Kama hujawahi kukutana na usumbufu, dharau na jeuri za watumishi wa serikali, utaendelea kutoona anachofanya Makonda

Kama hujawahi kukutana na usumbufu, dharau na jeuri za watumishi wa serikali, utaendelea kutoona anachofanya Makonda

Ukweli ni kwamba yawezekana Makonda ana mapungufu yake kama mwanadamu mwingine yeyote. Lakini kwa kero za nyingi ya ofisini za uma hasa unapokuwa unahitaji huduma yenye viashiria vya maslahi, utazungushwa na kusumbuliwa kwa vitu vidogo sana, unapoteza muda, gharama ya fedha na gharama zingine nyingi.

Kusema kweli kuna wakati mjane mmoja alikuwa anafuatilia mirathi ya mme wake yaani amekamilisha kila kielelezo kinachotakiwa lakini ilimchukua miaka 3 kupata hiyo hela huku akienda maofisini kila wiki.

Kuna wakati unawaza kama bunduki zingekuwa zinauzwa kiholela basi wengi wa watumishi wa umma wangesha kula chuma.

Yawezekana approach ya Makonda sio nzuri kama ndivyo lakini naomba tunapomkosoa tuje na majawabu ya kuondoa hizi dharau za watumishi wa umma kwa watu ambao kimsingi ndio mabosi wao.
Bila kubadili kazi kuwa za mikataba Watumishi wa Umma wataendelea kuzingua sana.

Private sector hakuna job security so upuuzi haupo.

Mwisho mama alikuja na wazo la kukopesha Wakuu wote wa taasisi magari Kwa Mishahara Yao na kuwa wanawapa Mafuta ya kupimiana kama Wabunge likaishia hewani.

Pia alikuja na wazo mtu akitumbuliwa arudhishwe kwenye Cheo na salary ya awali ila nalo likaishia hewani hivyo hivyo.

Naamini akija Rais mwingine hili litafanyiwa kazi maana waliotangulia wamezingua.
 
Bila kubadili kazi kuwa za mikataba Watumishi wa Umma wataendelea kuzingua sana.

Private sector hakuna job security so upuuzi haupo.

Mwisho mama alikuja na wazo la kukopesha Wakuu wote wa taasisi magari Kwa Mishahara Yao na kuwa wanawapa Mafuta ya kupimiana kama Wabunge likaishia hewani.

Pia alikuja na wazo mtu akitumbuliwa arudhishwe kwenye Cheo na salary ya awali ila nalo likaishia hewani hivyo hivyo.

Naamini akija Rais mwingine hili litafanyiwa kazi maana waliotangulia wamezingua.
Swadakta. Huo 👆 👆 👆 ndo mwarobaini halisi lakini wahusika kwa maksudi na kwa manufaa yao binafsi, waliupiga dana dana, waliunyamazisha na hawata kaa waukubali kwani wanajua utakuwa ni mchungu mno kwao haumezeki yan.
 
Watumishi wengi wa umma ni tatizo kubwa sana, ila wanapobinywa wanakimbilia kuomba huruma za umma.

Wengi ndio wanalitia hasara Taifa na kuumiza watu ambao hawawahusu ili wao wapate kuishi vizuri na familia zao.

Hili Taifa linahitaji ukombozi na mabadiriko makubwa sana ya mifumo.
 
Kama hakuna kitu amefanya kwanini mnampigia kelele aache anachofanya?
Watu (esp. Watumishi na wafanyabiashara) kelele wanazompigia ndo wanampigia promo na kumpandishia munkari. Atawabutua kweli kweli. Bora wangekaa kimya.
 
Back
Top Bottom