milele amina
JF-Expert Member
- Aug 16, 2024
- 6,045
- 8,080
Hiyo ni vision ya taifa au ya ccm?Vision ipi tofauti na visio ya Taifa 2050?
Hayo yote anayoongea Yako kwenye Vision ya Nchi ya 2050 hawezi.kija na vision yake na hakuna Nchi ya kuendeshwa na mawazo binafsi ya mtu mmja,haipo na hatutakiwi.kurudi zama za Mwendazake
Kafulila ana ndoto hizo,ni kweli umeme tulionao kibindoni,kwa miaka 5 ijayo hautatosha kabisa ukuzaji viwanda vikubwa.===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila akihojiwa katika Kipindi Cha One on One Cha Wasafi TV amesema Tanzania katika miaka 25 ijayo inatarajia kujenga Uchumi mkubwa karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya Leo.
Kafulila anaendelea kwa kusema kama Africa ya Kusini ya leo Wana Umeme unaofikia Megawatt 60,000 huku sisi tukitarajia kujenga Uchumi marambili ya Uchumi huo wa Africa Kusini leo maana yake lazima tuwe na Umeme unaozidi umeme wa Africa ya Kusini ya leo ambao ni zaidi ya Megawatt 60,000.
Swali tunaloweza kujiuliza kwa pamoja, ni Je, bila kushirikisha mitaji na Ujuzi toka sekta binafsi PPP Tanzania kwa kutumia Kodi na Mikopo pekee tunaweza kufikia kumiliki umeme wa Megawatt zaidi ya 60 ifikapo mwaka 2050 Jibu ni "HAPANA" lazima PPP ichukue nafasi kwenye hili kwa manufaa ya kizazi hiki na manufaa ya kizazi kijacho.
View attachment 3202423
====
Kwa uhalisia wa mambo na endapo bwawa la Nyerere litakamisha uzalishaji tutakuwa na up to ~3,500 MW.Ndio JNHPP pekee tuna 2,100
Kabla tuliokuwa na Megawatt zaidi ya 1,000 bado kule Maragalasi etc
Ya Taifa,nyie punguani mliposhirikishwa kitu Cha maana kwenu mlichoongeaga ni Katiba Mpya 😂 😂Hiyo ni vision ya taifa au ya ccm?
Itakuwa megawatt 5,000Kwa uhalisia wa mambo na endapo bwawa la Nyerere litakamisha uzalishaji tutakuwa na up to ~3,500 MW.
Ni mbobezi wa nini??Katika waongo wabobezi Kafulila yumo
Nipe mahesabu;Itakuwa megawatt 5,000
Sio swala la Mungu kukutupa au hapana Bali matumizi ya akili kwenye Rasilimali zilizopo.Kafulila ana ndoto hizo,ni kweli umeme tulionao kibindoni,kwa miaka 5 ijayo hautatosha kabisa ukuzaji viwanda vikubwa.
Lakini Mungu aja tutupa kwa kutumia rasilimali zetu tuna uwezo wa kufua hata Mega Watt 200,000 na zaidi kwa vyanzo hivi.:-
1.Kufua umeme kwa kujenga mitambo midogo midogo ya nuclear kutokana na utitili wa madini ya uranium yanayopatikana maeneo mbali mbali nchini kwetu.
Serikali ya Uganda inayoongozwa na Museveni imeishatenga eneo mahususi la kujenga mitambo ya kufua umeme wa nuclear.
Mradi huu PPP hatumuhitaji kwa maslahi mapana ya taifa letu.
Bila kumungunya maneno bingwa wa kujenga mitambo salama na bila masharti magumu ni France.
2.Solar power,Wind turbine Power,Geothermal power,Battery Power n.k serikali na taasisi binafsi wanaweza kuzalisha nishati ya kututosheleza sisi na hata majirani zetu kuwaunganisha kwenye grid ya taifa.
Lakini bado tuna machungu ya makampuni binafsi za Richmond, IPTL,Songas.
Ni bora kwanza kuunda sheria,au kanuni zenye kumlinda mtumiaji asinyonywe kama huku nyuma.
Mwisho Kafulila tumia muda huu kuishawishi serikali kujenga uwezo wa wananchi waweze kusimamia na kumiliki miradi mikubwa mikubwa.
Installed capacity ya kabla ya bwawa ilikuwa megawatt 2,000 plus kutoka vyanzo vyote.Nipe mahesabu;
1. Nyerere 2115
2.
3
4
5
6
Richmond, Songas, IPTL kwa ufupi ni aibu kubwa,just to refresh your memory.Sio swala la Mungu kukutupa au hapana Bali matumizi ya akili kwenye Rasilimali zilizopo.
Tanzania haijawahi kuwa na ushamba wa vyanzo vya Nishati hata siku Moja Wala watu wa kutekeleza hayo.
As we speak miradi kadhaa ya vyanzo vipya inaendelezwa na mingine Iko kwenye hatua za maandalizi.
Akikuelewa unitag, mkuu!Jamaa ana VISION sijui kama utanielewa hapa
Hata Zambia, Mozambique,Zimbabwe wote wanazalisha megawatt nyingi kushinda Tanzania,Kenya nk achilia mbali South Africa.Richmond, Songas, IPTL kwa ufupi ni aibu kubwa,just to refresh your memory.
Miradi mingine inayoendelea ni midogo sana .Mtoa hoja alisema unatoa 4,000 MW,reference to SA anazalisha by today 60,000 MW.na akasema by 2050 tumejipanga kuwa na uchumi mkubwa kuliko SA ya leo inayozalisha 60,000 MW.
Kwa lugha nyepesi to move from 4000 to above 60,000 inataka akili ya ziada.
Kusema tu miradi mingine in progress bila angalau ina capacity gani hukajibu swali la mleta hoja.
Jambo la muhimu ni usimamizi wa miradi ya umeme kama serikali ikiamua kujenga miradi hii bila kushirikiana na sekta binafsi. Ila kama kuna uwezekano wa kutafuta muwekezaji kwenye suala la umeme basi iwe kampuni kutoka nchi ambayo Tanzania ina mahusiano mazuri. Sekta ya umeme ni nyeti sana na huenda ikaleta changamoto endapo nchi ngeni ikiamua kuiwekea Tanzania vizuizi vya kiuchumi kwasababu ya mahusiano yasiyo imara===
Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Ubia nchini PPPC Bwana David Kafulila akihojiwa katika Kipindi Cha One on One Cha Wasafi TV amesema Tanzania katika miaka 25 ijayo inatarajia kujenga Uchumi mkubwa karibu mara mbili ya Uchumi wote wa Africa ya Kusini ya Leo.
Kafulila anaendelea kwa kusema kama Africa ya Kusini ya leo Wana Umeme unaofikia Megawatt 60,000 huku sisi tukitarajia kujenga Uchumi marambili ya Uchumi huo wa Africa Kusini leo maana yake lazima tuwe na Umeme unaozidi umeme wa Africa ya Kusini ya leo ambao ni zaidi ya Megawatt 60,000.
Swali tunaloweza kujiuliza kwa pamoja, ni Je, bila kushirikisha mitaji na Ujuzi toka sekta binafsi PPP Tanzania kwa kutumia Kodi na Mikopo pekee tunaweza kufikia kumiliki umeme wa Megawatt zaidi ya 60 ifikapo mwaka 2050 Jibu ni "HAPANA" lazima PPP ichukue nafasi kwenye hili kwa manufaa ya kizazi hiki na manufaa ya kizazi kijacho.
View attachment 3202423
====
Nani huyo?Ni yule mbunge machachari wakati wa Dr. Silaa. Alichangamsha sana bunge.
Nani huyo?Analeta siasa kwenye mambo ya kitaalam.
Umeongea vema mkuuJambo la muhimu ni usimamizi wa miradi ya umeme kama serikali ikiamua kujenga miradi hii bila kushirikiana na sekta binafsi. Ila kama kuna uwezekano wa kutafuta muwekezaji kwenye suala la umeme basi iwe kampuni kutoka nchi ambayo Tanzania ina mahusiano mazuri. Sekta ya umeme ni nyeti sana na huenda ikaleta changamoto endapo nchi ngeni ikiamua kuiwekea Tanzania vizuizi vya kiuchumi kwasababu ya mahusiano yasiyo imara