Kaburi la Petro(Simoni bar-yona) lipo Jerusalem na siyo Roma

Kaburi la Petro(Simoni bar-yona) lipo Jerusalem na siyo Roma

Asante sana mkuu kwa kuongeza ufahamu mkubwa ndani yangu!!! Kuna prof Mmoja aliwahi kusema adui wa ukristo ni Roman Catholic, hawana muda na kuuishi ukristo bali mapokeo yao ambayo ni kivuli cha maovu
100%WAKATOLIKI SI WAKRISTO NA HAWAJAWAHI KUWA WAKRISTO.HII ITABAKI KUWA NI DOLA YA KIRUMI.MAINJINIA WA NWO.
 
Kwa zaidi ya maika 2000 watu wamekuwa wakiaminishwa kuwa Mtume Petro aliuwawa Roma na kuzikwa huko kwenye eneo lililojulikana kama tropaion. Tena imekuwa ikifundishwa na Kanisa Katoliki kuwa Petro ndiye alikuwa Papa wa kwanza lakini ukweli ni kwamba katika maisha yake yote Petro hakuwahi kabisa kuwa Papa achilia mbali kufika tu ROMA. Maisha yake yote Petro au Kefa kama wengine wanavyomwita hakuwahi kabisa kukanyaga ardhi ya Roma.

Mwaka 1958 huko Jerusalemu katika eneo lijulikanalo kama "Dominus Flevit" kwenye mlima wa Mizeituni ambapo kwa sasa hivi pamejengwa kanisa linaloitwa Franciscan Monastery yalichimbuliwa mabaki ya mifupa yaliyokuwa ndani ya boksi(ossuaries)na juu ya boksi hili kulikuwa na maandishi yaliyoandikwa kwa lugha ya Aramaic yakisomeka "Simon Bar Jona". Eneo ilipopatikana mifupa hiyo pia ilipatikana mifupa ya watu wengine ikiwa imehifadhiwa ndani ya maboksi hayo na juu yake yakiwa yameandikwa majina yao. Majina hayo ni pamoja na Mariam, Martha na Lazaro. Inaaminika kuwa Wakristo wa Mwanzo kabisa baada ya kupaa kwa MESSIAH kwenda mbinguni, walichagua kuzikana eneo hilo la Mlima wa Mizeituni, kwasababu imeandikwa kwenye Biblia kuwa siku MESSIAH atakaporudi tena duniani atasimama juu ya Mlima huo, soma ZEKARIA 14:3-4. Kutokana na imani waliyokuwa nayo, Wakristo hao waliamini kuwa itakuwa vema kama watazikwa eneo hilo ili siku ile BWANA YESU atakapokuja na kuwafufua, wawe wa kwanza kumlaki BWANA kwenye Mlima huo wa Mizeituni.

Franciscan "Terra Santa" Monastery, Jerusalem, mahali ambapo mifupa ya Petro ilipopatikana.
View attachment 669269
Mifupa hiyo inayoaminika kuwa ni ya Petro, ilichimbuliwa na Archeologist wa Kiitaliano ambaye alikuwa ni Priest wa Kikatoliki akijulikana kama P.B. Bagatti. Baada ya kuichimbua mifupa hii na kujiridhisha yeye na wenzake aliokuwa nao, Bagatti alikwenda Vatican na kumjulisha Papa wa wakati ule aliyekuwa akiitwa Pius XII. Papa Pius XII alopoambiwa habari hizo na kuoneshwa ushahidi wote, alijibu tu kwa kusema; “inawezekana ikawa kweli hiyo ni mifupa ya PETRO, na inabidi tufanye marekebisho makubwa, lakini kwa sasa hivi kaeni kimya kabisa”. Bagatti akamuuliza Papa Pius XII, Je, unaamini itakuwa ni mabaki ya Petro? Papa Pius XII akamjibu kwa kusema; “kwa ushahidi ulionionesha, naamini itakuwa ni mifupa ya Petro”.

Cha ajabu ni kwamba mpaka Papa Pius XII anafariki dunia Octoba 9, 1958 hakuweka hadharani kabisa uvumbuzi huo uliofanywa na Archeologist Bagatti. Mwaka huo huo Bagatti ndipo akaamua kuandika kitabu akielezea kupatikana kwa mifupa ya Petro huko Jerusalem, kitabu hicho kinachoitwa, "Gli Scavi del Dominus Flevit", kilichochapishwa mwaka 1958. Kitabu hichi kiliandikwa na P. B. Bagatti akishirikiana na Archeologist mwenzake J. T. Milik, ambao wote walikuwa pia ni Ma-Priest wa Kanisa Katoliki. Bagatti anaonekana kuficha baadhi ya mambo na haelezei kwa undani hasa nini kilifanyika. Hii inadhihirisha wazi kabisa kuwa walifungwa mdomo na Kanisa Katoliki ili wasiweke kila kitu hadharani kwani kama wangefanya hivyo ingekuwa ni sawa na kulivua nguo kanisa, kwani kwa miaka yote kanisa Katoliki limekuwa likifundisha kuwa Petro aliishi Roma kwa miaka 24 na kuuawa na kuzikwa huko.
View attachment 669271
View attachment 669272
Maneno hayo hapo juu yanasomeka "Simoni Bar Yona"​

Ushahidi mwingine unaoonesha wazi kabisa kuwa Petro hakuwahi kabisa kufika Roma, ni Biblia. Mtume Paulo katika Waraka zake zote hakuna mahali ameandika kuwa Petro alikwenda Roma na kuishi huko. Paulo alikuwa ni mtu anayependa sana kuandika kila kitu anachokutana nacho. Isingewezekana kabisa Petro ahamie Roma na kuishi huko kwa miaka 24 halafu Paulo asiandike, achilia mbali Petro mwenyewe asiandike kabisa Waraka wowote ule akielezea maisha yake akiwa Roma. Haiingii akilini hata kidogo mtu kama Petro eti akaishi mahali kwa miaka 24 akihubiri Injili, halafu jambo hilo lisiwemo kabisa ndani ya Biblia.

Isitoshe ukisoma Biblia utaona Paulo anaelezea wazi kabisa kuwa Petro alikuwa ni Mtume kwa ajili ya Wayahudi, soma WAGALATIA 2:7-8. Pia tukisoma Biblia tunaona BWANA anamtokea Anania kwenye maono na kumwambia aende akaonane na Sauli(Paulo), sababu yeye BWANA amemchagua SAULI(PAULO)kuwa Mtume wa Mataifa, soma MATENDO YA MITUME 9:10-15. Pia ukisoma Waraka wote wa Petro hakuna mahali popote Petro ameandika kuwa yupo Roma.

Kutokana na yote hayo na ushahidi wa mifupa iliyopatikana Jerusalem, ni kielelezo tosha kuwa Roman Catholic Church wanafundisha “uwongo” na wanafanya kila wawezalo kuuficha UKWELI. Kanisa hili limejaa mafundisho ya uwongo na kwa miaka mingi sana limewapotosha watu wengi sana. Kanisa hili lina intelijesia kali sana kiasi kwamba wanaweza kuficha habari yoyote ile isiwafikie watu, lakini kamwe hawawezi kushindana na MUNGU hasa pale anapoamua UKWELI lazima ujulikane.

Tokea mwaka 1958 ilipogundulika mifupa hii ya PETRO huko Jerusalem, Kanisa Katoliki limekuwa likificha uvumbuzi huu kwa kila namna. Eneo ambapo ilipatikana mifupa hii linamilikiwa na Kanisa hilo hivyo imekuwa rahisi wao kuuficha ukweli lakini pia ndani ya kanisa wapo baadhi ya Ma-Priest ambao huwa hawawezi kukaa kimya na wamekuwa wakivujisha siri hizi.
Ndugu naomba nami nichangie kidogo. Ukristu ni utaratibu wa maisha unaotusaidia kuwa kalibu na Mungu yaani kunda upya mausiano yetu na Mungu. Kutokana na zambi ya kukosa utii , wazazi wetu wa mwanzo walivunja hayo mausiano. Kwa hiyo Petro kufa kwake Roma au sehemu nyingine aimfanyi mtu flani awe mkristu, ama kama Petro alikuwa papa wa kwanza au la aimfanyi mtu kuwa mkristu. Mkristu ni kristu mwengine. Yaani yule aishie yale kilisto aliyoyafundisha . Unaweza sema utayajuaje yale Kristu aliyoyafundisha , kupitia Makanisa haya haya tulionayo . Biblia inasema Kayafa alitabili ni heri mtu mmoja afe kwa ajili ya wengi si kwa sababu alikuwa mtu mtakatifu, hapana bali kwa sababu alikuwa kuwani mkuuu . na kunasehemu nyingine inasema wao wamekaa katika viti vya Musa yaani makuani na makasisi, wasikilizeni wasemacho bali matendo yao msiyafuate . Mungu alimtumia Paul aliyekuwa mzambi kuwaokoa maelufu . Kwa hiyo amini unachoamini na usipambane na kuvuluga watu wengine wanavyo amini.
 
100%WAKATOLIKI SI WAKRISTO NA HAWAJAWAHI KUWA WAKRISTO.HII ITABAKI KUWA NI DOLA YA KIRUMI.MAINJINIA WA NWO.

Unamfahamu msabato Carson,aliyekuwa mgombea Wa kiti cha Uraisi pamoja na Donald Trump? Sasa huyo anasema Usabato unatumia Biblia na Mapokeo. Je,kwa nini ninyi mkitumia mapokeo inakuwa sawa ila wakatoliki inakuwa nongwa?
 
Ndugu naomba nami nichangie kidogo. Ukristu ni utaratibu wa maisha unaotusaidia kuwa kalibu na Mungu yaani kunda upya mausiano yetu na Mungu. Kutokana na zambi ya kukosa utii , wazazi wetu wa mwanzo walivunja hayo mausiano. Kwa hiyo Petro kufa kwake Roma au sehemu nyingine aimfanyi mtu flani awe mkristu, ama kama Petro alikuwa papa wa kwanza au la aimfanyi mtu kuwa mkristu. Mkristu ni kristu mwengine. Yaani yule aishie yale kilisto aliyoyafundisha . Unaweza sema utayajuaje yale Kristu aliyoyafundisha , kupitia Makanisa haya haya tulionayo . Biblia inasema Kayafa alitabili ni heri mtu mmoja afe kwa ajili ya wengi si kwa sababu alikuwa mtu mtakatifu, hapana bali kwa sababu alikuwa kuwani mkuuu . na kunasehemu nyingine inasema wao wamekaa katika viti vya Musa yaani makuani na makasisi, wasikilizeni wasemacho bali matendo yao msiyafuate . Mungu alimtumia Paul aliyekuwa mzambi kuwaokoa maelufu . Kwa hiyo amini unachoamini na usipambane na kuvuluga watu wengine wanavyo amini.
Acha kabisa kujidanganya mkuu, UKRISTO siyo kuamini kila kitu hata kama ni uongo. Ukisoma vizuri kwenye Biblia kuna sehemu imeandikwa hivi;..... "lakini tumekataa mambo ya aibu yaliyositirika, wala hatuenendi kwa hila wala kulichanganya neno la MUNGU na uongo, bali kwa kuidhihirisha iliyo kweli twajionesha kuwa na haki, dhamiri za watu zikishuhudia mbele za MUNGU". 2 WAKORINTHO 4:2

Ni makosa kulichanganya NENO la MUNGU na hadithi za uongo kama lifanyavyo Kanisa Katoliki. Ikiwa neno la MUNGU ni KWELI kwanini Kanisa Katoliki linachanganya na mafundisho ya uongo?

Petro hakuwahi kuishi Roma wala hakuwahi kabisa kuwa Papa wa kwanza wa kanisa katoliki, wala Petro hakufia Roma; sasa ikiwa ndiyo hivyo kwanini kanisa hili katoliki linafundisha uongo??

Mbaya zaidi swala la Petro siyo uongo pekee unaofundishwa na Kanisa Katoliki, bali kuna mambo mengi sana ya uongo na yenye kupotosha yanayofundishwa na kanisa katoliki. Je wewe unaona ni sawa tu Waumini waendelee kupotoshwa??


Ikiwa Kanisa Katoliki kweli ni kanisa la MUNGU ambaye kwake hakuna uongo hata tone moja, Je huoni kama ni muhimu hili kanisa likafundisha mafundisho ya KWELI bila kudanganya???

Mkuu 0890 fahamu kwamba ikiwa kanisa fulani linafundisha mambo ya uongo basi kanisa hilo siyo la MUNGU, maana MUNGU hafungamani na uongo hata kidogo. Kanisa linalofundisha uongo ni kanisa la Shetani Ibilisi maana yeye ndiye "baba" wa uongo.
 
Kila kitu wanachofundisha Wakatoliki ambacho ni cha UWONGO nilishaandika humu. Ni mambo mengi sana, lakini kwa faida ya wengi nitaandika "uzi" kamili unaoonesha uwongo wote wa Kanisa Katoliki. Tega sikio mkuu na siku nikiandika nitaku-tag ili uwe wa kwanza kusoma. Wala usiwe na haraka, nitakuandikia kila kitu.

Usisahau kunitag mkuu,pls


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kwa taarifa yako hata mimi nilikuwa MKATOLIKI na baada yakufundishwa UWONGO, niliamua kuitafuta KWELI. Nilipoijua KWELI nikaona nisikae kimya wacha niwajulishe na wengine ili na wao waijue KWELI. Huwezi kuujua uchafu wa nyumba kama uko nje ya nyumba na hujawahi kuingia ndani.

Kwa taarifa yako Bagatti alihojiwa na akakiri kila kitu ingawa hakuandika kwenye kitabu chake. Kuna watu waliongea na akina Bagatti na wakaamua kwenda Jerusalemu kuutafuta UKWELI na wakauona kwa macho yao. Sasa wewe endelea kuogelea kwenye UWONGO wa Kanisa Katoliki. Hata baadhi ya Mapre wa Kanisa Katoliki wapo Jerusalemu na wanakuambia ni kweli Petro alifia Jerusalemu na kuzikwa huko. Lakini kamwe hawewezi kusimama hadharani na kuongea hivi vitu.
Waliwezaje kuuona kwa macho yao wakati unasema yamefichwa?
Je,una waamini vipi hao watu?
Una ushahidi gani wa kutuaminisha kuwa walichokuwa wakikisema ni cha kweli?

Una dai kwamba kanisa ndio linaficha ukweli wakati huo huo waliokupa ukweli ni member wa hilo kanisa,je una waamini vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Unasema kuwa Perto aliishi roma miaka 24 na kufia huko.
Unasema kuwa kanisa katoliki ndio linafundisha hivyo!
Tuambie ni kitabu gani cha kanisa Katoliki kimeandika mafundisho hayo na mm nikakisome maana mm n Mkatoliki na sijawahi kukutana na hayo mafundisho!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Biblia imeandikwa na Wakatoliki,na kuna hoja naiona hapa ikisema kuwa walioandika biblia waliongozwa na roho mt.
Na kuna hoja inadai kuwa wakatoliki ni waongo.

Je,roho mt huwa anaishi na waongo na kuwaongoza waongo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila kitu wanachofundisha Wakatoliki ambacho ni cha UWONGO nilishaandika humu. Ni mambo mengi sana, lakini kwa faida ya wengi nitaandika "uzi" kamili unaoonesha uwongo wote wa Kanisa Katoliki. Tega sikio mkuu na siku nikiandika nitaku-tag ili uwe wa kwanza kusoma. Wala usiwe na haraka, nitakuandikia kila kitu.
Uhakikishe unaweka na vifungu vya biblia, biblia ambayo imeandika na Wakatoliki unaosema ni waongo.Na sa tunaamini kuwa biblia imeandikwa kwa maongozi ya roho mt.
Na roho mt haishi wala kuwaongoza waongo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sina haja ya kukutajia majina yao sababu hayatakusaidia kitu chochote kile. Wewe kama hata Biblia huiamini, utawaamini watu usiowajua? Biblia yenyewe inakuonesha wazi kabisa kuwa Petro au Kefa hakuwahi kufika Roma, lakini bado unabishana nayo. Bakia hivyo hivyo mkuu.
Lkn biblia si iliandikwa na Wakatoliki?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa taarifa yako hata mimi nilikuwa MKATOLIKI na baada yakufundishwa UWONGO, niliamua kuitafuta KWELI. Nilipoijua KWELI nikaona nisikae kimya wacha niwajulishe na wengine ili na wao waijue KWELI. Huwezi kuujua uchafu wa nyumba kama uko nje ya nyumba na hujawahi kuingia ndani.

Kwa taarifa yako Bagatti alihojiwa na akakiri kila kitu ingawa hakuandika kwenye kitabu chake. Kuna watu waliongea na akina Bagatti na wakaamua kwenda Jerusalemu kuutafuta UKWELI na wakauona kwa macho yao. Sasa wewe endelea kuogelea kwenye UWONGO wa Kanisa Katoliki. Hata baadhi ya Mapre wa Kanisa Katoliki wapo Jerusalemu na wanakuambia ni kweli Petro alifia Jerusalemu na kuzikwa huko. Lakini kamwe hawewezi kusimama hadharani na kuongea hivi vitu.
Bagatti ni mkatoliki au msabati?
Kwanini unaamini nusu na huamini nusu ukatoliki?
 
Uhakikishe unaweka na vifungu vya biblia, biblia ambayo imeandika na Wakatoliki unaosema ni waongo.Na sa tunaamini kuwa biblia imeandikwa kwa maongozi ya roho mt.
Na roho mt haishi wala kuwaongoza waongo

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu hebu amka kutoka kwenye usingizi uliolala, nani kakuambia Biblia iliandikwa na Wakatoliki? Hivi Paulo alikuwa Mkatoliki? Petro alikuwa Mkatoliki? Isaya alikuwa Mkatoliki? Ezekieli alikuwa Mkatoliki? Mathayo alikuwa Mkatoliki? Musa alikuwa Mkatoliki? Yohana alikuwa mkatoliki?????......... Hakuna hata mwandishi mmoja wa Biblia aliyekuwa Mkatoliki, isitoshe wakati Biblia inaandikwa hakukuwa na Kanisa la Katoliki.

Kwa taarifa yako kabla hata ya kuwepo kwa kanisa Katoliki tayari Vitabu vyote vinavyotumiwa kwenye Biblia vilikuwa vinatumiwa na Kanisa La MUNGU lililokuwa Smyrna ambalo lilikuwa likiongozwa na Polycarp ambaye alikuwa ni mwanafunzi wa Yohana yule aliyeandika kitabu cha UFUNUO.


Polycarp na wenzake walifanya canonization ya Biblia tangu karne ya kwanza kabla hata kanisa katoliki halijazaliwa!
 
Back
Top Bottom