Kama Cloutus Chama tunayemwimba kwenye mpira wetu wa Bongo kwenye Timu yake ya Taifa hayupo hata reserve basi Ligi yetu ya Bongo ina walakini

Ni kichefuchefu kabisa mpira wa Bongo.

Ndiyo maana mimi baada ya kuutizama mpira wa hivi karibuni kati ya Mbumbumbu SC vs Vyura FC nili post hivi👇👇

 
Chama hajaitwa Kwasababu za kinidhamu na sio uwezo, aliitwa akachelewa ku report akapigwa chini sii vinginevyo
 
Juzi kati nilikuwa nasoma majina ya Wachezaji walioitwa kwenye Timu ya Taifa ya Zambia na Kocha Mkuu wa timu hiyo Bw. Micho. Nilistaajabu nilipoona jina la mchezaji na kiungo pendwa wa ligi yetu kutokuwemo kwenye orodha ya wachezaji wa timu hiyo.
Kocha wa Zambia, Micho, alimuondoa kwa hasira ile mara ya mwisho kwenye mechi za kirafiki kwa kuwa Chama alichelewa kuwasili. Kumbuka Simba ilicheza mechi Dodoma, baada ya siku hiyo ligi zilisimama. Chama alijitetea kwamba Dodoma hadi Dar kuna umbali, lakini Micho hakumwelewa. Rungu kama hilo lilimkuta pia Aubrey Chirwa wa Azam FC (ingawa ninyi mnamwita Obrey). Lakini kwa Chirwa ilikuwa ni uzembe maana alikuwa Dar akaachwa na ndege, na hata maafisa wa Azam walimlaumu. Kwa hiyo Chama na Chirwa waliitwa timu ya Zambia, ila Micho alichukulia kama wamefanya dharau
 
... inaonesha kuwa ni utovu wa nidhamu wa kutozingatia muda.Kwa hili naungana na kocha.
Hoja yako ilikuwa ni kwamba Chama hajaitwa kwa sababu ya kuwa na kiwango duni kulinganisha na walioitwa. Umeandika maelezo mengi na marefu kumbe haukufanya uchunguzi hata walau kidogo tu kwenye media za Zambia ili unapoanzisha thread uwe na uhakika na kile unachoripoti. Angalia sasa unavyohaha. Umehama kwenye kiwango duni umehamia kwenye nidhamu, ambayo haikuwa hoja yako na wala haukuitolea maelezo popote. Siku nyingine usikurupuke kuanzisha uzi kama hujui Kiingereza

 
Yote haya baada ya press ya Mo Dewji kuwa jamaa kashasaini
 
Atajifanya hajakuelewa
 
Mkuu,, kwenye inchi ya watu vipofu ikitokea mtu mwenye Jicho moja,,
huwa mfalme..
Chama nilishagunduwa muda mrefu hakuna kitu mle.
Wachezaji wengi wa Malawi,Zimbabwe, Zambia, Botswana, Mozambique, Congo,,Lesotho,Swaziland.. Ghana,Nigeria..
Dreams zao ni kucheza south Africa..
Na ukiona tupo nae huku Africa mashariki ,,elewa bado hajafikia viwango vya south Africa..
Tatizo bongo tuna overrate wachezaji wa nje,,na kuwapa mishahara minono,,huku tuki wa underrate wachezaji wetu wazawa kwa kuwapa mishahara kiduchu..
Pamoja na viwango vyao kufanana uwanjani..
 
Cha Arusha au Cha Tarime hiki kijani?
Yanga Chama anawaumaaaaaaaaa! Na vile mbinu yao ya kuwadanganya mashabiki imebuma wamebadilisha gia angan sahiz ni watu wa kuibua mara hili mara lile ila kiukweli,,, utopolo united mtapata tabu sana.
 
Huyu hajui anachokisema, chama c alichelewa mechi iliyopita alipoitwa kambani yeye na chirwa na micho akasema hadharan wameonyesha utovu wa nidham na hawahitaji tena?

Unaweza kuta huyu ni mchambuz wa soka lakin hajui chochote kuhusu hili
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…