Kama haupo vizuri kiroho ni ngumu ku-run biashara kubwa

Kama haupo vizuri kiroho ni ngumu ku-run biashara kubwa

Mkuu huu mchango wako ni wa thamani sana...

Unajua ndio maana hata watu wanaogopa kuoa, sisi watu weusi tusipoangalia mbeleni wanaume hawatakuwa na nguvu yoyote kimaamuzi tuweni makini sana na zawadi ya maisha tuliyopewa.

Watu hawataki kujua nini chanzo cha hofu zao zinazowaambia wasioe, wanakubaliana nazo, wanasema bora liende, KATAA NDOA... Ndio wameona ni solution...
Nasisitiza KATAA NDOA
 
Wakuu ulimwengu wa biashara upo kiroho zaidi

Ukiachana na kuwa smart kichwani Ila inabidi uwe vizuri kiroho.

Nimefanya biashara kubwa nimejionea hili swala.

Don't hustle in vain nigga

Pray pray pray.
Ukiachana na kiroho pia inahitaji roho ngumu na ukauzu.
Roho ngumu na ukauzu unakuja kwa mfano uko na duka mtaani na jirani yako anakuja kukopa inabidi umchane aondoke mikono mitupu au ukimkopesha asiporudisha inabidi umfuate nyumbani kwake ukataifishe vitu vyake mbele ya mke wake na watoto.
Na roho ngumu nyingine ni pale umenunua mzigo na umeshajipigia hesabu faida yako itakayopatikana lakini ikatokea kwenye usafirishaji kila mahali unapigwa mkono usimame ili muyajenge na wakubwa sasa wakati mwingine inabidi utoke nduki ili kuilinda ile faida yako vinginevyo ukisema kila mtu umsikilize faida yote itaishia barabarani hii ni watu wachache sana wanaimudu
 
Kweli kuna mfanyakazi mwenzetu anafanya biashara ya mikopo ya kausha damu sasa ukienda kukopa pesa hakupi kwanza lazima akwambie ukae nje kwanza kama nusu saa ndiyo anatoka nje kukupa jibu, na jibu lake inategemea na nyota yako ina nguvu au haina nguvu.
Na ukikopa pesa ata elf kumi kuilipa ni ngumu unashangaa matatizo yanaongezeka.
Kausha damu anakufunga njia zote za kupata riziki, kama uliweka dhamana ya nyumba, inakwenda
 
Kuna jambo hapa niliseme, mtu kama Steve Jobs ndiye angekuwa tajiri namba moja duniani hata Bill Gates asingemfikia, ni kwamba walimzuia kiroho, lakini Steve Jobs ndiye angepaswa kuwa tajiri namba moja na hata sasa asingekosekana kwenye top3.
Mkuu hapa naomba utupe ufafanuzi kidogo, ni kwa jinsi gani walimzuia kiroho, na ni wakina nani walimzuia kiroho
 
Ukitaka nguvu ya kiroho ni lazima uwe na utaratibu wa kusoma biblia kila siku amka ata mara tatu kwa wiki usiku saa kumi kumshukuru Mungu omba rehema omba hitaji lako Mungu akutendee acha dhambi toa sadaka ya kupanda mbegu sadaka ya ujenzi,toa malimbuko toa zaka hivi ndio unavyoenda kupata utajiri
This is the way
 
Hamna asiyeamin aliyewahi kufanikiwa, wewe bado mdogo!!!!

Ni lazima iwe na vitu vya spiritual unavyoviamini, na hiii ni Siri ya Kila mafanikio.

Sio biashara TU, hata kudumu na cheo.

Hiyo nguvu ya Spiritual yaweza kuwa ya YESU au Kishetani
Mngoni kwema?
 
Mkuu hapa naomba utupe ufafanuzi kidogo, ni kwa jinsi gani walimzuia kiroho, na ni wakina nani

Ni kwamba kampuni ya Apple ilianzishwa na Jobs, Wozniak na Wayne.

Wayne akaja akamuuzia hisa zake Jobs, kwa hivyo Jobs akawa na karibia 45% ya umiliki wa Apple Inc, wakaendelea Steve kaenda kumchukua John Sculey nadhani kutoka Pepsi ili aje kusaidia kwenye mauzo, Sculey alipokuja Wakamfanyia figisu Jobs hadi wakamfukuza Apple, na Steve akauza hisa zake karibia zote.

Steve akaenda kuanzisha kampuni inaitwa NEXT, na akawekeza kwenye kampuni ya Animation inaitwa Pixar, sasa, NEXT ya Steve ikawa na Technology bora sana (ndio hiyo ilitumika kutengeza bidhaa kama ipod zilizopendwa sana).

Upande wa Apple wakati Jobs akiwa NEXT kampuni ya Apple ilianza kufilisika, ndio wakamfuata Steve wakainunua NEXT(Technology) wakamuajiri Steve kuwa C.E.O wa kulipwa mshahara wa kawaida...

Steve anakufa ana hisa hazizidi asilimia 1(1%) katika Apple.

Na ukumbuke wakati anaianzisha Apple alipouziwa hisa na Wayne alikuwa na zaidi ya 45% hisa za Apple.

Sasa chukua thamani ya Apple Inc leo alafu uangalie 45% ya thamani ya Apple ni lazima Steve angekuwa Top 3 na hata jina la Bill Gates lisingevuma sana.


Steve Jobs alikuwa na tabia kuwafokea wakati mwingine kujibizana na wafanyakazi wake, jambo hili naamini alikuwa na vita kubwa ya kiroho, hii ikichagizwa na upande wake mmoja kuwa ni muarabu.

Angekuwa mzungu mwenzao bila shaka asingeteseka vile.

Kuhusu nani alikuwa akimloga, naomba nisitaje mtu, ila baada ya kifo cha Steve Jobs, katika Interview moja Bill Gates anajigamba anasema maneno yanayofanana na haya "Steve Jobs alikuwa mchawi, ila mimi nilikuwa mchawi zaidi yake".
 
Wakuu ulimwengu wa biashara upo kiroho zaidi

Ukiachana na kuwa smart kichwani Ila inabidi uwe vizuri kiroho.

Nimefanya biashara kubwa nimejionea hili swala.

Don't hustle in vain nigga

Pray pray pray.
PRAY HARD, WORK SMART
 
1739908348893.png
 
Wachungaji wetu wanatuambia pray pray pray, ila wao wanakusanya sadaka zetu ndio hizo wanakula. Mbona wao wasi pray pray pray wakapata kila kitu?

Nyie matajiri acheni kutuongopea sisi tu pray wakati nyie mnaendelea kupiga hela kwa njia mnazozijua. Sisi tuna pray miaka nenda rudi ndio kwaanza umasikini unatuandama 😐
Kuna namna ya kuomba au kusali ni kama vile kuna namna ya kufanya kazi kwa mafanikio.
 
Ila haya mambo huwa ni siri mkuu hatujui na kule ulaya wanafanya matambiko gani kwenye biashara zao.
Ukifuatilia wale matajiri/wafanyabiashara wa kihindi/kiarabu kuna vitu huwa wanafanya ili kulinda biashara zao.
Kwa upande wa wale waarabu kils mwezi huwa wanaita mahustadh wanasoma dua kali kisha wanaandaa kitu kama hela au chakula/bites wanaenda kutoa sadaka sasa hizo dua zinakuwa zinapandana kila mwezi baada ya hapo anakuwa ameshajikinga yeye pamoja na biashara yake haingiliki kizembe ndio maana wachawi wanaogopa wafanyabiashara wakubwa huwa wanasumbua wachuuzi wadogowadogo
Kwamba kuamini kuna uhusiano gani na mafanikio? Vip ambao hawaamini ila wamefanikiwa pia ?
 
Back
Top Bottom