Kafulila: Serikali inakopa T-bills kwa 5% wakati Msumbiji 17%, Kenya 16%, Malawi 16%, Zambia 10%, Namibia 9%, Uganda 9%, SA 8%. Uelekeo wetu ni sahihi

Sasa unataka watembee kwa miguu?
 
Mkuu Dunia yote inanuka madeni lazima na sisi tukope ili kuendelea
 
Kachukue taarifa za BOT mkuu hili liko hivyo tunakopa kwa 5% toka kwa watu binafsi na mashika mbalimbali
Mkuu angalia usije ukakurupuka wenye akili wakakuona upstairs una makamasi kama ya huyo tumbiri anayetafuta sifa za kisiasa.
BOT inapo issue T-bill kwa umma katika riba kubwa au ndogo inategemeana na lengo la kiuchumi ambalo Serikali inataka kulifanikisha.hapo issue sio riba kubwa au ndogo inategemeana na jambo la kiuchumi lililopelekea Serikali ku offer hizo hati fungani.
Kenya anaweza offer 16% lakini lengo Lake ni ku curb inflation,Tanzania unaweza ku offer 5% but lengo lake ni kupata pesa kupeleka kwenye uchaguzi,Namibia anaweza ku offer 9% a lengo lake anataka kupata pesa apeleke kwenye kujenga mradi.
 
Nadhani hoja ni rates Wala sio matumizi, Kumbuka unapokopa kwa 17% anayeumia ni Mwananchi,

Unadhani Mwananchi anauelipa riba ya 17% maumivu yake ni sawa na yule anayelipa riba 5%?
 
mbona mnamtetea sana huyo mtu ila hali halisi inajionyesha mtaani halafu tuna uhakika gani kama 5% kweli au ndio zile habari za kuambizana tuko uchumi wa kati.....

ukiona mtu anatetewa sana kuna mawili uwezo mdogo au watetezi wana kafungu kao
Mtaani kwako kukoje kulinganisha na lini? Leta majibu
 
ficha ujinga saa hizi walipo wana magari mazuri tu sasa hayo mapya ya nini labda na hiyo hela iingeweza fanya mambo mangapi yanayogusa moja kwa moja mwananchi?
Magari hayo yalinunuliwa na Kikwete miaka 10 iliyopita yamechoka naamini
 
Kukopa na kujenga miradi ndio maisha ya Dunia mkuu wangu, It is inevitable
 
Hebu chukua hesabu rahisi si Ina maana kama nchi hizi zikiuza hati fungani kwa mtu wa ndani mathalani" tutumie Euro"1000 zikiiva Tanzania itarejedha 1000+(1000x5%)=€1,050,Kenya=1,160,SA=1,
080,Msumbiji=1,170,Malawi=1,160,Zambia=1,100,Namibia=1,090.Sasa kama hizi hesabu ni sawa ni wapi wakopeshaji wa ndani wanafaidi!na tafsiri yake ni nini.
 
Hoja hapa ni rahisi Mkuu,

Serikali inaangalia unafuu kwa wananchi walio wengi ambao ni masikini na walala hoi.

Wanaonunua hizi bonds ni taasisi kubwa au Matajiri wakubwa,

Sasa huwezi kunufaisha Matajiri ukawaumiza walala hoi,

Ndio maana Kafulila anamsifu Mama ni Kwa dhana kama hizi.
 
Sisi tunawapa na rasilimari pori,na miradi itakayofanyika wao wanapewa kipaombele,huwezi pewa kitu if there is no return of investment hakuna hio formula duniani
 

Ujinga kabisa!! Kwa ujinga kama huu, naye Kafulila anajiona ni muelewa wa masuala ya uchumi!!

Nani alikuambia kuwa serikali kukopa treasury bills kwa riba ndogo kunaashiria uchumi mzuri?

Kwanza kiuhalisia ni kuwa hizo nchi ambazo serikali inawakopa wananchi wake kwa treasury bills zenye riba kubwa, zinawanufaisha zaidi wananchi wao kuliko wananchi wa Tanzania wanaoikopesha Serikali kwa riba ndogo zaidi.

Lakini jambo jingine, hizo treasury bills za Tanzania ni za muda gani, na hizo za nchi nyingine ni za muda gani? Mnaweka tu sweeping statements kwa mambo msiyoyajua sawasawa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…