Nyendo
JF-Expert Member
- Jun 4, 2017
- 1,336
- 4,731
Sanaa ni ufundi wa kuwasilisha fikra na mawazo ya binadamu kwa njia aidha ya kuchora, kuchonga, uandishi, upambaji, mitindo, ufinyanzi, uimbaji, Uigizaji na vitu vingine vifafananavyo na hivyo, ni hali ya kuyapa umbo au (kibebeo) mawazo ili yaweze kufika kwa hadhira ili aidha kuelemisha, kuburudisha, kuonya au kuweka kumbukumbu ya jambo fulani.
Kazi zote za sanaa kwa ujumla wake zina lengo moja la kufikisha ujumbe au mawazo ya msanii husika. Pamoja na umuhimu huo wa kazi za sanaa lakini pia kazi za sanaa zinaweeza kutatua changamoto ya Ajira kwa vijana au kwa mtu yeyeto anayefanya kazi ya sanaa.
Baadhi ya faida za kazi ya sanaa:
Jamii zetu kwa sasa kwa kiasi kikubwa zinaendeleza zaidi sanaa ya Muziki na kusahau kuendeleza na sanaa nyingine kwa nguvu ileile kama itumikayo katika sanaa ya muziki.
Baadhi ya Changamoto iwakutayo wasanii wanaofanya sanaa nyingine
Ni wito wangu kwa vyombo vya habari vijitahidi kutangaza kazi zingine za sanaa ili wasanii wanaojitahidi kufanya kazi hizo waweze kupata kipato na pia sanaa iweze kufika mbali ili kutatua tatizo la ajira katika nchi yetu.
Pia Baraza la sanaa liwe bega kwa bega na wasanii katika kutatua changamoto za wasanii kama wizi wa kazi zao, kuhakikisha wanapata hati miliki na pia kuwaelekeza njia nzuri ya kuwasilisha kazi zao na si kusubiri wakosee na kuwapa adhabu tu.
Kazi zote za sanaa kwa ujumla wake zina lengo moja la kufikisha ujumbe au mawazo ya msanii husika. Pamoja na umuhimu huo wa kazi za sanaa lakini pia kazi za sanaa zinaweeza kutatua changamoto ya Ajira kwa vijana au kwa mtu yeyeto anayefanya kazi ya sanaa.
Baadhi ya faida za kazi ya sanaa:
- Kuongeza kipato
- Kutunza na kukuza Lugha
- Kutoa ujumbe wenye lengo fulani( kuonya, kuelimisha na kuburudisha)
- Kuongeza misamiati
Jamii zetu kwa sasa kwa kiasi kikubwa zinaendeleza zaidi sanaa ya Muziki na kusahau kuendeleza na sanaa nyingine kwa nguvu ileile kama itumikayo katika sanaa ya muziki.
Baadhi ya Changamoto iwakutayo wasanii wanaofanya sanaa nyingine
- Kukosa ufadhili
- Kukosa majukwaa kuwasilisha kazi zao
- Sera zinazorudisha nyuma juhudi za wasanii
Ni wito wangu kwa vyombo vya habari vijitahidi kutangaza kazi zingine za sanaa ili wasanii wanaojitahidi kufanya kazi hizo waweze kupata kipato na pia sanaa iweze kufika mbali ili kutatua tatizo la ajira katika nchi yetu.
Pia Baraza la sanaa liwe bega kwa bega na wasanii katika kutatua changamoto za wasanii kama wizi wa kazi zao, kuhakikisha wanapata hati miliki na pia kuwaelekeza njia nzuri ya kuwasilisha kazi zao na si kusubiri wakosee na kuwapa adhabu tu.