Kaimu RPC Mwanza: Risasi zilipigwa hewani bahati mbaya ikampata mtu Mmoja na kumwua...

Kaimu RPC Mwanza: Risasi zilipigwa hewani bahati mbaya ikampata mtu Mmoja na kumwua...

Polisi waache hivyo hivyo , ndio maana wanaweza kuuza sehemu yao ya kazi ?
 
huyo mama anatudanganya kwa kuwa watanzania ni wadhaifu and we are always silent due to our cowardness!!
 
Kwa hiyo huyo jamaa aliyeuwawa naye alikuwa angani? Itafika mahali wananchi tukichoka kusikia hizi lugha za kitoto kutakuwa hapatoshi. Mara kitu chenye ncha kali, mara kitu kizito chenye mshindo, na sasa ni angani ila ni bahati mbaya.


Huenda aliyeuwawa alikuwa hewani akifanya utafiti wa mvua za Lowassa (zile za Thailland)
 
Bullets fired straight up in the air fall at terminal velocity which is much less than velocity bullet leaves barrel of the gun. A 0.30 calibre bullet falls with terminal velocity 90 m/s while 0.50 calibre bullet falls with terminal velocity 150 m/s. Certainaly free falling bullets can cause injuries usually to head or feet.( wanafizikia remember this: at terminal velocity mg= kv^2 A level physics)
 
Bobuk anasema anaitwa Lilian Matola , anayemjua zaidi atupe habari zake , inadaiwa alikuwa mahiri sana kwenye somo la ukakamavu , a.k.a kwata . Mengine kama elimu ,uadilifu , uaminifu , utii , etc, tujuzeni.
 
Ni kweli ilimpata wakati inatoka juu kuja chini...."descending"
mkuu risasi ikishalipuka wakati inaenda hewan (ascending) inapoteza nguvu kbsa, ikirudi chin km karatas tu, haina madhara.

km unaweza refer (Projectile) fiziksi hiyo
 
Huyu mama Ag RPC anaitwa Lilian Matola. Sijui hata kama kweli alisoma Physics ya form II vinginevyo ni aibu tupu. Risasi ipigwe HEWANI halafu itelemke chini by gravitational force, inaweza kweli kumua mtu achilia mbali kumjeruhi?!

Uwongo mwingine ni wa kulidhalilisha JESHI la POLISI, na ku prove "folkore" kwamba POLISI wengi ni form four failure!
ukifuatilia utakuta ndo wale wanaonunua vyeti,
Si ajabu Lilia Matola origino yupo secta nyingine na anafanya kazi kwa umakin mkubwa.
 
Maswali mengine unatafuata ku-overload kichwa mwishowe uwe kichaa, we amini tu hivyo.

Kwani walithubutu kusema kuna marehemu alifariki kwa kuchomwa na kitu chenye ncha Kali lakini sio risasi, si uliamini?

Na ukaambiwa marehemu Mwandosya hakuuliwa na Polisi ingawa picha zilionyesha hivyo, si uliamini? Mbona hii hutaki kuamini sasa??
 
Kuna mwandishi alimwuliza walikuwa wakiongea kwa njia ya simu,imekuwaje risasi zipigwe juu then ziue akajibu hilo wanalichunguza.

hapa patamu,yan risasi ilikaidi badala ya kwenda juu ikamfuata machinga kweli hizi risasi lazima zichunguzwe,dah Matola naye anafuata mlemle.
 
hapa tanzania polisi wanaongoza kuua,kisha ajali za barabarani!jee tuna haja ya kuwa na jeshi la polisi?
 
Labda juu kulikuwa na askari mwengine anapiga chini risasi....
Kama wa chini anapiga hewan,
Na wa hewan anapiga chini.
 
Walipigwa na vitu vyenye ncha kali as per intelijensia ya polisi
 
Nilikuwa namdadisi mtaalamu wa milipuko,akawa ananieleza risasi ukiipiga juu ikimaliza mita zake inashuka na inakuwa haina nguvu haiwezi tena kuua mtu,huyo aliyeuawa mwanza alipigwa risasi,na swali aliloniuliza huyo mtaalamu wa milipuko je inakuwaje vurugu za wamachinga uende na bunduki ?je unaweza kumpiga mtoto wako kwa kutumia panga kama akikukosea?
One million dollar question,,,je polisi wameruhusiwa na nani kuua raia?na kwa nini wanatumia nguvu kubwa sana siku hizi?enzi za nyerere,mwinyi,mkapa kulikuwa na kamatakamata za uzururaji lakini hatukuwahi sikia mtu kauawa inakuaje sasa hv polisi wanakuwa hivyo?je ni kuwatisha wananchi wasijaribu kufuatilia haki zao?


hata lile la machozi iringa lilirushwa juu?


Utetezi feki kabisa
 
Mimi nilikuwepo eneo la tukio, ni kweli kabisa zile risasi zilipigwa juu hewani ambako kwa bahati mbaya ilimpata mtu mmoja aliyekuwa akipita huko juu angani akitembea kwa miguu bila hata mabawa, imedhihirika kuwa mtu huyo ni muumini wa mzee wa upako:shut-mouth:
 
Back
Top Bottom