Kama huna fikra za kikandamizaji, hauwezi kuishadadia Urusi

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2011
Posts
21,470
Reaction score
40,593
Kama huamini kwamba Kiongozi anatakiwa kuabudiwa, hauwezi kuishadadia Urusi. Kama wewe unaamini kila mtu ana haki ya kuelezea hisia zake bila ya kutishwa na dola, huwezi kuishabikia Urusi.

Kama unataka Kiongozi akiwa madarakani asitumie madaraka hayo kujitajirisha, wewe na Urusi hamfanani. Kama unapenda demokrasia duniani, kaa mbali na Urusi. Kama unachukia viongozi Katili, jitenge na Urusi.

Kama siyo tabia yako kupenda wanasiasa wanaopenda rushwa na wanaozuia kukamatwa, iache Urusi ikae mbali na wewe.
 
Sikujua kama wewe ni mjinga kiasi hiki
 
Kuliko kumtetea rais kama huyu wa ukeaine kwenye picha acha tu niendelee kumtetea mrusi
 
Mwamposa:"Demokrasia ni sawa sawa na devil gasia
 
Mwamposa:"Demokrasia ni sawa sawa na devil gasia
Na yeye anatajirika kama matajiri wa Urusi. Anauza maji lakini halipi kodi kwa biashara ya maji na mafuta anayofanya. Biblia inasema, mmepewa bure toeni bure. CCM wanafaidika kwa dozi ya Ganzi anayotoa Mwamposa kwa watanzania ambao wametupwa nje na mfumo wa Afya nchini.
 
Ahaaaaaaa
 
Kwahiyo anakula pamoja na CCM!?
 
Watu tumelishwa matango pori kua marekani pekee ndio anademokrasia wengine wote hawana.Kunaambo mengi ya ajabu sana huko marekani ambayo nikinyume na haki za binadamu na demokrasia kwa ujumla.
 
Watu tumelishwa matango pori kua marekani pekee ndio anademokrasia wengine wote hawana.Kunaambo mengi ya ajabu sana huko marekani ambayo nikinyume na haki za binadamu na demokrasia kwa ujumla.
Kama jambo gani kwa mfano. Kwa kulinganisha uhuru wa Raia Marekani na Urusi, Marekani ni kama mbinguni kwa warusi.
 
Mkuu nakupinga, hayo maswala ya haki haki ndo yanasabisha kuenea kwa ushoga na pia wanawake wanapewa kichwa kujiona wako sawa na wanaume,
Kuna mahali nimeuliza kwamba Sodoma na Gomora ushoga ulienezwa na Marekani?? Hoja hapa ni kwamba ili uikubali urusi ni lazima uwe na chembe chembe za kupenda kukandamiza wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…