Kafulila: Milango iko wazi kwa mtu au kikundi kununua vichwa na mabehewa ya SGR kisha kuyaendesha kwa miundombinu ya serikali kwa sharti la ubia

Kafulila: Milango iko wazi kwa mtu au kikundi kununua vichwa na mabehewa ya SGR kisha kuyaendesha kwa miundombinu ya serikali kwa sharti la ubia

Kila jambo likishafanyiwa majaribio maeneo mengi kinatengenezwa Standard Unit, PPP sio jambo geni hata hapa Tanzania kwa mfano SONGAS ni mradi wa PPP sijui kama unafahamu hili
Sina hakika kiwango cha uelewa ulicho nacho km kinaweza kupambanua tofauti ya mambo zaid ya mawili..nimekupa mifano biashara ya Almasi kwa mfano kwa nini Botswana inafanya vzr Tanzania haifanyi vzr..nani anaweka hizo standard unit, kwenye maeneo gani? Economic Parameters haziko sawa kwa nchi na nchi, unawekaje standard unit..maelezo yako ni ya jumla jumla tu, wewe umewahi sikia serikali hata kusema sekta zenye potential ya PPP ikizitaja? unadhani mambo ya gas ni sawa na biashara ya DART? ukifanikiwa PPP biashara ya gas then ni principle utafanikiwa PPP kwenye usafirishaji..ndio hivyo? Uonavyo wewe mambo hayo mawili yanalingana?
 
===
Mkurugenzi wa Ubia nchi Bwana David Kafulila ameiambia ARIDHIO ya TBC kuwa Sasa ni rasmi mtu au kikundi chochote chenye Uwezo na nia ya kununua na kuendesha vichwa na treni za SGR wanakaribishwa kufanya hivyo Kwa sharti la Ubia na Serikali ya Jamhuri ya Muungano ya Tanzania chini ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Kafulila anasema kama ilivyo kwa miundombinu ya usafiri na usafirishaji ya Serikalí akitolea mfano wa barabara kuna watu wamenunua Mabasi na wanayaendesha na Serikali inapata kodi lakini kubwa ni Wananchi kupata huduma Bora huduma nzuri na kwa wakati ndivyo itakavyokuwa kwa SGR huku akitolea mfano wa mradi mkubwa kati ya DART na Mbia ambao kwa kiwango kikubwa uko tayari na mabasi zaidi 170 yanaletwa kwa kuanzia.

Kafulila anasema Serikali inafanya haya ili kuchachusha Uchumi wa nchi ( economic stimulus ) ambayo ndio hasa sera za Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan na kwa sera hizi ndio zinaifanya Tanzania kuendelea kusalia kileleni kwenye nchi zote za maziwa makuu.

View attachment 3057496
Watakuwepo waliotumia nauli na posho za serikali kupiga oda za injini na mabehewa kwani baadhi waliporudi walisikika wakitoa mchongo huo, sasa nimeelewa kwanini wanataka majina yao yaandikwe.
 
Sina hakika kiwango cha uelewa ulicho nacho km kinaweza kupambanua tofauti ya mambo zaid ya mawili..nimekupa mifano biashara ya Almasi kwa mfano kwa nini Botswana inafanya vzr Tanzania haifanyi vzr..nani anaweka hizo standard unit, kwenye maeneo gani? Economic Parameters haziko sawa kwa nchi na nchi, unawekaje standard unit..maelezo yako ni ya jumla jumla tu, wewe umewahi sikia serikali hata kusema sekta zenye potential ya PPP ikizitaja? unadhani mambo ya gas ni sawa na biashara ya DART? ukifanikiwa PPP biashara ya gas then ni principle utafanikiwa PPP kwenye usafirishaji..ndio hivyo? Uonavyo wewe mambo hayo mawili yanalingana?
Swala la uelewa wangu halina maana zaidi ya Majibu ya hoja zako,

1. Unamaanisha Tanzania ilipoamua kuanzia hii Sheria ya PPP hawakufanya research?

2. miradi mikubwa kama hiyo ya SONGAS ya PPP hata kama gas unafikiri terms of agreement zinatofautia ?

3. Nadhani utambue tu kuwa hii nchi ni kubwa kuliko Mimi na wewe na inaweledi wengi kuliko Mimi na wewe,

Then, truest the process.
 
Swala la uelewa wangu halina maana zaidi ya Majibu ya hoja zako,

1. Unamaanisha Tanzania ilipoamua kuanzia hii Sheria ya PPP hawakufanya research?

2. miradi mikubwa kama hiyo ya SONGAS ya PPP hata kama gas unafikiri terms of agreement zinatofautia ?

3. Nadhani utambue tu kuwa hii nchi ni kubwa kuliko Mimi na wewe na inaweledi wengi kuliko Mimi na wewe,

Then, truest the process.
Ukubwa wa nchi na wingi wa weledi unaousema kungekuwa na failures zote hizo almost ktk kila sekta..wapi serikali inafanya vzr? Taja..kilimo? Mifugo? Uvuvi je? wapi..elimu? miaka zaidi ya 60 tulioanza nao baada ya kupata uhuru..unajua wao walipo? Malaysia, Singapore, South Korea..hata Kenya, Ghana..nk mnadangayana serikalini kuna wenye uwezo wa kubuni na kusimamia, tungekuwa hapa? Kafulila ndiyo think tank ya serikali..r you serious!
Maswali yote nimekuuliza hujajibu hata moja..
1. Taja PPP pilot project yoyote iliyopo kwa sasa..
2. Kuna ulazima gani ku-invite PPP pasina kuwa na mradi wa majaribio..
3. Kuna haraka gani kufanya PPP kwa sasa..
4. Kuna tatizo gani Botswana Almas zao zinawapa faida hapa Tanzania ni tofauti..
5. Kuna nini zaid kilichopo Kenya kufanya uchumi wao uwe imara zaid ya Tanzania..
Waulize hao weledi unaowasema tusikie..
Kuna mentality ya hovyo ndani ya serikali kudhani kuna monopoly ya brain na creativity..which s very wrong! Hata Rais Samia mara kadhaa amesema..inaonekana mambo mengi yanayosemwa nje ya serikali ni bora zaidi ya yanayofanyika au kutoka ndani ya serikali..which s true!
 
Katika jambo lolote ni vema kufanya majaribio kupima kiwango cha matokeo..mazuri, wastani, mabaya..hakuna mradi wowote wa PPP hadi sasa ambao umejaribiwa au uko kwenye majaribio..sielewi kwa nini huyu mtu kila mara anarudia kitu kile kile, anabadilishabadilisha maneno, mara..kuchachusha sijui kuvutia..anza kwanza huo wa DART kwa majaribio kupima sera ya PPP inafaa au haifai au wapi parekebishwe kabla ya hii mingine..ana matatizo gani huyu??
Kuna hii PPP ya Mwendokasi, tuone itakavyokuwa.
 
Katika jambo lolote ni vema kufanya majaribio kupima kiwango cha matokeo..mazuri, wastani, mabaya..hakuna mradi wowote wa PPP hadi sasa ambao umejaribiwa au uko kwenye majaribio..sielewi kwa nini huyu mtu kila mara anarudia kitu kile kile, anabadilishabadilisha maneno, mara..kuchachusha sijui kuvutia..anza kwanza huo wa DART kwa majaribio kupima sera ya PPP inafaa au haifai au wapi parekebishwe kabla ya hii mingine..ana matatizo gani huyu??
Huna chochote unachojua, Simply hujitambui
 
Bahkhesa kawekeza treni uganda Kwa ajili ya mizigo yake, treni luxury yà kitalii inayosimama kila eneo na kushusha watalii watalii maeneo ya vivutio vya utalii iwasubiri hata masaa manne kuendelea na safari au kigeuza Mo Dewji ndio kaomba kuendesha hiyo treni ya kitalii

Watalii waweza ishia hata ubungo tu au pugu au mlimba au morogoro na wakageuza muda wao wanataka wenyewe kuanzia muda wa kuondoka au kurudi sio Kwa ratiba ya TRC tu kuona mandhari au wao wakijipangia wenyewe sisi tunataka kuondoka muda huu hatutaki ratiba ya TRC
Ni sawa tu na kukodi gari ya tours au taxi ikupeleke utakako Kwa muda wako
Bakhressa kawekeza treni Uganda kwa ajili ya mizigo yake? Kawekeza au ni mteja?
Namaanisha anatumia treni kusafirisha mizigo yake?, mwekezaji yeye anafanya operations. Kuna kitu unachanganya maana ya kuwekeza na kuwa mteja, mfano mm ni natumia bandari ya dar kujngiza mizigo yangu hiyo haimaanishi mm ni mwekezaji wa bandari
Hata hivyo shirika la reli Uganda halina mwekezaji.

Hiyo treni ya utalii nadhani jiridhishe tena na hiyo taarifa, au naomba uniwekee hiyo taarifa nione. Maana SGR ni njia moja tu haiwezi treni hiyo unayosema kusimama hata masaa hayo manne kusubiri mtalii aliyeshuka kufanya utalii
 
Bakhressa kawekeza treni Uganda kwa ajili ya mizigo yake? Kawekeza au ni mteja?
Namaanisha anatumia treni kusafirisha mizigo yake?, mwekezaji yeye anafanya operations. Kuna kitu unachanganya maana ya kuwekeza na kuwa mteja, mfano mm ni natumia bandari ya dar kujngiza mizigo yangu hiyo haimaanishi mm ni mwekezaji wa bandari
Hata hivyo shirika la reli Uganda halina mwekezaji.

Hiyo treni ya utalii nadhani jiridhishe tena na hiyo taarifa, au naomba uniwekee hiyo taarifa nione. Maana SGR ni njia moja tu haiwezi treni hiyo unayosema kusimama hata masaa hayo manne kusubiri mtalii aliyeshuka kufanya utalii
Bakresa ni mteja sio mwekezaji Uganda, nadhani ni option nzuri Bakresa kubakia kuwa mteja tu
 
Back
Top Bottom