Familia za Makada na Viongozi wa Chadema ziko wap?
Watanzania wenzangu kabla ya kukubali na kufuata yale wanayopanga kufanya Chadema kwa Watanzania tujiulize hizi familia za viongozi na Makada wa Chadema wako wapi?
LISSU: Familia yake mke na watoto wapo Marekani, Wanasoma na Kuishi huko
LEMA: Familia yake ipo Canada
MBOWE: Familia yake mke yupo Uingereza na watoto wake wako Dubai
WENJE: Familia yake ipo Canada
MARIA SARUNGI: Amehamisha Makazi yake Kenya
MANGE KIMAMBI: Huyu familia yake ipo Marekani
Hawa wote wamehamishia familia zao nje ya Nchi wao wao wakiendeleza harakati za uchonganishi wa Watanzania kwa Serikali yao.
Je hamuoni kua hawa wanamaslai yao binafsi.
Ikiwa kweli wanauchungu na hayo madai yao kwanini uratibu wa haya maandamano wasilete familia zao ziwe mstari wa mbele kuandamana na kudai madai yao.
Watanzania wenzangu tusifuate mkumbo wa kuchonganishwa na Serikali katika jambo ambalo serikali kupitia kwa mkuu wa nchi ameshasema linafanyiwa kazi.
Ikumbukwe Madhara ambayo yatakayopatikana baada ya Hayo Maandamano Batili ni makubwa sana na huwenda yakakuletea shida.
Je, umejiandaa kukabiliana nayo? Una bima ya Afya kujitibu majeraha?
Kijana na Mtanzania Mwenzangu Tumia akili Usifate Mkumbo❗️
PIA SOMA
-
Kuelekea 2025 - Freeman Mbowe: Tutaandamana kudai watu waliopotea
Mbowe amekosea kupanga maandamano kwa kusema Samia Must Go.
Hilo ni kosa la kimkakati .
Maandamano ya Samia Must Go hayafai kufanywa na Chama cha Saisa yanatakiwa yafanywe na wanaharakati au wananchi wenyewe bila kutumia Chama .
Alitakiwa aseme CCM must go au Masauni, IGP, DCI, na Awadhi must Go lakini sio Rais . Rais ataondoka kwa Kura 2025 na sio kwa maandamano ya chama cha siasa.
Kama wanaweza kuandamana kumtoa Rais bas wajue watauawa wengi sana na mwisho kweli Samia ataondoka lakini Jeshi litashika nchi na siasa zitasimama kwa muda usiojulikana .
Mbowe alitakiwa atafakari sana kabla ya kumtaka Samia atoke Madarakani kwa sababu waliozunguka hasa wale watekaji watataka kuonyesha kuwa wapo kwa ajili ya kumlinda Rais dhidi ya Wapinzani wake na wao ni wanufaika wa vyeo na ulaji . Kwa sasa wetu hawapiganii maslahi ya nchi bali matumbo yao na ndivyo ilivyo kwa CCM na serikali yake. Wazanzibari wanakwapua mali zote za Tanganyika na ardhi ya yote halafu wanakwenda kuilinda nchi yao na kuwamaliza watetezi wote wa Tanganyika .
Sasa ni vipi hawa wageni na raisi wao wanaondoka madarakani ni kwa sanduku la Kura seikali za mitaa na uchaguzi mkuu.
Kuhusu familia ya Mbowe kufichwa nje ya nchi . Hili ni wazo la kijinga kabisa . Hata Samia anapotoa maelekezo kwenye vyombo vya dola vilivyojaa watoto wa maskini na wanaolipwa mishahara midogo isiyolingana na hata pesa ya kunywa chai ya Abduli akienda Dubai bado hatangulizi watoto wake wala ndugu zake wala mume wake ili akapigwa mawe na Waandamanaji.
Unapozungumzia wananchi kupigwa risasi lazima mzungumzie pia watoto wa maskini walioko kwenye majeshi yetu watakaojenga uhasama na raia kwa manufaa ya Wakubwa walioficha mapesa nje ya nchi na kujilimbikizia mali kila sehemu na wao hawatapigwa hata jiwe. Kenya walitumia akili sana walitaget mali za wale wote wanaowaumiza wananchi na kuzipiga moto na nyingine kuzipora . Mali ndizo zinazowapa kiburi wauaji wanaoua watu ili kupata vyeo kutoka kwa rais anayewatuma walinde cheo cheke badala ya usalama wa watu na mali zao .
Hata Mtume Mohamad alipokuwa anasimamisha haki na kupinga dhulma zilizokuwa zinafanywa na watu wa umma wake wakati huo hakuwa anakwenda vitani na Wake zake.
Hata Daudi hakwenda vitani na Wake zake na watoto wake wakiwa wadogo.
Watoto wa Kina Lisu na bado ni wadogo. Wanalelewa huwezi kuwaingiza kwenye siasa kama wale wa Akina Mwigulu .
Mwigulu hawezi kupeleka mtoto wake CCP na kisha awe polisi wa kikosi cha Fanya Fujo Uone . Zaidi atapelekwa kubwa kwenye ofisi nyeti kama kada wa CCM na sio kwenda kupiga watu mabomu ya machozi na kuua watu na wakati mwingine nao kujeruhiwa na wananchi.
CCM msifurahie watoto wa maskini waliopo kwenye vyombo vya dola kuua watu ili nyie mbaki madarakani . Mnawajengea uhasama watoto wa watu ambao hata wakiuawa hua hamfidii familia zao na zaidi hata pesa za mazishi hamwapi na wanaoiba pesa zao hamwachukulii hatua .
Kutuma Majeshi kuwapiga wananchi wanaopinga mauaji ni mauaji makubwa yatakayovuruga amani ya nchi.
Kwa uelewa wangu duniani kote serikali iliua watu wengi haiwezi kubaki madarakani kwa amani tena . Na vifo vya watu havileti amani mpaka silaha zitakazowekwa chini na kuzungumza mezani.
Samia ameamua kuchagua njia ya mauaji kupata heshima na kuwatia adabu wale wasio na nidhamu.
Hii njia aliyoipenda ni mbaya sana mana itaua zaidi na itajenga chuki kubwa sana. Watanganyika hawapendi kuuana lakini kuna dalili mbaya sana Huyu Mzanzibari anataka kulipiza kisasi cha Wenzake wa kule Zanzibar waliokua wameuawa na serikali yake ya CCM lakini pia anataka kutuletea migawanyiko ya kisiasa kwa watanganyika ambao kwa sasa tatizo kubwa ni ufisadi na mauaji yanayofanywa kwa ufadhili wa wageni na mafisadi kugawa mapesa kwa wauaji.
Binafsi namshauri Mbowe ajitokeze hadharani kwanza Akanushe na aweke hiyo clip ya kikao chao cha ndani kule Arusha ili wananchi tuone ukweli na kupuuza Usanii wa CCM na Makada wake ndani ya vyombo vya dola . Hawa Makada ndani ya vyombo vya dola hua wanatumika ndani ya upinzani kujifanya kuwa walikua wanateka Watu kwa kuagizwa na Mbowe. Cha ajabu mtu anajitokeza anasema alikua anateka watu kwa kuagizwa na Mbowe halafu hakamatwi ili aeleze alikowapeleka wale aliowateka ili vitendo hivyo vikomeshwe . Sasa hapo utajua tu kuwa ni makada wao waliowapandikiza ndani ya wapinzani halafu baadae wanatoka wanarudi CCM na kulipwa pesa zao na kuwapaka matope viongozi wa upinzani.
Lakini pia Mbowe atafakari sana suala la Samia must go ! Je,wataweza kuandamana kwa kiwango cha kuwarudisha Nyuma Makada wa CCM wanaoongoza vyombo vya dola chini ya polisi.? Kuishinda taasisi ya CCM ndani ya polisi ni kuishinda CCM moja kwa moja . Lakini je, Awadhi , Kingai, Wambura , Masauni watakubali kupoteza nafasi zao kwa kuruhusu maandamano wakati Rais ameshawapa hati ya kuua bila kuchukuliwa hatua.?
Je,polisi watatii katiba au Rais au Mungu au Umma wa watanzania ?
Bila shaka viongozi wa polisi pamoja na CCM hawamuogopi Mungu wala Umma wala Katiba bali yule Rais anaye anayewapa vyeo baada ya kuua.
Tuliombee taifa Mungu atuepushe na majanga yanayopangwa na serikali na pia wapinzani nguvu ya maamuzi ibakie kwa Mungu mwenyewe juu ya umma wa watu aliowaumba na kuwaweka humu Tanganyika kabla ya hivi vyeo vya Urais ,uIGP na uwaziri.
Uhai wetu ni Muhimu kuliko madaraka ya mtu