Kama alivyotuvusha kwenye janga la Corona, na hili la MAFUTA Magufuli angetuvusha!

Yote kwa yote tutakubaliana kuwa Magufuli angefanya maamuzi kuwasaidia watanzania wasiteseke na hii gharama za mafuta.
Hicho ni kivuli tu...economic recessions huwa hazina mbabe hata super powers huwa zinawakumba and they cannot mitigate kwa sababu myumbo/mdondoko wa uchumi huja na some unavoidable factors kama vita.... inayoendelea huko Ukraine. Ila sasa wabishi kuelewa kama wewe na kundi la wenzio mtakuwa mkilaumu tu Serikali bila kufahamu kwamba msambazaji mkubwa wa mafuta duniani muda huu yupo kwenye vita. Kwa hiyo huyo Magufuli angewalipia nyie hayo mafuta? na kwa muda gani?!! kuna vitu msiwe mnajitoa akili.
 
Kwahiyo hujui kwamba Corona ndio iliyomsomba?
 
Hilo zee jizi liuwaji limeshakufa na halitarudi tena
 
Kumbuka kuna familia zinapoteza wapendwa wao kwa sababu ya kukithiri madawa ya kulevya.

Familia nyingi zinapoteza wapendwa wao kwa sababu ya miundombinu hafifu na huduma mbovu za umma.

Familia nyingi zinapoteza wapendwa wao kwa sababu ya mfumuko wa bei unaowaumiza sana wenye uwezo wa chini hadi kushindwa kugharamia chakula, dawa na huduma nyingine za msingi.

Umezifikiria?
 
Magu angetoa ruzuku kufidia kwa muda na ninaamini angeongea na Putin kama India na China tukanunua direct toka Russia... Hangaya hana uwezo huo... anaweza kutoa tu machozi kwa wimbo wa Christian Bella pale Chinangali sio kwa issue za masilahi mapana kwa nchi kama hili.

Kipindi chake ilipanda sukari tu...mijitu ikatoa povu kama imetiwa pilipili... sasa hivi kila kitu juu inasifia na kutetea... pumbavu kabisa
 
Kwaiyo baada ya kupanda Sukari aliiagizia Magunia kwa Magunia kutoka India sio au alifanyaje!

Sasa kama Sukari ilimshinda atayaweza Mafuta?
 
Magu alikuwa kiongozi haswa tukiweka mapungufu yake pembeni. Alitupenda watoto wake.

Nakuhakikishia asingeacha nchi nzima inalia vilio vya shida na yeye anakaa anatazama tu.
Alifanya nini...?😳😳, Unamjua magufuli wa kwenye magazeti wewe
 
Magufuli hayupo Chato, baba yetu yupo mioyoni mwa kila mtanzania.

Kipindi kama hiki uwa tunamkumbuka sana sababu ya uwezo wake wa kuchukua maamuzi ya kusaidia watu wa chini.
Tatizo huwa hamfuatilii Mambo,Belarus palikua na lock down!?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…