Kadi za michango zimenizidia!!

Kufanya harusi kwa kutegemea pesa za kuchangiwa na watu ni Upumbavu.

Mi nadhani ifike mahali tuelekeze nguvu zetu kuchangia wanaougua na wanaopatwa na shida mbalimbali lakini siyo kuchangishana mipesa kwa ajili ya harusi.
Mkuu unayoyasema ni kweli kabisa mm sibishi
 
Mimi mchango wa sherehe sichangi kabisa,mchango ntakaotoa ni wa mgonjwa au msiba tuu,inakuwaje unataka kufanya sherehe kwa bajeti ya mifuko ya watu?siku nikiwa na sherehe ntafanya kwa bajet Yangu over.
 
Pole DJ.

Waambie tu ukweli kuwa mpunga hautoshi!!
 
Kukomoana kwa viwango vikubwa Na kushtuana ndo sitaki
La kuwekeana viwango ndo linalokera zaidi, haiwezekani we mwenyewe upange bajeti ya kufanya sherehe ya mamilioni kwa kutegemea watu wakuchangie, watu ambao wana majukumu yao binafsi, kusomesha, kuuguza nk sio haki kabisa.

Binafsi, sitakuja nimchangie yeyote yule, labda nimkopeshe. Binafsi Kwanza si mpenzi wa sherehe kabisa, hivyo haitaniathiri, kusaidiana ni ktk majanga sio sherehe, ufanisi wa sherehe ni kujipanga kusherehesha sio kuchangiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…