CM 1774858
JF-Expert Member
- May 29, 2021
- 5,621
- 5,029
Kwa unyenyekevu sana naomba kupitia tweet hii ya Mhe David Zacharia Kafulila.
Nawaomba mnaoshangaa Mhe Rais Dkt Samia Suluhu kukopa sana niwaombe pia kupitia tweet hii mshangae pia namna Rais Samia anavyokuza Uchumi kwa kiwango ambocho hakijawahi kushuhudiwa kwa miaka mingi.
Hebu nisaidieni ni Rais gani wa Tanzania tangu tupate Uhuru alikuza Uchumi kwa US$ 18bilioni ndani ya miaka Mitatu kama alivyofanya Rais Samia l eo?
Kama kweli kuna jambo mnaweza kumlalamikia Rais Samia kamwe haliwezi kuwa ni jambo la Ukopaji na ukuzaji wa Uchumi Tanzania.
Pia soma Deni La Taifa; Nyerere, Mkapa, Mwinyi, Kikwete na Magufuli kwa pamoja walikopa Trillioni 56.5. Samia kwa miaka 3 amekopa Trillioni 42