Kahama VS Njombe/Mafinga

Kahama VS Njombe/Mafinga

Wakurugenzi wa Bohari ya Dawa (MSD) wamefanya ziara kwenye kiwanda cha kuzalisha mipira ya mikono cha MSD kilichopo Idofi,Makambako Mkoani Njo mbe.

Wakurugenzi hao wameshuhudia namna mpira ya mikono inavyozalishwa, kuanzia hatua ya kwanza hadi kukamilika kwake, zinapowwkwa kwenye vifungashio.

Akizungumza katika ziara hiyo Mkurugenzi wa Utawala na Rasilimali Watu wa MSD Mboyi Wishega amesema tayari kiwanda hicho kimepata ithibati ya ubora, yaani GMP, ambayo inawezesha kiwanda hicho kuanza kuzalisha na kuuza bidhaa ya mipira ya mikono.

Wishega ameeleza kuwa iwanda hicho kina uwezo wa kuzalisha mipira ya mikono 20,000 kwa saa sawa na jozi 10,000 za mipira ya mikono kwa saa.

Ameongeza kuwa kuanza kwa uzalishaji kiwandani hapo utapunguza uagizaji wa bidhaa za mipira ya mikono kutoka nje ya nchi na kupunguza matumizi ya fedha za kigeni.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja na Uendeshaji Dkt. Pamela Sawa amesema uzalishaji huo utasaidia kuboresha utoaji huduma kwa wateja wa MSD kwani upatikanaji na ubora
wa bidhaa hii sasa utasimamiwa kwa ufasaha na Bohari ya Dawa (MSD), ambaye ndiye msambazaji wa bidhaa za afya kwa vituo vya kutolea huduma za afya nchini.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa TEHAMA Amani Abdul Dello amesema amefurahishwa na mifumo iliyofungwa kwenye kiwanda hicho na kuongeza kuwa, kwa kiwanda hicho kupata ithibati ya ubora (GMP) ni hatua sahihi kukiwezesha kiwanda hicho kuanza kuzalisha na kuuza bidhaa hiyo nchini.
1708269587815.jpg
1708269600701.jpg
 
MKOA WA RUVUMA WAKUSANYA MAPATO KWA ASILIMIA 134
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kufanikiwa kukusanya mapato ya ndani zaidi ya shilingi bilioni 29.5 sawa na asilimia 134 katika kipindi cha mwaka 2022/2023.
Kanali Thomas ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.
Amesema TRA katika kipindi hicho wamefanya kazi nzuri ya kukusanya mapato kwa kuwa wamevuka lengo la makusanyo ya zaidi ya shilingi bilioni 21 ambapo amesema Uchumi wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika.
“Mkoa unaendelea kuimarika kiuchumi kwa kuimarika kwa miundombinu,shughuli za uzalishaji mali,biashara na ukewekezaji shughuli za uchimbaji madini hasa makaa ya mawe,maboresho ya uwanja wa Ndege wa Songea na biashara na nchi jirani za Msumbiji na Malawi’’,alisistiza RC Thomas.
Ameyataja mazingira ya kujifunzia na kufundishia wanafunzi yamekuwa bora zaidi ambapo Mkoa uliletewa fedha za kujenga shule mpya 12 za msingi kupitia BOOST kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7,7 pia serikali ilileta fedha zaidi ya shilingi bilioni tano kujenga sekondari mpya tisa kupitia program ya SEQUIP.
Kulingana na Mkuu wa Mkoa katika kipindi cha mwaka 2022/2023 serikali imetoa shilingi milioni 900 kukarabati hospitali kongwe ya Tunduru na zaidi ya shilingi bilioni tatu zimetolewa na serikali kujenga hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya Songea.
Ameongeza kuwa serikali imetoa shilingi bilioni 9.3 kujenga vituo vya afya 14 na kwamba serikali imenunua mashine ya CT scan na digital xray kwa ajili ya hospitali ya Rufaa ya Mkoa na mashine ya Xray kwa ajili ya hospitali ua Halmashauri ya Madaba.
 
WACHINA KUWEKEZA HEKARI 10,000 KILIMO CHA MAZAO YA MIFUGO MADABA
Wawekezaji wa Kampuni ya Xiwang kutoka nchini China wamepewa shamba lenye Hekari 10,000 lililopo Kijiji cha Ngadinda Kata ya Gumbiro Halmashauri ya Wilaya ya Madaba wilayani Songea mkoani Ruvuma kwaajili uwekezaji wa kilimo cha mazao ya mifugo.
Mbunge wa Jimbo la Madaba Mheshimiwa Joseph Mhagama akizungumza kwenye eneo hilo amesema shamba hilo la Serikali lilikuwa na hekari 15,000 ambapo hekari 5000 wamepewa wananchi kwaajili ya kilimo.
“Wananchi mmepewa hekari 5000 na eneo lililobaki tunampa mwekezaji naomba tutoe ushirikiano kwa mwekezaji”,alisema Mhagama.
Meneja wa Kampuni ya XIWANG Savio Chanahi amesema wamejipanga kuzalishaji mahindi ya njano,soya na ufuta na watakuwa wanabadilisha mazao kwa kurutubisha ardhi ili kulinda mazingira.
Amesema Wizara itakapowakabidhi rasmi Shamba hilo ndani ya miezi miwili wataanza kupeleka vifaa kwa ajili ya kuanza kazi.
1708524112765.jpg
 
MKOA WA RUVUMA WAKUSANYA MAPATO KWA ASILIMIA 134
Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma Kanali Laban Thomas ameipongeza Mamlaka ya Mapato Tanzania(TRA) kwa kufanikiwa kukusanya mapato ya ndani zaidi ya shilingi bilioni 29.5 sawa na asilimia 134 katika kipindi cha mwaka 2022/2023.
Kanali Thomas ametoa pongezi hizo wakati anazungumza kwenye ufunguzi wa Kikao cha Baraza la Ushauri la Mkoa (RCC) kilichofanyika kwenye ukumbi wa Manispaa ya Songea.
Amesema TRA katika kipindi hicho wamefanya kazi nzuri ya kukusanya mapato kwa kuwa wamevuka lengo la makusanyo ya zaidi ya shilingi bilioni 21 ambapo amesema Uchumi wa Mkoa wa Ruvuma umeendelea kuimarika.
“Mkoa unaendelea kuimarika kiuchumi kwa kuimarika kwa miundombinu,shughuli za uzalishaji mali,biashara na ukewekezaji shughuli za uchimbaji madini hasa makaa ya mawe,maboresho ya uwanja wa Ndege wa Songea na biashara na nchi jirani za Msumbiji na Malawi’’,alisistiza RC Thomas.
Ameyataja mazingira ya kujifunzia na kufundishia wanafunzi yamekuwa bora zaidi ambapo Mkoa uliletewa fedha za kujenga shule mpya 12 za msingi kupitia BOOST kwa gharama ya zaidi ya shilingi bilioni 7,7 pia serikali ilileta fedha zaidi ya shilingi bilioni tano kujenga sekondari mpya tisa kupitia program ya SEQUIP.
Kulingana na Mkuu wa Mkoa katika kipindi cha mwaka 2022/2023 serikali imetoa shilingi milioni 900 kukarabati hospitali kongwe ya Tunduru na zaidi ya shilingi bilioni tatu zimetolewa na serikali kujenga hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Ruvuma katika eneo la Mwengemshindo Manispaa ya Songea.
Ameongeza kuwa serikali imetoa shilingi bilioni 9.3 kujenga vituo vya afya 14 na kwamba serikali imenunua mashine ya CT scan na digital xray kwa ajili ya hospitali ya Rufaa ya Mkoa na mashine ya Xray kwa ajili ya hospitali ua Halmashauri ya Madaba.
Ila Hawa nao wanachekesha yaani Bil.29 ndio wanasherehekea?
 
Aisee Kwa Sasa Mbeya inajengwa magorofa mengi sana ya watu binafsi.👇👇
IMG_20240221_175903_890.jpg
IMG_20240221_175903_503.jpg
IMG_20240221_182818_176.jpg
IMG_20240221_175612_648.jpg
IMG_20240221_175610_771.jpg
IMG_20240221_172707_401.jpg
IMG_20240221_172706_451.jpg
IMG_20240221_172436_090.jpg
IMG_20240221_172404_119.jpg


Hoja kuu ya Sasa ni urefu ndio Bado
 
Back
Top Bottom