwa. Sio rahisi kuwaua wote, wanaweza kukimbia misituni, Rwanda baadaye wakarudi.

Kwahiyo suluhisho pamoja na kuwa litahusisha jeshi lakini pia political and social, integration ya hawa Wanyarwanda waliozaliwa DRC wenye haki kama Wacongo wengine pamoja na kumbana Kagame, kuimarisha na kulijengea uwezo jeshi la Congo.

Itabidi Kudhibiti jeshi la Rwanda kuingia DRC, lakini pia kuhakikisha wazaliwa wa DRC wenye asili ya Rwanda hawabaguliwi.
 
Hii mbona kama imeandikwa na AI au mtu asiyejua kiswahili vizuri.
 
Kagame naye ana - back up ya kisirisiri Israel, US, UK na wengine. Huu mtifuano utaishia wapi?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…