Kagoda: Ni Rostam

Kagoda: Ni Rostam

Vigogo waanza kumalizana kimya kimya
HOFU imezidi kutawala kwa baadhi ya vigogo wa siasa, hasa kuwepo kwa taarifa za kulishwa sumu kwa baadhi ya vigogo na watu wanaoijua siri ya uanzishwaji wa Kampuni ya Kagoda Agricultural iliyochota sh bilioni 40 katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mmoja wa wafanyabiashara na wanasiasa maarufu hapa nchini (jina tunalo), anadaiwa naye kulishwa sumu na mwenzake ambaye inasemekana amekuwa na siri nzito kuhusu uanzishwaji wa kampuni hiyo, mahali fedha zilipopelekwa na matumizi yake.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari cha Tanzania Daima Jumapili, kimesema kupewa sumu hiyo kunatokana na hofu waliyonayo baadhi ya vigogo kuwa kuna uwezekano mkubwa baadhi ya watu wakatoa siri kuhusu uchotwaji wa fedha.

Hofu hiyo imeongezeka zaidi hivi sasa baada ya kuwepo kwa taarifa za wakili maarufu hapa nchini, Beredi Maregesi, wa Kampuni ya Maregesi Law Chambers kulishwa sumu kama ile anayodaiwa kupewa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), marehemu Daudi Ballali, aliyefariki dunia mwaka jana huku akikabiliwa na shutuma nzito za uidhinishaji wa fedha za EPA kwa kampuni 22.
Ballali ambaye alilazimika kukimbilia nchini Marekani kwa matibabu, inadaiwa aliwahi kueleza kiini cha kuumwa kwake kuwa ni kupewa sumu na mwanasiasa mmoja ambaye inadaiwa kuwa ni miongoni mwa watu waliochota fedha BoT.

Taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili, imezipata zinadai hivi sasa baadhi ya wanasheria walioshiriki au kujua siri za Kagoda wamekuwa na wasiwasi mkubwa juu ya maisha yao, kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo hivi sasa. Wakati wanasheria hao wakiwa na wasiwasi huo, kigogo wa siasa anayedaiwa kulishwa sumu hiyo inayofanya kazi taratibu, amekuwa akipata matatizo ya kiafya na huenda katika siku za hivi karibuni akapelekwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi, baada ya hospitali za hapa nchini kuonekana kutokuwa na uwezo wa kumtibu.

Chanzo cha habari kimedai kuwa kama kweli kigogo huyo atakuwa amelishwa sumu hiyo, uwezekano wa kupona ni mdogo, kwani sumu hiyo huenda mbali zaidi kwa kuingia kwenye mifupa.

“Kama kweli amelishwa sumu ninayoijua, uponaji wake utakuwa mdogo, hata kama atapelekwa katika hospitali za nje,” kilisema chanzo hicho ambacho hakikutaka kutajwa jina lake.

Kigogo huyo inasemekana ndiye aliyekuwa na mipango imara ya kuwaokoa baadhi ya vigogo waliodaiwa kuhusika na Kampuni ya Kagoda ambayo katika siku za hivi karibuni wamiliki wake wametajwa lakini baadhi ya watu wanapinga kuwa si wamiliki halisi, bali ni kivuli cha vigogo wa siasa ambao walichukua fedha hizo kwa ajili ya kuwasaidia katika masuala yao ya siasa.

Baadhi ya wanasheria walio karibu na Maregesi wameweka bayana kuwa matumizi ya kijasusi, hasa ya kuwekeana sumu si mazuri na ni vema serikali ikachunguza madai hayo ili kubaini kama yana ukweli wowote kuliko kuyapuuza, kwa kudai kuwa huo ni uzushi.

Maregesi anadaiwa kuwa mtu wa karibu wa marehemu Ballali na anazijua siri nyingi, pamoja na mali za gavana huyo, jambo linalomfanya kuonekana mtu muhimu katika ushahidi endapo kampuni ya Kagoda ingefikishwa mahakamani.

Pamoja na wasiwasi huo wa kufikishwa mahakamani kwa Kampuni ya Kagoda, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, wamekwisha kuweka bayana kuwa hawajapata ushahidi wa kutosha wa kuweza kuifikisha mahakamani Kampuni ya Kagoda.

Kagoda ni miongoni mwa kampuni 22 zilizochota kiasi cha sh bilioni 133 katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ambapo mpaka sasa watuhumiwa 20 na kampuni zao wameshafikishwa mahakamani, huku Kagoda iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ikiwa haijafikishwa mahakamani kwa kile kinachodaiwa kutokuwapo kwa ushahidi wa kuiburuza mahakamani.

Hawa TANZANIA DAIMA wameanza lini huu UPUMBAVU wa kutoa amnesty kwa criminals????? anayezungumzwa hapa ni rostam, wanajaribu kujenga sababu ili ionekane ana sababu ya kwenda nje ya nchi kwa kigezo cha matibabu, then baadae kdg iwe rahisi kupoteza idendities zake kama ilivyotokea kwa balali... nani atajua kama amekufa au hajafa????

Acheni ujinga huu!!
 
Mkapa na Rostam watajwa
Peter Noni, Malegesi wamo

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele
USHAHIDI wa kwanza na muhimu kwamba fedha zilizoibwa na Kampuni ya Kagoda kutoka Benki Kuu (BoT) uliidhinishwa na viongozi wakuu nchini, sasa umepatikana, MwanaHALISI limeelezwa.

Waraka wa wakili aliyeshuhudia mikataba ya Kagoda na makampuni mengine ya kupata fedha hizo, unamtaja rais mstaafu Benjamin Mkapa kuwa miongoni mwa waliofanikisha mpango huo.

Katika andishi rasmi kwa Kamati ya rais Jakaya Kikwete ya kushughulikia wizi kwenye akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), wakili huyo anakiri kuwa ni yeye alifanya attestation – “kushuhudia mikataba ya Kagoda na makampuni mengine ya nje.”

Bhyidinka Michael Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi – Malegesi Law Chambers – ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba hiyo ndani ya ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.


Aidha, kwa ushahidi wa Sanze, mbunge Rostam Aziz, ndiye kinara wa mpango mzima uliofanikisha wizi wa zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka BoT.

“Niliitwa na Bw. Malegesi ofisini kwa Bw. Rostam Aziz, 50 Milambo, Ofisi za Caspian Construction Limited. Nilipofika…niliwakuta Bw. Rostam Aziz, Peter Noni na Bw. Malegesi, wakaniambia fedha hizo zinahitajika kwa ajili ya kugharamia uchaguzi wa CCM na rais wake,” ameeleza Sanze.

Wakili anaeleza kuwa alikuta “documents – nyaraka zimeshaadaliwa ambazo niliombwa nizi-sign (niziweke saini). Nikauliza hizo fedha zinakotoka na nitathibitisha vipi kabla ya kusaini.”

Andishi la wakili linaeleza kuwa Rostan Aziz, Peter Noni na Bered Malegesi walimthibitishia Sanze kuwa Rostam alikuwa kwenye kikao ambako rais mstaafu Mkapa alitoa maelekezo kwa Gavana Ballali kutoa fedha hizo kwa Rostam kwa ajili ya uchaguzi.


Wakati huo Peter Noni alikuwa Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi katika BoT. Hivi sasa ni Mkurugenzi wa Mpango ya Kimikakati. Ballali alikuwa gavana wa BoT. Alifariki dunia mwaka jana nchini Marekani.

Sanze anasema Malegesi aliishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Philip Mangula kuwa yaliyosemwa na Rostam yalikuwa kweli.

Hata hivyo Sanze anaongeza kuwa, “Rostam mwenyewe alisema, ‘system yote inajua.’” Anasema kwamba baada ya maelezo hayo ya Rostam, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini.

Kwa mujibu wa andishi la Sanze ambalo linathibitishwa kwa saini yake, Malegesi alimwita Noni ofisini mwake baada ya jina la Sanze kutajwa magazetini akihusishwa na Kagoda, lakini aliambiwa kuwa “nitulie tu serikali inalishughulikia swala hilo.”


Haya hivyo, Sanze anasema katika andishi hilo kuwa baada ya kumaliza kazi yake ya kushuhudia mikataba hakufuatilia kilichoendelea.

Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.

Hata hivyo, haijathibitishwa iwapo kweli kulikuwa na kikao kinachomtaja Mkapa akiamuru gavana Ballali kutoa fedha kwa Rostam, kwani kauli ya Sanze inatokana maelezo ya Malegesi na Rostam Aziz; ama ukiwa ukweli au njia ya kumshawishi Sanze kushuhudia mikataba ya Kagoda.

Kwa miezi 15 sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikikana kushiriki au kutumia fedha zilizotokana na wizi uliofanywa na Kagoda ingawa kimeshindwa pia kuthibitisha kilipopata mabilioni ya shilingi kugharamia kampeni zake ghali za uchaguzi mkuu wa 2005.

Katibu Mkuu Yusuph Makamba na Katibu Mwenezi John Chiligati wamekana chama chao kutumia fedha za EPA katika uchaguzi mkuu wa 2005. Wamesema kama kuna aliyechukua fedha hizo, basi hakutumwa na chama chao bali ni kwa matumizi yake binafsi.


MwanaHALISI liliwasiliana na wakili Sanze kupitia simu yake ya mkononi, likitaka kujua undani wa andishi lake. Sanze alimwambia mwandishi wa habari hizi, “Siwezi kujibu swali hilo.”

Alipoulizwa kwa nini aliitwa na Malegesi kushuhudia mikataba wakati yeye Malegesi alikuwepo alisema, “Hilo muulize Malegesi mwenyewe.”

Kuhusu kampuni yake kupata mgao na kuchangia CCM na kama kuna risiti inaonyesha walitoa mchango huo, Sanze alisema kwa ufupi, “Sijui lolote. Niambie wewe. Sijui zilitoka mwaka gani.”

Alipong’ang’anizwa kuhusu kuchangia CCM alijibu, “Nikuulize wewe kama zilitoka lini.”

Wakati wote simu ya Malegesi ilijibu kuwa haipatikani. Simu ya Rostam Aziz ilijibu pia kuwa hapatikani lakini ujumbe ulioandikwa na kumwomba awasiliane na mwandishi, ulionyesha kuwa umepokelewa. Hata hivyo, hadi tunakwenda mitamboni, Rostam hakuita.

Namba ya simu ya Mangula nayo ilisema kuwa hapatikani. Mwanasheria Mkuu wa serikali Johnson Mwanyika hakupatikana kuzungumzia andishi la Sanze.

Wiki iliyopita vyombo vya habari viliripoti kuwa 26 Januari mwaka huu, Malegesi alikula kitu kilichodaiwa kuwa sumu na kulazimika kulazwa hospitali ya Mikocheni, Dar es Salaam.

Uvumi ulioenea jijini Dar es Salaam unasema inawezekana Malegesi amelishwa sumu kwa makusudi kwa kuwa ni mtu muhimu katika sakata la Kagoda linalogusa watu wengi na wa nyadhifa mbalimbali.

Ni miezi tisa sasa tangu Daudi Ballali aage dunia kutokana na kile kilichodaiwa “kulishwa sumu” huku akieleweka kuwa mtuhumiwa mkuu au shahidi muhimu katika wizi mkubwa ndani ya BoT.


Gazeti la Nipashe Jumapili, 8 Februari 2009 limeandika kuwa Malegesi alitumia siku 11 hospitalini Mikocheni akipata matibabu ya kuondolewa sumu anayodaiwa kuipata kwenye chakuka.

Muuguzi mmoja aliliambia gazeti hilo kwamba hawawezi kutoa taarifa yoyote juu ya aina ya sumu au lolote walilobaini katika vipimo bila ruhusa ya mgonjwa mwenyewe.

Kampuni ya Kagoda ilikwapua zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka akaunti ya EPA, ikiwa ni wiki moja baada yakusajiliwa. Kampuni ilitawanya fedha hizo katika matawi saba ya Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.

Ni takriban mwaka mmoja sasa tangu rais aunde Kamati ya watu watatu kuchunguza wizi katika akaunti ya EPA, ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa serikali Johnson Mwanyika. Wengine ni Mkurugenzi wa TAKUKURU, Edward Hosea na Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema.

Haijafahamika iwapo wote ambao Sanze ametaja kwenye andishi lake walihojiwa na Kamati. Lakini taarifa zilizopo zinasema rais mstaafu Mkapa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, hawajawahi kuhojiwa.

Mwishoni mwa mwaka jana, waandishi wa habari walimuuliza Waziri Mkuu Mizengo Pinda iwapo serikali inaogopa kukamata na kushitaki wahusika katika Kagoda; lakini alijibu kuwa, “Wahusika wote watafikishwa mahakamani.”

He' we go again, tuone sasa hivi tutaishia wapi maana tumekuwa tukikwazwa na mambo mengi hapa kati kuingiliana.
 
Vigogo waanza kumalizana kimya kimya
HOFU imezidi kutawala kwa baadhi ya vigogo wa siasa, hasa kuwepo kwa taarifa za kulishwa sumu kwa baadhi ya vigogo na watu wanaoijua siri ya uanzishwaji wa Kampuni ya Kagoda Agricultural iliyochota sh bilioni 40 katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA) kupitia Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Mmoja wa wafanyabiashara na wanasiasa maarufu hapa nchini (jina tunalo), anadaiwa naye kulishwa sumu na mwenzake ambaye inasemekana amekuwa na siri nzito kuhusu uanzishwaji wa kampuni hiyo, mahali fedha zilipopelekwa na matumizi yake.

Kwa mujibu wa chanzo cha habari cha Tanzania Daima Jumapili, kimesema kupewa sumu hiyo kunatokana na hofu waliyonayo baadhi ya vigogo kuwa kuna uwezekano mkubwa baadhi ya watu wakatoa siri kuhusu uchotwaji wa fedha.

Hofu hiyo imeongezeka zaidi hivi sasa baada ya kuwepo kwa taarifa za wakili maarufu hapa nchini, Beredi Maregesi, wa Kampuni ya Maregesi Law Chambers kulishwa sumu kama ile anayodaiwa kupewa aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu (BoT), marehemu Daudi Ballali, aliyefariki dunia mwaka jana huku akikabiliwa na shutuma nzito za uidhinishaji wa fedha za EPA kwa kampuni 22.
Ballali ambaye alilazimika kukimbilia nchini Marekani kwa matibabu, inadaiwa aliwahi kueleza kiini cha kuumwa kwake kuwa ni kupewa sumu na mwanasiasa mmoja ambaye inadaiwa kuwa ni miongoni mwa watu waliochota fedha BoT.

Taarifa ambazo Tanzania Daima Jumapili, imezipata zinadai hivi sasa baadhi ya wanasheria walioshiriki au kujua siri za Kagoda wamekuwa na wasiwasi mkubwa juu ya maisha yao, kutokana na mwenendo wa mambo ulivyo hivi sasa. Wakati wanasheria hao wakiwa na wasiwasi huo, kigogo wa siasa anayedaiwa kulishwa sumu hiyo inayofanya kazi taratibu, amekuwa akipata matatizo ya kiafya na huenda katika siku za hivi karibuni akapelekwa nje ya nchi kwa matibabu zaidi, baada ya hospitali za hapa nchini kuonekana kutokuwa na uwezo wa kumtibu.

Chanzo cha habari kimedai kuwa kama kweli kigogo huyo atakuwa amelishwa sumu hiyo, uwezekano wa kupona ni mdogo, kwani sumu hiyo huenda mbali zaidi kwa kuingia kwenye mifupa.

“Kama kweli amelishwa sumu ninayoijua, uponaji wake utakuwa mdogo, hata kama atapelekwa katika hospitali za nje,” kilisema chanzo hicho ambacho hakikutaka kutajwa jina lake.

Kigogo huyo inasemekana ndiye aliyekuwa na mipango imara ya kuwaokoa baadhi ya vigogo waliodaiwa kuhusika na Kampuni ya Kagoda ambayo katika siku za hivi karibuni wamiliki wake wametajwa lakini baadhi ya watu wanapinga kuwa si wamiliki halisi, bali ni kivuli cha vigogo wa siasa ambao walichukua fedha hizo kwa ajili ya kuwasaidia katika masuala yao ya siasa.

Baadhi ya wanasheria walio karibu na Maregesi wameweka bayana kuwa matumizi ya kijasusi, hasa ya kuwekeana sumu si mazuri na ni vema serikali ikachunguza madai hayo ili kubaini kama yana ukweli wowote kuliko kuyapuuza, kwa kudai kuwa huo ni uzushi.

Maregesi anadaiwa kuwa mtu wa karibu wa marehemu Ballali na anazijua siri nyingi, pamoja na mali za gavana huyo, jambo linalomfanya kuonekana mtu muhimu katika ushahidi endapo kampuni ya Kagoda ingefikishwa mahakamani.

Pamoja na wasiwasi huo wa kufikishwa mahakamani kwa Kampuni ya Kagoda, Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) na Waziri wa Katiba na Sheria, Mathias Chikawe, wamekwisha kuweka bayana kuwa hawajapata ushahidi wa kutosha wa kuweza kuifikisha mahakamani Kampuni ya Kagoda.

Kagoda ni miongoni mwa kampuni 22 zilizochota kiasi cha sh bilioni 133 katika Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje (EPA), ambapo mpaka sasa watuhumiwa 20 na kampuni zao wameshafikishwa mahakamani, huku Kagoda iliyochota kiasi cha sh bilioni 40 ikiwa haijafikishwa mahakamani kwa kile kinachodaiwa kutokuwapo kwa ushahidi wa kuiburuza mahakamani.


Halafu? Atafia huko na kuzikwa huko!!!!!! Makubwa!

 
Kwa nini Kimei na maafisa wake wa 'benki ya wazalendo' hawabanwi kueleza mabilioni hayo walimlipa nani? Kumbukumbu ziko hapo CRDB na inashangaza BoT haifanyi chochote dhidi ya benki hii kwa kukiuka taratibu za malipo. Kwa ujum la ni kazi rahisi sana kama wana ubavu wa kufanya hivyo.
 
Hakuna mtu atakaeifungulia mashitaka Kagoda Agricultural ltd. Hakuna mwenye uwezo wa kufanya hivyo. Hawatashitakiwa na serikali hii. Sababu ni kwamba, viongozi waliopo wameingia madarakani kwa kutumia Kagoda. Kagoda ndio silaha yao. Yaani ni kama Iran au North Korea na mabomu yake ya Nuclear. Ndio kinga yao kuweza kushinda uchaguzi 2005. Sasa nadhani watakuwa wanatafuta ki-Kagoda kingine kwa ajili ya 2010, wakati kila mtu ameweka macho yake kwenye Kagoda Agri... Hizi ndizo zinazoitwa chenga za akili na macho.
 
ooh inatisha, naogopa wajameni.
nchi hii kila mtu na kamuhogo kake. ni kula tu. ipo siku watasga meno wao na vizazi vyao. AMEN.
 
Kama ni kweli kuwa fedha zilizochotwa na Kagoda kutoka EPA partly zilitumika kufadhili kampeni za CCM kny uchaguzi mkuu wa 2005, basi tusitegemee haki kutendeka in the 4th phase gvt kwa sababu, fedha hizo ndizo zilizoiwezesha kushika dola.......simply 'Ukijikwaa kwa mguu wa Kushoto na kuanguka, mguu wa kulia hauwezi kuuhukumu ule wa kushoto uliojikwaa na kusababisha kuanguka kwako''

The only way ya kupata haki hapa re. Kagoda sagga na mengineyo.....ni mpaka tutakapo kuwa na a new regime in Tanzania, then hawa watuhumiwa wetu wanaweza kuhukumiwa kwa haki ya kweli, vinginevyo tutazidi kupigana machanga ya macho bila ya haki kutendeka!
 
Last edited:
Kama ni kweli kuwa fedha zilizochotwa na Kagoda kutoka EPA partly zilitumika kufadhili kampeni za CCM kny uchaguzi mkuu wa 2005, basi tusitegemee haki kutendeka in the 4th phase gvt kwa sababu, fedha hizo ndizo zilizoiwezesha kushika dola.......simply 'Ukijikwaa kwa mguu wa Kushoto na kuanguka, mguu wa kulia hauwezi kuuhukumu ule uliokwaa kwa kusababisha kuanguka kwako''

The only way ya kupata haki hapa re. Kagoda sagga na mengineyo.....ni mpaka tutakapo kuwa na a new regime Tanzania, then hawa watuhumiwa wetu wanaweza kuhukumiwa kwa haki ya kweli, vinginevyo tutazidi kupigana machanga ya macho bila ya haki kutendeka!

Hatutasubiri mpaka new regime tutapiga kelele, tunataka wananchi wajue kuwa serikali iliyoko madarakani haipo kisheria kwa kuwa waliiba pesa za wanchi na kuwaacha wafe na njaa na magonjwa ili wao waingie madarakani. then tutawaachia wananchi wenyewe waamue kama wanataka kuendelea kuishi na umasikini wao wakati viongozi wa ccm wakiendelea kutembelea mashangingi kinyume cha sheria au waadabishe kwa kuwanyima madaraka.

Pamoja na kuwa hakuna chama cha upinzani kilichojiandaa kuchukua madara baada ya CCm lakini inahitajika kuwaadabisha CCM sasa wakati umefika wawe na nidhamu kwenye pesa za wananchi.
 
Ni katika sakata la Kagoda
PM, DCI, DPP waweseka

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele

SERIKALI imeshindwa kusema lolote kuhusiana na kushiriki katika wizi wa mabilioni ya shilingi kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.

Taarifa za gazeti hili, toleo la wiki iliyopita, zilimnukuu wakili mmoja wa mjini Dar es Salaam akisema, chini ya kiapo, kwamba aliambiwa na Rostam Aziz kuwa fedha hizo zaidi ya Sh. 40 bilioni zilikuwa ni za kugharamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa 2005.


Wakili huyo, Bhyidinka Michael Sanze, ananukuliwa akiwasiliana na Kamati ya Rais ya Kushughulikia wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwamba miongoni mwa wahusika wakuu katika wizi huo, ni rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Wengine aliowataja ni Rostam, Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, gavana wa BoT, Dk. Daud Ballali, Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi BoT, Peter Noni na wakili wa kujitegemea, Bered Malegesi.

Mwanasheria mashuhuri nchini, Mabere Marando alipotakiwa maoni yake juu ya kigugumizi hiki cha serikali, alisema, "(Serikali) hawawezi kusema kitu."

Alisema, "Mimi nadhani serikali imepigwa na butwaa. Hawakujua kama vitu hivi vitaibuliwa. Hawakujua haya! Inawezekana wameshangaa haya mliyoandika."

Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi – Malegesi Law Chambers – ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba ya uchotaji fedha alipokuwa katika ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na Rostam, mfanyabiashara na mbunge wa Igunga.

Sanze, katika hati ya kiapo, anadai kuelezwa na Rostam kuwa alikuwa kwenye kikao cha Mkapa, Mangula na Ballali ambapo anasema "alishuhudia Mkapa akitoa amri kwa Ballali" ya kutoa fedha hizo na kumkabidhi yeye (Rostam).


Siku nane tangu taarifa hizo zitoke, serikali haijesema lolote na viongozi mbalimbali ambao gazeti hili limejitahidi kuwasiliana nao, ama wamesema hawataki kuzungumza lolote au hawana la kusema.

MwanaHALISI ilimtafauta Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili kutaka kujua msimamo wa serikali baada ya ushahidi huo kuanikwa hadharani, lakini hakuweza kupatikana.

Msaidizi wake, Ole Kuyani alimtaka mwandishi kuwasiliana na msaidizi mwingine alimyetaja kwa jina moja la Ibambiro, kwa maelezo kwamba huyo ndiye yupo karibu zaidi na bosi wake kwa wakati huo.

Ibambiro alipatikana na baada ya kuelezwa kile ambacho MwanaHALISI inahitaji kutoka kwa waziri mkuu, aliahidi kupiga simu baada ya kuwasiliana na Pinda.

Gazeti lilipoona kimya kimekuwa kirefu, lilipiga tena simu ofisini kwa waziri mkuu, lakini aliyepokea alijibu kwa ufupi. "Tumekuahidi kukupigia. Subiri utapigiwa."

Hadi tunakwenda mitamboni, ofisi ya waziri mkuu haikupiga simu MwanaHALISI.


Waziri mkuu Pinda aliahidi wananchi kupitia vyombo vya habari Desemba mwaka jana, kwamba "Serikali haigopi Kagoda na kwamba masuala yote yanafuatiliwa na yataelezwa bayana uchunguzi utakapokamilika."

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alipoulizwa Polisi inachukua hatua gani baada ya kupatikana ushahidi wa Sanze kuhusika kwa Kagoda na vigogo wengine katika ukwapuaji wa fedha BoT, alisema "hilo aulizwe Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP)."

"Nimekuelewa. Lakini kwa ujumla, sisi hatujadili ushahidi hadharani. Ushahidi unajadiliwa mahakamani," alisema Manumba.


Juhudi za gazeti kumpata DPP hazikuweza kuzaa matunda. Awali alipopigiwa simu juzi Jumatatu, DPP Eliezer Feleshi alipokea na baada ya mwandishi kujitambulisha alisema, "nipo kwenye kikao, nipigie baadaye."

Alipoulizwa apigiwe baada ya muda gani, Feleshi alisema, "ni baada ya saa moja." Gazeti liliendelea kumtafuta Feleshi juzi Jumatatu lakini simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa. Hadi tunakwenda mitamboni Feleshi alikataa kujibu simu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika hakupatikana, lakini msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Omega Ngole, alipoulizwa juu ya msimamo wa ofisi yake, kuhusiana na waliotajwa na wakili Sanze katika sakata la Kagoda, alisema hayo ni mambo ya kujadili ofisini.

Simu ya Mwanyika Na. 0713 324854 kila ilipopigwa ilitoa jibu, "simu unayopiga haipatikani, jaribu tena baadaye." Ilipigwa tena na tena, lakini jibu bado lilikuwa ni hilohilo.

Kwa mujibu wa andishi la Sanze, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini baada ya kuthibitishiwa na Malegesi kuwa alishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Mangula. Sanze alisisitiza, "Rostam mwenyewe alisema, ‘system yote inajua.'"

Alipoulizwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba amepokeaje taarifa zilizotolewa na Sanze kuhusu "sakata la Kagoda" hasa kwa kuwa zimetaja viongozi wa CCM, aliingia kati na kusema, "Kama ni masuala ya Kagoda, mimi sina la kuzungumza."

Mwandishi alipomueleza kuwa inajulikana wakati wa "sakata la Kagoda" yeye hakuwa katibu mkuu wa CCM, isipokuwa Sanze anasema fedha zimewasilishwa katika chama, Makamba alisisitiza, "Kama ni Kagoda hilo sina jibu."

Makamba akakata simu. Gazeti linamtafuta Makamba ili pamoja na mambo mengine, ajibu swali: Zipo taarifa zozote katika chama zinazoonyesha kwamba Rostam Aziz aliingiza fedha zilizochotwa EPA, katika kampeni za CCM?


Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IGP), Said Mwema hakupatikana. Simu yake Na. 0754 785557 ilikuwa inaita bila kupokelewa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hoseah, alipoitwa kwa simu yake Na. 0784 763741, simu yake ilikaa kimya. Baadaye ilipopigwa tena ilijibu, "samahani simu unayopiga haipatikani kwa sasa."

Mwanyika ndiye alikuwa mwenyekiti wa Timu ya Rais ya kufuatilia yaliyogunduliwa na maodita wa Ernst & Young katika ukaguzi wa akaunti ya EPA kwa mwaka 2005/2006. Wajumbe wengine wa timu hiyo ni IGP Mwema na Hoseah.

MwanaHALISI iliwasiliana na Dk. Willibrod Slaa, mbunge wa Karatu na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ili kutoa maoni yake ambapo alisema serikali haiwezi kujibu lolote kwa sababu inajua kila kitu kuhusu Kagoda.

"Nyaraka mlizotumia, hata mimi ninazo. Nimejiridhisha kwamba haya mliyosema ni sahihi, na kwamba serikali inayajua. Lakini haitaki kusema ukweli huu kwa sababu, inahusika katika wizi huu," alisema Dk. Slaa.

Wakili Marando anafika mbali zaidi. Anasema, "Serikali haijapuuza, tatizo hawajui la kufanya. Nimeiona affidavit (hati ya kiapo) ya Sanze ni sahihi."

Anasema, "Mimi sioni kama Watanzania watasahau haya. Serikali na CCM wanajua kwamba viongozi wa vyama vya upinzani watatumia hoja hizo katika kampeni."


Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.

Hadi sasa, watuhumiwa 20 wamefikishwa mahakamani kuhusiana na sakata la ufisadi wa fedha za EPA, lakini kumekuwa na ugumu kwa serikali kushughulikia wahusika wa Kagoda.
 
Kwanini mambo haya yote yasifike mahali yakawagharimu kwenye uchaguzi hapo 2010? Watanzania tubadilike na tutumie makosa haya kuwaondoa madarakani na kwenye majimbo ya uchaguzi.
 
Kazi ipo.Iam dwarfed by these scandls.Jamani hivi serikali maana yake nini hasa.Kama mambo yenyewe ndio haya, kuna haja ya kuwa na serikali kweli?Wale tulio wapa dhamana kutuongoza na kutulinda, sasa ndio wamekuwa vinara wa kututafuna!Mmm,inatisha sana.Watanzania mbona tumelala sana,hawa jamaa wana nia ya kutu exterminate kabisa,tuwakataeni jamani.Mungu wao ni shetani,ndiye wanayemtumikia.

Mkapa na Rostam watajwa
Peter Noni, Malegesi wamo

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele
USHAHIDI wa kwanza na muhimu kwamba fedha zilizoibwa na Kampuni ya Kagoda kutoka Benki Kuu (BoT) uliidhinishwa na viongozi wakuu nchini, sasa umepatikana, MwanaHALISI limeelezwa.

Waraka wa wakili aliyeshuhudia mikataba ya Kagoda na makampuni mengine ya kupata fedha hizo, unamtaja rais mstaafu Benjamin Mkapa kuwa miongoni mwa waliofanikisha mpango huo.

Katika andishi rasmi kwa Kamati ya rais Jakaya Kikwete ya kushughulikia wizi kwenye akaunti ya Madeni ya Nje (EPA), wakili huyo anakiri kuwa ni yeye alifanya attestation – "kushuhudia mikataba ya Kagoda na makampuni mengine ya nje."

Bhyidinka Michael Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi – Malegesi Law Chambers – ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba hiyo ndani ya ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na mfanyabiashara na mbunge wa Igunga, Rostam Aziz.


Aidha, kwa ushahidi wa Sanze, mbunge Rostam Aziz, ndiye kinara wa mpango mzima uliofanikisha wizi wa zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka BoT.

"Niliitwa na Bw. Malegesi ofisini kwa Bw. Rostam Aziz, 50 Milambo, Ofisi za Caspian Construction Limited. Nilipofika…niliwakuta Bw. Rostam Aziz, Peter Noni na Bw. Malegesi, wakaniambia fedha hizo zinahitajika kwa ajili ya kugharamia uchaguzi wa CCM na rais wake," ameeleza Sanze.

Wakili anaeleza kuwa alikuta "documents – nyaraka zimeshaadaliwa ambazo niliombwa nizi-sign (niziweke saini). Nikauliza hizo fedha zinakotoka na nitathibitisha vipi kabla ya kusaini."

Andishi la wakili linaeleza kuwa Rostan Aziz, Peter Noni na Bered Malegesi walimthibitishia Sanze kuwa Rostam alikuwa kwenye kikao ambako rais mstaafu Mkapa alitoa maelekezo kwa Gavana Ballali kutoa fedha hizo kwa Rostam kwa ajili ya uchaguzi.


Wakati huo Peter Noni alikuwa Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi katika BoT. Hivi sasa ni Mkurugenzi wa Mpango ya Kimikakati. Ballali alikuwa gavana wa BoT. Alifariki dunia mwaka jana nchini Marekani.

Sanze anasema Malegesi aliishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Katibu Mkuu wa CCM, Bw. Philip Mangula kuwa yaliyosemwa na Rostam yalikuwa kweli.

Hata hivyo Sanze anaongeza kuwa, "Rostam mwenyewe alisema, ‘system yote inajua.'" Anasema kwamba baada ya maelezo hayo ya Rostam, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini.

Kwa mujibu wa andishi la Sanze ambalo linathibitishwa kwa saini yake, Malegesi alimwita Noni ofisini mwake baada ya jina la Sanze kutajwa magazetini akihusishwa na Kagoda, lakini aliambiwa kuwa "nitulie tu serikali inalishughulikia swala hilo."


Haya hivyo, Sanze anasema katika andishi hilo kuwa baada ya kumaliza kazi yake ya kushuhudia mikataba hakufuatilia kilichoendelea.

Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.

Hata hivyo, haijathibitishwa iwapo kweli kulikuwa na kikao kinachomtaja Mkapa akiamuru gavana Ballali kutoa fedha kwa Rostam, kwani kauli ya Sanze inatokana maelezo ya Malegesi na Rostam Aziz; ama ukiwa ukweli au njia ya kumshawishi Sanze kushuhudia mikataba ya Kagoda.

Kwa miezi 15 sasa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikikana kushiriki au kutumia fedha zilizotokana na wizi uliofanywa na Kagoda ingawa kimeshindwa pia kuthibitisha kilipopata mabilioni ya shilingi kugharamia kampeni zake ghali za uchaguzi mkuu wa 2005.

Katibu Mkuu Yusuph Makamba na Katibu Mwenezi John Chiligati wamekana chama chao kutumia fedha za EPA katika uchaguzi mkuu wa 2005. Wamesema kama kuna aliyechukua fedha hizo, basi hakutumwa na chama chao bali ni kwa matumizi yake binafsi.


MwanaHALISI liliwasiliana na wakili Sanze kupitia simu yake ya mkononi, likitaka kujua undani wa andishi lake. Sanze alimwambia mwandishi wa habari hizi, "Siwezi kujibu swali hilo."

Alipoulizwa kwa nini aliitwa na Malegesi kushuhudia mikataba wakati yeye Malegesi alikuwepo alisema, "Hilo muulize Malegesi mwenyewe."

Kuhusu kampuni yake kupata mgao na kuchangia CCM na kama kuna risiti inaonyesha walitoa mchango huo, Sanze alisema kwa ufupi, "Sijui lolote. Niambie wewe. Sijui zilitoka mwaka gani."

Alipong'ang'anizwa kuhusu kuchangia CCM alijibu, "Nikuulize wewe kama zilitoka lini."

Wakati wote simu ya Malegesi ilijibu kuwa haipatikani. Simu ya Rostam Aziz ilijibu pia kuwa hapatikani lakini ujumbe ulioandikwa na kumwomba awasiliane na mwandishi, ulionyesha kuwa umepokelewa. Hata hivyo, hadi tunakwenda mitamboni, Rostam hakuita.

Namba ya simu ya Mangula nayo ilisema kuwa hapatikani. Mwanasheria Mkuu wa serikali Johnson Mwanyika hakupatikana kuzungumzia andishi la Sanze.

Wiki iliyopita vyombo vya habari viliripoti kuwa 26 Januari mwaka huu, Malegesi alikula kitu kilichodaiwa kuwa sumu na kulazimika kulazwa hospitali ya Mikocheni, Dar es Salaam.

Uvumi ulioenea jijini Dar es Salaam unasema inawezekana Malegesi amelishwa sumu kwa makusudi kwa kuwa ni mtu muhimu katika sakata la Kagoda linalogusa watu wengi na wa nyadhifa mbalimbali.

Ni miezi tisa sasa tangu Daudi Ballali aage dunia kutokana na kile kilichodaiwa "kulishwa sumu" huku akieleweka kuwa mtuhumiwa mkuu au shahidi muhimu katika wizi mkubwa ndani ya BoT.


Gazeti la Nipashe Jumapili, 8 Februari 2009 limeandika kuwa Malegesi alitumia siku 11 hospitalini Mikocheni akipata matibabu ya kuondolewa sumu anayodaiwa kuipata kwenye chakuka.

Muuguzi mmoja aliliambia gazeti hilo kwamba hawawezi kutoa taarifa yoyote juu ya aina ya sumu au lolote walilobaini katika vipimo bila ruhusa ya mgonjwa mwenyewe.

Kampuni ya Kagoda ilikwapua zaidi ya Sh. 40 bilioni kutoka akaunti ya EPA, ikiwa ni wiki moja baada yakusajiliwa. Kampuni ilitawanya fedha hizo katika matawi saba ya Benki ya CRDB jijini Dar es Salaam.

Ni takriban mwaka mmoja sasa tangu rais aunde Kamati ya watu watatu kuchunguza wizi katika akaunti ya EPA, ikiongozwa na Mwanasheria Mkuu wa serikali Johnson Mwanyika. Wengine ni Mkurugenzi wa TAKUKURU, Edward Hosea na Inspekta Jenerali wa Polisi Saidi Mwema.

Haijafahamika iwapo wote ambao Sanze ametaja kwenye andishi lake walihojiwa na Kamati. Lakini taarifa zilizopo zinasema rais mstaafu Mkapa na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, hawajawahi kuhojiwa.

Mwishoni mwa mwaka jana, waandishi wa habari walimuuliza Waziri Mkuu Mizengo Pinda iwapo serikali inaogopa kukamata na kushitaki wahusika katika Kagoda; lakini alijibu kuwa, "Wahusika wote watafikishwa mahakamani."
 
Hapa ni budi wananchi tuamue maamuzi magumu,definetly gharama kubwa za kampeni za CCM zilitokana na ufisadi huu kwenye Coffers za serikali.Kutokana na hali hii si rahisi wahusika wa Kagoda kupelekwa mbele ya sheria.Kulingana na ushahidi huu uliotolewa asasi za kiraia zingechukua jukumu la kumobilise maandamano ya kushinikiza kuundwa kwa serikali ya mpito.
Haiwezekani kuendelea kutawaliwa na serikali iliyoundwa kwa njia ya kifisadi kufuata utawala wa sheria.Hii indhihirisha wazi kuwa ni ndoto kwa nchi yetu kupata uongozi imara kuipeleka nchi yetu kwenye neema.Matamshi yaliyotolewa na Rais wa kuifanya morogoro ghala la chakula ni changa la macho.Rasilimali iliyochotwa na kikundi hiki ilitosha kabisa kutengeneza mpango wa kilimo endelevu kwa mikoa ya morogoro,mbeya,Ruvuma,Iringa na Rukwa ndani ya miaka mitano kutosheleza mahitaji ya chakula.
Shime watz tutafakari tumekosa uongozi!
 
Ni katika sakata la Kagoda
PM, DCI, DPP waweseka

Na Saed Kubenea
Mwanahalisi~Maslahi ya Taifa Mbele

SERIKALI imeshindwa kusema lolote kuhusiana na kushiriki katika wizi wa mabilioni ya shilingi kupitia kampuni ya Kagoda Agriculture Limited.

Taarifa za gazeti hili, toleo la wiki iliyopita, zilimnukuu wakili mmoja wa mjini Dar es Salaam akisema, chini ya kiapo, kwamba aliambiwa na Rostam Aziz kuwa fedha hizo zaidi ya Sh. 40 bilioni zilikuwa ni za kugharamia Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi mkuu wa 2005.


Wakili huyo, Bhyidinka Michael Sanze, ananukuliwa akiwasiliana na Kamati ya Rais ya Kushughulikia wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT), kwamba miongoni mwa wahusika wakuu katika wizi huo, ni rais mstaafu Benjamin Mkapa.

Wengine aliowataja ni Rostam, Katibu Mkuu wa CCM, Philip Mangula, gavana wa BoT, Dk. Daud Ballali, Mkurugenzi wa Mipango na Uchumi BoT, Peter Noni na wakili wa kujitegemea, Bered Malegesi.

Mwanasheria mashuhuri nchini, Mabere Marando alipotakiwa maoni yake juu ya kigugumizi hiki cha serikali, alisema, “(Serikali) hawawezi kusema kitu.”

Alisema, “Mimi nadhani serikali imepigwa na butwaa. Hawakujua kama vitu hivi vitaibuliwa. Hawakujua haya! Inawezekana wameshangaa haya mliyoandika.”

Sanze, wakili katika kampuni ya mawakili ya Malegesi – Malegesi Law Chambers – ya Dar es Salaam, anasema katika andishi lake kuwa alishuhudia mikataba ya uchotaji fedha alipokuwa katika ofisi za kampuni ya Caspian Construction Limited ambayo inamilikiwa na Rostam, mfanyabiashara na mbunge wa Igunga.

Sanze, katika hati ya kiapo, anadai kuelezwa na Rostam kuwa alikuwa kwenye kikao cha Mkapa, Mangula na Ballali ambapo anasema “alishuhudia Mkapa akitoa amri kwa Ballali” ya kutoa fedha hizo na kumkabidhi yeye (Rostam).


Siku nane tangu taarifa hizo zitoke, serikali haijesema lolote na viongozi mbalimbali ambao gazeti hili limejitahidi kuwasiliana nao, ama wamesema hawataki kuzungumza lolote au hawana la kusema.

MwanaHALISI ilimtafauta Waziri Mkuu Mizengo Pinda ili kutaka kujua msimamo wa serikali baada ya ushahidi huo kuanikwa hadharani, lakini hakuweza kupatikana.

Msaidizi wake, Ole Kuyani alimtaka mwandishi kuwasiliana na msaidizi mwingine alimyetaja kwa jina moja la Ibambiro, kwa maelezo kwamba huyo ndiye yupo karibu zaidi na bosi wake kwa wakati huo.

Ibambiro alipatikana na baada ya kuelezwa kile ambacho MwanaHALISI inahitaji kutoka kwa waziri mkuu, aliahidi kupiga simu baada ya kuwasiliana na Pinda.

Gazeti lilipoona kimya kimekuwa kirefu, lilipiga tena simu ofisini kwa waziri mkuu, lakini aliyepokea alijibu kwa ufupi. “Tumekuahidi kukupigia. Subiri utapigiwa.”

Hadi tunakwenda mitamboni, ofisi ya waziri mkuu haikupiga simu MwanaHALISI.


Waziri mkuu Pinda aliahidi wananchi kupitia vyombo vya habari Desemba mwaka jana, kwamba “Serikali haigopi Kagoda na kwamba masuala yote yanafuatiliwa na yataelezwa bayana uchunguzi utakapokamilika.”

Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai (DCI), Robert Manumba alipoulizwa Polisi inachukua hatua gani baada ya kupatikana ushahidi wa Sanze kuhusika kwa Kagoda na vigogo wengine katika ukwapuaji wa fedha BoT, alisema “hilo aulizwe Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP).”

“Nimekuelewa. Lakini kwa ujumla, sisi hatujadili ushahidi hadharani. Ushahidi unajadiliwa mahakamani,” alisema Manumba.


Juhudi za gazeti kumpata DPP hazikuweza kuzaa matunda. Awali alipopigiwa simu juzi Jumatatu, DPP Eliezer Feleshi alipokea na baada ya mwandishi kujitambulisha alisema, “nipo kwenye kikao, nipigie baadaye.”

Alipoulizwa apigiwe baada ya muda gani, Feleshi alisema, “ni baada ya saa moja.” Gazeti liliendelea kumtafuta Feleshi juzi Jumatatu lakini simu yake ilikuwa inaita bila kupokelewa. Hadi tunakwenda mitamboni Feleshi alikataa kujibu simu.

Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika hakupatikana, lakini msemaji wa Wizara ya Sheria na Katiba, Omega Ngole, alipoulizwa juu ya msimamo wa ofisi yake, kuhusiana na waliotajwa na wakili Sanze katika sakata la Kagoda, alisema hayo ni mambo ya kujadili ofisini.

Simu ya Mwanyika Na. 0713 324854 kila ilipopigwa ilitoa jibu, “simu unayopiga haipatikani, jaribu tena baadaye.” Ilipigwa tena na tena, lakini jibu bado lilikuwa ni hilohilo.

Kwa mujibu wa andishi la Sanze, alishuhudia mikataba hiyo kwa kusaini baada ya kuthibitishiwa na Malegesi kuwa alishakwenda kujiridhisha kwa Ballali na Mangula. Sanze alisisitiza, “Rostam mwenyewe alisema, ‘system yote inajua.’”

Alipoulizwa Katibu Mkuu wa CCM, Yusuph Makamba amepokeaje taarifa zilizotolewa na Sanze kuhusu “sakata la Kagoda” hasa kwa kuwa zimetaja viongozi wa CCM, aliingia kati na kusema, “Kama ni masuala ya Kagoda, mimi sina la kuzungumza.”

Mwandishi alipomueleza kuwa inajulikana wakati wa “sakata la Kagoda” yeye hakuwa katibu mkuu wa CCM, isipokuwa Sanze anasema fedha zimewasilishwa katika chama, Makamba alisisitiza, “Kama ni Kagoda hilo sina jibu.”

Makamba akakata simu. Gazeti linamtafuta Makamba ili pamoja na mambo mengine, ajibu swali: Zipo taarifa zozote katika chama zinazoonyesha kwamba Rostam Aziz aliingiza fedha zilizochotwa EPA, katika kampeni za CCM?


Inspekta Jenerali wa Polisi nchini (IGP), Said Mwema hakupatikana. Simu yake Na. 0754 785557 ilikuwa inaita bila kupokelewa.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), Edward Hoseah, alipoitwa kwa simu yake Na. 0784 763741, simu yake ilikaa kimya. Baadaye ilipopigwa tena ilijibu, “samahani simu unayopiga haipatikani kwa sasa.”

Mwanyika ndiye alikuwa mwenyekiti wa Timu ya Rais ya kufuatilia yaliyogunduliwa na maodita wa Ernst & Young katika ukaguzi wa akaunti ya EPA kwa mwaka 2005/2006. Wajumbe wengine wa timu hiyo ni IGP Mwema na Hoseah.

MwanaHALISI iliwasiliana na Dk. Willibrod Slaa, mbunge wa Karatu na Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ili kutoa maoni yake ambapo alisema serikali haiwezi kujibu lolote kwa sababu inajua kila kitu kuhusu Kagoda.

“Nyaraka mlizotumia, hata mimi ninazo. Nimejiridhisha kwamba haya mliyosema ni sahihi, na kwamba serikali inayajua. Lakini haitaki kusema ukweli huu kwa sababu, inahusika katika wizi huu,” alisema Dk. Slaa.

Wakili Marando anafika mbali zaidi. Anasema, “Serikali haijapuuza, tatizo hawajui la kufanya. Nimeiona affidavit (hati ya kiapo) ya Sanze ni sahihi.”

Anasema, “Mimi sioni kama Watanzania watasahau haya. Serikali na CCM wanajua kwamba viongozi wa vyama vya upinzani watatumia hoja hizo katika kampeni.”


Hii ni mara ya kwanza Mkapa kutajwa katika sakata la kampuni ya Kagoda Agriculture Limited, lakini ni mara nyingi Rostam amehusishwa na ukwapuaji huo ndani ya BoT.

Hadi sasa, watuhumiwa 20 wamefikishwa mahakamani kuhusiana na sakata la ufisadi wa fedha za EPA, lakini kumekuwa na ugumu kwa serikali kushughulikia wahusika wa Kagoda.

Watabana Wataachia tuu!
 
Mkuu Invisible naona umeamua kupambuzuuke sasa, duh hiyo Kagoda yupo peke yake huyo Mkuu! naona zingine wapo mbili au zaidi. kazi ipo hapa...
Haya ndio Maswali CCM wajibu na KIGODA na Mwakyembe. Sio kutupa viini macho vya KIKABURU na UFISADI mtupu
 
Hivi ndio tumeshasahau?

Tufanye nini sasa?? Wenye nchi tuliowapa kura ndo wameshaamua kwamba EPA sio issue..tusubiri 2011 tuanze kusikia hela za campaign 2010 zilikotoka tuje jf tudiscuss then its 2015 🙁
 
Should the all these contributions of wana JF be taken seriously. I mean what will happen siku tukimpa invisible au Mwanakijiji au mshiiri au bubu au msemakweli au mzalendo au steveD au yoyote humu nchi.

Jamani yangu macho na masikio mambo yatakuwa haya haya au mabaya zaidi. Tusikae tu kuongea na kusubiri mambo ya badilike yenyewe. Tunasubiri nini, nafasi zetu za kula siku tukipata vyeo au tunasubiri kufa na maneno yetu kinywani.

Kinachotakiwa sasa ni kuorganise some kind of action. JF itusaidie kwa hilo, kuorganise a concrete opposition action, open and transparent ambayo itasaidia kufichua na kuhamasisha umma kuhusu ufisadi. Na hii ndiyo itapeleka Tz kwenye next level, ile ya civil disobidience kama nchi za wenzetu, civil disobidience inayotosha kumfanya rais ajiuzulu.

Tusisubir hadi tuanzishe vyama vya siasa. Kwanza haviko effective kuleta mabadiliko. Kila mtu aanze sasa. Baadhi yetu (mmoja mmoja) tunaweza kupoteza maisha, ndiyo, lakini hiyo itakuwa ni sadaka itakayosaidia nchi. Na damu ya mtu haipotei bure. Sijapata bado clear idea of how this course of opposition action and civil mobilisation inavyoweza kufanywa, lakini discussions humu JF zingelenga kuchangia mawazo ya kuelekea huko.

We should be discussion on what to do, on solutions. Hiyo ndio itaonyesha nia yetu hasa ya kubadilisha nchi hii. la sivyo tunapiga tu kelele kwa sababu haujapa ulaji (wa kifisadi), siku tukiupata tutanyamaza kimya kama sio sisi.
 
Acheni mambo yenu ya kiswahili.....kila kitu Rostam Rostam. kwani viongozi wengine hamuwaoni? Rostam Aziz alitumiwa na CCM kama 'scapegoat' kwenye hio kesi ya kagoda. Hela zote zilitumiwa kwenye campaign ya 2005 na Rostam hakuchukua hata senti. Habari ndio hiyo!
 
Acheni mambo yenu ya kiswahili.....kila kitu Rostam Rostam. kwani viongozi wengine hamuwaoni? Rostam Aziz alitumiwa na CCM kama 'scapegoat' kwenye hio kesi ya kagoda. Hela zote zilitumiwa kwenye campaign ya 2005 na Rostam hakuchukua hata senti. Habari ndio hiyo!

Asimame na aueleze umma wa Watanzania kuwa yeye alitekeleza tu na matokeo yake ni Kikwete ndani ya Ikulu. Kama hasemi basi wimbo utabaki pale pale!
 
Back
Top Bottom