Kama dunia inazunguka, kwanini miamba na milima haiporomoki? Na kwa nini bahari isimwage maji yake?

Kama dunia inazunguka, kwanini miamba na milima haiporomoki? Na kwa nini bahari isimwage maji yake?

Mkuu Seanherms,

Nielewe ndio wakati unaandika vitu potofu????

Ukisema density ya kitu haibadiliki watu wakakukosoa sema kwanza ulikosea katika maelezo yako halafu jirekebishe.

Usiseme "elewa ninachoongelea." Nielewe nini wakati umepotoka?

Anyhow, mass sio uzito, na mass ya kitu huweza kubadilika. Na density pia hubadilika.

Mkuu hakuna sehemu nimesema mass ni uzito...bali nilisema mass ni tungamo.Tena nikasema sina uhakika kwa hayo maneno mawili ya kiswahili pia nikasema uzito ni weight..Naomba uoneshe ni wapi nimepotosha itanisaidia mimi na wengine

Kuhusu mass kutokubadilika nimeeleza vizuzi kwenye hiyo comment pale juu kua kitu hicho hicho hakibadiliki mass lakin weight inabadilika..

Au labda wwe unasema kwa kitu hicho hicho mass itabadilika ukienda sehemu tfaut na duniani?

Mkuu Anheuser

Karibu
 
Last edited by a moderator:
ngoja niweke kifurushi nirudi kuanzia leo ntakua muumini wa huku
 
Kuna vitu vinanitatiza sana sijui ni sababu ya kutaka kujua kila kitu Mimi sio mtaalam wa Geography japo wakati nipo sekondari tu kwa nadharia na kuna concept inasema dunia huwa inazunguka au inajizungusha kwenye mhimili wake. Ila maswali ninayojiuliza inazunguka vipi? Na kwanini isifike kipindi leo tujione tupo upande huu kesho upande mwingine? au mwaka huu tupo upande huu mwaka kesho tupo upande mwingine.

Na pia pia kama inazunguka nilitegemea kwa hali ya kawaida kama unavyozungusha kitu chochote chenye maji kisicho na mfuniko maji yale yatamwagika lakini maji ya bahari mbona hayamwagiki? au ndio hiyo gravity? Na pia effect ya miamba na milima hainokeni labda kupomoka zaidi ya ile wanayosema plate movement kwenye Physical Geography.

Swali la msingi kama inazunguka Je, kwanini kila siku tunajiona tupo sehemu ileile?

Kwa nini usijiulize mbona huanguki?mimi nikushauri urudi darasani.
 
seanherms umefunguka vizuri kabisa japo naomba ufafanuzi hapo unaposema ulimwengu unafanana kila mahali, ukatoa mfano wa nyota, ni kweli kuwa popote utakapokuwa mpangilio wa nyota utauona vilevile, mi nadhani hii ni kwa sababu nyota nazo ziko.kwenye mwendo sambamba na dunia
Nashangazwa kuambiwa eti nyota ni zina ukubwa sawa au zaidi yadunia sasa universe inaishia wap kukiangalia nyota zote zile mbinguni
 
Gravity ya Jua ndio inafanya Dunia pamoja na sayari nyingine zote ziwe hapo zilipo. Ni gravitational force iliyonyuma ya vitu hivi. Hata jua liko hapo pamoja na nyota nyingine zote katika galaxy tuliyomo kwa mvuto (gravity) wa super massive blackhole katikati ya Milkyway.

Asante kwa elimu yako nzuri, hakika nimejua mambo magumu kwa wepesi, rabda km ningepataga mwalimu mzuri km wewe basi nisingekimbia physics. Samahani naomba unieleweshe juu ya galaxy na universe
 
Ivi kwamfano Gravity force ikipotea, na sayari zikajiachia... Huko chini zitakapokwenda, kuna mwisho? Kukoje?
Au mfano chombo kikitoka nje ya dunia, alaf kisiamue kwenda Kwenye sayari yoyote, bali kikaenda chini na kuziacha sayari juu.. Kule kitakapokwenda, je, kuna mwisho? Kukoje?
Naomba msaada wakuu
 
Asante kwa elimu yako nzuri, hakika nimejua mambo magumu kwa wepesi, rabda km ningepataga mwalimu mzuri km wewe basi nisingekimbia physics. Samahani naomba unieleweshe juu ya galaxy na universe

Shukrani tamadunimusic. Kuna mada kadhaa tofauti niliwahi kupost lakini hii ambayo kwa sasa ni closed topic kuhusu nyota na galaxies inaweza kuwa muafaka kwa ombi lako. Click hapa
 
Last edited by a moderator:
What will happen kama dunia ikipoteza force of gravity;je vitu vitangukia wapi

simple! chukua kitu kama jiwe au hata kipande cha chuma kufunge na kamba kisha shika upande mmoja anza kuzungusha kwa namna yoyote kwa muda halafu achia hiyo kamba! kitakachotokea ndivyo itakavyo tokea gravitation force itakapo potea! (ila haitakaa ipotee! labda dunia ipigwe na kimondo kikubwa kuizidi!)
 
Mkuu Mlaleo

Lakini mwisho wake hutua chini si eti eeh?

Gravity ya mwezin ni ndogo kiasi cha kumfanya mtu awe kama unyoya sasa sijui huo unyoya ukiachiwa mwezin unakuwa kwenye hali gani.
 
Last edited by a moderator:
Maswali mengine bwana, tusomage tu tujibu pepa maisha yaendelee
 
Kuongezea😛ia unapozidi kuiacha dunia maili nyingi pia gravity inapungua kias kitu kubadili muelekea yaan badala ya kuelekea duniani kinakuwa kinaelekea angahewa(free space).Mfano mtu aliye mwezini hawez kutembea sawa na aliye ardhini......Pia bila gravity maana yake hata mvua isingeshuka bali hata formation yake isingekuwepo na kama ni kunyesha ingenyesha kuelekea vile mvuke uendapo.Kuto kuhisi mnyongea...tutambue dunia inazunguka ktk mwendo kasi mkubwa lakini kutokana na ukuwa wa dunia mnyongea huo tunauona kuwa mdogo(tizama kusogea kwa kivuli cha kilichopo ardhini.Kumbuka dunia ipo ndani ya ulimwengu ambao unafanana Pande zote uangaliapo toka dunia na huenda ukazongwa na mawingu ama nyota usiku.Pia upo nje ya dunia walioko ndani tena tabaka la juu ni wale wachimba madini migodini...Upo ktk uso wa dunia na unasukumiwa hapo na iyo gravity..Ili kutoka inakupasa utumie kifaa chenye uwezo wa kukinzana na iyo nguvu mf ndege,roket nk.Naruhusu kukosolewa
 
Nashukuru kwa mwaliko Kituko

Kwenye Dunia kupoteza au kuongeza uzito, ni kweli yote mawili yanaendelea hata dakika hii. Labda cha msingi ni kipi kati ya matukio haya mawili yanafanyika kwa uwingi zaidi ya kingine na impact yake ni ipi eventually? Katika kupoteza uzito umegusia man made crafts ambazo hazirudi duniani (satellites, space shuttles etc). Impact yake katika Dunia kupungua uzito ni ndogo sana (negligible) lakini ni mojawapo ya matukio yanayopunguza uzito "technically". Lakini hii sio natural occuring hivyo haiwezi kuwa inaendelea tu yenyewe. Mimi ntaongezea katika frame yako hii.

Vipi kuhusu hydrogen inayopotelea angani kila siku? Hii ndio kubwa zaidi katika kupotea uzito kwa Dunia. Hewa hii iko ndani ya atmoshpere na inapenya nje na kupotelea nje yake. Of-course ikishatoka nje haiwezi kurudi. Kwa mwaka hydrogen inayopotea ni tani takribani laki moja kwa mwaka.

Katika kuongezeka uzito kuna vumbi linaloingia duniani kwa kiasi kikubwa sana kutoka nje ya atmosphere. Vumbi hili kisayansi ni part ya vimwondo kwa kuwa ni vitu vilivyo na asili ya nje vinaingia Duniani. Vumbi hili ni takribani tani elfu arobaini kwa mwaka.

Kwa factors hizi mbili kubwa Dunia inapoteza uzito zaidi ya kuongeza. Lakini hewa hii ya hydrogen ina ukomo hivyo ukiweka scenario kwamba imeendelea kupungua mpaka ikaisha. Dunia imekuwa nyepesi na haina hewa. Kwa upande mwingine vumbi linalogia duniani halina ukomo au litaendelea kuingia Duniani kwa kipindi kirefu sana hata baada ya hydrogen kupotelea huko outer space.

Lakini haya yote hayaleti msimamo wa asilimia mia wa situation ya dunia baada ya kipindi kirefu. Kuna unexpexted outside force (Mfano kimwondo kikubwa sana) ambayo inaweza ikabadili mwenendo wa factors hizi na mambo yakawa tofauti sana.
 
Back
Top Bottom