Kaka yetu anasaidia ndugu wa mke wake, sisi hatusaidii

Kaka yetu anasaidia ndugu wa mke wake, sisi hatusaidii

Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu


Fikra za kimasikini sana ndugu yangu. Kwanini unasubiri kusaidiwa je una kilema chochote? Kwanini wewe usiwe ndiye msaidiaji

Inawezekana kabisa tatizo likawa ni nyie ndugu na wala sio kaka zenu. Huwezi kuwa na ndugu tegemezi maana ukishafanya makosa ya ndugu kukutegemea basi watakutegemea maisha yao yote. Sehemu ambayo ni muhimu kusaidiana kama ndugu ni kwenye elimu tu. Lakini sijui miradi ya biashara au pesa za kujikimu wakati upo mtaani nashauri usisaide kabisa ndugu
 
Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu
“niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini.”

Yaani alikulipia shule lakini bado unalalamika. Tatizo hakuamini ndiyo maana ameenda mpaka bank kuweka pesa. Kama shule imeisha Kwanini bado unafuatilia maisha yake na kuwa omba omba
 
Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu
Acha utegemezi, fanya kazi. Na kama bado mtoto kaombe kwa wazazi wako ndio wana wajibu na wewe
 
Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu
Kwa kumkomoa nawewe saidia ndugu wa mkeo...
 
Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu
Temana nae mtakuwa mnakutana misibani na kwenye vikao vya ukoo. Tafuta vyako jombaa dunia ya leo undugu umeshakwisha.
 
Shemeji yako anatowaaa yote kwa kaka yakoo..... Lazima Bro na yeye ampeee helaaaa yote...

Relax Broooo
 
Mtegemea cha ndugu hufa maskini.

Jamaa linamind kutokulelewa bila aibu 😂😂

Tafuta zako uache kupangia wengine matumizi ya hela zao.
 
Nadhani wadau hawajamuelewa ndugu mtoa mada au wameamua kuchanganya fikra hasi juu ya hoja ya mtoa mada.........

Sote tunafahamu hali na mifumo ya familia zetu.....kwa namna moja au nyingine sisi ni masikini na kuinuka kwetu basi lazima tujue kuwa Kuna watu waji sacrifice kwa namna moja au nyingine juu ya mafanikio yetu.............

Wakati mwingine wazazi huchangisha fedha za ada kutoka kwa ndugu na jamaa pasi na wewe kujua ili ufike mbali na utimize ndoto zako......hatupaswi kuona kuona kuwa hapo tulipo Leo kumetokea tu la hasha bali kwa juhudi za watu wengi na wengine hata hatuwajui.........

Tunafahamu kuwa hatuwezi kuwalipa fadhila wote waliotia nguvu kwenye mafanikio yetu lakini tunaweza kulipa fadhila japo kwa kidogo tulicho jaaliwa........

Ni usaliti mkubwa sana na machungu kwa ndugu jamaa na marafiki kuona kuwa yule mtu ambaye walikuwa wanajitoa kwa ajili yake baada ya kufikia kilele Cha mafanikio amewageuzia mgongo........

Ni ukweli kuwa wakati mwingine ndugu na jamaa zetu ni wachoyo wa fadhila na wasio na shukrani lakini udhaifu haifai kuwa tiketi ya kuwapa mgongo watu wa jamii yako na kuwahudumia watu wa jamii zingine kwa sababu yoyote Ile...... Kumbuka damu ni nzito kuliko maji....na zimwi likujualo halikuli ukakwisha.....
 
Nilikuwa na rafiki yangu mmoja ambaye nafahamu familia yake jinsi ilivyochoka lakini mama na baba yake waliji sacrifice kwa ajili yake mpaka kuuza mali zao ili mtoto wao atimize ndoto yake..........

Kwa juhudi, bidii na maarifa akafanikiwa kufika chuo kikuu na huko ndiko alipokutana na mwanamke wa ndoto zake aliyemfanya awakatae ndugu zake Tena kwa majina kuwa ni washamba.....kwa kifupi walifanikiwa kufunga ndoa na yule Binti na waliishi maisha ya kujitenga na familia yake....walijaaliwa watoto wawili huku juhudi zake akizielekeza kwa mashemeji......alikuja kupatwa na stroke iliyomsumbua sana.....mke na ndugu wa mume walimnyanyasa sana ikabidi waende wakamchukue na mpaka leo yupo kijijini kwao anatunzwa na mtoto wa mdogo wake.......
 
Katika maisha kosea vyote ila sio kuoa. Huyu kaka etu ana roho ya uchuro yani sisi wadogo zake tumbo moja tukiwa na shida ya kifedha jibu lake atasema Sina pesa ukibahatika sana basi utapewa nusu tu au unapewa kwa masimango lakini ndugu zake mke wake anawajali anacheka nao kila shida anawasaidia.

Mama mkubwa ametuambia karogwa na mke wake sisi kama ndugu tutafute mganga tumnasue maana huenda kapewa rimbwata. Huwezi sahau nyumbani kwenu ukawa unatunza watu ambao sio nduguzo, kwanini Hao watoto wasipewe hela na ndugu zao huko halafu waje kwa kaka etu kuwa ombaomba, kila nikienda kumsalimia broo nawakuta wapo, kila rikizo za shule na vyuo wakifunga wanaenda kwa broo.

Halafu utasikia shemeji shemeji, shemeji ya minyoko. Kuna siku miaka mitatu nyuma nilikwazika kweli, niliomba pesa ya ada akasema hawezi nipa mkononi akaenda benki akalipia, ila ndugu wa mke wake akitaka pesa ya Ada anampa cash in hand ila mimi haniamini. Binafsi nimeacha hata kwenda kumsalimia ila ipo siku atanikumbuka tu
Na wewe nenda kwa mume wa dadako (shemeji yako) kadeke.
 
Back
Top Bottom