Kaimu RPC Mwanza: Risasi zilipigwa hewani bahati mbaya ikampata mtu Mmoja na kumwua...

Kaimu RPC Mwanza: Risasi zilipigwa hewani bahati mbaya ikampata mtu Mmoja na kumwua...

Huyu mama Ag RPC anaitwa Lilian Matola. Sijui hata kama kweli alisoma Physics ya form II vinginevyo ni aibu tupu. Risasi ipigwe HEWANI halafu itelemke chini by gravitational force, inaweza kweli kumua mtu achilia mbali kumjeruhi?!

Uwongo mwingine ni wa kulidhalilisha JESHI la POLISI, na ku prove "folkore" kwamba POLISI wengi ni form four failure!
Kama hujui askari wengi ni wale waliofeli form four - ndio maana maelezo yao mengi huwa hayatofautiani na hata punguani hawezi kukubaliana nayo - kazi ipo
 
imeshakuwa ni utaratibu wa jeshi letu la polisi kuua raia na kitu ambacho sielewi ni hawa wanaojiita watetezi wa haki za binadam wanachokifanya ni kuishia kutoa logistics na details kibao za jinsi raia wanavyouawa na jeshi la polisi lakini step forward hazionekani
 
Jeshi letu la polisi linatia aibu, kinyaa na linafikirisha.......sijui baada ya maelezo ya yule mama kwa waandishi wa habari Saidi Mwema au viongozi wengine wa jeshi walijisikiaje? ni aibu, wapige risasi hewani halafu impate MACHINGA!

Hata alivyokuwa anaongea unajua kabisa hajiamini coz anaongea uongo.....RIP MACHINGA, SHAME ON YOU JESHI LA POLISI.
 
Nilikuwa namdadisi mtaalamu wa milipuko,akawa ananieleza risasi ukiipiga juu ikimaliza mita zake inashuka na inakuwa haina nguvu haiwezi tena kuua mtu,huyo aliyeuawa mwanza alipigwa risasi,na swali aliloniuliza huyo mtaalamu wa milipuko je inakuwaje vurugu za wamachinga uende na bunduki ?je unaweza kumpiga mtoto wako kwa kutumia panga kama akikukosea?
One million dollar question,,,je polisi wameruhusiwa na nani kuua raia?na kwa nini wanatumia nguvu kubwa sana siku hizi?enzi za nyerere,mwinyi,mkapa kulikuwa na kamatakamata za uzururaji lakini hatukuwahi sikia mtu kauawa inakuaje sasa hv polisi wanakuwa hivyo?je ni kuwatisha wananchi wasijaribu kufuatilia haki zao?
 
Kwa hakika ningekuwa mume wa yule mama aliyeongea upuuzi jana kwa waandishi wa habari, angekula BAN ya kutoona unyumba mpaka ukweli ujulikane, potelea mbali akienda tafuta bwana sehemu nyingine.
 
Huyo mpiga debe alikuwa amepanda muembe akiangua maembe,mimi nilikuwa jirani yake,aliyosema Mama RPC ni kweli tupu.
 
Swali la kujiuliza hapo kama risasi ilipigwa juu iweje imlenge mtu kifuani au siku hizi risasi huwa inabadiliswa uwelekeo na upepo?Je mhanga alikuwa kalala kwa mgongo ndio ikamdondokea?Kama kiongozi wa jeshi ni muongo kuna haja gani sisi raia kuwa wakweli?
 
Sasa naanza kuamini kuwa damu inayomwagwa ya Watanzania wasio na hatia ni tambiko ili CCM ishinde mwaka 2015
 
Wanajeshi wakiwa wanazikwa risasi hupigwa juu lakini hatujawahi kusikia aliyekufa
 
Kwa utetezi wa kitoto

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Jana nilimcikia yule mwanamke polisi alivyokuwa anaelezea.. Nilichogundua rasmi jana (japo nilikuwa ninaelewa hili) ni kwamba Polisi wa Tanzania wanaongoza kwa kusema uongo..! Ati mmachinga alimkunja askari wa jiji na kumtolea sime..! Mashahidi wote waliohojiwa wamesema tofauti..!
 
Sasa unataka ufe wewe au uhai wa huyo jamaa....unathamani gan kwangu acha afe
 
Yaani hiyo kwao ndo kauli yenye unafuu, tegemea kupata kauli za ajabu sana huko mbeleni
Itafika kipindi tutaambiwa kuwa risasi ilijifyatua yenyewe
 
Yupo atakayesema:'CHADEMA' inahusika moja kwa moja na vurugu hizi'.Tuvute subira tuendelee kuona madudu ya chama na Serikali yangu
 
Nimemsikiliza huyo Mama hata jina lake sikutaka kulijua.
Anasema Police walifika pale kutuliza ghasia, huku wakirusha au piga risasi juu kwa BAHATI MBAYA ikampata Raia Mmoja.

Nataka kujua hawa waliojeruhiwa walikuwa wamekaa hewani huko zilipo pigwa Risasi.

...huyo mama yupo sawa kweli...alafu anasema wanachunguza, wanachunguza nini wakati Risasi zilipigwa hewani na ilimpata bahati huko huko juu.

Mi nilijua kwamba hawawezi kuja na jipya hapo. polisi wa siku hizi sio wa kweli na ukiongozana nae ogopa kabisa!
 
Aliyeuawa atakuwa ni kunguru, binadamu akafanye nini hewani!?? hivi bado tu hamjawajua polisi wenu!????
 
Back
Top Bottom