Kagera sugar mmeshindwa kuifunga Yanga leo ikiwa imechoka basi Yanga itaendelea kuwa unbeaten mpaka mwisho

Kagera sugar mmeshindwa kuifunga Yanga leo ikiwa imechoka basi Yanga itaendelea kuwa unbeaten mpaka mwisho

Mtanzanias

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2021
Posts
1,747
Reaction score
3,725
Nilitegemea sana Yanga leo kucheza chini ya kiwango na hilo limeonekana dhahiri shahiri wachezaji wamechoka sana ratiba ya ovyo ovyo hii sijawai kuona, Pamoja na yote wachezaji wamecheza kikubwa na kushinda kikubwa cha muhimu leo ilikuwa ni point 3 na zimepatikana ashukuriwe Mungu.

Pongezi sana kwa kipa makini Djigui Diara ameonyesha thamani yake iliyomfanya alipiwe tiket ya ndege kutoka Mali kutua Tanzania ni bonge la kipa, Timu inayocheza kibingwa ata ikicheza vibaya lazima iweke mpira kambani na kuondoka na point 3 muhimu
 
Pongezi kwa Yanga African kwa unbeaten 46. Lakini pole kwa wazee wa Miwa dah hii mechi mlistahili kitu. Mpira wakati mwingine ni bahati. Ila pia Kama Kagera watacheza hivi mechi zote zilizosalia basi watakuwa washindi wa pili nyuma ya Yanga.
 
ratiba ipi sawa aise... Mbona kule ulaya timu inatoka kucheza Europa alhamisi then jumamosi timu hiyo hiyo inakuwa na mechi nyingine...

#Tusidekezane...
 
Yanga wamepambana sana ila Madaktari na watu wa physical wa Yanga wafanye kitu, Miili ya wachezaji baada ya hii mechi itakua na Hali mbaya sana.

Maji, matope uwanjani na uchovu unaweza leta injury nyingi au Homa Kali Kwa wachezaji.

Wasichukulie poa, tumepata point 3 lakini Miili ya wachezaji kesho itakua imevunda vibaya Kwa baadhi ya wachezaji hasa waliocheza kule Tunis.
Leo baada ya mechi wasiwatie kwenye barafu, wapige massage tu.

Enzi sisi tunacheza ikitokea mmecheza mechi mfululizo Kwa kipindi kifupi tulikua tukimeza dawa za kutuliza maumivu wakati wa warm-up katika mechi husika ya muda uo ilisaidia kuondoa uchovu, kwasasa nafikiri Wana njia Bora zaidi ki Afya.
 
ratiba ipi sawa aise... Mbona kule ulaya timu inatoka kucheza Europa alhamisi then jumamosi timu hiyo hiyo inakuwa na mechi nyingine...

#Tusidekezane...
Ulaya Logistics zinaruhusu kuanzia viwanja mbaka usafiri wa anga. Kwa apa kwetu Ili ufike Tunis unahitaji connection ya ndege na unaweza kufika eneo husika la kufanyia connection mfano Dubai ukajikuta ndege inayo kwenda(Tunis), unapo kusudia inaondoka massa 6-8 yanayo fuatia.
 
ratiba ipi sawa aise... Mbona kule ulaya timu inatoka kucheza Europa alhamisi then jumamosi timu hiyo hiyo inakuwa na mechi nyingine...

#Tusidekezane...
Kwaiyo miundombinu ya ulaya unafananisha na Tanzania, ingekuwa ni simba ndo imepewa ratiba ya ivyo isingetoboa hii mechi ingefia pale kirumba
 
Nilitegemea sana Yanga leo kucheza chini ya kiwango na hilo limeonekana dhahiri shahiri wachezaji wamechoka sana ratiba ya ovyo ovyo hii sijawai kuona, Pamoja na yote wachezaji wamecheza kikubwa na kushinda kikubwa cha muhimu leo ilikuwa ni point 3 na zimepatikana ashukuriwe Mungu.

Pongezi sana kwa kipa makini Djigui Diara ameonyesha thamani yake iliyomfanya alipiwe tiket ya ndege kutoka Mali kutua Tanzania ni bonge la kipa, Timu inayocheza kibingwa ata ikicheza vibaya lazima iweke mpira kambani na kuondoka na point 3 muhimu
Mmewekeza sana kwenye uchawi na makafara.
 
Diarra ni miongoni mwa makipa bora sana hapa africa [emoji1487][emoji1487][emoji1487][emoji1487][emoji1487][emoji1487][emoji1487]TIMU BORA IMESHINDA HONGERA WATANI[emoji1488][emoji1488]
Pongezi inatoka moyoni kweli?
1661791911648.jpg
 
ratiba ipi sawa aise... Mbona kule ulaya timu inatoka kucheza Europa alhamisi then jumamosi timu hiyo hiyo inakuwa na mechi nyingine...

#Tusidekezane...
Umewahi kufika Ulaya? Vinchi ni vidogo yaan unasafiri kutoka nchi moja kwenda nyingine safari ya masaa 2 tu, hapo shida nn??
Afrika tuko nyuma na zaidi, miundombinu yetu ya ndani ni mibovu, achilia mbali ukubwa wa bara na umbali wa safari.
 
Ratiba nyepesi umaskini wa kushindwa kukodi ndege ya moja kwa moja unawacost. Timu kubwa kila game za kimataifa mnategemea kusafiri na ndege za abiria, ile waiting time ya airport kuconnect flight sio mchezo!
 
Ulaya Logistics zinaruhusu kuanzia viwanja mbaka usafiri wa anga. Kwa apa kwetu Ili ufike Tunis unahitaji connection ya ndege na unaweza kufika eneo husika la kufanyia connection mfano Dubai ukajikuta ndege inayo kwenda(Tunis), unapo kusudia inaondoka massa 6-8 yanayo fuatia.
Tatizo mlikuwa mnapiga kelele miaka iliyopita ili Simba apangwe ratiba ngumu.
Ninyi baada ya ushindi badala ya kurudi mkaanza kuzurula na ngamia kama vile mmechukua kombe tayari,halafu leo mnajiliza liza hapa.

Leo mshukuru wale wachawi wenu ila nao leo walikuwa wamechoka almanusra.
 
Nilitegemea sana Yanga leo kucheza chini ya kiwango na hilo limeonekana dhahiri shahiri wachezaji wamechoka sana ratiba ya ovyo ovyo hii sijawai kuona, Pamoja na yote wachezaji wamecheza kikubwa na kushinda kikubwa cha muhimu leo ilikuwa ni point 3 na zimepatikana ashukuriwe Mungu.

Pongezi sana kwa kipa makini Djigui Diara ameonyesha thamani yake iliyomfanya alipiwe tiket ya ndege kutoka Mali kutua Tanzania ni bonge la kipa, Timu inayocheza kibingwa ata ikicheza vibaya lazima iweke mpira kambani na kuondoka na point 3 muhimu
Y.A🔥🔥🔥🔥
 
ratiba ipi sawa aise... Mbona kule ulaya timu inatoka kucheza Europa alhamisi then jumamosi timu hiyo hiyo inakuwa na mechi nyingine...

#Tusidekezane...miundombinu ya ulaya unalinganisha na bongo fala kweli yaani kutoka tunisia kuja mwanza unalinganisha na kutoka spain kuja london?
 
Ratiba nyepesi umaskini wa kushindwa kukodi ndege ya moja kwa moja unawacost. Timu kubwa kila game za kimataifa mnategemea kusafiri na ndege za abiria, ile waiting time ya airport kuconnect flight sio mchezo!
Tukodie
 
Back
Top Bottom