Kaburi la Petro(Simoni bar-yona) lipo Jerusalem na siyo Roma

Kaburi la Petro(Simoni bar-yona) lipo Jerusalem na siyo Roma

Unamfahamu msabato Carson,aliyekuwa mgombea Wa kiti cha Uraisi pamoja na Donald Trump? Sasa huyo anasema Usabato unatumia Biblia na Mapokeo. Je,kwa nini ninyi mkitumia mapokeo inakuwa sawa ila wakatoliki inakuwa nongwa?
Carson nafikiri kwa sasa ni waziri ktk serikali ya D .TRUMP lkn kwanini kila anaekosoa au kupinga mwenendo fulani kuhusu ukatoliki anaonekana ni Msabato, na si Muislamu au mluttheri.hata km wasabato wanaushambulia sana ukatoliki lkn haihalalishi hilo.
 
Bagatti ni mkatoliki au msabati?
Kwanini unaamini nusu na huamini nusu ukatoliki?
Ukatoliki umejaa mafundisho mengi sana ya uongo na yenye kupotosha. Kanisa Katoliki halifundishi UKWELI hata kidogo, hili ni kanisa linalofundisha mambo ya KIPAGANI zaidi kuliko KWELI ya MUNGU.

Wengi wanaoamini mafundisho ya katoliki ni "vipofu" wa imani, lakini vipofu hawa siku wakipewa macho na wauone UKWELI ndipo watajua kuwa walikuwa wakidanganywa. Muombe MUNGU akupe macho uone KWELI ilipo.
 
Ukatoliki umejaa mafundisho mengi sana ya uongo na yenye kupotosha. Kanisa Katoliki halifundishi UKWELI hata kidogo, hili ni kanisa linalofundisha mambo ya KIPAGANI zaidi kuliko KWELI ya MUNGU.

Wengi wanaoamini mafundisho ya katoliki ni "vipofu" wa imani, lakini vipofu hawa siku wakipewa macho na wauone UKWELI ndipo watajua kuwa walikuwa wakidanganywa. Muombe MUNGU akupe macho uone KWELI ilipo.
Wewe ni mpumbavu au?,mbona kama umepagawa hivi nyoko wewe?. Mi nmekuuliza Bagatti ni mkatoliki au?. Unajibu majibu ya hovyo Hovyo.
 
Wewe ni mpumbavu au?,mbona kama umepagawa hivi nyoko wewe?. Mi nmekuuliza Bagatti ni mkatoliki au?. Unajibu majibu ya hovyo Hovyo.
Mkuu nimekujibu kwa kufuatia swali lako la mwisho. Hebu soma post yako uone kuna maswali mawili umeuliza hapo. Kuhusu imani ya Baggati jibu ni ndiyo, Baggati alikuwa ni Mkatoliki, tena siyo mkatoliki tu bali alikuwa "kasisi" wa kanisa katoliki.
 
Mkuu nimekujibu kwa kufuatia swali lako la mwisho. Hebu soma post yako uone kuna maswali mawili umeuliza hapo. Kuhusu imani ya Baggati jibu ni ndiyo, Baggati alikuwa ni Mkatoliki, tena siyo mkatoliki tu bali alikuwa "kasisi" wa kanisa katoliki.
Kwahiyo wewe na upuuzi wako unamwamini Bagatti MKATOLIKI kwakuwa tu kasema unachokipenda lkn upande wa pili unasema wakatoliki wanafundisha uongo kwakuwa hupendi kile wanachofundisha?
Tukikuuta wewe mjinga tutakuwa tunakosea?,acha unafiki na kiherehere maana unachofanya ni kuingilia mambo ya wakatoliki yasiyokuhusu. Kwanini usiwaache na mambo yao maana ushahidi wako pia ni wa mkatoliki huon kama unajiweka kweny kundi la wapumbavu kubishia ukatoliki wakati huo huo unatumia ukatoliki kuhararisha kubisha kwako?
 
Ukatoliki umejaa mafundisho mengi sana ya uongo na yenye kupotosha. Kanisa Katoliki halifundishi UKWELI hata kidogo, hili ni kanisa linalofundisha mambo ya KIPAGANI zaidi kuliko KWELI ya MUNGU.

Wengi wanaoamini mafundisho ya katoliki ni "vipofu" wa imani, lakini vipofu hawa siku wakipewa macho na wauone UKWELI ndipo watajua kuwa walikuwa wakidanganywa. Muombe MUNGU akupe macho uone KWELI ilipo.

1. Kujigeuza na kuwa mpiga ramli Wa tarehe ya kurudi Yesu, sio upofu Wa kiimani? Willam Miller na kundi lake, umesahau kwamba walijipa uwezo Wa kuifahamu tarehe ya kurudi Yesu?

2. Je, sio upofu Wa imani Ellen White kuwafundisheni kwamba shetani ndiye atakayeba dhambi za Osama Bin Ladeni kudungua majengo ya WTC September 11?

3. Sio upofu Wa kiimani Ellen kuwakatazeni kula Nguruwe wakati yeye alikuwa anaifukamia?
 
Hata wakisema Petro alizikwa Chattle sioni shida yoyote . Swala la Petro alizikwa wapi haina mafungamano yoyote na imani yangu kwa Mungu maana alikuwa ni mtu kama mimi.
Anataka tujue kaburi sijui anataka tukatambikie ?????????
Babu yangu mwenyewe sijui kaburi lake ije kuwa huyo babu wa wayahudi. !!!!!!!!!

Taabu ya wasabato wanautamani Sana ukatoliki. Sana Sana maana hata makanisani mwao. Hawaishi kuuhubiri ukatoliki. Na wanausoma kuliko wanavyosoma biblia.
Wasabato wameshagawanyika
Mafungu marungu
1) sabato masalia.
2) sabato watunza siku ya sabato
3) sabato maboresho, wanataka kurekebisha usabato.
 
Kwa zaidi ya maika 2000 watu wamekuwa wakiaminishwa kuwa Mtume Petro aliuwawa Roma na kuzikwa huko kwenye eneo lililojulikana kama tropaion. Tena imekuwa ikifundishwa na Kanisa Katoliki kuwa Petro ndiye alikuwa Papa wa kwanza lakini ukweli ni kwamba katika maisha yake yote Petro hakuwahi kabisa kuwa Papa achilia mbali kufika tu ROMA. Maisha yake yote Petro au Kefa kama wengine wanavyomwita hakuwahi kabisa kukanyaga ardhi ya Roma.

Mwaka 1958 huko Jerusalemu katika eneo lijulikanalo kama "Dominus Flevit" kwenye mlima wa Mizeituni ambapo kwa sasa hivi pamejengwa kanisa linaloitwa Franciscan Monastery yalichimbuliwa mabaki ya mifupa yaliyokuwa ndani ya boksi(ossuaries)na juu ya boksi hili kulikuwa na maandishi yaliyoandikwa kwa lugha ya Aramaic yakisomeka "Simon Bar Jona". Eneo ilipopatikana mifupa hiyo pia ilipatikana mifupa ya watu wengine ikiwa imehifadhiwa ndani ya maboksi hayo na juu yake yakiwa yameandikwa majina yao. Majina hayo ni pamoja na Mariam, Martha na Lazaro. Inaaminika kuwa Wakristo wa Mwanzo kabisa baada ya kupaa kwa MESSIAH kwenda mbinguni, walichagua kuzikana eneo hilo la Mlima wa Mizeituni, kwasababu imeandikwa kwenye Biblia kuwa siku MESSIAH atakaporudi tena duniani atasimama juu ya Mlima huo, soma ZEKARIA 14:3-4. Kutokana na imani waliyokuwa nayo, Wakristo hao waliamini kuwa itakuwa vema kama watazikwa eneo hilo ili siku ile BWANA YESU atakapokuja na kuwafufua, wawe wa kwanza kumlaki BWANA kwenye Mlima huo wa Mizeituni.


Franciscan "Terra Santa" Monastery, Jerusalem, mahali ambapo mifupa ya Petro ilipopatikana.
View attachment 669269
Mifupa hiyo inayoaminika kuwa ni ya Petro, ilichimbuliwa na Archeologist wa Kiitaliano ambaye alikuwa ni Priest wa Kikatoliki akijulikana kama P.B. Bagatti. Baada ya kuichimbua mifupa hii na kujiridhisha yeye na wenzake aliokuwa nao, Bagatti alikwenda Vatican na kumjulisha Papa wa wakati ule aliyekuwa akiitwa Pius XII. Papa Pius XII alopoambiwa habari hizo na kuoneshwa ushahidi wote, alijibu tu kwa kusema; “inawezekana ikawa kweli hiyo ni mifupa ya PETRO, na inabidi tufanye marekebisho makubwa, lakini kwa sasa hivi kaeni kimya kabisa”. Bagatti akamuuliza Papa Pius XII, Je, unaamini itakuwa ni mabaki ya Petro? Papa Pius XII akamjibu kwa kusema; “kwa ushahidi ulionionesha, naamini itakuwa ni mifupa ya Petro”.

Cha ajabu ni kwamba mpaka Papa Pius XII anafariki dunia Octoba 9, 1958 hakuweka hadharani kabisa uvumbuzi huo uliofanywa na Archeologist Bagatti. Mwaka huo huo Bagatti ndipo akaamua kuandika kitabu akielezea kupatikana kwa mifupa ya Petro huko Jerusalem, kitabu hicho kinachoitwa, "Gli Scavi del Dominus Flevit", kilichochapishwa mwaka 1958. Kitabu hichi kiliandikwa na P. B. Bagatti akishirikiana na Archeologist mwenzake J. T. Milik, ambao wote walikuwa pia ni Ma-Priest wa Kanisa Katoliki. Bagatti anaonekana kuficha baadhi ya mambo na haelezei kwa undani hasa nini kilifanyika. Hii inadhihirisha wazi kabisa kuwa walifungwa mdomo na Kanisa Katoliki ili wasiweke kila kitu hadharani kwani kama wangefanya hivyo ingekuwa ni sawa na kulivua nguo kanisa, kwani kwa miaka yote kanisa Katoliki limekuwa likifundisha kuwa Petro aliishi Roma kwa miaka 24 na kuuawa na kuzikwa huko.
View attachment 669271
View attachment 669272
Maneno hayo hapo juu yanasomeka "Simoni Bar Yona"​

Ushahidi mwingine unaoonesha wazi kabisa kuwa Petro hakuwahi kabisa kufika Roma, ni Biblia. Mtume Paulo katika Waraka zake zote hakuna mahali ameandika kuwa Petro alikwenda Roma na kuishi huko. Paulo alikuwa ni mtu anayependa sana kuandika kila kitu anachokutana nacho. Isingewezekana kabisa Petro ahamie Roma na kuishi huko kwa miaka 24 halafu Paulo asiandike, achilia mbali Petro mwenyewe asiandike kabisa Waraka wowote ule akielezea maisha yake akiwa Roma. Haiingii akilini hata kidogo mtu kama Petro eti akaishi mahali kwa miaka 24 akihubiri Injili, halafu jambo hilo lisiwemo kabisa ndani ya Biblia.

Isitoshe ukisoma Biblia utaona Paulo anaelezea wazi kabisa kuwa Petro alikuwa ni Mtume kwa ajili ya Wayahudi, soma WAGALATIA 2:7-8. Pia tukisoma Biblia tunaona BWANA anamtokea Anania kwenye maono na kumwambia aende akaonane na Sauli(Paulo), sababu yeye BWANA amemchagua SAULI(PAULO)kuwa Mtume wa Mataifa, soma MATENDO YA MITUME 9:10-15. Pia ukisoma Waraka wote wa Petro hakuna mahali popote Petro ameandika kuwa yupo Roma.

Kutokana na yote hayo na ushahidi wa mifupa iliyopatikana Jerusalem, ni kielelezo tosha kuwa Roman Catholic Church wanafundisha “uwongo” na wanafanya kila wawezalo kuuficha UKWELI. Kanisa hili limejaa mafundisho ya uwongo na kwa miaka mingi sana limewapotosha watu wengi sana. Kanisa hili lina intelijesia kali sana kiasi kwamba wanaweza kuficha habari yoyote ile isiwafikie watu, lakini kamwe hawawezi kushindana na MUNGU hasa pale anapoamua UKWELI lazima ujulikane.

Tokea mwaka 1958 ilipogundulika mifupa hii ya PETRO huko Jerusalem, Kanisa Katoliki limekuwa likificha uvumbuzi huu kwa kila namna. Eneo ambapo ilipatikana mifupa hii linamilikiwa na Kanisa hilo hivyo imekuwa rahisi wao kuuficha ukweli lakini pia ndani ya kanisa wapo baadhi ya Ma-Priest ambao huwa hawawezi kukaa kimya na wamekuwa wakivujisha siri hizi.
Unataka kwenda kutambika ????
 
1. Kujigeuza na kuwa mpiga ramli Wa tarehe ya kurudi Yesu, sio upofu Wa kiimani? Willam Miller na kundi lake, umesahau kwamba walijipa uwezo Wa kuifahamu tarehe ya kurudi Yesu?

2. Je, sio upofu Wa imani Ellen White kuwafundisheni kwamba shetani ndiye atakayeba dhambi za Osama Bin Ladeni kudungua majengo ya WTC September 11?

3. Sio upofu Wa kiimani Ellen kuwakatazeni kula Nguruwe wakati yeye alikuwa anaifukamia?
Nani kakuambia mimi ni Mfuasi wa Ellen White? Mkuu siyo kila mtu anayeishika Sabato ni mfuasi wa Ellen White. Fahamu kwamba kuna madhehebu zaidi ya 500 yanayoabudu siku ya Sabato.
 
Ila katika ushahidi hawajaonesha njia iliyotumika kuthibitisha hiyo mifupa ni ya Petro. Inaweza isiwe ya Petro. Wanaweza kua waongo ila hamaanishi wewe umesema ukweli
 
Nani kakuambia mimi ni Mfuasi wa Ellen White? Mkuu siyo kila mtu anayeishika Sabato ni mfuasi wa Ellen White. Fahamu kwamba kuna madhehebu zaidi ya 500 yanayoabudu siku ya Sabato.

Nisamehe Mkuu! Kumbe wewe sio msabato Wa kawaida. Kwa hiyo wewe unajitofautisha vipi na Wasabato wengine?
 
Kukaa kwenye dini kwa kudhani unaijua dini na historia yake ni kupotea. Au kuamini dini au dhehebu lako liko sahihi upungufu wa kufikiri
 
uhalisia wa PETRO na kanisa KATOLIKI....

sasa naomba tumtazame MTUME PETRO (KHALIFA WA KWANZA WA KRISTO) JAPO KIUFUPI MAISHA YAKE MPAKA KIFO CHAKE.....


Petro alifia wapi na kwa sababu gani na nini kiliendelea baada ya hapo

Ni kweli kabisa kwamba kama walivyo binadamu wengine, Petro alizaliwa na kuishi, kipindi na muda wake wa kuishi ulipomalizika alikufa.

Petro mtume ndiye alikabidhiwa kanisa na Bwana wetu Yesu Kristo kabla ya kifo na ufufuko wake rej.Mt 16:18.

Jina lake halisi lilikuwa Simon Bar-Yona mwenyeji wa Galilaya.Kazi yake ilikuwa ni uvuvi kabla hajaitwa kuvua watu kama tunavyosoma Mt 4:18-20.

Pamoja na kwamba Petro anatufundisha mambo mengi,Biblia haituelezi mwisho wa maisha yake.Tunachoambiwa ni kwamba,baada ya mitume kumpokea Roho Mtakatifu,siku ile ya pentekoste walianza kazi ya Kutangaza habari za ufufuko wa Yesu.

Kazi ya kutangaza habari za ufufuko wa Yesu ilikuwa ngumu na iliwabidi mitume wasambae huko na huko ili kueneza habari hiyo kwa watu.Habari za mitume na kazi zao baada ya kumpokea Roho Mtakatifu tunazipata kutoka katika kitabu cha Matendo ya mitume. Sasa,kuhusiana na Petro,maelezo ya wazi kutoka katika Biblia Takatifu yanaanza pale tunapoelezwa juu ya Philip ambaye baada ya kumpokea Roho Mtakatifu alienda hadi Samaria na huko akafanikiwa kupata wafuasi wengi.

Aliporudi kanisa la Yerusalemu likamtuma Petro ili akatoe msaada zaidi huko rej.Mdo 8:14-16,baada ya hapo tunaambiwa kwamba Petro alikwenda hadi Kaisaria akambatiza Kornelio rej.Mdo 9:32,

halafu alipotoka huko Petro alirudi Yerusalemu akakamatwa na Herode Agrippa akafungwa rej Mdo 12:1-3,na baada ya kuokolewa kwa muujiza na malaika toka gerezani,Biblia inatuambia kwamba aliamua kuwa mhubiri wa mataifa rej.Mdo12:17-19.

Maelezo hayo ndiyo yaliyo wazi kabisa kutoka katika Biblia yetu.Hapa ndipo sasa utajiri wa kanisa katoliki unapodhihirishwa wazi linapotumia vyanzo vikuu viwili vya mafundisho ya imani yaani Biblia Takatifu na Mapokeo.Utajiri tulionao kutoka katika mapokeo ndio unaoweza kutufanya kupata na kujua mambo na habari muhimu kuhusu petro.

Watu wa madhehebu mengine yasiyo ya kikatoliki hawana na hawapendi kutumia chanzo hiki cha mafundisho ya imani yaani mapokeo ndiyo maana kwao inaweza kuwa vigumu kujua kama alikufa na kuzikwa mahali fulani ingawa wanaamini kwamba aliishi kwani hilo halimo katika Biblia Takatifu.

Kutokana na mapokeo Petro baada ya kutoka Yerusalemu inasadikika kwamba alikwenda kati ya Antiokia au Alexandria.Ndiyo maana ukisoma Mdo 15:7-11 pale katika mkutano wa Yerusalemu Petro anaongea kama mmisionari na ukisoma pia Gal 2:7-8 Petro anatajwa kama mtu aliyewahubiria wayahudi.Sasa,alipotoka huko yaani Antiokia au Alexandria ndipo alikwenda Roma na huko akachaguliwa kuwa kiongozi mkuu wa mitume na Askofu wa kwanza wa Roma.Kama kiongozi wa Roma Petro alifanya kazi katika mazingira magumu maana ilimbidi apingane na utawala wa kirumi uliokuwa chini ya Nero aliyekuwa adui wa wakristo.

Mababa wa kanisa yaani wale ambao walikuwa wanafunzi wa mitume au wafuasi wa wanafunzi wa mitume, wanatupatia habari nyingi zaidi kuhusu Petro.Wa kwanza anayetupatia habari hizo ni Clement wa Roma.Huyu ndiye aliyekuwa askofu wa tatu wa Roma baada ya Petro na Linus.

Katika barua yake kwa wakorintho aliyoiandika mwaka 96 BK aliwataarifu wakorintho kwamba Petro na Paulo waliuawa huko Roma na aliyewaua ni Nero kutokana na wivu na chuki kwa kanisa.Ukitaka kuelewa juu ya mateso waliyoyapata hawa wawili naomba usome 2kor 11:23-27.

Baada ya mateso kutoka kwa Nero kuzidi, Petro aliamua kutoroka kutoka Roma.Mapokeo yanatudhihirishia kwamba alipokuwa akiondoka kutoka mjini Roma, alikutana na Yesu ndipo Petro akamuuliza Yesu akisema, “ QUO VADIS”,tafsiri yake “unakwenda wapi”?.Yesu akamjibu, “nakwenda huko Roma unakotoka nikasulibiwe tena”.

Hapo Petro alijisikia vibaya kuona kwamba anayakimbia mateso aliyokubali kuyapokea siku alipokubali kwa dhati kuwa mfuasi wa Yesu.Akaamua kurudi tena Roma.

Baba wa kanisa Tacitus katika maandishi yake anasema kwamba aliporudi Roma alikamatwa na kusulibiwa akachagua kuteswa msalabani kichwa chini miguu juu maana Petro mwenyewe alisema kwamba hakustahili kusulibiwa kama Bwana wake Yesu Kristo.
 
Baada ya kifo chake, Petro alizikwa mahali ambapo leo hii kanisa linalojulikana kama kanisa la Mt Petro limejengwa yaani huko Vatican Roma. Kinachotuthibitishia hilo ni kile kilichotokea mwaka 1939 hadi 1949 wakati kanisa hilo la Mt.Petro lilipokuwa likifanyiwa ukarabati. Wajenzi waliligundua kaburi lake na kwa uhakika wote walielewa kwamba ndilo hasa lenyewe walipokuta ukuta mwekundu wenye maandishi ya kigiriki yaliyosomeka, “PETROS ENI ” tafsiri yake kwa kiingereza ni“PETER IS INSIDE”,na kwa kiswahili,“PETRO YUMO NDANI”.

Mwaka 1950 siku ya Krismasi Baba mtakatifu Papa Pius XII alithibitisha hilo.Mambo haya ya kale sisi tunashindwa kuyaelewa kwa urahisi kwa sababu hatujihusishi sana nayo kama ndugu zetu wa nchi zilizoendelea wale wanaoitwa archeologists.


MWISHO NAOMBA UELEWE KUWA BABA MTAKATIFU AU PAPA NI NANI HASA

naomba nieleze kinagaubaga kuhusu Baba Mtakatifu au Papa ni nani, sawia na mamlaka yake katika Kanisa Katoliki.

Papa au Baba Mtakatifu ni wakili wa Yesu Kristo, Halifa wa Mtume Petro, Mkuu wa Kanisa Katoliki, Askofu wa jimbo la Roma, na Baba wa Kanisa la Magharibi ambalo kabla ya Mtaguso wa Mkuu wa pili wa Vaticano, lilitumia lugha ya Kilatini katika Ibada zake. Zaidi ya hapo Baba Mtakatifu ni Mkuu wa Jimbo la Kanisa la Italia na ni Rais wa Nchi ndogo ya Vaticani.

Kadiri ya Imani Katoliki, cheo cha Baba Mtakatifu kinatokana na ujumbe aliopewa Mtume Petro na Bwana wetu Yesu Kristo mwenyewe. Mtume Petro, kufuatana na ushahidi dhahiri alikufa Roma, na kaburi lake liligunduliwa chini ya Altare kuu ya Kanisa la Mtakatifu Petro huko Roma.

Tukirejea kwenye sheria za Kanisa Katoliki ambazo ni ufafanuzi wa zile amri Kumi za Mungu, sheria namba 331, inasema hivi nanukuu; “Askofu wa Kanisa la Roma ambaye katika yeye inadumu ofisi iliyokabidhiwa na Bwana kwa Petro mwenyewe, wa kwanza katika Mitume na inayopaswa kupitishwa kwa Mahalifa wake ni Mkuu wa jopo la Maaskofu, wakili wa Kristo na mchungaji wa Kanisa zima hapa duniani; hivyo kwa dhati ya ofisi yake anayo madaraka ya kawaida, ya juu, kamili, yanayojitegemea, naya jumla katika Kanisa, ambayo anaweza daima kuyatumia kwa uhuru”. Mwisho wa nukuu. Pia sheria ya Kanisa Katoliki namba 333, inasema, nanukuu; “Baba Mtakatifu hupata madaraka kamili na ya juu katika Kanisa kwa njia ya uchaguzi halali alioukubali mwenyewe pamoja na kupewa uaskofu. Hivyo Yule aliye Askofu tayari hupata madaraka hayo tangu wakati anapokubali uchaguzi wake kuwa Baba Mtakatifu. Lakini kama Yule aliyechaguliwa hana uaskofu, anabidika kupewa uaskofu mara moja”. Mwisho wa nukuu, hata hivyo kifungu cha pili cha sheria hiyo namba 333, kinasema hivi, nanukuu, “Ikitokea kuwa Baba Mtakatifu anajiuzulu ofisi yake, ili iwe halali inatakiwa ajiuzulu kwa hiari na tendo hilo lidhihirishwe ipaswavyo, lakini si kwamba likubaliwe na yeyote”. Mwisho wa nukuu.

baada ya maelezo hayo mafupi kuhusu Baba Mtakatifu kama ni nani na wadhifa wake katika Kanisa Katoliki, naomba sasa twnde kwenye chimbuko la jina papa

chimbuko la jina hili Papa, hadi wakawa wanapewa viongozi hawa wa dunia wa Kanisa Katoliki, ni kwamba jina hili Papa ni neno la Kiitaliano ambalo limetokana na neno la Kigiriki Pappas, ambalo kwa kiingereza ni Fadher na Baba kwa lugha yetu ya Kiswahili.

Neno hili Papa lilitumiwa na Mapadre wa Makanisa ya Kigiriki. Na hapo ndipo sasa Mababa wa Kanisa Katoliki wakaona ni jina linalofaa apewe kiongozi wa dunia wa Kanisa Katoliki, yaani Baba Mtakatifu, kulingana na hadhi yake kama Baba wa Wakatoliki wote duniani.

Baba Mtakatifu ni kilele cha muundo wote wa daraja za Kanisa, na uwezo wote wa kimuundo katika Kanisa unatoka kwake, na hivyo tunaweza kusema ni sawa na Baba wa familia katika hali ya kawaida, kuwa yeye ni kichwa cha familia na anayo madaraka yote ya ndani ya familia ile. Ndivyo ilivyo kwa Baba Mtakatifu kama halifa wa Mtume Petro, Askofu wa Roma, wakili wa Yesu Kristo hapa duniani na mkubwa wa Kanisa Katoliki (rej. Mt 16:18-19; Yn 10:16). Nanukuu, “Nami nakuambia: Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga Kanisa langu, wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Nami nitakupa wewe funguo za ufalme wa mbinguni; na lolote utakalolifunga duniani, litakuwa limefungwa mbinguni, na lolote utakalolifungua duniani, litakuwa limefunguliwa mbinguni”. Mwisho wa nukuu (rej. Mt 16:18-19).

Zaidi ya hapo, zamani hizo, jina hili Papa (yaani Baba), lilitolewa kwa Maaskofu, na lilitumiwa sana katika mzingo wa Kimonaki na likawa jina la kawaida kwa Mapadre wa Kanisa la Orthodoksi na pia Mapadre wa sehemu fulani za Kanisa Katoliki la Roma.

Na huko Misri jina hilo Papa lilikuwa ni haki ya Askofu wa Alexandria tu. Lakini kuanzia katikati ya karne ya sita (6th c), na kuendelea hadi hivi leo, jina hilo Papa limewekwa maalumu kwa ajili ya Askofu wa Roma tu, yaani kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani. Na utume huo uliwekwa kisheria na Baba Mtakatifu Gregori wa VII.

Sanjali na hilo kuna sababu za kimazingira kuwa Waitaliano ndiyo waliopokea mafundisho ya Mitume wenye sifa bora, nao ni Mtume Paulo na Mtume Petro ambaye alikuwa kiongozi wa Mitume na halifa wa Yesu Kristo. Inasadikika kwamba Mitume hao wakuu yaani Perto na Paulo waliacha mafundisho ya Yesu mikononi mwa Waroma na ndiyo maana mpaka leo hii makao makuu ya Kanisa Katoliki yapo Roma. Kutokana na mapokeo ya Kanisa sisi tunajua kwamba Mtume Petro kama kiongozi wa Kanisa la Roma alikamatwa na Mfalme Nero pamoja na Paulo Mtume na Wakristo wengine wengi.

Na baada ya kufungwa katika gereza la Mamertino, Petro alisulubiwa katika shamba la kuzikia lililokuwa katika ukingo wa mlima Vatikano mwaka Sitini na Saba (67), na hivyo Wakristo wa zamani walijenga kumbukumbu hapo.

Tena, mara baada ya Mfalme Mkuu Konstantino kutoa uhuru wa dini, Wakristo kwa msaada wa Kaisari huyo walijenga Kanisa la kwanza juu ya kaburi la Mtume Petro, wakiliacha kaburi chini ya Altare. Na kwa udhibitisho walichimba kwa miaka mingi chini ya Altare ya Kanisa la Mtume Petro, na mwisho wakafika kwenye kaburi lenyewe kwa kukuta maneno “Petro iki” yaani Petro yu hapa.


Ndugu ili kudhibitisha ukuu wa Kanisa la Roma mapokeo yanasema ;

Askofu wa Lione (Ufaransa), mwaka 115, Mt. Ireneo aliyekuwa mfuasi wa Mt. Polycarpi ambaye ni mwanafunzi wa Mtume Yohane, aliandika maneno yafuatayo katika kitabu chake kinachoitwa Dhidi ya Waasi sura ya II.

Nanukuu, “Mafundisho ya Mitume duniani kote yaweza kupatikana katika kila Kanisa, na kila mtu anaweza kuyapata, sisi tunaweza kuleta orodha ya Maaskofu waliopata cheo kutoka kwa mitume na mahalifa wao, mfuatano hadi siku hizi zetu. Lakini ingekuwa kazi ya kuchosha mno kuleta katika kitabu hiki mfuatano huo wa Mitume katika Kanisa. Ni bora nilete mapokea ya kitume na mafundisho ya imani ya Kanisa kubwa zaidi, ya zamani zaidi na lililojulikana kwa watu wote, ambalo liliwekwa kwa kimsingi huko Roma na Mitume wenye sifa bora, yaani Petro na Paulo. Kanisa hili limefika kwetu hadi leo kwa njia ya mfuatano wa Maaskofu na Mahalifa wao. Sasa basi kila Kanisa, yaani waamini wa duniani kote lazima wakubaliane na kushirikiana na Kanisa la Roma, kwa sababu ya cheo chake bora sana”. Mwisho wa nukuu.

Na zaidi ya hapo kuna uhakika kuwa mapokeo ya Mitume yanahifadhiwa huko Roma na baada ya Mitume waadhama kuweka misingi ya Kanisa la Roma na kuliongoza, uaskofu walipitisha wao kwa Linus kwa ajili ya uongozi wa Kanisa zima. Linus huyu ni Yule anayekumbukwa na Mtume Paulo katika waraka wake wa pili kwa Timotheo, (rej. 2Tim 4:21).

ndugu kutokana na ukweli huo kuwa misingi ya Kanisa Katoliki iliwekwa Roma na Mitume hao maarufu, yaani Petro na Paulo, bila shaka utakubaliana nami kuwa Waitaliano ni moja ya watu walioachiwa Kanisa na kuchukua jukumu la kuendeleza kazi ya uenezaji wa neno la Mungu duniani kote, kama ilivyokuwa ujumbe wa Kristo mwenyewe kwa Mitume wake.
Nanukuu, “Basi, enendeni mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi, mkiwabatiza kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, na kuwafundisha kuyashika yote niliyowaamuru ninyi. Na tazama mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari”. Mwisho wa nukuu (rej. Mt 28:19-20). Kwa udhibitisho wa hilo na mengi zaidi ya hayo nilio kueleza toka mwanzo unaweza kutafuta na kukisoma kitabu chenye kichwa cha habari PAPA NI NANI, kilichoandikwa na Padre Medri na Padre Magnus Lunyungu

From
SALA NA KAZI
 
Ni kweli kabisa ila jambo hili linazimwa sana ili lisienee duniani....hata nami nlipofahamu nlishangaa sana kwani ni habari zinazofichwa na ulimwengu!!
 
Back
Top Bottom