Kafulila: Milango iko wazi kwa mtu au kikundi kununua vichwa na mabehewa ya SGR kisha kuyaendesha kwa miundombinu ya serikali kwa sharti la ubia

Mkuu,

Nadhani mambo ya Serikali ni mambo ya wengi

Nadhani tuamini anachotuambia kwani hata hivyo hana muda mrefu kwenye hii nafasi.

Rais Samia ameshamiria kuinua uchumi wa Watanzania wote.

#2025 MAMA MITANO TENA
Serikali ina uhakika gani sera ya PPP itakuwa na matokeo mazuri? uko wapi mradi wa majaribio wa PPP? Jana ameongelea DART leo SGR kesho ATCL..mtu wa aina hii unaweza kuamini anachokisema? Ukimwamini utakuwa mjinga zaidi ya ujinga alio nao yeye!
 
Bakhresa atanunua tu,siku nimekuta treni inavuta behewa zaidi ya kumi za Azam pekee.
Balhresa Hana shida Uganda Railway Yuko kule na ndio Mwekezaji mkubwa ana uzoefu na mkurigenzi WA TRC alimtaja kuwa NI mmojawapo WA waliosema wako wako tayari wengi Tu wataweza Kwa ajili ya kusafirisha mizigo Yao wakiwemo Akina Dangote Cement,kampuni kubwa za mafuta NK
Kwao sio kitu kikubwa Sana kumiliki treni binafsi

Pia Kadogosa alimtaja Mo Dewji kuwa kaomba kuleta treni luxury ya utalii
 
Ni ngumu sana kuiua SGR amini hii kitu nakwambia

Kwani what does it take? Sio kuiharibu. Ni kuifanya isiwe preferred. Kwani sasa hivi mwendokasi si ni usafiri wanapanda watu wasio na option nyingine?? Nani anaeafford bolt au gari yake mwenyewe anapanda mwendokasi??
 
Naangalia utekelezaji wake maana wanaiona hiyo SGR kama barabara ambayo magari yanaweza kupishana kirahisi.
Reli inatakiwa kuwa busy kama barabara

Haiwezekani kuna maeneo ukiona treni ni kila baada ya siku mbili au Tatu au baada ya masaa 10 kibiashara ya treni hailipi Sana inatakiwa walau kila masaaa mawili au moja Tu kuna treni unaiona
 
Reli inatakiwa kuwa busy kama barabara

Haiwezekani kuna maeneo ukiona treni ni kila baada ya siku mbili au Tatu au baada ya masaa 10 kibiashara ya treni hailipi Sana inatakiwa walau kila masaaa mawili au moja Tu kuna treni unaiona
Kama zimejengwa line mbili mwanzo mwisho sina pingamizi.
 
Watanganyika baada ya kukopa matrilioni kujenga SGR sasa tunatayarishwa kisaikolojoa kuibiwa kupitia hocho kinachoitwa PPP. Kwa nini tusiendeshe welnyewe kama tumeweza kujenga tunashindwaje kuendesha?

Kama wao serikalini hawawezi watangaze nafasi za kazi wazalendo tuajiriwe tuuendeshe. Afadhali Angesema waatafuta menejimenti toka nje iliituendeshee SGR kuliko hicho kinachoitwa ubia.

Kwanza mtanganyika gani ataruhusiwa kupewa huo ubia? Majina tayari ya huyo mbia wanayo mfukoni sasa wanazuga tu.


Moja ya nafasi zinazotakiwa kufutwa serikLini ni hii ya Kafulila na hicho kinachoitwa ppp.

Njia zote kuu za uchumi zilipaswa kumilikiwa na umma tu na pale ambapo tuko dhaifu tukodishe competent manage.ment tuwaalipe mshahara tu lakini faida iwe ya kwetu..

Ingekuwa nchii hii mgombea binafsi anaruhusiwa ningegombea ubunge ili nikaongeze nguvu na wazalendo wengine kupigania mali za Tanganyika zisiendelee kuporwa kwa mgongo wa ubia au uwekezaji.

Tuamke kupigania mgombea binafsi ili kuondoka a na kuendelea kuwa mateka.
 
Wao wenzake walioongea kabla yake ni Wakurugenzi wa Ubia?
 
Hii reli bado sana kuingia kwenye mfumo huo wa soko jambazi Rostam azizi na genge lake la wahuni na raia feki wanatolea macho huu mradi ili wautie mifukoni mwao kama walivyo fanya kwenye gesi na mbuga za wanyama nk
 
Huu uzi ngoja nimtag mwanangu
MamaSamia2025
Unamsikia kafulila anataka watanzania wakawekeze hapo 😄
Au sisi ndiyo mwisho wetu viwanda vya pombe,juice unga soda nk

Ova
Ubia na serikali bado hautakuwa na tija. UDART hata ile UDA ilikuwa ni ubia lakini matokeo yake kila mtu anajua. Serikali ingetengeneza tu miundombinu na kuwaachia watu waweke treni zao kama yenyewe haiwezi kuendesha.
 
Serikali ina uhakika gani sera ya PPP itakuwa na matokeo mazuri? uko wapi mradi wa majaribio wa PPP? Jana ameongelea DART leo SGR kesho ATCL..mtu wa aina hii unaweza kuamini anachokisema? Ukimwamini utakuwa mjinga zaidi ya ujinga alio nao yeye!
DART mchakato unaendelea kama walivyokwambia,SGR ndio milango imefunguliwa hapo tatizo ni wapi?
 
Tatizo letu uendeshaji
Ubia na serikali bado hautakuwa na tija. UDART hata ile UDA ilikuwa ni ubia lakini matokeo yake kila mtu anajua. Serikali ingetengeneza tu miundombinu na kuwaachia watu waweke treni zao kama yenyewe haiwezi kuendesha.
 
Mchechu na ndie msimamizi mkuu wa uwekezaji anasema serikali itakopa kuweka mabasi barabarani hayo mabasi serikali itakopa Kwa niaba ya Mwekezaji au?

Uongo hauna maisha ajibu hilo
Mkuu wa uwekezaji ndio nini?
 
Wahenga wanasema "Kuchamba kwingi mwishowe utatoka na kinyesi".

Hebu tuipe muda hii SGR iwe stable kwanza tuache huku kuchambachamba, angalau tufanye 5yrs with close competent supervision
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…