Kama ilipo Israel siyo Israel, Wayahudi wanaotajwa kwenye Quran na Biblia walikuwa wanaishi wapi?

Kama ilipo Israel siyo Israel, Wayahudi wanaotajwa kwenye Quran na Biblia walikuwa wanaishi wapi?

Nimesema kimantiki Kwa muktadha wa hoja yako. Kama umesema ukristo ndiyo dini maarufu duniani. Bila shaka kitabu chake hunukuliwa zaidi kutokana na ubora na udhaifu wake.

Ndiyo maana nauliza vitabu vingine kama Quran siyo hadithi za kutungwa?
Mkuu naliona tatizo hapa, Inamaanisha hii hukuisoma?

Screenshot_20241228-132107~2.png

Hilo neno kila dini hukuliona, Mbona unauliza nilichojibu tayari?
 
Mkuu naliona tatizo hapa, Inamaanisha hii hukuisoma?

View attachment 3186923

Kwa MTAZAMO WANGU HAKUNA TATIZO.
Hapo si tumeshatoka? Ulisema dini zote ni hadithi za kutungwa. Nikakukubalia.

Swali langu likawa kama ni dini zote ni hadithi za kutungwa ni kwa nini Biblia ndiyo inayoongoza kwa kununuliwa, ukasema Kwa kuwa ukristo ni dini maarufu duniani.

Mimi nikakuuluza ni maarufu kuliko ubudha au uislamu? Maana sioni kama vitabu vya dini hizo vikinukuliwa Sana kuonesha kuwa dini ni hadithi za kutungwa.

Ndipo nikakuuliza Quran nayo ni hadithi za kutungwa?
 
Kwa MTAZAMO WANGU HAKUNA TATIZO.
Hapo si tumeshatoka? Ulisema dini zote ni hadithi za kutungwa. Nikakukubalia.

Swali langu likawa kama ni dini zote ni hadithi za kutungwa ni kwa nini Biblia ndiyo inayoongoza kwa kununuliwa, ukasema Kwa kuwa ukristo ni dini maarufu duniani.

Mimi nikakuuluza ni maarufu kuliko ubudha au uislamu? Maana sioni kama vitabu vya dini hizo vikinukuliwa Sana kuonesha kuwa dini ni hadithi za kutungwa.

Ndipo nikakuuliza Quran nayo ni hadithi za kutungwa?
Kipi ambacho hukielewi hapo? Neno "kila" linamaanisha nini?
Screenshot_20241228-132908~2.png
 
Mayahudi hayana kwao
Sio Mayahudi ni WAYAHUDI wape heshima zao. Kiswahili ukishaweke prefix MA kabla ya neno linakuwa na sifa mbaya. Machaga, makurya, masukuma,manyaturu, maketewe,marangi, mangoni .. Na nimesoma kitabu fulani kinategemewa na dini fulani nacho kimeandika kwa dhihski hivyo hovyo
 
Sio waliondoka, walipateka kwa kigezo wametumwa na Mungu wao wakawapiga wakanaani na kuwahamisha kisha wakasema ni kwao.
Waliishi hapo kwa muda mrefu kisha nao wakavamiwa na kuhamishwa pakamilikiwa na wengine, wengine hao nao wakaja kupigwa pia kama ilivyo desturi ya mwenye nguvu mpishe.
Kihistoria wenye kudai lile eneo ni wakanaani ambao ndio wakwanza kupigwa na wayahudi.
Asili ya wayahudi ni Iraq ya leo ambapo Ibrahim babu wa wayahudi na wapalestina alipakimbia ndio maana nasema ikiwa kila jamii itataka irudi kwenye asili yake, basi tutauana wote tubaki wachache mwisho tujikute tunarudi pale mto Euphrate nchini Iraq kama isemavyo biblia.
Wewe unadhani kwanini sisi wabantu wa Tanzania tusitake kuwapiga wambuluee/wairaq na kuwataka warudi kwao Iraq?
Au unadhani kwanini wambulu wasirudi kwao Iraq na kuiacha Tanzania yenye mandhari nzuri ambayo wameridhika nayo huku wakikubali kuishi na sisi tukichanganya vizazi?

Jibu litakuwa sisi sote tuna utu na tunajichukulia hapa duniani tumekutana tu hivyo tuishi kwa upendo bila kubaguana.
We mwamba umeingea point sana.Tena umenyoosha ukweli halisi bila kuegemea upande.Ndo mtu wa kwanza kuiona anaongea ukweli huu humu.Chukua maua yako
 
Wapalestina sio wafilisti, wafilisti ni wazungu mostly toka Ugiriki na Italy, wapalestina ndio descendant wa Daud,

Na mkuu kujua zaidi hili kisayansi tafuta Ashkenaz yoyote msomi (sio hawa kina Netanyahu waliokimbia shule) then sikiliza lecture zao wengi huwa wanachambua hizi Dna.

Kuna proffesor Ashkenaz jew anaitwa Chomsky ni katika wasomi wakubwa Dunia yetu hii, ameelezea sana kuhusu Historia yao ya uashkenaz na taifa la Israel mcheki.

Pia kuna hii Tedtalks ya Nathaniel Ameelezea Vizuri Dna za wapalestina nae ni Ashkenaz

View: https://www.ted.com/talks/nathaniel_pearson_the_splendid_tapestry_how_dna_reveals_truths_ancient_lasting?subtitle=en

Acha uongo mzee.wafilisti=philistines=Palestine.Daudi hana nasaba ya Palestine(philistines or Palestine).Daudi ni muisrael.Ila ukweli ni huu.Ile nchi kwanza walikaa WA Palestine (wafilisti or philistines),wayebusi,waanaki,wahivi.Waisraeli walikuja wakawapora ardhi kwa mujibu wa maelekezo ya MUNGU wao.Wakaja warumi wakawatoa,wakaja tena WA Palestine (wafilisti or philistines).Baada ya vita vya pili waisrael wakarejea tena hapo kwa mkono wa muingereza.Hakuna ukweli mwingine wowote tofauti na huo.Vinginevyo ni uongo tu.Hizo DNA zimegunduliwa juzi juzi tu,hiyo mifupa halisi ya kina Yesu waliitoa wapi hadi wakaipima wakajua sio hawa wa leo?
Halafu unatakiwa utumie akili yako ya kuzaliwa sio mihemko tu isiyo na maana.Unasema hawa ni wazungu toka ulaya mashariki,mbona hakuna nchi hata moja duniani inayoongea kiebrania lugha ya biblia zikiwemo hata hizo za ulaya mashariki tofauti na Israeli ya sasa?Dunia nzima ni nchi moja tu inayoongea lugha ya kiebrania ambayo ndiyo lugha mama ya waisrael wa kwenye biblia ni hawa waisraeli wa sasa peke yao,na wanaofuata misingi ya torati kama waisraeli wa kale Dunia nzima ni hawahawa waisraeli wa leo,leo unawezaje kusema sio hawa kwa chuki zako tu dhidi yao?Na hizo chuki ndizo zinazodhihirisha kuwa hawa ni waisraeli wa kale kabisa,maana tangu wanafika hapo ni uhasama wa hali ya juu sana na majirani zao.Hawajawahi kuwa marafiki kasoro taifa la Saudia tu.Maana hao ni watoto wa Ismael,waliambiwa wasipigane nao maana MUNGU wao hakuwapa hiyo nchi.Hiyo nchi amewapa ndugu zao waismaeli.Ndiyo maana hadi leo Israeli hawezi kuitaka Saudia au kupigana na Saudia.
 
Kipi ambacho hukielewi hapo? Neno "kila" linamaanisha nini?
View attachment 3186927
Ninachotafuta ni uhakika maana ya kila siyo Kila. Maana ya kila ni vile tu avijuavyo mtu na siyo nje ya hapo.

Nikataka kujua pia kwenye hiyo Kila vitabu vya dini ni vya kutungwa kama na Quran nayo imo.

Inaonekana unapenda fasihi andishi. Kwenye uandishi unaweza kuabdika "Kila mtu alikuwepo pale..." Lakini kiuhalisia huwa haiwi kweli kila mtu kuwa alikuwepo eneo ulilokusudia.

Ishara ya kuwa Quran ni hadithi za kutungwa ni ipi?
 
You mind crippled, argue not with sound mind people.

Bad lucky are the parents who begotten such a retarded girl who is rich in nothing than her idiocy.
Huyo ni mwanaume anajivika uhusika wa mwanamke
 
Acha uongo mzee.wafilisti=philistines=Palestine.Daudi hana nasaba ya Palestine(philistines or Palestine).Daudi ni muisrael.Ila ukweli ni huu.Ile nchi kwanza walikaa WA Palestine (wafilisti or philistines),wayebusi,waanaki,wahivi.Waisraeli walikuja wakawapora ardhi kwa mujibu wa maelekezo ya MUNGU wao.Wakaja warumi wakawatoa,wakaja tena WA Palestine (wafilisti or philistines).Baada ya vita vya pili waisrael wakarejea tena hapo kwa mkono wa muingereza.Hakuna ukweli mwingine wowote tofauti na huo.Vinginevyo ni uongo tu.Hizo DNA zimegunduliwa juzi juzi tu,hiyo mifupa halisi ya kina Yesu waliitoa wapi hadi wakaipima wakajua sio hawa wa leo?
Halafu unatakiwa utumie akili yako ya kuzaliwa sio mihemko tu isiyo na maana.Unasema hawa ni wazungu toka ulaya mashariki,mbona hakuna nchi hata moja duniani inayoongea kiebrania lugha ya biblia zikiwemo hata hizo za ulaya mashariki tofauti na Israeli ya sasa?Dunia nzima ni nchi moja tu inayoongea lugha ya kiebrania ambayo ndiyo lugha mama ya waisrael wa kwenye biblia ni hawa waisraeli wa sasa peke yao,na wanaofuata misingi ya torati kama waisraeli wa kale Dunia nzima ni hawahawa waisraeli wa leo,leo unawezaje kusema sio hawa kwa chuki zako tu dhidi yao?Na hizo chuki ndizo zinazodhihirisha kuwa hawa ni waisraeli wa kale kabisa,maana tangu wanafika hapo ni uhasama wa hali ya juu sana na majirani zao.Hawajawahi kuwa marafiki kasoro taifa la Saudia tu.Maana hao ni watoto wa Ismael,waliambiwa wasipigane nao maana MUNGU wao hakuwapa hiyo nchi.Hiyo nchi amewapa ndugu zao waismaeli.Ndiyo maana hadi leo Israeli hawezi kuitaka Saudia au kupigana na Saudia.
Wafilisti=Wazungu
Palestine = wayahudi wa kale/Kanaanite
Israel Mizrahi = wayahudi wa kale/Kanaanite
Ashkenazi jews = wazungu toka Ulaya.

Watu pekee hapo Palestina wanofanana na wafilisti ni hao Ashkenazi jews sababu wote ni wazungu.

Video nimekuwekea juu, studies zipo kibao nimeweka juu, kama shida ni kujua ukweli Soma.

Mihemko na unachotamani kwenye nafsi yako haimaanishi ni ukweli.

Wayahudi wapo makabila 12 mengi Yamepotea hawayajui unahisi yapo wapi? Wapo Mars ama wapo eneo lao ambalo miaka nenda miaka rudi wayahudi waliishi?
 
Hii ndio tofauti kubwa pekee ni sawa leo watokee wa Catholic waseme kwao ni Vatican sababu ndio nyumbani kwa wa Rome lakini sababu Vatican hapatoshi tuchukue Rome pia. Wayahahudi ni dini na wanaweza kuwepo popote kuna waarabu wengi tu na ni mayahudi hakuna shida. Hawa wazungu waliotoka sijui Poland na nchi za ulaya mashariki ndio shida kubwa. Netanyau halikuwa jina lake alitoka Poland baada ya wao kuhamia Israel na jina akabadilisha Nentanyau.
Waindi wangapi wanaishi Tanzania lakini unajua kabisa huyu waindi yeye kutoka poland sio tatizo ila sikubaliani na Nentanyau anachofanya Gaza
 
Ninachotafuta ni uhakika maana ya kila siyo Kila. Maana ya kila ni vile tu avijuavyo mtu na siyo nje ya hapo.

Nikataka kujua pia kwenye hiyo Kila vitabu vya dini ni vya kutungwa kama na Quran nayo imo.

Inaonekana unapenda fasihi andishi. Kwenye uandishi unaweza kuabdika "Kila mtu alikuwepo pale..." Lakini kiuhalisia huwa haiwi kweli kila mtu kuwa alikuwepo eneo ulilokusudia.

Ishara ya kuwa Quran ni hadithi za kutungwa ni ipi?
Kwanza neno "Kila dini" linamaanisha dini zote lakini mimi kujiita Ibn Unuq isikufanye udhani mimi ni muislamu.

Ninakwenda kukuonyesha kuwa kitabu cha Qur'an ni fictios story;

Siku za Mwenyezi Mungu Sawa na Miaka 1000 au Miaka 50,000 kulingana na maelezo ya Allah?
  • Hakika siku moja mbele za Bwana ni kama miaka elfu ya hesabu yako. [Quran 22:47]
  • Kwake Yeye Siku ambayo muda wake utakuwa miaka elfu moja ya hisabu yenu (Quran 32:5).
  • Malaika na Roho hupanda kwake katika siku ambayo kipimo chake ni miaka khamsini elfu. Kwa hiyo, ni ipi? Je, siku ya Mwenyezi Mungu ni sawa na miaka 1,000 ya ardhi au miaka 50,000 ya ardhi? [Quran-70:4].
2.Kwa mujibu wa Qur'an, milima iliundwa ili kuimarisha ardhi na kuzuia kuyumba kwake, kama inavyoelezwa katika aya zifuatazo:

“Na tumeweka katika ardhi milima ili isiyumbe nayo.” (21:31)

“Na ameiweka ardhi milima ili isikuyumbisheni...” (16:15)

“Na ameweka katika ardhi milima iliyo dhabiti...” (31:10)


Hata hivyo, maarifa ya kisasa ya kijiolojia yanaonyesha kuwa milima huundwa na harakati za mabamba ya tectonic, ambazo pia husababisha matetemeko ya ardhi. Kwa hiyo, madai kwamba milima inazuia matetemeko ya ardhi yanapingwa na ushahidi wa kisayansi. Badala yake, milima ni matokeo ya mchakato wa kijiolojia unaohusiana na harakati hizo. Hii inaonyesha muandishi wa Qurani alikua hajui kuhusiana na Jiolojia - Milima ndiyo ardhi hiyohiyo ila yeye katofautisha Milima na Ardhi.

3. Kulingana na Quran Ulimwengu una miaka 4,137 tu!

Ikiwa tunaamini nadharia ya uumbaji wa Kurani, umri wa ulimwengu huu mzima ni chini ya miaka elfu tano. Maandiko ya Kiislamu yanasema kuwa Mwenyezi Mungu ameziumba mbingu hii na ardhi kutokana na utupu ndani ya siku sita na baada ya hapo akamuumba Adam binadamu wa kwanza; na Mtume Muhammad alikuwa ni kizazi cha 90 cha Adam. Kwa mujibu wa hesabu, kwa kuzingatia miaka 30 kuwa ni tofauti ya umri kati ya vizazi viwili vilivyofuatana, Mwenyezi Mungu aliumba mbingu hii na ardhi miaka 4,137 tu iliyopita. Kinyume chake, wataalamu wa kijiolojia wanasema kwamba dunia ina zaidi ya miaka bilioni 4.5. Swali ni nani yuko sahihi juu yake? Mwenyezi Mungu alikuwa sahihi au wanasayansi wa kisasa wako sawa?

4.Qur'an inatoa maelezo ya hatua za uumbaji wa mwanadamu, ikieleza kwamba mtu ameumbwa kutoka tone la manii, damu iliyoganda (alaqa), mifupa, na kisha mifupa kuvikwa nyama. Aya kuu ni:

"Kisha tukaliumba tone kuwa pande la damu iliyoganda, kisha tukaliumba donge hilo kuwa mifupa, kisha mifupa tukaivika nyama..." (23:14)

"Amemuumba mwanadamu kwa pande la damu iliyoganda." (96:2)


Changamoto za kisayansi:

Damu iliyoganda: Sayansi haikubaliani na maelezo ya Qur'an kuhusu kiinitete kuwa pande la damu iliyoganda, kwani hakuna hatua yoyote ya ukuaji wa kiinitete ambapo inaonekana kama damu iliyoganda. Hii ni dhana iliyotokana na mawazo ya kale ya Wagiriki, hususan Aristotle, ambayo si sahihi kisayansi.


Mifupa na nyama: Quran inaonyesha kuwa mifupa huundwa kwanza kisha nyama huvishwa juu yake. Hata hivyo, embryolojia ya kisasa inaonyesha kuwa mifupa na misuli hukua pamoja kutoka kwenye tishu sawa (mesoderm), sio kwa mpangilio wa kufuatana.


•Chanzo cha maelezo: Maelezo ya Qur'an yanafanana na nadharia za zamani za Kigiriki, hasa za Galen, ambazo sasa zimeonekana kuwa si sahihi kisayansi.

Kwa hiyo, maelezo haya yanapingana na sayansi sahihi kuhusu ukuaji wa kiinitete, ambayo inaonyesha kuwa maendeleo ya kiinitete ni mchakato endelevu na usio na hatua zilizotengwa wazi kama zilivyoelezwa kwenye Quran, Hii inaonyesha muandishi hakua mtaalamu wa Mwili wa binadamu.

5.Qur'an inaonekana kumchanganya Mariamu (mama yake Isa) na Miriam (dada yake Haruni na Musa, binti wa Imran), ambao waliishi takriban miaka 1400 tofauti. Aya zinazozua changamoto ni:

I. "Ewe dada yake Harun, baba yako hakuwa mtu mwovu..." (19:27-28)

II. "Na Mariamu, binti wa Imran, aliye linda tupu yake..." (66:12)

Changamoto kuu ya kihistoria ni kwamba Qur'an inaonekana kuunganisha vizazi viwili tofauti, huku Mariamu akihusishwa na familia ya Haruni na Musa, jambo ambalo halilingani na historia ya Kiyahudi na Kikristo.


6.Qur'an inaruhusu ngono na wake pamoja na vijakazi waliomilikiwa, kama inavyoelezwa katika aya zifuatazo:

• "Wanajizuilia matamanio yao isipokuwa kwa wake zao au vijakazi wao, kwani hao ni halali kwao..." (23:5-6; 70:22-30)


•"Mmeharimishiwa wanawake walioolewa isipokuwa wale ambao mkono wenu wa kulia umewamiliki..." (4:24)


•"Tumekuhalalishia wake zako na vijakazi mliopewa kuwa ngawira..." (33:50)

Aya hizi zinaonyesha kuwa wakati wa uislamu wa awali, ngono na wake na vijakazi ilikuwa halali. Hata hivyo, hili limeibua changamoto za kimaadili katika zama za kisasa, ambapo utumwa haukubaliki na haki za binadamu zinapewa kipaumbele.

Maswali muhimu yanayoulizwa ni:

Je, mwongozo huu bado unafaa kwa wakati huu?

Katika jamii za kisasa, mtu akifanya ngono na kijakazi, je, hilo linaweza kutetewa kwa msingi wa maadili ya sasa?

Wataalamu wengi wa Kiislamu wanaelezea kuwa aya hizi zilizingatia mazingira ya kihistoria, lakini maadili ya sasa yanahitaji kutafsiriwa upya kulingana na haki za binadamu.

7.Kasoro za Kikosmolojia: Ni Mbingu au Dunia Iliumbwa Kwanza?

Aya za Qur'an zinaonyesha mtazamo tofauti kuhusu uumbaji wa mbingu na dunia:

I. Dunia iliumbwa kwanza:
"Yeye ndiye aliye kuumbieni vyote vilivyomo katika ardhi. Kisha akazielekea mbingu na kuzifanya anga saba..." (2:29)

II. Mbingu iliumbwa kwanza:
"Je, nyinyi ndio wagumu zaidi kuumba, au mbingu aliyoijenga? ... Na baada ya hayo akaitandaza ardhi." (79:27-30)

Changamoto ya kisayansi ni kwamba aya hizi zinaweza kufasiriwa kuwa na mchanganyiko wa mpangilio wa uumbaji, huku zikionekana kupingana kuhusu kipi kilitangulia kati ya mbingu na dunia.

8.Ukinzani wa Namba: Siku za Uumbaji.

Qur'an inaeleza tofauti kuhusu muda uliotumika kuumba mbingu na dunia:

I. Siku 6:
"Mola wenu ni Mwenyezi Mungu aliyeziumba mbingu na ardhi kwa siku sita." (7:54, 10:3, 11:7, 25:59)

II. Siku 8 (kwa hesabu):
"Je! Mnamkataa aliyeumba ardhi katika siku mbili?" (41:9)

"Akaweka juu ya ardhi milima... na akapima humo riziki kwa siku nne." (41:10)

"Basi akazikamilisha mbingu saba katika siku mbili." (41:12)

Hesabu:

Uumbaji wa dunia: Siku 2

Riziki na milima: Siku 4

Uumbaji wa mbingu: Siku 2
Jumla: 2 + 4 + 2 = Siku 8.

Hii inapingana na madai ya aya nyingine kwamba uumbaji ulifanyika kwa siku 6. Changamoto hii imeibua maswali kuhusu uthabiti wa taarifa hizi katika Qur'an.

Kwa kuzingatia mifano iliyotolewa hapo juu, kuna ukinzani na makosa ya kihistoria, kisayansi, na kiidadi katika baadhi ya aya za Qur'an. Hii inaweza kuonyesha changamoto katika dhana kwamba Qur'an ni neno la Mungu Mjuzi wa yote, ambaye hawezi kufanya makosa.

Kama kweli Mungu ni Mjuzi wa kila kitu, basi haipaswi kuwepo ukinzani katika maelezo ya kihistoria, kisayansi, au mahesabu ndani ya maandiko hayo.

Hii inaleta swali kuhusu ukamilifu wa maarifa yanayodaiwa kutoka kwa Mungu wa Qur'an.

Aidha, ukinzani huu unaweza kuashiria kuwa Qur'an iliandikwa kwa utashi wa watu binafsi, ikichanganya maarifa na imani za wakati huo. Hii inaweza kueleza kwa nini baadhi ya maelezo yanalingana na dhana potofu za kisayansi na historia za kale. Ikiwa kweli Qur'an ingekuwa neno la Mungu mwenye maarifa yote, basi haingekuwa na hitilafu hizo, na maelezo yake yangekuwa thabiti na sahihi katika nyanja zote.

Ahsante!
 
Kwanza neno "Kila dini" linamaanisha dini zote lakini mimi kujiita Ibn Unuq isikufanye udhani mimi ni muislamu.
Hapana. Udodosaji wangu uko kwenye kupanua uelewa Wa watu kuhusu hoja tunayoijadili. Siyo kutokana na Jina unalolitumia.

Neno "Kila" humaanisha kinachojulikana na mtu husika na wala hilo neno halimaanishi "ote".

Neno "-ote" huweza kuthibitishwa wakati neno Kila ni kiashiria jambo husika liko kwa ukubwa unaofikia karibia na -ote kwa mtizamo wa Mtumiaji.

Maelezo yako mengine nimeyapenda maana yanaongeza uelewa.

Kwa kuwa hivi vitabu ulivyovitaja kuwa vina hadithi za kutungwa ndvyo nilivyovitumia kujenga hoja ya bandiko hili. Jee rejea ya hoja kuhusu Israel inayotajwa na vitabu hivi, inafaa kuaminiwa?
 
Kwa ivo walikuwa wanaishi wapi zama hizo za Quran na Biblia. Au walikuwa wanakuja na kuondoka?
Wayahudi wenyewe sio hao kina Netanyahu, kina Yesu walikuwa kama sisi wakakimbilia ethiopia, hao ni wazungu wamepelekwa na Nato wakatawale Uarabuni.
 
Hapana. Udodosaji wangu uko kwenye kupanua uelewa Wa watu kuhusu hoja tunayoijadili. Siyo kutokana na Jina ubalolitumia.
Okay, Ahsante!
Neno "Kila" humaanisha kinachojulikana na mtu husika na wala hilo neno halimaanishi "ote".

Neno "-ote" huweza kuthibitishwa wakati neno Kila ni kiashiria jambo husika liko kwa ukubwa unaofikia karibia na -ote kwa mtizamo wa Mtumiaji.
Mtu anaposema dini zote anamaanisha dini zinazojulikana. Hii inahusisha imani, maadili, na mafundisho ya dini tofauti tofauti, kama vile Uislamu, Ukristo, Ubudha, Hinduism, na dini nyingine nyingi, pamoja na dini za asili na za kimapokeo.

Neno kila pia linaweza kutumika Positively kutoa heshima kwa dini zote kwa njia ya ujumla, bila kubagua au kutofautisha kati ya dini hizo.

Mfano: Kila dini inafundisha upendo kama nguzo kuu [Hapa neno kila limejumuisha - Dini zote]
Maelezo yako mengine nimeyapenda maana yanaongeza uelewa.

Kwa kuwa hivi vitabu ulivyovitaja kuwa vina hadithi za kutungwa ndvyo nilivyovitumia kujenga hoja ya bandiko hili. Jee rejea ya hoja kuhusu Israel inayotajwa na vitabu hivi, inafaa kuaminiwa?
Hoja yangu kuu ni kwamba dini nyingi, ikiwa ni pamoja na Biblia, zina hadithi zinazozungumzia miji na matukio ambayo ni ya kubuni na siyo ya kithibitisho katika uhalisia.

Hii ni kwa sababu miji inayozungumziwa mara nyingi haipo katika historia ya kimazingira, na hivyo, inapaswa kutazamwa kama simulizi au mafundisho ya kiimani, badala ya ukweli wa kihistoria.

Hivyo, dini nyingi ni hadithi zilizojengwa ili kufundisha maadili na imani, lakini si za kuaminiwa kama ukweli wa kithibitisho cha mambo halisi ikiwemo watu pamoja na hiyo miji.
 
Wayahudi wenyewe sio hao kina Netanyahu, kina Yesu walikuwa kama sisi wakakimbilia ethiopia, hao ni wazungu wamepelekwa na Nato wakatawale Uarabuni.
Upo sawa mkuu lkn mizwazwa iyo aitokuelewa,
 
Upo sawa mkuu lkn mizwazwa iyo aitokuelewa,
Wakiambiwa YESU alikuwa mweusi awataki kuamini mana propaganda ya kuwa YESU kaka mzungu malaika Dada mzungu yani mungu mzungu na demu wake ndio malaika akili izi tupa kule afu mbaya zaid kitu cheusi ni janga mijitu yakutisha imewekwa kwenye weusi manake nyeusi ni raana na mweusi uyouyo ashtuki ufala huu yeye ndio anadhidi kutangaza kuwa ni raana langi nyeusi na mwenyewe ni mweusi akitokea mzungu akimwambia Acha ufala ww mungu alikuwa mweusi sio mzungu. Uyouyo mweusi anabishana na mzungu kuwa ww ujui maandiko MZUNGU anashangaa uyu mweusi anajiuliza ayo maandiko kaandika nani adi yeye amuamini uyo mzungu wkt adi Leo Wazungu wanawachukia watu weusi wanawaita manyani sasa mzungu uyu awe yeye ndio mwandishi wa maandiko uku moyoni anachuki na langi nyeusi unategemea ungeandika YESU alikuwa mweusi tena iyo miaka ya nyuma ndio ilikuwa na chuki za mweusi za hatari. Watafiti wengi wanaamin YESU ALIKUWA MWEUSI lkn Weusi wenyewe ndio wakwanza kupinga!!! Anataka munguwake awe nzungu nzungu nzungu langi nyeusi ndio langi OG KISAYANSI wamedhibitisha unatakiwa utulie ujitambue kwanza ndio ujue kuwapigania na wengine.
 
Back
Top Bottom