Kafulila: Serikali inakopa T-bills kwa 5% wakati Msumbiji 17%, Kenya 16%, Malawi 16%, Zambia 10%, Namibia 9%, Uganda 9%, SA 8%. Uelekeo wetu ni sahihi

Sisi tunawapa na rasilimari pori,na miradi itakayofanyika wao wanapewa kipaombele,huwezi pewa kitu if there is no return of investment hakuna hio formula duniani
T-bonds hata wewe unaweza ukakopa tu mkuu wangu
 
Kumbuka T-bills ni mikópo mkuu,

Sasa kama serikali itakopa Kwa riba kubwa Pesa toka BAKRESA halafu wewe ukaja kumlipa hiyo riba Bakresa unadhani ni maana ya hilo?
 
Nimeshasema kuwa Mheshimiwa Kafulila ni hazina kwa Taifa letu .anawaumbua na kuwapa uelewa mkubwa sana wananchi.ndio maana jana niliandika humu jukwaani kuwa Kafulila ni Mwiba mkali sana kwa CHADEMA.kwa kuwa hoja zake ni nzito na zenye kuambatana na takwimu safi kabisa. Sasa waambie CHADEMA waje wapinge hapa kwa hoja na takwimu.watakachoweza ni kutukana matusi.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]2mbili Yuko hivi tu hata kabla ya Mchange na Zuhura Yunus,

Ni mtu wa fact tu, Ukifura pata maji kidogo tuendelee

Hana facts zozote ni mtu wa kuokoteza vitaarifa bila ya kuwa na uwezo wa kuchambua kitaalam.

Sidhani kama anaelewa hata hiyo business ya treasury bills and bonds inavyofanya kazi. Treasury bills ni mnada. Kunapokuwa na opportunities chache za uwekezaji au faida ndogo sana ukiweka pesa yako bank, wengi wenye hela mnaamua kuikopesha Serikali ambapo ni mkopo mnaipa serikali kwa vipindi vifupi vifupi kwa riba inayotegemea mnada unavyoamua.

Kunapokuwa na wengi wanaotaka kuikopesha Serikali, riba inashuka. Hivyo kwa Tanzania kuwa na riba ndogo kwenye treasury bills kunaashiria fursa chache za uwekezaji au mazingira mabaya ya uwekezaji, na hivyo mtu anaona aheri aikopeshe Serikali yenyewe ili kuepuka usumbufu unaosababishwa na Serikali yenyewe kwenye uwekezaji. Na kwa kuwa mpo wengi, riba inashuka. Kwenye biashara ya treasury bills, hakuna TRA, OSHA, TBS wala tozo.

Hizo nchi zenye riba kubwa ina maana wenye hela wanaona wana uwezo wa kutengeneza faida kubwa zaidi kwa kuwekeza maeneo mengine kuliko faida wanayoweza kuipata kwa kuikopesha Serikali. Hivyo wachache walioamua kuikopesha serikali, wanaikopesha kwa riba kubwa.
 
mbona mnamtetea sana huyo mtu ila hali halisi inajionyesha mtaani halafu tuna uhakika gani kama 5% kweli au ndio zile habari za kuambizana tuko uchumi wa kati.....

ukiona mtu anatetewa sana kuna mawili uwezo mdogo au watetezi wana kafungu kao
Acha ngonjera hapa .hoja hujibiwa kwa hoja .kama una hoja zenye ushahidi basi mpinge na kumkosoa Mheshimiwa Kafulila kwa takwimu na siyo maneno maneno
 
Kuna kitu hujakifahamu vizuri mkuu,

Mwisho wa Siku deni litalipwa na Wananchi,

Unadhani mwananchi atakayerejesha 17% na huyu wa 5% nani anafaida,?

Watu wanawekeza kwenye 5% ndio Maana zinauzwa.
 
Ufafanuzi mzuri wenye akili ndani yake .
 
 
Kafulila akifanya hivi Watanzania wote wakapata taarifa hizi maswali mengi yatakwisha
Taarifa zinatoka sana tuu sema amekuwa popular kama Makonda.

Kuna watu wanajua Mkaonda ndio amekuwa anatatua kero za watu kisa branding wakati Mimi nawajua ma RC kibao tuu kabla ya Makonda na WA kwanza alikuwa Makalla akiwa Dar.
 
Kwanza Ukiwa mbumbumbu wa Uchumi lazima ushangae.

Ila Iko hivi Ili uendeshe uchumi kukopa na kukopesha ni lazima ,Ili uchumi ukue kukopa na kukopesha ni lazima.

Kiufupi kukopa na kukopesha ni economic tool,wachumi wanajua how economic regulation is dome.

Mwisho Hakuna Nchi ambayo haikopp hapa Duniani,haipo hata hao wanaotoa mikopo hukopa pia.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…