Pac the Don
JF-Expert Member
- Feb 17, 2021
- 6,170
- 7,710
Mzee mikataba na sheria mpya za madini serikali yenyewe kipind cha hayati walibadili sheria kwa matakwa ya wawekezaji, makinikia yanaendelea kwenda nje kama kawaida na mamb ya smelter yakaishia pale. Barick wakaambiwa kujenga smelter hapa bongo ni uamuzi wao wajenge au wasijenge, na kuhusu miamala ya kibenk ilikua ufanyike hapa lkn wakabadili sheria ambayo wao serikali waliiweka na baada ya hapo mialama ikawa inafanyika Bank za nje.Tunarud misiri mdogo mdogo, baada ya Musa kufariki
Mwendazake dishi lilikuwa limeyumba kidogo, sasa kama mtu anasema siku ina masaa 48 na anarudia mara mbilimbili unategemea mzima huyo. Kuna siku akasema kabla hajanunua ndege zake za atcl nauli ya kutoka Dsm to kigoma kwa ndege ilikuwa zaidi ya milioni 8!! Akaja kudanganya kuwa wakati anaingia madarakani wafanyakazi walikuwa wanalipwa mshahara tar. 20 ya mwezi unaofuata, bila aibu siku nyingine akasema alikuta bei ya sukari juu yeye ndiye kaishusha, The guy was a psycho caseMwendazake alikuwa laghailaghai, anadanganya hata akisima a madhabahuni.
Lilikuwa kosa kubwa sana kumsadiki bwana yule
Yalikuwa yanasafirishwa kwenda wapi? Kiwanda cha kuchenjua makinikia kinajengwa Kahama na mkataba wake ulisainiwa January 2021.Watanzania bana, makinikia yanasafiri muda tu, mwendazake alikuwa mtu wa kupiga comedy show za kibabe jukwaani, kisha nyuma ya pazia maisha yanaendelea.
Hayo makinikia yapo safarini zaidi ya miaka 2-3, leo wabunge aliowapachika waje wambadilishie katiba atawale milele, atake asitake, hakuwaachia maagizo ya nini kingine wafanye endapo atarudi kwa Muumba wake. Ndiyo hao kila mtu anatafuta kuonekana ni mbunge machachari anaajua kuihoji serikali.
PM naye anataka kutambulika,kama msimamizi mkuu wa shughuli za serikali, basi tafrani tupu.
Everyday is Saturday............................... 😎
Fala mkubwa hujui chochote mfuate huyo Lissu wako huko kwa mabeberu huyo Rais Wa Chama Cha Mashoga wa SA.Magufuli alikuwa ujinga wa Watanzania walio wengi na ndiyo ukawa mtaji wake kwa propaganda za UWONGO. Wasomi na wajuzi wa mambo akawanyamazisha kwa sheria mbaya za mtandao, takwimu na sheria ya habari. Amedanganya na ikawa ndiyo hulka yetu na mpaka alipokufa tukadanganywa kwa siku 7 kuwa yupo anachapa kazi.
Barrick amerudi kama Twiga Corporation na tukapewa 16 ya second class shares (No voting ppwers), tukaahidiwa 50/50 ya economic benefits (wajinga wanadhani economic benefits =Commercial profits).
Bado Mahakama zetu hazitakuwa na jurisdiction kwenye business dispute (lazima twende London), smelter ya makinikia hakuna. Na kimkataba wa 1998 makinikia yanayokadiriwa kuwa na 0.7 Kg kwa 20ft container ni mali yao, ya kwetu ni Gold na Silver tu ambayo wanailipia. Ile USD 190 Bilion aka noah moja kwa Mtanzania imebaki ndoto za mwendawazimu na Goodwill ya USD 300 Million inamezwa ma madai ya kodi ambazo hatukuwafidia.
Hapo ndipo unamkumbuka Tundu Lissu, kuliko kumpiga risasi walipaswa wamuinguze kwenye Negotiation Team ya Prof Kabudi
Lisu katoka wapi hapa acha siasa kwenye mambo ya msingi. Kamwaga data hapa challenge facts zake sio Lisu Lisu huku ni kuingia chaka.Fala mkubwa hujui chochote mfuate huyo Lissu wako huko kwa mabeberu huyo Rais Wa Chama Cha Mashoga wa SA.
Pamoja kabisaHayo yameanza kusafirishwa tangu 2018. Vipi ile Noah yako inaendeleaje?
Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
No usihofu makinikia bado yataendelea kuzalishwa. Ikikamilika udongo huo utaletwa hapo kuwa processed.Kwahiyo SMELTER yetu hapa Ilemela useless tena?
Sinema la kihindi magu katupiga sanaWaziri Mkuu Kassim Majaliwa kupitia majibu yake bungeni ametuarifu kuwa Serikali imeruhusu usafirishaji wa makinikia nje ya nchi.
Usafirishaji wa haya makinikia nje ya nchi ndio ililteta mgogoro na kampuni hiyo ya uchimbaji dhahabu kiasi kwamba tukaaminishwa kuwa kampuni ilikuwa inatuibia maliasili yetu kwa kusafirisha huo mchanga nje ya nchi.
Waziri Kabudi ndio alikuwa chief negotiator wetu kwenye huo mgogoro na hiyo kampuni.
Ningemuomba atuwekee wazi mambo yafuatayo:
1. Sababu zilizofanya kubadili msimamo hata kuruhusu kampuni iendelee kusafirisha huo mchanga ili hali tuliaminishwa kuwa wangejenga SMELTER hapa nchini.
2. Tuliaminishwa kuwa tulikuwa tunaidai kampuni ya Barrick us$ 191 billion; mpaka Rais akaahidi kuwa baada ya malipo kila mmoja wetu angepata NOAH moja, halafu mkabadilika na kukubali kulipwa us$300 mill. kama kishika uchumba nazo zingelipwa kidogo kidogo!! Kitu gani kiliwasibu?
3. Kwanini mlikubali kuwa migogoro yote na Barrick iamuliwe nje ya nchi na sio Tanzania?
Mwendazake na baraza lake la mawaziri walijua yanakokwenda, Kakonko anazo Bill of Lading,Yalikuwa yanasafirishwa kwenda wapi? Kiwanda cha kuchenjua makinikia kinajengwa Kahama na mkataba wake ulisainiwa January 2021.
Nyie ni wasahaulifu tu, mmesahau kuwa kwenye mkataba mpya wa makubaliano na Barick tuliridhia makinikia yaanze kusafirishwa kwenda nje?, hii ni contrary na sheria aliyoitunga Magufuli mwenyewe ya smelter ijengwe nchiniWamegundua Tanzania kuna Ombwe la uongozi sasa, na wanataka kulitumia kwa advantage yao. Wakati wa magufuli walikubali kabisa kuwa usafirishaji wa makinikia siyo halali, na wakakubali kujenga kinu cha kuchuja dhahaba hapa hapa. Majuzi nilisoma kuwa walikuwa wameanza taratibu za kujenga kinu hicho cha kufua dhahabu huko Geita. Sasa wameona ombwe, basi wamejitututumua; na inawezekana awamu ya nne iko kwenye background hiyo.
JE RAIS SAMIA JUZI KARIAKOO ALIKUWA ANAZURURA?Hotuba za mwanzo Mama, alisema kuna baadhi ya Makampuni ya madini yameanza kugoma vile walivyokuwa wamekubaliana. Aliongea alipodai kuwa yeye ni Rais, na mwenye jinsia ya kike. Nadhani ni hili la makinikia ni moja ya mambo ambayo yamegomewa.
Hivi unadai kuuza makinikia, unatambuaje thamani ya madini yaliyoko ndani. Mfano Waziri Mkuu kadai kuna aina tano za madini. Watajuaje ujazo na thamani ya hayo madini kabla hayajachenjuliwa? Hata dhahabu ili ujue thamani yake ni mpaka imefikia hatua ya mwisho.
Waziri Mkuu angeeleza ni fedha kiasi gani wanauza kwa kontena, kuliko kudai kuwa serikali inapata fedha nyingi bila kutaja kiwango. Walidai itanunuliwa Smelter ili kila kitu kifanyike nchini! Mpaka Mbunge kufikia kuhoji, maana yake hata yeye au Bunge linajua kuwa kulikuwa na makubaliano. Navyo mjua Ndungai swali lingeulizwa na anajua kuna msimamao wa Bunge na serikali angemlinda Waziri Mkuu, mpaka anaruhusu hilo swali ni kweli kila mtu anashangaa.
Waziri Mkuu tukuombe uache kudanganya. Watanzania tunakumbukumbu! Yangekuwa yanauzwa toka wakati wa Magufuli, angeweka wazi kiasi gani tunapata. Yeye alikuwa anaeleza wazi. Ni sawa kwenye Tanzanite alieleza kiasi tulichokusanya baada ya ukuta kujengwa. Mbona kwenye hili hakuwahi kutamka kuwa tunapata fedha nyingi kwa kuuza makinikia? Hata katika report ya CAG hakuna kipengele kinachohusiana na uuzwaji wa Makinikia nje ya nchi! Ili kujua ni kiasi gani tunafaidika na Makinikia!
Nukuu ya enzi hizo kwa watanzania;
"RAIS NI MZIMA NA ANACHAPA KAZI KAMA KAWAIDA. AU MNATHANI RAIS NI WAKUZURURA KARIAKOO"
Tukishakubaliana huwezi kumjua shoga kama wewe siyo shoga. Hivyo basi hata wewe magu2016 unapumuliwa.Fala mkubwa hujui chochote mfuate huyo Lissu wako huko kwa mabeberu huyo Rais Wa Chama Cha Mashoga wa SA.