Kagame awatuhumu SADC na Ramaphosa kuwaunga mkono Congo. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama SADC ni Rais Samia!

Kagame awatuhumu SADC na Ramaphosa kuwaunga mkono Congo. Mwenyekiti wa Kamati ya Usalama SADC ni Rais Samia!

Nimekupa mfano tu....,kama Congo wananunua vitu minor kama mkaa..,utawauzia vitu vingapi vikubwa unavyozalisha? Kusipokuwa na wananunuaje?
Umesema kwa nini hatuingili mgogoro wa Somalia....ni jambo lisilo na uwiano na maelezo yangu kuhusu DRC....kwa sababu nilisema upande wa mashariki ya Congo ,kutokana na kijiografia watatarajiwa kuitumia zaidi Dar port kwa export jambo ambalo linainufaisha Tanzania. Somalia siyo land locked,wana bandari..na position yao kijiografia haiitegemei Tanzania..kwa hiyo hatuwezi kunufaika directly na Somalia...,kwa hiyo kwa nini tuhusike Somalia. Lakini Mashariki ya Congo ikiwa na misukosuko, Tanzania inaathirika moja kwa moja kiuchumi na kibiashara.
Umesema nikasome historia ya huo mgogoro....na kwamba rais Kabila na aliingia mikataba na Rwanda. Sijui unamaanisha nini kuhusu hilo....au una maanisha misemo ya vichochoroni inayodai kwamba Kabila alikubaliana na Rwanda kwamba endapo Rwanda itamsaidia kumuondoa Mobutu madarakani,malipo kwa Rwanda iwe ni kumegewa Kivu kaskazini?
Hayo ni maneno ya vichochoroni kwa sababu hata huyo Kagame hajawahi kudai hilo popote na kamwe hawezi kudai.
Madai ya Rwanda na Uganda yalikuwa kuna waasi wamefanya makazi ndani ya Congo lakini wana malengo ya kuzipiga nchi zao. Wote Uganda na Rwanda wakaingia na kuweka kambi ndani ya Congo na kujihusisha na uchimbaji wa madini. Uganda kaondoa majeshi miaka michache tu nyuma baada ya kitisho cha kushtakiwa kimataifa. Lakini wote Uganda na Rwanda wakatumia ujanja wa kutengeneza waasi wa kuchonga M23 ili wafanye yale yale kwa niaba yao.
Unapoandika kwa kirefu hivi jitahidi uweke paragraph

Ulichonacho ni uoga dhidi ya Rwanda, wala hakuna kingine. Hii hofu kakutegenezea nani?
 
Nawakumbuka hawa watabe enzi za Jk, sielewi kwanini JWTZ imekuwa hivi nasikitika sana pia nakumbuka operations za Comoro, Shelisheli na Bujumbura, JWTZ wakati huo nitaikumbuka Sana
Unataka ifanyaje?
 
Unasema somalia haituhusu na haina athari , hawa magaidi wa kiislanu waliosumbua Kilwa na kule kusini na pia upande wax¹ msumbiji wana mahusiano na Alshabaab na wanasaidiwa mafunzo na silaha, je hiyo siyo athari?
Ni kweli nimesema Somalia haituhusu directly kama ambavyo Congo inavyotuhusu moja kwa moja. Pata picha hiyo rabsha ya juzi tu huko Goma, maelfu ya malori yaliyokuwa yaelekee Congo upande wa Goma na Bukavu yamesimama. Hiyo ina maana kusimama kwa ajira katika mnyororo mzima wa biashara ya malori...kuanzia kwa wamiliki,madereva,migahawa...bila kusahau wapelekaji wa bidhaa zenyewe.
Uwepo wa Alshab Somalia ,Tanzania inahusika nayo vp? Kama ni suala la magaidi au vyovyote utakavyowaita hilo ni suala lanTanzania kukabiliana nalo hapa ndani kwa sababu athari ya ugaidi iko ndani. Ulitaka Tanzania ikashambulie Somalia kwa magaidi wanaozalishwa Tanzania? Kwa taarifa yako wapiganaji wa Alshabaab wanatoka nchi mablimbali lakini hawaendi Somalia kujifunza ugaidi, bali wanaenda kupigana vita baada ya kuivishwa kiimani huko walikotoka. Kwa hiyo kama vijana wa kitanzania wakienda Somalia kujiunga na Alshabaab basi ujue wameivishwa kiimani humu ndani Tanzania. Na kama kuivishwa huko kiimani ni ugaidi,basi huo ugaidi wamejifunzia humu ndani . Sasa unaenda kuishambulia Somalia kwa lipi?
 
Amiri jeshi anateua washauri wake wa karibu mzee wa hovyo Wassira, anayejua kuzozana na Heche, maDC kama Chalamila ataweza kumdhibiti Kagame?

Anasubiri uchaguzi aibe kura na wapinzani wakikataa kuibiwa awatume policcm wawapige virungu, risasi awateke awauwe awafunge basi. Hana akili wala uwezo wa kudeal na Kagame, atapata ushauri gani kwa babu Wassira
 
Mama kaufyata. Wenzake wa SADC wameufyata

..Mama ndiye Mkuu wa Troika ya Ulinzi na Usalama ndiye aliyetakiwa awaongoze na kuwatia ujasiri wenzake.

..Mzee Mugabe alipokuwa Mkuu wa Troika ya ulinzi ya Sadc aliwatimua m23 na Rwanda wakiwa ktk viunga vya Kinshasa, huyu wa kwetu anasalimu amri wakiwa Kivu!!
 
..Mama ndiye Mkuu wa Troika ya Ulinzi na Usalama ndiye aliyetakiwa awaongoze na kuwatia ujasiri wenzake.

..Mzee Mugabe alipokuwa Mkuu wa Troika ya ulinzi ya Sadc aliwatimua m23 na Rwanda wakiwa ktk viunga vya Kinshasa, huyu wa kwetu anasalimu amri wakiwa Kivu!!
Huo uwezo anao?
 
Hivi majeshi wacongo wanashindwa kujilinda wenyewe na hao waasi mpaka kutegemea majeshi ya sadc?
 
Nimemwona rais wa Zimbabwe, ni wazi Pamoja na Angola watatia timu. Sasa mpambani umeanza
Kwahiyo hii vita inakwenda kuwa vita kuu ya ukanda wa maziwa makuu ??!
Wataingia waliomo na wasiokuwamo !
Museveni tayari yumo DRC anasema anawasaka waasi !
Na pia anapeleka majeshi yake South Sudan kumsaidia Salva Kiir !
Ngoja Tusubiri tuone nani naye atapeleka majeshi kumsaidia Riek Marshall !

Na RSF ya Sudan nao wanataka kuunda Serikali kwenye maeneo waliyoyateka !

Kidogo kidogo Africa inataka nayo ipiganishe Vita kuu ya Afrika 😳🙄 !
Ngoja Tusubiri tuone !
 
Na ili nendeni mkaliangalie kamaliza.
KAZI ni kipimo cha utu
 
Mkuu nadhani kagame atakuwa ana enjoy sana watz kuwa na rais tuliye naye.

Miaka ile Joyce Banda alivyo leta zengwe ziwa Nyasa tz tulikuwa na confidensi kuwakong'ota malawi.

Sasa unaweza chukua picha kama hiyo majirani wanaconfidensi kias gani dhidi yetu.

Chukilia mfano tuu nyumba/familia inayo ongozwa na mama huwa haiogopwi na wala hains utisho.

Sasa ukiangaloa Kagame sio tuu kwamba ni raisi,ila pia ni Mwanaume, mtu mzima (nadhan kumzidi raisi samia), Mwanajeshi,Jenerali, mwana intellenjia, ana uzoefu wa vita na mtusi(Jamii ambayo nafasi ya mwanamke ni kama vile ilivyo kwa wasukima na wamasai).

Kwahyo hakuna namna anaweza kuigopa tz kwa sasa, japokuwa anajua vzuri uimara wa JWTZ. Ila anajua nafas ya mkuu wa nchi haitishi ktk ulimwengu wa roho na wa mwili pia.
Najuw PK anafurahi hizi pambio za mitano tena kwa SSH kwakuwa hatumii nguvu nyingi kuidharau tz.

Kwahyo tukae kwa kutulia sis tumechagua gender equality ila hata USA hawajawah kufany hivo na sio rahisi.
 
Back
Top Bottom