Kagame na Siasa za ubabe: Kupiga kura na kuchangia chama tawala si hiari, ni lazima!

Kagame na Siasa za ubabe: Kupiga kura na kuchangia chama tawala si hiari, ni lazima!

Anonymous

Senior Member
Joined
Apr 6, 2006
Posts
118
Reaction score
339
1719011754972.png

Paul Kagame

Siku za nyuma, Katibu Mkuu wa chama tawala, RPF inkotanyi, bwana Wellars Gasamagera, alitamka wazi kuwa, RPF haiwezi kuachia madaraka kwa mtu mwingine au chama chochote.

Ikumbukwe, chaguzi zote zilizopita, matokeo ya uchaguzi yalionyesha kiongozi wa chama hicho, ambaye mara zote ni Paul Kagame, zimeleta matokeo ya kujiuliza mara mbili mbili. Hajawahi kupata chini ya 95%.

Japo yawezekana ni kweli kuwa Kagame anapendwa na raia wake kwa kiasi kikubwa, lakini haijawahi kutokea nchi nyingine hasa za Afrika, kuwa na uchaguzi wa namna hiyo.

Kujiunga chama tawala si hiari
Japo kwa usiri mkubwa, lakini watu wote hasa wanaopatikana kiurahisi (wanafunzi vyuoni, wafanyakazi sehemu mbalimbali, wafanyabiashara, nk)nchi nzima, wote hulazimishwa kujiunga na chama hicho, hata kama hujapenda.

Wafuasi wa chama husakwa kwa njia mbalimbali na bila ridhaa, huorodeshwa na kulishwa kiapo. Ukishakula kiapo, ni sawa na umejitia kitanzi.

Kuchangia chama tawala ni lazima
Kwanza kabisa, bila kujali hali yako kiuchumi, lazima utoe kile utakachoombwa.

Hivi majuzi wakati wa mchakato wa vuguvugu la Uchaguzi linaloendelea, kumekuwepo malalamiko ya wafanyakazi waliokatwa kiasi furani cha mishahara yao - kama michango ya uchaguzi. Hapo hapo, kama wanachama, pia michango ya chama inaendelea. Na matokeo yake, taarifa hutolewa kwamba wametoa kwa hiari yao.

Wananchi wanaolipwa hadi laki na nusu kwa mwezi walilazimishwa kutoa elfu 20 ya Rwanda (yaani, 20,000 ya Rwanda ni takribani TZS 40,000). Na wakuu wa shule za sekondari, wao wanatakiwa kutoa laki 2 za Rwanda. Familia za walalahoi, kila familia ni elfu 3 (sawa na TZS 6,000).

Hizi pesa hukatwa kwenye mishahara(kwa wafanyakazi) na huletewa fomu na kusaini kuwa wametoa kwa hiari.

Na, ndo mnaposikia kwamba Bajeti ya Taifa la Rwanda inajitegemea kwa 85%, mbinu zinazotumika ni hizi hizi. Pia kwenye Mamlaka ya Mapato, faini na hesabu zisizo na maelezo, huwaha na mbinu hizo hizo. Trafiki wanatumia mbinu zilezile, za kukubambikia makosa na huwezi kukataa kulipa. Huku ukijenga nyumba nzuri bila maelezo ya kutosha juu ya pesa umepata wapi, elewa hiyo si nyumba yako yako tena. Iwe umenunua gari au ardhi, na maelezo yako hayatoshi kueleza ulipatapata vipi pesa, elewa ndo kwaheri!

Bahati mbaya, kwa kuwa ni agizo la serikali, wengi wao hubaki na mateso mioyoni mwao na hawana wa kuwasaidia.

Ukivunja kiapo, utakiona cha moto
Kwenye kiapo, unakiri mwenyewe kwamba ukienda kinyume na kiapo hicho, basi wewe uchukuliwe hatua kama adui yeyote.

Hii ndo imepelekea baadhi ya watu kukosa uhuru na kujawa na hofu.

Ubaguzi wa waziwazi
Juzi, Juni 20, 2024 Waziri wa Mambo ya Maafa, Mej. Jenerali (mstaafu) Albert Murasira alinukuliwa akiongea kuhusu raia wa Rwanda waliomaliza kifungo katika gereza la Umoja wa Mataifa, kwamba kuna wadhifa wamevuliwa hivyo hawana nafasi kwao.

Kauli hii hii, hutumika pia kwa familia za watu zinazohusishwa na mauaji ya 1994 dhidi ya kabila la watutsi. Hawa, hutengwa kimtindo katika shughuli mbalimbali hasa za kisiasa.

Ikumbukwe pia kuwa serikali hii ndo iliyohimiza watu kuwa kosa la mtu ni lake tu, ila imefikia hatua hata wengine wanaonja machungu ya dhambi ambazo hawajazitenda au zilitendwa na wazee wao.

Sasa, demokarasia inayohubiriwa Rwanda iko wapi? Je, uhuru wa kujieleza, uko wapi?!

Inakuwaje vyombo vya dola haviruhusu wananchi kuongea kwa uhuru ili mamlaka husika ziweze kujua kero za wananchi na kuzitatua (maoni yasiyohitajika huminywa na kupitisha tu yenye kusifia)?

Kuna wanyarwanda wengi, wamefilisiwa na kuharibiwa maisha na mfumo wa utawala. Wao wenyewe wakiwa wahanga wa siasa hiyo, familia zao ndio huathirika zaidi.

Uenguaji wagombea kibabe
Kama kweli uchaguzi ni wa haki, kwanini kuna mbinu za kuwamaliza wengine wasishiriki kwenye mchakato huu? Haiwezekani watu zaidi ya sita wadaiwe kuwa na kosa la aina moja, na hivyo kupelekea kukosa sifa za kushiriki.

Yupo mgombea aliyesingiziwa kuwa na ukichaa. Tuseme wako sahihi, lakini ilikuwaje akaundiwa akatakiwa kuchunguzwa afya ya akili, wakati jamii ilikuwa inamwona yupo tu sawa?
 
Warwanda hata hawana shida n raisi wao. Kwanza wanampenda. Juu ya yote, huyu raisi ndiye aliyepokea kijiti baada ya vita kuu ya kinyama ya ndani.

Kagame alipoingia serikalini, alitunga sera na sheria kali za kupinga ubaguzi wa kikabila, kuwaunganisha na kulijenga taifa moja lenye maono ya pamoja kama taifa. Alifanikiwa, na sasa Rwanda ni nchi yenye amani n wananchi wake wana Furaha.

Kama umepata nafasi ya kujadili hali yao ya kisiasa, wenyewe wanasema Kagame yupo pale sababu bado wananchi wanamtaka aendelee kuwaongoza.

So ninadhani itapendeza kuwaachia nchi yao, wana Furaha. Sio kama Congo au Sudan, Warwanda wana furaha. Tuyaache mambo yao, hayatuhusu, theyre happy under his reign
 
Warwanda hata hawana shida n raisi wao. Kwanza wanampenda. Juu ya yote, huyu raisi ndiye aliyepokea kijiti baada ya vita kuu ya kinyama ya ndani...
Hapana nakataa waRwanda hawana furaha kbsa na Rwanda haina maendeleo! Kagame yupo madarakan mwaka wa 30 huu anaongoza kanchi ambacho kanaingia mara kadhaa Tabora lakin ukitoka nnje ya kigali(kasehemu kadogo sana haka) ni vumbi tupu na nyumba za udongo ambazo hapo kigali pia zipo! Hayo ndo maendeleo? Rwanda is just another overrated piece of shit.
 
Tatizo ni nini? Kwanini alazimishe ikiwa yeye ndiye anaamua nani ashinde nani afe?

Sioni sababu ya yeye kufanya hivyo, kwa sababu hata wasipo kuwa wananchama yeye bado rais, na hata wasipopiga kura kabisa yeye bado rais.

Nini hasa sababu ya yeye kulazimisha wananchi wawe wananchama wa chama tawala? Kama ni mishahara ana control yeye, ana weza kukata hata 75%.

Hapa kwetu uchaguzi kama Rwanda tu na chawa wanaongezeka , shida iko wapi?
 

Siku za nyuma, Katibu Mkuu wa chama tawala, RPF inkotanyi, bwana Wellars Gasamagera, alitamka wazi kuwa, RPF haiwezi kuachia madaraka kwa mtu mwingine au chama chochote.

Ikumbukwe, chaguzi zote zilizopita, matokeo ya uchaguzi yalionyesha kiongozi wa chama hicho, ambaye mara zote ni Paul Kagame, zimeleta matokeo ya kujiuliza mara mbili mbili. Hajawahi kupata chini ya 95%.

Japo yawezekana ni kweli kuwa Kagame anapendwa na raia wake kwa kiasi kikubwa, lakini haijawahi kutokea nchi nyingine hasa za Afrika, kuwa na uchaguzi wa namna hiyo.

Kujiunga chama tawala si hiari
Japo kwa usiri mkubwa, lakini watu wote hasa wanaopatikana kiurahisi (wanafunzi vyuoni, wafanyakazi sehemu mbalimbali, wafanyabiashara, nk)nchi nzima, wote hulazimishwa kujiunga na chama hicho, hata kama hujapenda.

Wafuasi wa chama husakwa kwa njia mbalimbali na bila ridhaa, huorodeshwa na kulishwa kiapo. Ukishakula kiapo, ni sawa na umejitia kitanzi.

Kuchangia chama tawala ni lazima
Kwanza kabisa, bila kujali hali yako kiuchumi, lazima utoe kile utakachoombwa.

Hivi majuzi wakati wa mchakato wa vuguvugu la Uchaguzi linaloendelea, kumekuwepo malalamiko ya wafanyakazi waliokatwa kiasi furani cha mishahara yao - kama michango ya uchaguzi. Hapo hapo, kama wanachama, pia michango ya chama inaendelea. Na matokeo yake, taarifa hutolewa kwamba wametoa kwa hiari yao.

Wananchi wanaolipwa hadi laki na nusu kwa mwezi walilazimishwa kutoa elfu 20 ya Rwanda (yaani, 20,000 ya Rwanda ni takribani TZS 40,000). Na wakuu wa shule za sekondari, wao wanatakiwa kutoa laki 2 za Rwanda. Familia za walalahoi, kila familia ni elfu 3 (sawa na TZS 6,000).

Hizi pesa hukatwa kwenye mishahara(kwa wafanyakazi) na huletewa fomu na kusaini kuwa wametoa kwa hiari.

Na, ndo mnaposikia kwamba Bajeti ya Taifa la Rwanda inajitegemea kwa 85%, mbinu zinazotumika ni hizi hizi. Pia kwenye Mamlaka ya Mapato, faini na hesabu zisizo na maelezo, huwaha na mbinu hizo hizo. Trafiki wanatumia mbinu zilezile, za kukubambikia makosa na huwezi kukataa kulipa. Huku ukijenga nyumba nzuri bila maelezo ya kutosha juu ya pesa umepata wapi, elewa hiyo si nyumba yako yako tena. Iwe umenunua gari au ardhi, na maelezo yako hayatoshi kueleza ulipatapata vipi pesa, elewa ndo kwaheri!

Bahati mbaya, kwa kuwa ni agizo la serikali, wengi wao hubaki na mateso mioyoni mwao na hawana wa kuwasaidia.

Ukivunja kiapo, utakiona cha moto
Kwenye kiapo, unakiri mwenyewe kwamba ukienda kinyume na kiapo hicho, basi wewe uchukuliwe hatua kama adui yeyote.

Hii ndo imepelekea baadhi ya watu kukosa uhuru na kujawa na hofu.

Ubaguzi wa waziwazi
Juzi, Juni 20, 2024 Waziri wa Mambo ya Maafa, Mej. Jenerali (mstaafu) Albert Murasira alinukuliwa akiongea kuhusu raia wa Rwanda waliomaliza kifungo katika gereza la Umoja wa Mataifa, kwamba kuna wadhifa wamevuliwa hivyo hawana nafasi kwao.

Kauli hii hii, hutumika pia kwa familia za watu zinazohusishwa na mauaji ya 1994 dhidi ya kabila la watutsi. Hawa, hutengwa kimtindo katika shughuli mbalimbali hasa za kisiasa.

Ikumbukwe pia kuwa serikali hii ndo iliyohimiza watu kuwa kosa la mtu ni lake tu, ila imefikia hatua hata wengine wanaonja machungu ya dhambi ambazo hawajazitenda au zilitendwa na wazee wao.

Sasa, demokarasia inayohubiriwa Rwanda iko wapi? Je, uhuru wa kujieleza, uko wapi?!

Inakuwaje vyombo vya dola haviruhusu wananchi kuongea kwa uhuru ili mamlaka husika ziweze kujua kero za wananchi na kuzitatua (maoni yasiyohitajika huminywa na kupitisha tu yenye kusifia)?

Kuna wanyarwanda wengi, wamefilisiwa na kuharibiwa maisha na mfumo wa utawala. Wao wenyewe wakiwa wahanga wa siasa hiyo, familia zao ndio huathirika zaidi.

Uenguaji wagombea kibabe
Kama kweli uchaguzi ni wa haki, kwanini kuna mbinu za kuwamaliza wengine wasishiriki kwenye mchakato huu? Haiwezekani watu zaidi ya sita wadaiwe kuwa na kosa la aina moja, na hivyo kupelekea kukosa sifa za kushiriki.

Yupo mgombea aliyesingiziwa kuwa na ukichaa. Tuseme wako sahihi, lakini ilikuwaje akaundiwa akatakiwa kuchunguzwa afya ya akili, wakati jamii ilikuwa inamwona yupo tu sawa?
Pole kwa wanaRwanda! Huyu ndie alikuwa mshauri wa awamu ya 5 Tz.
 
Hapana nakataa waRwanda hawana furaha kbsa na Rwanda haina maendeleo! Kagame yupo madarakan mwaka wa 30 huu anaongoza kanchi ambacho kanaingia mara kadhaa Tabora lakin ukitoka nnje ya kigali(kasehemu kadogo sana haka) ni vumbi tupu na nyumba za udongo ambazo hapo kigali pia zipo! Hayo ndo maendeleo? Rwanda is just another overrated piece of shit.
Maisha yao yanakuhusu?marekani,uingeteza,nk wao wanafuraha?wewe unafuraha ipi ktk nchi yako?
 
KWenye kumiliki mali bila maelezo umezitoa wapi pesa mbona inatumika nchi nyingi? Tanzania mnauza nchi kujenga majumba mnazania na nchi zingine wanafanya hivyo? Nem
 
Kama kweli ni jirani muungwana,ulizieni hali ilivyo mpakani mwa Rwanda na Tanzania. Inakuwaje kwenye ujirani mwema,watanzania hawapati huduma Rwanda mpakani? Na kuna nini,kiaksi cha kutoruhusu wanyarwanda kirahisi kwenda Tanzania? Maeneo hayo,bidhaa hasa mahitaji ya nyumbani,ni duni. Lakini,ingiza vyakula kutoka Tanzania,uone mziki wake!

Vitu vingine,basi tu
 
Hayo ya dikteta Kagame hayastaajabishi kwani bado yapo kwenye mataifa mengi ya kiafrika Tanzania ikiwemo.
 
UPDATES

Wagombea wa Kiti cha Urais, Frank Habineza kutoka Chama cha Kijani (Green Party) na Mgombea Binafsi, Philipe Mpayimana wamendelea kunadi sera zao katika maeneo mbalimbali ikiwa leo ni siku ya tatu tangu kuanza kwa Kampeni. Tofauti na mwaka 2017, mwaka huu idadi ya Watu wanaohitaji kusikia sera za Wagombea hawa imeongezeka.

Moja ya sera zinazopewa kipaumbele kikubwa kwa Wagombea wote wawili ni kupunguza Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) kutoka 18% ya sasa hadi 14%. Sera hii imepokelewa kwa shamgwe kubwa na Wananchi, hatua inayoashiria kuwa Kodi hii ni mojawapo ya changamoto zilizopo katika biashara nchini.

Katika kunadi sera zao jambo jingine walilolinadi Wagombea hawa ni kuhusu kuongeza uwezo wa Wanyarwanda kupata chakula. Wamesema endapo watachaguliwa, watajitahidi kuhakikisha Nchi inakuwa na uwezo wa kuzalisha chakula cha kutosha ili kupunguza mlipuko wa bei za vyakula. Wameahidi kupigania hilo hadi pale Mwananchi atakapokuwa na uhakika wa kupata walau milo mitatu kwa siku kutoka mlo moja kwa siku au hata kutopata chochote.

Hata hivyo katika Kampeni hizi, jambo la kusikitisha na la wazi kabisa ni kuwa Wagombea hawa hawana uwezo wa kumkabili Mgombea wa chama tawala cha RPF, Paul Kagame na hili linadhihirika wazi kwa kuangalia kuanzia maandalizi ya maeneo ya Wagombea kufikia, mapokezi na ulinzi wao.

Katika hatua nyingine, umeshuhudiwa mkusanyiko wa Watu kwa Wagombea wa tiketi ya chama tawala, RPF na kwa mkusanyiko huu ni wazi chama hicho kimepungukiwa wafuasi na sasa wengi wao wanahudhuria kwa kulazimishwa. Magari yanakodiwa kuwabeba Watu na kuwapeleka katika eneo la tukio ila cha ajabu baada ya zoezi husika hawarudishwi.

Lakini pia, ukiwaangalia Watu hawa ni walewale wa hali ya chini kabisa ambao hata nauli za kuwarudisha walikotoka hawana. Fikiria mtu katolewa umbali wa zaidi ya Kilometa 20 kisha anatelekezwa arudi kwa mguu na sehemu yenyewe hakuna hata magari ya abiria.

Aidha, katika Watu hawa wa hali ya chini wengine baada ya kumaliza hupelekwa kwenye Klabu za pombe na kupewa pombe za Kienyeji kama shukrani.
 
Back
Top Bottom