Kafulila: Tanzania kwa mara ya kwanza tunajenga barabara za kisiasa za kulipia 150km kutoka Kibaha Pwani-Morogoro bila Fedha ya Serikali

Ni nadra sana kwa viongozi wa juu wa Serikali hii kutoa Majibu namna hii kwa wananchi,
Nampongeza Kafulila na viongozi wengine waingi utaratibu huu wa kutoa ufafanuzi
 
Kwani sisi hatuna hiyo TZS2T?
 
Hii kitu ipo sana huko Ulaya na Asia mfano ni Chine,
Tumechelewa sana.
Unahakika hizo barabara China zimejengwa na watu binafsi, na siyo serikali? Toa mfano mmoja tu wa barabara za namna hiyo unatosha.

Sasa angalia hapa tunavyopigwa na hawa akina Kafulila. Gharama ya ujenzi huo inatengenezwa kuwa kubwa kwa maksudi, ili huyo wanayempa ulaji huo, na yeye atupige zaidi na kwa muda mrefu sana. Ndiyo maana kawataja watoto, anajuwa mwekezaji huyo atakamua hadi kizazi hiki kilichopo leo kiwe kimekwisha kabisa!
Hiyo ni hela kiasi gani atakachokusanya hapa!
 
Tupambaneni tunaweza
Serikali ya huyu mama hawataki kabisa kusikia lugha ya aina hiyo unayotumia wewe.
Mungu atuonee huruma, serikali ya aina hii tukiendelea nayo miaka mingine zaidi ya 2025, tuakuwa watumwa.
Kiongozi huyu anaua kabisa uthubutu wetu wa kujifanyia baadhi ya mambo yetu wenyewe. Kila kitu anataka kufanyiwa tu, sijui alilelewa namna gani huyu.
Haya ni matokeo ya kulelewa kama yai vile, hujiamini kwa chochote, hata kupanda misitu tu, nchi yetu ipendeze, inalazimu tuwalete watu toka jangwani, kusikokuwa na misitu, waje hapa kututumia sisi kufanya kazi ambayo tuna uwezo nayo.
 
Wewe unatakaje mkuu mbona kama unalalamika sana?
 
Ni ngumu, hii kazi inafanywa na watu wengi sio rahisi kufanya huo uhuni msikilize Vizuri Kafulila
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…