Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Tatizo la Law School si dogo ambalo ati kila Tom, Dick au Harry anaweza kuwa na ufumbuzi au ushauri.

Kwa sampuli hii:

1. Profesa Cyriacus Binamungu (Mzumbe): anasema kuna shida kwa walimu katika taasisi hiyo (LST).

“Wanafunzi wanaandaliwa vizuri (vyuoni) isipokuwa kutakuwa na shida LST, walimu hawazingatii ufundishaji, wanafikiria mishahara, akipokea hajali mwanafunzi kaelewa au la.”

2. Profesa Costa Mahalu, (VC Saut): anasema ni aibu kwa taasisi hiyo kutokana na matokeo hayo, pia inapaswa ijitafakari.

“Haiwezekani wanaofeli mtihani wa uwakili pale LST hawana ujuzi na maarifa katika masomo yao kutoka vyuo walivyosoma. Hapana! Kuna tatizo na lazima utafutwe ufumbuzi,”

Profesa Mahalu anasema matokeo mabaya yanasababishwa na makundi matatu ya walimu wanaowafundisha wanafunzi hao wa uwakili.

(a) Matatizo ya uwezo,
(b) wanaopenda kuogopwa na wanafunzi,
(c) wale wasiotaka mafanikio ya wengine, ambalo ndiyo lililo hatari zaidi.

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

Profesa Mahalu anashauri kulindwa msingi wa kuanzishwa kwa LST ambao ni kutoa elimu kwa vitendo kutoka kwa majaji, mahakimu na mawakili wanaoshughulika na mashauri kila siku mahakamani.

“Maprofesa waliobobea katika nadharia wasipelekwe kuwafundisha wanafunzi pale LST kwa sababu kufanya hivyo ni kukiuka lengo la msingi la kuanzishwa kwa chuo hicho.”

Kabla ya taasisi hiyo, anasema Mahalu mawakili walipata maarifa kwa miezi tisa kutoka kwa mawakili na mahakimu waliopo kazini.

“Taifa lilipata wanasheria na mawakili nguli, nikiwemo mimi, Jaji mkuu mstaafu, Othman Chande na Waziri Mkuu mstaafu Mizengo Pinda mwaka 1974. Wahadhiri wa LST wajitafakari kwa matokeo haya.”
___________

Watu kama hawa walipaswa kuwamo kwenye tume ya Dr. Ndumbaro.

LST kuna matatizo na walimu yasiyokuwa ya kufumbiwa macho. Fika LST kuutambua ukwasi wa walimu hawa wenye kujiita 'fulani the don.'

Kwa hakika muda wa kuyatanzua makando kando yao ni sasa.

Wameyakoroga wenyewe, hawana budi kuyanywa.

Source:

Profesa Shivji asema tatizo ni mfumo ufaulu mtihani Uanasheria
 
LST kuna matatizo na walimu yasiyokuwa ya kufumbiwa macho. Fika LST kuutambua ukwasi walimu hawa wenye kujiita 'fulani the don.'
Kama utaupuuza ukweli kwamba wanafunzi ndiyo wenye shida basi mleta mada una wivu ama chuki binafsi na walimu wa shule ya sheria.

Wanafunzi wanachangia kufeli kwao kwa 75+%. Muda mwingi wanadanga, wanalewa, wanabet, wanawaza ukahaba, n.k.

Hawawezi kuandika sentensi nzuri za kiswahili na hata kiingereza. Unapata wapi ujasiri wa kuwalaumu walimu pekee?
 
Kama utaupuuza ukweli kwamba wanafunzi ndiyo wenye shida basi mleta mada una wivu ama chuki binafsi na walimu wa shule ya sheria.

Wanafunzi wanachangia kufeli kwao kwa 75+%. Muda mwingi wanadanga, wanalewa, wanabet, wanawaza ukahaba, n.k.

Hawawezi kuandika sentensi nzuri za kiswahili na hata kiingereza. Unapata wapi ujasiri wa kuwalaumu walimu pekee?

Nikurejeshe kwa maoni ya msomi Nguli Prof. Mahalu:
______
Profesa Mahalu anasema matokeo mabaya yanasababishwa na makundi matatu ya walimu wanaowafundisha wanafunzi hao wa uwakili.

(a) Matatizo ya uwezo,
(b) wanaopenda kuogopwa na wanafunzi,
(c) wale wasiotaka mafanikio ya wengine, ambalo ndiyo lililo hatari zaidi.

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

-----------

Kama ukweli huu hauuoni ninadhani wewe unaweza kuwa ni wale watajwa kwenye group (c) hapo. Bila shaka ni wale wenye makasiriko na mafanikio ya wengine.

Wenye makasiriko na mafanikio ya wengine anasema Prof. Mahalu ni wabaya zaidi.

Zingatia: Profesa Mahalu, aliwahi kuwa Dean wa kitivo cha sheria UDSM na VC wa kilichokuwa Chuo Kikuu cha Bagamoyo na sasa hivi ni VC Saut.
 
Mahalu atakuwa anaitaka nafasi ya kuteuliwa kuwa mkuu wa shule ya sheria kama haoni nafasi kubwa ya wanafunzi kuchangia kufeli kwao.
 
Kwa ujumla UDSM ni chuo cha kidikteta na udikteta huu unasababishwa na ukabila uliokithiri.

Kuna kabila hapo UDSM huwa hawafeli hata kama ni kialaza.

Kingine ngono. Kuna digrii nyingi za mabinti ni za ngono.

Unakuta binti anabakizwa kuwa tutorial asistant na GPA kubwa ila kichwani boga. Anabebwabebwa tu..

Hebu kila chuo kinachofundizha sheria kiwe na law school hapohapo chuoni.
 
Wanafunzi waache Janja janja KAMATA Wote hakuna kulegeza kwenye vigezo au ufaulu kamata Wote

Kwa hakika wakamatwe wote wenye janja janja ila si kutokana na walimu hawa:

(a)wenye matatizo ya uwezo,
(b) wanaopenda kuogopwa na wanafunzi,
(c) wale wasiotaka mafanikio ya wengine.

Walimu hao hawapaswi kuwapo katika ufundishaji popote pale.

Wao ni batili kama ulivyo ufundishaji na utahini wao.
 
Kama utaupuuza ukweli kwamba wanafunzi ndiyo wenye shida basi mleta mada una wivu ama chuki binafsi na walimu wa shule ya sheria.

Wanafunzi wanachangia kufeli kwao kwa 75+%. Muda mwingi wanadanga, wanalewa, wanabet, wanawaza ukahaba, n.k.

Hawawezi kuandika sentensi nzuri za kiswahili na hata kiingereza. Unapata wapi ujasiri wa kuwalaumu walimu pekee?
Mkuu umeelewa hoja za Costa Mahalu ?
 
Mahalu atakuwa anaitaka nafasi ya kuteuliwa kuwa mkuu wa shule ya sheria kama haoni nafsi kubwa ya wanafunzi kuchangia kufeli kwao.

Haya mambo siyo size yako.

"Haya mambo siyo size ya Tom, Dick au Harry."

Kwanini una makasiriko hivi na wanafunzi? Kwanini hautaki uchunguzi huru?

Au wewe ni yule kibopa wa pale law school mwenye kujiita "fulani the don?"

Kwani ukwasi wenu si matokeo ya kugawana malipo ya wanafunzi, kulazimisha kuuza vitabu, kuzifanya supp kuwa biashara nk?

Kwani wapi hapa nchini ada yote ya mwaka mzima hulipwa once off and in advance. Hata IST na Feza kuliko jaa wa wenye nazo fees si kwa hivyo.

Sababu za wanafunzi kufeli ni nyingi hata za Prof. Bizimungu, Mahalu nk zimo.

NInakazia: Uchunguzi huru ni muhimu. Kadhia ya Law School Wasomi Nguli wasikilizwe.
 
Sababu za wanafunzi kufeli ni nyingi hata za Prof. Bizimungu, Mahalu nk zimo.
Zipo kwa uchache lkn si kwa kiwango cha kupigiwa kelele kiasi hiki.

Wanafunzi wana msingi mbovu tangu walikotoka kabla ya kuingia law school. Na wakifika law school wako bize na ujinga.
 
Kwa ujumla UDSM ni chuo cha kidikteta na udikteta huu unasababishwa na ukabila uliokithiri.

Kuna kabila hapo UDSM huwa hawafeli hata kama ni kialaza.

Kingine ngono. Kuna digrii nyingi za mabinti ni za ngono.

Unakuta binti anabakizwa kuwa tutorial asistant na GPA kubwa ila kichwani boga. Anabebwabebwa tu..

Hebu kila chuo kinachofundizha sheria kiwe na law school hapohapo chuoni.

UDSM inakujaje hapa mkuu? Kumbuka LST inachukua wanafunzi wa vyuo vikuu vyote wenye sifa.

Angalizo: Dr. Tulia Ackson, Dr. Asha Rose Migiro kukutajia wachache wameanza kama Tutorial Assistants faculty of Law UDSM.

NInakazia wengine kina sisi si vibaya kujikita kwenye u Simba na Yanga.
 
Kwa ujumla UDSM ni chuo cha kidikteta na udikteta huu unasababishwa na ukabila uliokithiri.

Kuna kabila hapo UDSM huwa hawafeli hata kama ni kialaza.

Kingine ngono. Kuna digrii nyingi za mabinti ni za ngono.

Unakuta binti anabakizwa kuwa tutorial asistant na GPA kubwa ila kichwani boga. Anabebwabebwa tu..

Hebu kila chuo kinachofundizha sheria kiwe na law school hapohapo chuoni.
We hujui hata unachoandika,taja hilo kabila unamwogopa nani km siyo chuki na umbea. Mi siamini chuo kikubwa km UDSM kuwe na kabila kina uwezo wa ku-dominate kati ya makabila zaidi ya 120 tena nyakati za leo ambapo makabila yote yameenda shule. Kuhusu mwenye GPA kubwa bado hakuna kitu kichwani huo ni wivu kwa kuwa we ulishindwa kupata GPA nzuri.

GPA inawakilisha wastani wa maksi ulizopata ktk masomo yote uliyasoma na kufanyia mitihani miaka yote uliyosoma chuoni. Mtu hawezi ku-maintain maksi za juu miaka yote bado tumuite kilaza, huo ni uwendwawazimu, we ulitaka watumie kipimo gani? Acha wivu ktk mafanikio ya wenzako we km umeshindwa kupata GPA kubwa waheshimu wenzio sio kuwaponda
 
Zipo kwa uchache lkn si kwa kiwango cha kupigiwa kelele kiasi hiki.

Wanafunzi wana msingi mbovu tangu walikotoka kabla ya kuingia law school. Na wakifika law school wako bize na ujinga.

Kwa maoni yako unaona chache. Wengine tunaona ndiyo zilizo kuu, na ndiyo maana unazisikia kelele hizi.

Kwa nini unadhani maoni yako ndiyo yaliyo sahihi? Nimekupa CV ya Prof. Mahalu Ili japo kukustua. Kwani CV yako inafikia kwa huyo gwiji?

Hapa ni maneno yake, beberu akisema "from the horse's mouth:"

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

Au wewe ni mkomavu kama warusi wa Buza tu?
 
We hujui hata unachoandika,taja hilo kabila unamwogopa nani km siyo chuki na umbea. Mi siamini chuo kikubwa km UDSM kuwe na kabila kina uwezo wa ku-dominate kati ya makabila zaidi ya 120 tena nyakati za leo ambapo makabila yote yameenda shule. Kuhusu mwenye GPA kubwa bado hakuna kitu kichwani huo ni wivu kwa kuwa we ulishindwa kupata GPA nzuri.

GPA inawakilisha wastani wa maksi ulizopata ktk masomo yote uliyasoma na kufanyia mitihani miaka yote uliyosoma chuoni. Mtu hawezi ku-maintain maksi za juu miaka yote bado tumuite kilaza, huo ni uwendwawazimu, we ulitaka watumie kipimo gani? Acha wivu ktk mafanikio ya wenzako we km umeshindwa kupata GPA kubwa waheshimu wenzio sio kuwaponda

Hao ndiyo kina Tom, Dick na Harry sasa kwenye ubora wao.
 
Kwani CV yako inafikia kwa huyo gwiji?
Mkuu kuwa na CV nchi hii hakumfanyi mtu kuepuka kutoa maoni yaliyoathiriwa na njaa.

Unakumbuka maoni ya prof. Shivji, Dr. Mwakyembe na prof. Kabudi wakati wa bunge la katiba?

Prof. Mahalu hawezi kuukwepa mtego huu ktk hili.
 
Nikurejeshe kwa maoni ya msomi Nguli Prof. Mahalu:
______
Profesa Mahalu anasema matokeo mabaya yanasababishwa na makundi matatu ya walimu wanaowafundisha wanafunzi hao wa uwakili.

(a) Matatizo ya uwezo,
(b) wanaopenda kuogopwa na wanafunzi,
(c) wale wasiotaka mafanikio ya wengine, ambalo ndiyo lililo hatari zaidi.

“Hata hapa Saut niliwakuta walimu wa aina hiyo. Tumefanya kazi kubwa kumaliza tatizo hilo,”

-----------

Kama ukweli huu hauuoni ninadhani wewe unaweza kuwa ni wale watajwa kwenye group (c) hapo. Bila shaka ni wale wenye makasiriko na mafanikio ya wengine.

Wenye makasiriko na mafanikio ya wengine anasema Prof. Mahalu ni wabaya zaidi.

Zingatia: Profesa Mahalu, aliwahi kuwa Dean wa kitivo cha sheria UDSM na VC wa kilichokuwa Chuo Kikuu cha Bagamoyo na sasa hivi VC ni Saut.
Sas hyu huyu professor mahalu s amewai kuwa na kashfa ya kuongeza gharama za ofisi ya ubalozi wa Italy ..na kesi kapamban nayo Hadi kuchomokaa ila kusema kweli kuwa wa kili kwa sas Ni dili kubwa mno

Kuna jamaaa namfahamu. Kipindi nasoma olevel yeye alikuwa Aleve fom 5 akiwa six mm Niko fom 5 ,sas baada ya muda chapu kamaliza nakisha kwenda mzumbe namm nikiwa najianda kwenda chuo Cha ija Cha korogwe tanga baadae nikagome kwenda chuo hicho ila mzeee wangu alikuwa na hamu sas mm kuwa wakili au hakimu


Lahaula baada yamiaka Kama mitano nikakutana na yule jamaaa katk eneo fln huko Arusha ambako tulikuwa TUnaenda kucheki kiwanja jamaa dalali akasema jirani yenu huu Ni wakili .bas kdg tu jamaa alitoka na gari ndipo dalali akatumbia kuwa jamaa si yule pale kumbee ndio huyo jmaaa nilisoma nae shule moja sas Ni wakili mkubwa sna huko Arusha anamiliki ma apartment za maana huko Arusha maeneo ya moivaro ..

Uwakili Ni dili Sana na Kaz za dhuluma mno
 
Mkuu kuwa na CV nchi hii hakumfanyi mtu kuepuka kutoa maoni yaliyoathiriwa na njaa.

Unakumbuka maoni ya prof. Shivji, Dr. Mwakyembe na prof. Kabudi wakati wa hunge la katiba?

Prof. Mahalu hawezi kuikwepa mtego huu ktk hili.

Haipo njia nyingine ya kutambua weledi wa mtu isiyoanzia kwenye CV ikafuatiwa na kauli zake na matendo yake.

NIsiache kukwambia Prof Mahalu amemaliza kila kitu kwenye kadhia hii katika namna rahisi na sahihi kwa Kila mtu kuelewa labda asiyetaja.

"Mzizi wa fitina LST uko kwenye makundi 3 ya walimu pale.'

Kumbuka opportunists hu side na establishments. Opportunists wata side na LST ambako ndiko kuliko na rupia.

Kwani gwiji Pascal Mayalla maoni yake kwenye kadhia hii ni gani?
 
Back
Top Bottom