Kafulila: 2008 SYNOVATE walisema tatizo namba moja la Watanzania ni maji

Mzee Nyerere

JF-Expert Member
Joined
Jun 24, 2024
Posts
219
Reaction score
279


Katika Ukurasa wake wa (X) zamani tweeter Mkurugenzi wa PPP-Cetre Tanzania Bw David Kafulila amesema kuwa utafiti uliofanywa na taasisi ya kitafiti ya Steadman au SYNOVETe mwaka 2008 ulibaini kuwa tatizo namba moja la Watanzania ni maji Safi na Salama.

Kafulila amesema kuwa Rais Samia katika kukabiliana na tatizo hili namba moja la Watanzania kwa wakati amekuwa akitoa pesa nyingi pengine kuliko Marais wote tangu Uhuru wa nchi hii.

Kafulila anasema, kabla ya mwisho wa mwaka wa Fedha wa Kila mwaka na katika miaka mitatu ya Rais Samia bajeti ya maji imetekelezwa kwa zaidi ya asilimia 75 na 92 miezi minne kabla ya wakati uliokusudiwa.

Mkurugenzi huyo pia ananakili baadhi ya miaka ya Fedha huko nyuma kabla ya Rais Samia bajeti ya maji ilitekelezwa kwa chini ya asilimia 40.

Hii ndio tofauti ya Rais Samia na Wengine ndio maana Mzee Kikwete ametamka wazi kuwa Rais Samia katika utekelezaji wa miradi ya maendeleo kampindua.

Hata hivyo takwimu zinaonesha upatikanaji wa Maji vijijini umepanda kutoka 70.1% mpaka 89.6% wakati upatikanaji wa Maji mjini umeongezeka kutoka 85% mpaka 90%.

#Mama Samia hakamatiki

Pia soma: Yasinsta Cornel: Ubadhirifu na Ucheleweshaji wa Miradi ya maji; Tatizo kwa upatikanaji wa maji nchini
 
Safi sana Mheshimiwa David Kafulila kiongozi Mwenye ujasiri na uthubutu wa kueleza ukweli juu ya masuala mbalimbali yaliyofanywa na Rais wetu na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan. Uzuri wa Mheshimiwa Kafulila anatoa na ushahidi kabisa wa kitakwimu.
Your browser is not able to display this video.
Your browser is not able to display this video.
 
Mama Samia anapiga kazi sana hakika mitano inamuhusu tu
 
Cde tuko pamoja sana
 
Huku kwetu maji sio tatizo tatizo pesa ya kulipa bili
 
Maji tatizo bado
 
Najaribu kufikiria kwa sauti namna Jiji kuu la Tanzania linavyopata shida ya maji siku hizi huku tatizo halijulikani halafu Kafulila anakuja na taarifa hii nashangaa. Sijui ni Tanzania gani anaizungumzia.

Vv
 
Maji tatizo bado
Wapi bado tatizo.kila mtanzania anaona na kushuhudia juhudi kubwa sana zilizofanywa na zinazoendelea kuchukuliwa na serikali katika usambazaji wa maji safi na salama.kwa kuanzisha miradi mikubwa ya maji na kuhakikisha maji yanawafikia wananchi mahali walipo.kikubwa ni sisi wananchi kuhakikisha tunatunza miundombinu ya maji kama vile mabomba,matenki,koki za maji n.k.
 
Najaribu kufikiria kwa sauti namna Jiji kuu la Tanzania linavyopata shida ya maji siku hizi huku tatizo halijulikani halafu Kafulila anakuja na taarifa hii nashangaa. Sijui ni Tanzania gani anaizungumzia.

Vv
Ni maeneo gani?
 
Magomeni wewe chawa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…