Kama hii ndiyo idadi ya CHADEMA kutoka mikoa kuja kwenye kesi ya Mbowe, basi chama kimepoteza mvuto kabisa

Kama hii ndiyo idadi ya CHADEMA kutoka mikoa kuja kwenye kesi ya Mbowe, basi chama kimepoteza mvuto kabisa

Sasa kama hako kakikundi kadooogooooo ka wanachadema kamelazimisha mahakama ihamie video conference, kama yangekuja mafuriko, basi kesi ingefutwa kabisaaaa!

Hebu nikurudishe 2020. Tundu Lissu alipokelewa na wanachadema kadhaa. Alipokwenda Dodoma kuchukua fomu, kulikuwa na watu wachache sana. Sasa Fast Forward alipofika Dodoma tena wakati wa kampeni. Uliona mtiti ule?
Kwanini? Ni kweli upinzani wana kazi kubwa saaaanaaa ya kuwaunganisha watanzania. Sisi sio kama Kenya. Wala sio kama Zambia. Watanzania wengi ni watii wa mamlaka. Lakini wanataka mabadiliko. Walishayakosa ndani ya ccm, wanayatafuta nje ya ccm. Hili ccm wanalijua, ndio maana hakuna uchaguzi halali Tanzania. Ila watanzania wanapoona hapa kuna uwezekano wa kuiweka kando ccm, wanajitokeza kwa wingi. Ndio maana Tundu Lissu alipata mafuriko ya watu siku za mwishoni wa kampeni. Na ndio maana ccm walianza kumwekea vikwazo kibao.
Kwa kufanikiwa huku, believe me, si wanachadema tu, bali watanzania wengi zaidi watampigania Mbowe. Na kama rais Samia anajitetea alikuwa kweli ana nia ya kukutana na wapinzani, "ratiba zikaingiliana", basi maana yake atalazimika kutafuta namna yakukutana nao
Unajipa moyo
 
Kwa wiki moja sasa Chadema walikuwa wakihamasishana kuhudhuria kwa wingi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wao Mbowe.

Kuanzia katibu mkuu wa chama John Mnyika alitokwa povu sana akiwaambia polisi liwalo na liwe maelfu ya wananchi watafurika mahakamani Kisutu siku ya tarehe 5, akaja John Pambalu mwenyekiti wa Bavicha Taifa naye akatishia nyau kuwa kuna maelfu ya wanachadema kutoka mikoa 5 watahudhuria kesi hiyo.

Leo wanachadema walioonekana wakiimba karibu na mahakama ya Kisutu hawajai hata kwenye kikanja!! Jirani yake wamachinga walikuwa wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

View attachment 1880704
Mnatishia kuua waandamanaji kupitia polisi halafu mnategemea mwitiko wa leo ndo uwe kipimo!

Acheni kutumia polisi kutishia watu maisha ndio mpime uungwaji mkono wa CHADEMA.
 
Kipind CDM wananguvu kubwa Katibu mkuu alikuwa Dr. Wilbroad Slaaa na Naibu wake alikuwa Zitto Zuber Kabwe.

Leo Katibu mkuu wa CDM na Naibu wake wote wawili uwezo wao kisiasa hauufikii wala kuukaribia uwezo wa Zitto Zuber Kabwe .

Usije ukakufuru kumfananisha Mnyika na Dr. Slaa.

Maelezo hayo juu ndio kiini cha hali ya uungwaji mkono wa watanzania Kwa CDM wakat ule na sasa.
Dhambi ya kubadili gia angani inawatesa
 
Kwa wiki moja sasa Chadema walikuwa wakihamasishana kuhudhuria kwa wingi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wao Mbowe.

Kuanzia katibu mkuu wa chama John Mnyika alitokwa povu sana akiwaambia polisi liwalo na liwe maelfu ya wananchi watafurika mahakamani Kisutu siku ya tarehe 5, akaja John Pambalu mwenyekiti wa Bavicha Taifa naye akatishia nyau kuwa kuna maelfu ya wanachadema kutoka mikoa 5 watahudhuria kesi hiyo.

Leo wanachadema walioonekana wakiimba karibu na mahakama ya Kisutu hawajai hata kwenye kikanja!! Jirani yake wamachinga walikuwa wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

View attachment 1880704
Wewe ulitaka wafike mahakamani au wasifike?
 
People need money not words.. Nani atakutatulia shida zako ukiwa huna hela Kisha unautumia huo muda kuandamana..?
Hao viongozi yakiwapata wanapitisha bakuli uwachangie! Sio ccm sio chadema they are all need money ndo maana tunawekewa mitozo ya kila namna so chagua ukasikilize kesi au utafute hela.
Wenzako wako kazini kuingiza pesa na kusaidia familia zao, wewe unaamka asubuhi kwenda mahakamani kupigwa kama siyo umsukule ni nini
 
Lengo lako la kutaka wanasiasa wanaoangalia masilahi ya wananchi kwanza kupitia upinzani kwa kweli bado halijatimia... i mean kwa sasa hakuna mpinzani wa aina hiyo hapa Tanzania. Shibodo aliwahi kuifadhili chadema kwa kuipa mabilioni ya shilingi kwa ajili ya kujenga au kuboresha ofisi za chama hicho nchi nzima na zingine wachimbishe vizima kwa ajili ya wananchi mbali mbali katika majimbo wanayoyasimamia. Ila kilichofanyika ni tofauti na alivyotarajia mfadhili wao. Mbowe alichukua yale mabilioni akaenda kuyaficha nje ya nchi na zilizobaki alienda kula bata na familia yake Dubai bila kuzuga japo kwa kupaka rangi ili kumhadaa mfadhili. Lkn kama hiyo haitoshi kila mwezi alikuwa anajilipa mamilioni ya shilingi kupitia ruzuku ya chama kwa kisingizio cha kujilipa madeni huku akiwaacha viongozi wa kwenye mashina ya chama wakifanya kazi ya kukitangaza chama bila mshahara, hapo hatujazungumzia mamilioni ya michango ya wabunge waliyochanga kwa miaka mi5, na ile waliyokuwa wanachangisha katika mikutano yao kipindi cha uchaguzi mkuu. Kifupi kama kweli jamaa wana uchungu na wananchi kama walivyotumia udhaifu wako kukudanganya basi Mbowe na genge lake wangejiuzulu kwa kukubali kupokea hao unaoita wanasiasa njaa na mafisadi waingie ndani ya chama na kuwapitisha kugombea nafasi kubwa za uraisi nk adi kupelekea chama kushindwa kushinda, na kupoteza matumaini ya wanachama wengi kwa chama na uongozi kwa ujumla. Ukiona mtu ametoa boko na bado hataki kuachia nafasi yake basi jua ana masilahi nayo.
Shibodo hana uwezo wa kutoa mabilioni hayo unayozungumzia. Aidha, kwa vile hesabu za Chadema zinakaguliwa na CAG, yote hayo unayozungumzia yangeisha jitokeza zamani. Kilichobaki ni hadithi za mtaani zisizo na mbele na nyuma. Unapozungumzia largesse ya Chadema inabidi ilinganishwe na ya CCM. CCM ilikuwa na kitengo chake cha biashara, ambacho kilikuwa na supermarkets, miradi mikubwa ya kufuga kuku, hoteli n.k. Kwa vile wakati ule chama na serikali ilikuwa ni kitu kimoja, miradi yote hii ilifadhiliwa na wakaazi wote wa Tanzania. Hiyo miradi iko wapi? Wananchi walichangishwa pesa kibao ili kujenga viwanja vya michezo katika baadhi ya mikoa Tanzania, hali ya viwanja hivyo ikoje baada ya kukabidhiwa kwa CCM?
Badala ya kujiuzuru kwa kupokea wanasiasa njaa, wakina Mbowe wanastahili pongezi kwa kuwastukia mapema kabla hawajaleta madhara makubwa. Uamuzi wa kumpokea Lowassa ulikuwa strategic kwa sbabu alikuwa na mvuto kuliko Slaa na alikuja na watu ambao walisaidia Chadema kuongeza idadi ya wabunge na hivyo kuwapa nafasi ya chama kikuu cha upinzani na kupata ruzuku ambayo iliwawezesha kujijenga kwenye grassroots. Hao mnaotaka kutuaminisha kuwa ndio walikuwa na mapenzi makubwa na Chadema wameisha rudi walikotoka na kuwaacha wenye mapenzi hasa ya dhati katika chama. Ingekuwa kweli Chadema wamepoteza matumaini ya wanachama wake wengi msingefanya juhudi mliyofanya kuhakikisha kuwa hawashindi katika chaguzi zote zilizofanyika wakati wa awamu ya tano. Ni aibu na fedheha kuona wasimamizi wa chaguzi wakijificha kutoka kwa wagombea, wakifunga ofisi zao ili wagombea wasirudishe fomu, wakipokea fomu kutoka kwa wagombea ambao hawakutumwa na chama wanachodai wanawakilisha. Na mwisho ni hii ya kupindisha taratibu na kulazimisha kuwepo kwa "wabunge" wanaowakilisha chama kilichowafukuza. Mambo yote hayo yanafanywa na chama ambacho kinadai asilimia zaid ya 90 ya wananchi wanakiunga mkono! Seriously?

Amandla...
 
Wanaelimisha nini kwa hizo purukushani zao na serikali? mimi sijataka wapoe au wawe wamoto bali watumie akili ili wajue wakati gani ufanye kitu gani na kwa vp ili upate unachokipigania na sio wakati wote kuingia kwenye purukushani na serikali ili usionekane umepoa et haki yako hujavunja.
tatizo la chadema wao wanajuwa kuwa kufungwa au kuleta fujo ndiyo kibali cha kuja kuwa madarakani kwa reference ya mandela lakini haakumbuki kuwa mandela hawawezi kujilinganisha naye mwenzaohakufanya vitu kihuni hivyo
 
Ndio hawa walitaka kukinukisha!!?
kama wasauzi....!!?
askari wangedaka mmoja wa mfano
wangevuta zivu na korodani
sidhani kama wangerudia huu mchezo wao wa kijinga jinga....
wanataka kutuharibia nchi tu
mama aheshimiwe.......
pira jingi linapigwa...
 
1628170839794.png

#UNCOUSIOUSLY FOLLOWERS WATU KAMA HAWA NI BORA WAKAIOMBA SEREKALI IWASAIDIE MAJEMBE WAKALIME KULIKO JINSI HII WANAVYOTUMIKISHWA PENGINE SI AJABU NA RUMANDE WAKAPELEKWA KWA KUTETEA MKATE WA WENGINE
 
CHADEMA WANATAKIWA WAJITAFAKARI WAANZE UPYA UPINZANI HAUENDI WANAVYOTAKA WAO HUO NI MFANO TU KUWA WAMESHAPOTEZA MVUTO NA USHAWISHI KWA WATANZANIA YAANI HATA ASILIMIA MOJA YA WATANZANIA HAWASAPOTI WANAYOYAFANYA WATU WACHACHE HIVYO NDIYO WANAPONGEZANA ETI WAMEFIKA ? NI UTOTO WA HALI YA JUU SANA HUO
Tumia hata robo ya akili kujua kuwa vitisho vya polisi ccm vinakiuka haki za binadamu.
 
Kwa wiki moja sasa Chadema walikuwa wakihamasishana kuhudhuria kwa wingi kwenye kesi ya ugaidi inayomkabili mwenyekiti wao Mbowe.

Kuanzia katibu mkuu wa chama John Mnyika alitokwa povu sana akiwaambia polisi liwalo na liwe maelfu ya wananchi watafurika mahakamani Kisutu siku ya tarehe 5, akaja John Pambalu mwenyekiti wa Bavicha Taifa naye akatishia nyau kuwa kuna maelfu ya wanachadema kutoka mikoa 5 watahudhuria kesi hiyo.

Leo wanachadema walioonekana wakiimba karibu na mahakama ya Kisutu hawajai hata kwenye kikanja!! Jirani yake wamachinga walikuwa wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

View attachment 1880704
😁😁😁😁 We unachekesha kweli WAKATI polisi wanatembeza virungu na matamko ya kutisha kibao🤣🤣🤣🤣
 
Kumbuka hata hao tulipiga kelele sana tu kuwa serikali dhalimu na taasisi zake zilikuwa zikibambikiza kesi.

Hata hii ni moja wapo.

Kumbuka Mbowe kesha shitakiwa kesi ngapi hadi leo. Haijawahi kutiwa hatiani hata katika moja ya hizo.

Bado haikifikirishi tu?

Subiri uone hata hii itakavyo kwisha.

Committing a crime is one thing and being convicted of the crime is quite another!
 
Back
Top Bottom