Kakosa Mume wa ndoto yake: Mdogo wangu wa mwisho kakosa mume kisa ana mtoto

Kakosa Mume wa ndoto yake: Mdogo wangu wa mwisho kakosa mume kisa ana mtoto

Wanaume kuna wakati mnashangaza sana. Unakuta mtu anasema hawezi kuoa single mama…. Hebu tuambieni kipi bora kuoa single mama ambae Yes alikosea but katunza mimba Kazaa mtoto na sasa ametulia Kajifunza kutokana na makosa AU bora kuoa binti alie bwia ma contraception hadi kizazi kimepinda au katoa mimba mpka kizazi kina makunyanzi utamuoa hata msipate mtoto? Kipi bora???
Wengi humu ni wazazi wa mabinti na wazazi watarajiwa unajuaje binti yako hata zaa kabla ya ndoa? Je vijana wakija kuonyesha interest utawaambia usimuoe binti yangu ni single maza?
Wangapi humu ni zao la single maza? Hivi mnavyo andika humu ndivyo mnavyoangalia mama zenu kua huyu Hana thamani ni single maza?
Na mshawahi kujiuliza anaempa binti mimba akamuacha yeye akaenda kuoa a fresh girl (as you think) is he not as guilty as well ???
Natamani ifike mahala jamii yetu isimnyooshee binti kidole kisa ni single mom bali tujikite pia kwenye kuongea na vijana wetu as they are also “single dads” na kuna mabinti pia hawatataka single dads kwa kuogopa pia baby mama dramas so it goes both ways!!!
Single mamas sio shida kikubwa jiridhishe kwamba ametulia na anajiheshimu hata Kama baba mtoto yupo kwenye picha, kuliko kuoa binti ambae anabwia ma P2 kila mwezi na Maria Stopes Ana Loyalty card!

Disclaimer: Read this with an open mind maana mtahisi ni maoni ya single mom which is quite the opposite [emoji3577]
Hapana jamii iendelee hivi hivi kuwanyooshea vidole ili mabinti wasiozaa wapate ari zaidi ya kujitunza kwa kutambua thamani yao kama wanawake. Kazi ya kuwasimanga Single mothers iendelee kwa kweli.
 
Mtoa mada kasema kuwa, yule mwamba amehoji.

Huyu mwanamke aliyezaa nje ya ndoa(ingawa anasema ilikuwa bahati mbaya) atawahusiaje wanawe na wao wasizae nje ya ndoa? kuwa aje awahusie pindi wakiwa wanazini kabla ya ndoa wawe makini wasipate mimba?.

Hizi hoja za yule mwamba ni nzito zinahitaji majibu.

Tupatieni majibu ya hizi hoja kwanza.
Kabisa,sio wanarukaruka kama bisi Tu hapa
 
Mara nyingi getting in trouble is not an issue the issue is how you get out of trouble,learn from it and move on.
Trust me anaweza kutumia mfano wake kuonya wanae na maisha yakaendelea.
Na malezi mazuri hayaangalii historia ya mzazi kuna wazazi ambao hawakua single mothers/fathers lakini ndio wanamalezi mabovu na watoto wenye kila tabia mbovu.
Unataka kuniambia mashoga baba zao walikua mashoga??? Mzazi ni sehemu tu ya malezi ya mtoto, dunia pia ina nafasi yake ambayo mzazi hawezi kuzuia! So hoja ya jamaa haina mashiko
I am sure unamifano kibao ya familia ambazo ziko vizuri Ila watoto wako hovyo.
Hii ni ishu ya Probability chance. Kinachoangaliwa ni je,kipi kina uwezekano mkubwa zaidi wa kutokea?. Kati ya Mzazi wa hovyo kulea watoto hovyo au Mzazi muadilifu kulea watoto hovyo au Mzazi wa hovyo kulea watoto waadilifu au Mzazi muadilifu kulea watoto hovyo?
 
Uwezi amini jamani, nina mdogo wa mwisho anamika 27 miaka mitano iliyopita alipata mtoto wa kiume. Ila aliyempa ujauzito baadae alioa mwanamke mwingine.

Mwaka jana mwezi wa 8 alimpata kaka mmoja hivi ni mzuri sana na anamaisha yake. Mimi nilimpenda sana yule kaka, mdogo wangu aliniambie huyu ndo mume anayemtaka japo hakumwambia mapema kuwa anamtoto tayari.

Ila mwezi uliopita yule kaka alimwambia kuwa anahitaji kumjua zaidi kuusu familia yake na mahusiano yake ya mwanzo kabla hawajafika deep relationship.

Mdogo wangu akasema sawa, mimi nilimwambia kuwa mwambie mapema kuwa unamtoto tayari, pia usimfiche kuhusu uliyezaa nae mwambie tuu mahusiano yashakufa na tayari yeye anamke tayari. Mwembie mtoto wako hataaribu mahusiano yenu. Pia amwambie tuu kuwa haukupanga kuwa na mtoto ilitokea tuu.

Sasa wiki iliyopita alimwambie kuwa yeye tayari anamtoto, na aliyezaa nae yani Baba mtoto hana mahusiano nae wamebaki kuhudumia tuu mtoto na kuwasiliana kuhusu mtoto tu.

Baada ya kumwambia hivyo yule kaka jamani, jioni yake hakuwa anajibu hata sms , hata akimpigia anamwambia yuko busy. Alimfanyi hivyo kama siku 4 hivi.

Sasa juzi wamekutana yule kaka jamani akamwambia kuwa wewe tayari unamtoto nje. Mimi nataka kuwa na mwanamke ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu wa ndoa peke yake.

Nilishangaa sana alimwambie kuwa kama unamtoto tayari tutawafundisha nini watoto wetu kuwa usizae kabla ya ndoa angali wewe tayari unamtoto kabla ya ndoa.

Huo ujasiri utautoa wapi. Lakini pia hata kuwaambia watoto usizini angalie wewe mama ushazini tayari.
Mawasiliano na baba mtoto yakizidi je mimi nitafanya nini. Mdogo wangu ameniambie hivyo.

Nimeshangaa sana jamani,

Hivi nyie wanaume mtoto anatatizo gani jamani. Kwani atazuia ndoa yenu isiwe na furaha jamani.

Kwa nini inakuwa ngumu kwenu kuoa mwanamke ambaye anamtoto tayari.

ACHENI UCHOYO NA ROHO MBAYA.
Sio uchoy na roho mbaya. Acheni zinaa, ukifanya zinaa tegemea mimba, acheni zinaa sbr mfunge ndoa.
 
Uwezi amini jamani, nina mdogo wa mwisho anamika 27 miaka mitano iliyopita alipata mtoto wa kiume. Ila aliyempa ujauzito baadae alioa mwanamke mwingine.

Mwaka jana mwezi wa 8 alimpata kaka mmoja hivi ni mzuri sana na anamaisha yake. Mimi nilimpenda sana yule kaka, mdogo wangu aliniambie huyu ndo mume anayemtaka japo hakumwambia mapema kuwa anamtoto tayari.

Ila mwezi uliopita yule kaka alimwambia kuwa anahitaji kumjua zaidi kuusu familia yake na mahusiano yake ya mwanzo kabla hawajafika deep relationship.

Mdogo wangu akasema sawa, mimi nilimwambia kuwa mwambie mapema kuwa unamtoto tayari, pia usimfiche kuhusu uliyezaa nae mwambie tuu mahusiano yashakufa na tayari yeye anamke tayari. Mwembie mtoto wako hataaribu mahusiano yenu. Pia amwambie tuu kuwa haukupanga kuwa na mtoto ilitokea tuu.

Sasa wiki iliyopita alimwambie kuwa yeye tayari anamtoto, na aliyezaa nae yani Baba mtoto hana mahusiano nae wamebaki kuhudumia tuu mtoto na kuwasiliana kuhusu mtoto tu.

Baada ya kumwambia hivyo yule kaka jamani, jioni yake hakuwa anajibu hata sms , hata akimpigia anamwambia yuko busy. Alimfanyi hivyo kama siku 4 hivi.

Sasa juzi wamekutana yule kaka jamani akamwambia kuwa wewe tayari unamtoto nje. Mimi nataka kuwa na mwanamke ambaye tutakuwa na watoto wetu tuu wa ndoa peke yake.

Nilishangaa sana alimwambie kuwa kama unamtoto tayari tutawafundisha nini watoto wetu kuwa usizae kabla ya ndoa angali wewe tayari unamtoto kabla ya ndoa.

Huo ujasiri utautoa wapi. Lakini pia hata kuwaambia watoto usizini angalie wewe mama ushazini tayari.
Mawasiliano na baba mtoto yakizidi je mimi nitafanya nini. Mdogo wangu ameniambie hivyo.

Nimeshangaa sana jamani,

Hivi nyie wanaume mtoto anatatizo gani jamani. Kwani atazuia ndoa yenu isiwe na furaha jamani.

Kwa nini inakuwa ngumu kwenu kuoa mwanamke ambaye anamtoto tayari.

ACHENI UCHOYO NA ROHO MBAYA.
Janiffer, kua mkweli kama.ni wewe unakubali kuolewa na mwanaume tyr ana mtoto ? Ukijua kabisa akishakuoa yule mtoto mtakua mnaish nae nyumba moja ??
 
Na hiyo ni haki yako, huhitaji hata kui justify kwa kutoa sababu za kimantiki, huhitaji sababu, ni upendeleo wako tu.

Sasa mtu akija na kukusema kwa hilo, atakuwa anakunyanyapaa tu katika kitu ambacho unakifanya kwa kutumia haki yako kabisa.

Hawa wanawake wanaolazimisha kupendwa na wanaume ambao hawawataki mimi nawaona wako desperate kupendwa.

Kupendwa hakulazimishwi.

Mwanamke mwenye uzuri wake anayejitambua atapendwa tu mwanamme anayependa mwanamke wa kumfaa.

Wanawake wasiwanyanyapae wanaume kwa sababu wanaume hawajawapenda. That is being desperate.

Wanashindwaje kuelewa suala basic kabisa kama vile mapenzi hayalazimishwi?
Hawawezi kuelewa kama wanareason kwa hisia badala ya uhalisia
 
Kiwanja tayari Kina risk kubwa ya kuwa na Migogoro..!

Aongeze Maombi.. !

Mara nyingi Singo Maza huolewa na Wanaofanana nao yaani Singo Faza. Wote wakijaaliwa watoto Kwenye ndoa hawaanzii Moja Kuhesabu..!
Na tatizo la single mom wengi nao huwa hawataki au hawapendi kuolewa na single Dad! Hapo ndiyo mziki mnene unawasumbua!!
 
Kama ninyi wanawake mnavyokuwa wagumu kutuelewa kuanzia maisha ya chini ya kulala sakafuni na sisi ni ngumu kuwaelewa story ya kuwa na mtoto halafu mnasema ilikuwa ni bahati mbaya au hamkuwa mkijitambua.

Yaani wewe ulale na mtu usijui matokeo yake kweli kama sio kufanyana vilaza ni nini basi hapo?
 
Hii nguvu vijana tunayoitumia kuwashambulia warembo walio single maza tungeiwekkeza kuwashambulia na kuwakataaa CCM na kazi zao zote hii nchi tungekuwa zaidi ya Nchi za scandinavia
Aliyekwambia ugomvi wa vijana na CCM ni wakimahusiano ya kimapenzi na watoto wa nje ya ndoa ni nani?! Yaani unashindwa kutofautisha Siasa na Mapenzi.
 
Mwambie mdogo wako kwa hali na mali atafute wasukuma hawa jamaaa huwa hawajali kbs if u have child or children...napga mishe lake zone huwa naona masela ya kingosha yakpenda hayaangalii....sooo my advice is that

Mwambie atafute wasukuma tuu ...hilo swala dogo sn kwao
Kwahiyo unataka kusema wanaume wa kisukuma hawana akili timamu si ndio?! Ngoja waje hapa.
 
Legezeni masharti mtatuua.....iwe tu hakuna mawasiliano basi walau
Hamna kitu cha namna hiyo. Hivi vitu mnachukulia poa sana ila vina madhara makubwa sana upande wa mwanaume kwa baadae. Kama wewe unahisi ni sawa then kutana na mwanaume hana hata mia mbovu halafu anzisha nae mahusiano na awe na watoto wake amepata na mwanamke mwingine au wanawake wengine, then wewe na yeye mpate watoto wenu then uwalee wote kama wanao huku na wewe ukichangia 50% ya gharama kuwasomesha kuwalisha, kuwavalisha na matunzo mengine.
 
Hivi hili swala singo faza huwa haliwahusu eeh
Single father umewahi sikia wapi? Mwanamke unapoanzisha mahusiano kindezi then huyo mtoto ni project yako wewe by 90% utadirect wewe sio mwanaume.

Na mwanaume akiwa anapenda sana mtoto wake hadi akamchukua yeye hautamuona kwako wewe mwanamke labda akishakuwa mkubwa, ila mtoto atalelewa upande wao kwa bibi yake na hautasikia kuna mwanamke anapiga simu kwako kukwambia chochote so utakuwa free.
 
Mwanamke; Kama unataka kuolewa, peleka mtoto kwa baba yake (miaka mitano si mbaya), kama hamtaki kata mawasiliano nae kabisa mpambanie mtoto wako.

Katika mahusiano mapya usitoe historia yako ya mahusiano ya nyuma kwa bwana mpya, au sema kwa ufupi sio unamwambia kuwa mpaka hapo yeye ni mwanaume wa 7 kwako ndani ya mwaka mmoja!

Kuwa makini, epuka kutapeliwa
Ni saba sio mitano. Mtoto anatakiwa kwenda kwa baba yake kuanzia miaka 7 kuendelea.
 
Mdogo wako alichumbiwa na mvulana na ametoswa kisa kazaa.

Mwambie tu mdogo wako aache kufukuzia wavulana maana hawana moyo wa kuishi na mwanamke aliyezaa.

Mwambie afukuzie wanaume watu wazima wenye akili hao huwa hawamkatai mwanamke eti kisa ana mtoto.
Mwanaume anaposimamia maslahi yake anaitwa mvulana, sijui utoto hajakua, mara hajitambui, au hawezi majukumu yaani maneno kadha wa kadha ili mradi tu kuprove nadharia kuwa mwanaume anatakiwa kubeba mizigo ya mwanamke hata kama haimhusu, huu ni upuuzi wa kihistoria ambao vijana wa sasa wanaukataa sababu wameshaona madhara yake.

Wanawake jamii imewafichia makucha sana especially maeneo ambayo wanakosea kwa makusudi na kujivika sura ya uhanga wa kusababishiwa kwamba haikuwa dhamira yao kukosea jambo ambalo si kweli.

Ukitaka uone makusudi ya watoto wa kike tazama hawa mabinti wa sasa age kuanzia 16 hadi 25 watazame matendo yao halafu jaribu kukaa nao chini uongee nao kuwapa nasaa na kukemea tabia zao. Kama sio kukuona una akili za kizee na kukijibu kwa kejeli na dharau basi watakaa kimya na kujifanya wamekuelewa kumbe moyoni na akilini ameshakupuuza.

Kuna binti alikuwa na miaka 21 anatoka na jamaa ana miaka 38 amejikoleza mbaya. Jamaa ameshazaa na wanawake watatu na kawatelekeza na watoto wao. Binti akaenda kuishi kabisa kwa jamaa eti anashindana na kuwakomesha wanawake waliokuwapo kimahusiano na mwanaume previously, kisa jamaa alikuwa kampangishia chumba akimlipia kodi na akamuweka katika duka lake auzee.

Tena mojawapo ya hao wadada alimfuata kwa busara kabisa kama mdogo wake akamwambia mdogo wangu mimi ni mkubwa sana kwako nakushauri kama dada yako nisikilize, achana na huyu mwanaume atakuharibia future yako wewe ni binti mdogo, tafuta mwenzako ambaye mtaweza jenga malengo pamoja na mtalewana huyu hakufai anakutumia tu sababu ya uzuri wako. Binti alimpuuza. Akaona wanamuonea gere, akaamua kujibebesha ujauzito wa jamaa as if mwenzake anashida na watoto zaidi.

Fast Forward leo hii, binti ana hali ngumu hawana maelewano na jamaa ananipigia simu na kunielezea tamthiria ya vituko anavyofanyiwa na jamaa na namna anajipanga sasa kutafuta mtu serious ili waanze mahusiano serious [emoji23][emoji23].

Mwingine nilikaa nae chini akiwa na miaka 21,ni mdogo wangu ambaye nasali nae jumuiya. Nilimsihi asije kuingia mahusiano na mume wa mtu au mtu mzima mwenye familia maana ndizo story alikuwa analeta sana. Aiseeee karudia huko huko tena. Nakuja mkuta ana mtoto amepata na kijana ambaye anafamilia yake ya watoto wawili na mke wa ndoa kabisa.

Sasa namtazama nasema huwa ni hamsikii au huwa mnataka kuona ladha ya ujinga kwenye matendo yenu. Sasa yupo busy kutafuta kazi ili alee mtoto mwenyewe,anajifanya amejutia sana maamuzi yake ya kupata mtoto na mwanaume wa mtu.

So mabinti huwa wanafanya kusudi wengi wao. Hizi mbaga za ilikuwa bahati mbaya sijui sikujua sijui nini na nini ni sound tu za kuficha uozo.
 
Mwanaume anaposimamia maslahi yake anaitwa mvulana, sijui utoto hajakua, mara hajitambui, au hawezi majukumu yaani maneno kadha wa kadha ili mradi tu kuprove nadharia kuwa mwanaume anatakiwa kubeba mizigo ya mwanamke hata kama haimhusu, huu ni upuuzi wa kihistoria ambao vijana wa sasa wanaukataa sababu wameshaona madhara yake.

Wanawake jamii imewafichia makucha sana especially maeneo ambayo wanakosea kwa makusudi na kujivika sura ya uhanga wa kusababishiwa kwamba haikuwa dhamira yao kukosea jambo ambalo si kweli.

Ukitaka uone makusudi ya watoto wa kike tazama hawa mabinti wa sasa age kuanzia 16 hadi 25 watazame matendo yao halafu jaribu kukaa nao chini uongee nao kuwapa nasaa na kukemea tabia zao. Kama sio kukuona una akili za kizee na kukijibu kwa kejeli na dharau basi watakaa kimya na kujifanya wamekuelewa kumbe moyoni na akilini ameshakupuuza.

Kuna binti alikuwa na miaka 21 anatoka na jamaa ana miaka 38 amejikoleza mbaya. Jamaa ameshazaa na wanawake watatu na kawatelekeza na watoto wao. Binti akaenda kuishi kibisa kwa jamaa eti anashindana na kuwakomesha wale wadada wenzake, kisa jamaa alikuwa kampangishia chumba akimlipia kodi na akamuweka katika duka lake auzee.

Tena mojawapo ya hao wadada alimfuata kwa busara kabisa kama mdogo wake akamwambia mdogo wangu mimi ni mkubwa sana kwako nakushauri kama dada yako nisikilize, achana na huyu mwanaume atakuharibia future yako wewe ni binti mdogo, tafuta mwenzako ambaye mtaweza jenga malengo pamoja na mtalewana huyu hakufai anakutumia tu sababu ya uzuri wako. Binti alimpuuza. Akaona wanamuonea gere, akaamua kujibebesha ujauzito wa jamaa as if mwenzake anashida na watoto zaidi.

Fast Forward leo hii, binti ana hali ngumu hawana maelewano na jamaa ananipigia simu na kunielezea tamthiria ya vituko anavyofanyiwa na jamaa na namna anajipanga sasa kutafuta mtu serious ili waanze mahusiano serious [emoji23][emoji23].

Mwingine nilikaa nae chini akiwa na miaka 21,ni mdogo wangu ambaye nasali nae jumuiya. Nilimsihi asije kuingia mahusiano na mume wa mtu au mtu mzima mwenye familia maana ndizo story alikuwa analeta sana. Aiseeee karudia huko huko tena. Nakuja mkuta ana mtoto amepata na kijana ambaye anafamilia yake ya watoto wawili na mke wa ndoa kabisa.

Sasa namtazama nasema huwa ni hamsikii au huwa mnataka kuona ladha ya ujinga kwenye matendo yenu. Sasa yupo busy kutafuta kazi ili alee mtoto mwenyewe,anajifanya amejutia sana maamuzi yake ya kupata mtoto na mwanaume wa mtu.

So mabinti huwa wanafanya kusudi wengi wao. Hizi mbaga za ilikuwa bahati mbaya sijui sikujua sijui nini na nini ni sound tu za kuficha uozo.
Umeeleweka mkuu, lakini sio sngle mther wte wanauhusiano na wazaz wa bba zao, wengne waliachana kwa karaha sana so hata comm hamna, wengne walishakabdh mtt upande wa baba so comm hamna, kwahyo sio single mother wote wanauhusiano na baba zao na pia sio wte walipata mimba kwa makusud,


Kuna wengine walianza relation pasipo hata kujielewa kama 15yrs au 16 yrs nalo ni tatzo ambalo linaplkea mtoto.
 
Kabisa, mke wangu alinikuta na mtoto mmoja. Sina mazoea ya kuwasiliana na mzazi mwenzangu, wakati mwingine hadi mwaka unaisha hatujawasiliana. Mtoto yupo kwangu sasa mke wangu atapata wasiwasi gani? Wanawake hawawezi tena walivyo na tamaa hawa watu.
Kama X tu akirejea na kibunda anamlainisha akili sembuse mwanaume ambaye amezaa nae mtoto. Unajua kuzaa na mwanaume sio jambo ndogo[emoji23],ndani ya nafsi yake kuna sauti inamwambia ulikabidhi uzazi wake kwa huyu mwanaume akakupa mbegu yake ukapata nae mtoto huyu ni baba mtoto wako yaani yeye anakumiliki wewe kama mama mtoto wake. So hata asipomwita kwa maswala ya uhusiano wao bado ana nguvu ya kumwita kwa nguvu ya jina la baba mtoto, atakataa?
 
Tena mojawapo ya hao wadada alimfuata kwa busara kabisa kama mdogo wake akamwambia mdogo wangu mimi ni mkubwa sana kwako nakushauri kama dada yako nisikilize, achana na huyu mwanaume
Ila unawalaumu zaidi wanawake lakini wanaowaribia future hao wanawake huwalamu 😂😂

Pamoja na hayo umesomeka
 
Back
Top Bottom