Kada ya Engineering, ualimu Tamisemi

Kada ya Engineering, ualimu Tamisemi

Lengo Magufuli hapa itakuwa namna gani atarudisha mkopo amesomesha vijana halafu hawarudishi kwa kisingizio cha kukosa ajira kaamua wahandisi wakale vumbi la chaki awakabe kisawasawa.​

Mshahara hapa ni 716,000 take home itachezea 540,000 lakini fursa naiona kwa wahandisi wa ujenzi maana halimashauri nyingi hazina wahandisi so wakurugenzi wanaweza kuwatumia wahandisi.​

TAMISEMI ni wizara kubwa ina taasisi kibao mfano TARURA, IDARA ZA UJENZI, DMDP nk kwahiyo unaweza omba kama ticha ukifika kwa mkurugenzi tengeneza connection akubakize.​

Ukienda kushangaa huko utaishia kuchomekea mashati ya kung'aa na suruari za vitamba na kulima kilimo cha mbogamboga, kuandaa andalio la somo mpaka ukome.​

Hii ndiyo Tanzania anayoitaka Mkuu wa Nchi. ERB wapo tu kazi kutumbua ada zetu na Hamna wanachokifanya wameshindwa kusimamia weledi wanaangalia pesa tu wamekomaa kuchangisha michango wajenge jengo sijui la maonesho gani.​

Wanatakiwa wajitathimini hawa kazi kukuza vitambi tu na wanapeana ajira tu kwenye board yao hutwahi kusikia wametangaza kazi pale ni kujuana.

Bilashaka lengo la magufuri anataka hawa engineers wakafundishe shule za technical kama ifunda,moshi tech,iyunga n,k
 
Sio kila kitu mnapinga, Technician wanaohitajika hapa ni kwa ajili ya kwenda kufundisha vyuo vya Maendeleo ya wananchi FDC bila shaka
Sina hakika kama viko chini ya tamisemi,kama viko chini yw tamisemi basi sawa
Ila ajira ni kwa ajili shule za msingi na sekondari hivyo hapo wanapelekwa shule ufundi kufundisha masomo ya ufundi
 
mkuu mbona una kichwa kigumu sana,,hii hali ilivyokua ngumu kwetu wahandisi huioni. na nan alikuambia elimu yetu inaweza kumfanya graduate akajiajiri bila kupata uzoefu wa kazi field.

nawajua jamaa zangu wengi tu kwasasa wanauza mitumba wengne wanafanya umachinga..sisi wengne angalau mjini hapa nyumbani tunajiongeza huku na huku siku ziende ila hali ni mbaya.

so ikitokea nafasi ka hiyo ukajitafute why usiombe kwanza..au unataka tukabe.

Bila shaka wewe ndiye mwenye kichwa kigumu zaidi/kilaza!
Ungesoma vyema nilichoandika ukielewe vizuri! Karudie uelewe, au pengine uwezo wako ni mdogo ndio maana umeshindwa kuelewa, na hiyo pengine inaweza kuwa sababu ya wewe kujiita engineer huku pengine ukitafuta ajira na kukosa kwa sababu ya kutokuwa na uwezo kwenye hiyo field!
Kiufupi nimegundua wewe ni engineer uchwara!!
 
Acha siasa! Engineer hawezi kuwa mwalimu? Chuo umefundishwa na nani?? Alafu engeneer level ya diploma kuna technical school nyingi,za kufundisha, vyipo vyuo vya kati mfano Focal development college( FDC) vipo chini ya wizara ya maendeleo ya jamii, vinatoa cheti cha ufundi kama wa veta! Unataka nani akafundishe? Kuitwa engineer na unauza mkaa hiyo ndo sifa?? Au kwenda kutoa ujuzi wako kwa wengine?

Wanaofundisha vyuoni siyo waalimu!
Hao ni wakufunzi!
Unatakiwa kutambua waalimu na wakufunzi wanatofautiana!
 
Duh CCM wameharibu nchi, unajua kuna mambo ukiyatafakari unaweza ukadhani labda sio Tanzania hii, Yani Engeneer akashike chaki, Hii ni haki kweli?
 
Duh CCM wameharibu nchi, unajua kuna mambo ukiyatafakari unaweza ukadhani labda sio Tanzania hii, Yani Engeneer akashike chaki, Hii ni haki kweli?
Pia masomo ambayo unapaswa kufundisha ni ya shule za kiufund au mathematics na physics??
 
Uko sahihi kabisa. Hii siri vijana wengi hawaijui. Hata uwe umesomea urubani, serikali ikitangaza nafasi za kazi ya kufagia na wakataja sifa ulizonazo, basi omba. Ukiajiriwa tu baada ya muda mfupi omba kuhamia kwenye urubani.

Hapa nilipo halmashauri haina engineer hata mmoja, imebidi DED achukue walimu wa Physics wasaidie. Sasa ukipangiwa huku kama Mwl baada ya miezi michache lazima DED atakuhamishia ujenzi na hawa walimu watarudishwa shuleni.
Sasa kwann serikali isitoe ajira ya mainjinia wakati wapo mtaani hawana kazi?

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Acha siasa! Engineer hawezi kuwa mwalimu? Chuo umefundishwa na nani?? Alafu engeneer level ya diploma kuna technical school nyingi,za kufundisha, vyipo vyuo vya kati mfano Focal development college( FDC) vipo chini ya wizara ya maendeleo ya jamii, vinatoa cheti cha ufundi kama wa veta! Unataka nani akafundishe? Kuitwa engineer na unauza mkaa hiyo ndo sifa?? Au kwenda kutoa ujuzi wako kwa wengine?
Anaye fundisha chuo sio mwalimu ni instructor.

Acha upotoshaji.

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
 
Kiukweli Magufuli natimu yake wametudharau sana wahandinsi, nchi hii yaviwanda,Serikali iliyoanzisha viwanda kila mahala kwa kadri wana CCM wanavyodai, miradi ya ujenzi kila mahala unamchukua kijana aliejiandaa kuwa muhandisi unataka akafundishe shule, kwa nini hawasemi na madoctor waombe kufundisha shule, kiukweli Magufuli na timu yako mmetudharau sana wahandisi.
Yaani wametudharirisha vibaya mno serikali hii yaani sisi wahandis tukawe walimu
 
Sasa kwann serikali isitoe ajira ya mainjinia wakati wapo mtaani hawana kazi?

Sent from my SM-A515F using JamiiForums mobile app
Sijui kwanini. Labda wana sababu.

Nilichojaribu kuonesha ni namna engineer au mwana taaluma yoyote anavyoweza kutumia fursa inapojitokeza. Yupo mwenye degree ya sheria aliomba utendaji wa kata (WEO) then baada ya mwaka akaomba kuhamia ofisi ya Sheria ya H/shauri.
 
Wajuzi tupeane elimu hapa, kwenye nafas hzi za ualimu za tamisemi kwenye masomo yakufundishia tuchague masomo ya fani .? Au masomo haya yakufundishia sekondari mfano physics na hesabu?? Naonba kuelewa katika hili wakuu
 
Back
Top Bottom