Kama ajira hazipo Kuna umuhimu wa vijana kwenda kwenye mafunzo JKT?

JKT HAIAJIRI
JWTZ HAITOI AJIRA
Kuna namna wanatakiwa kufanya na wakita kupunguza vijana wanaoingia jkt kutojiusisha na wizi mtaani wasifundishwe matumizi ya silaa uyo kijana natoka jkt anajua kufungua silaa yote na kuifunga upya anajua kulenga shabaa vyema huoni ni hatari?
 
Kuna namna wanatakiwa kufanya na wakita kupunguza vijana wanaoingia jkt kutojiusisha na wizi mtaani wasifundishwe matumizi ya silaa uyo kijana natoka jkt anajua kufungua silaa yote na kuifunga upya anajua kulenga shabaa vyema huoni ni hatari?
Kuzuia kutoa baadhi ya masomo wala haiwezi kua muarubaini
Muarubaini ni kutoa mafunzo ya kweli ya kizalendo yatakayowafanya askari kuishi kwa viapo vyao moyoni na akilini
Ujuzi wa silaha sio tu service man anaweza kuutumia vibaya hata askari aloandikishwa anaweza kukengeuka

Kikubwa ni kua na base nzuri ya uzalendo na kuipenda motherland
 
Kuna dogo mmoja ana ELIMU nzurii alipo potezewa muda enzi za Magu kurudi mtaan wenzake wamepiga A GREAT LEAP siku izi hapokei simuuu
 
Ukitaka kujua kama huwa wanadata waangalie wale suma jkt wakiwa limdo ndo utaelewa
 
Ni kweli inasikitisha sana. Kuna kijana mmoja nilimpambania akapata nafasi ya kwenda JKT. Dogo kapigika kule Cheetah kwa miaka 2. Juzi nakutana naye amepakizwa kwenye guta na mwenzie.

Kwa furaha namuuliza za siku afande, nikijua amerudi likizo ya mwisho wa mwaka. Naona respond ya dogo haipo kama nilivyomchangamkia na nimjuavyo.

Akaniambia mkataba umeisha na wamenirudisha nyumbani. Dogo nilimtoa kwenye bodaboda aende huko sasa amerudi na kuwa msaidizi wa rafiki yake muendesha guta aliyekuwa anapiga naye bodaboda kabla ya kwenda JKT.

Dah, iliniuma sana na nilitaka nilete uzi hapa kulalamika hilo. Wanamapotezea muda watoto wa watu. Waache huu ukuda.
 
Yupo mwingine aliniomba ushauri
Alikua anaweza kuunda silaha
Nkamsend 834 kaingia kafanya kozi mkataba unakarbia kuisha kila nkimpigania mibanga yangu haitoshi
Siku hizi hadi naogopa kupokea simu zake
 
Lakini kwa askari inawezekana sawa ila ni ngumu sana na sheria zipo wazi za jeshi kumuhukumu how service man kashatoboa mkataba kajiunga na majangiri unampataje? Utamuhukumu kwa sheria ya kiraia na sio ya kijeshi tena mkataba wake umeisha
 
Lakini kwa askari inawezekana sawa ila ni ngumu sana na sheria zipo wazi za jeshi kumuhukumu how service man kashatoboa mkataba kajiunga na majangiri unampataje? Utamuhukumu kwa sheria ya kiraia na sio ya kijeshi tena mkataba wake umeisha
Ni sahihi ndio maana vipo vyombo vingine vinavyochunga na kulinda nidham za raia na kutoa hukumu za kiraia
Ambazo so far nazo zina meno ya kumwajibisha Askar wa akiba kipindi akizingua
 
Kuna dogo mmoja ana ELIMU nzurii alipo potezewa muda enzi za Magu kurudi mtaan wenzake wamepiga A GREAT LEAP siku izi hapokei simuuu
Ana stress watu hawajui tu ukienda jkt unapoteza mawasiliano kabisa connection ile inapungua so unaporudi mtaani unalazimika iutafuta upya connection na inakuwa ngumu sna
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…