Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Kama kilichoripotiwa na CAG ni Kweli, basi Magufuli alikuwa sahihi mara 3...

Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli. Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea. Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufidadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Huwa siamini kama ni wewe wa zamani au mwenyewe alikufa kilaza mmoja akawa anatumia id yake
 
JPM hakuwa ethical. Alitegemea "ubabe" tu. Binafsi, suala la Uwanja wa Ndege wa Chato, ilikuwa indicator ya kwanza kabisa kuwa hayupo ethical kabisa.....mengine yakafuata. Ukabila, ukanda, mauwaji, utekaji, uonevu, udhalilishaji, kutofuata sheria/katiba, kuminya uhuru wa maoni, kuminya uhuru wa habari nk nk. Kwa kipimo changu cha ethicality, JPM hajawahi kupita hata mara moja.

Hii haina maana hakuna mazuri alofanya. Yapo mengi tu. Kama watangulizi wake pia walifanya mengi mazuri na mabaya...naye pia vivyo hivyo.
 
Anachojaribu kusema ni hiki

Kama Magufuli alikuwa nduli, fashisti na fisadi basi alikuwa mzuri. Mtu Fisadi anakwapua pesa halafu anapeleka umeme kila kijiji na Elimu bure nchi nzima na zahanati nchi nzima na miradi ya barabara nk hadi vichochoroni. Mistendi kibao hadi mingine inaitwa stendi ya Ndugai hilo fisadi na fashisti na nduli wananchi tunalikubali sababu lilikuwa linakwapua na kuwapelekea wanyonge miradi kibao.

Lingebaki liendelee kufisadi na kupelekea wanyonge

Haya tunasubiri msio nduli na mafashisti na msio mafisadi tuone kama spidi ya maendeleo kwa wanyonge ya hilo nduli,fashisti na fisadi tuone kama spidi hiyo mtaiweza.Tuone nani zaidi kati ya nduli fashisti na Fisadi Papa Magufuli na ambao sio nani zaidi .Wanyonge ndio watakuwa mahakimu kwa hili
Hayo aliyaanza kikwete na magufuli kaendeleza. Hizo barabaraza kuunga kila mkoa alizijenga kikwete akaondoka ameacha mikoa miwili. Ila nashangaa kila jambo mnampa magufuli kama hata waliyofanya wengine kama vile aliikuta nchi haina kitu hata kimoja.
Leo mnapingana na report ya CAG aliyemteua mwenyewe.
 
Nime note kitu kimoja kutoka kwako nayo ni 'wapinzani' kumbe ulishajiweka tawi la watawala?

Ok ni haki yako lakini kwa binadamu kamili angehoji je, kwanini aliyeninasibu kuwa msafi mithili ya sufi apende kufanya mambo gizani kiasi kile?

Kweli mtu msafi ajiondoe kwenye mikataba ya uwazi?

Kwanini mtu msafi hakuitaji transparency ili umma umsaidie kuwa msafi?

Mnachofanya sasa ni nafsi zinawasuta, mmeachwa kwenye tope msijue nani atawachomoa, mli compromise nafsi zenu kwa vitu vya kipuuzi na kishenzi.

Kinachowauma zaidi mlizoea kuuza maneno sasa hakuna atakaewaamini tena.

Kwa tuliomfahamu Magufuli tangu enzi hatukua tayari kuuza nafsi zetu kwa sifa za kipuuzi na kijumla jumla namna ile.
Pole sana mtafute kazi ya kufanya sasa.
Uyo MM ni sukuma gang au mfia meko wanateseka sana kuona mwendazake anavyo funuliwa sasa
 
tusimsingizie Magufuli kwa kila kitu.

Kuna kikundi ama kingenge cha wahuni sijui kinalipwa na nani kutaka kumchafua Magufuli na report ya cag
Tulia wewe! Kama unaona uchungu mfuate huko, mwenzio kakimbia msala.
 
Nime note kitu kimoja kutoka kwako nayo ni 'wapinzani' kumbe ulishajiweka tawi la watawala?

Ok ni haki yako lakini kwa binadamu kamili angehoji je, kwanini aliyeninasibu kuwa msafi mithili ya sufi apende kufanya mambo gizani kiasi kile?

Kweli mtu msafi ajiondoe kwenye mikataba ya uwazi?

Kwanini mtu msafi hakuitaji transparency ili umma umsaidie kuwa msafi?

Mnachofanya sasa ni nafsi zinawasuta, mmeachwa kwenye tope msijue nani atawachomoa, mli compromise nafsi zenu kwa vitu vya kipuuzi na kishenzi.

Kinachowauma zaidi mlizoea kuuza maneno sasa hakuna atakaewaamini tena.

Kwa tuliomfahamu Magufuli tangu enzi hatukua tayari kuuza nafsi zetu kwa sifa za kipuuzi na kijumla jumla namna ile.
Pole sana mtafute kazi ya kufanya sasa.
Jibu rahisi... Ninkwamba


: Transparency isingekuruhusu kuoakuwa pesa zote na kwenda kujenga mahospitali....binge lisingekubali.

:Transparency isingekuruhusu ujenge mabarabara kamanlile la kijazi

: Transparency isingekuruhusu uwakataze hela watu wasile ukimbize kwenye miundo mbinu....

Hata hivyo Binafsi nilidhani angekiwa na kikundi anachokiamini awe anashauriana nacho. Ungekiwa ubabe usio na makosa.

Endelea......
 
Mwandishi ni kama vile hutaki kuamini kuwa Magufuli alikuwa fisadi namba moja wa Tanzania katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Ripoti rasmi za kiuchunguzi wa pesa (CAG) za sasa zinaonyesha hivyo. Ni upigaji mtupu.

Kwanini ushangae hilo sasa wakati wakosoaji wa Magufuli walikuwa wakiyasema hayo kwa miaka mitano yote?

Ni akina nani waliohoji upotezi wa Trilioni 1.5 zilizotajwa na Professor Assad?
Kwanini Professor Assad alifukuzwa kimizengwe?

Kwanini vyombo vya habari vilizibwa midomo?

Kwanini wapinzani walipotezwa, kununuliwa, kuteswa na kuuwawa?

Kwanini wapinzani walinyimwa fursa ya kufanya siasa, kushika ikulu, kuingia bungeni, kutawala serikali za mitaa au mabaraza ya halmashauri ?

Kwanini genge la Magufuli lilikuwa likiratibu utawala wa Magufuli udumu milele?

Kwanini tender zote za miradi mikubwa ziwe siri ya Magufuli na ikulu tu?

Kwanini genge la Magufuli lilitaka kupindisha mambo kwa gharama yoyote ili kukamata kiti cha urais hata baada ya Magufuli kuwa mahututi/kufariki dunia?

Ukweli unaweza kuchelewa kujionyesha, lakini muda utaufunua ukweli wote. Muda umefika sasa kwa utawala wote wa Magufuli kupimwa upya. Tusiogope kusema ukweli hata kama ukweli huo utatufedhehesha baadhi yetu.
Hapa ndipo elimu inapaswa kuheshimiwa Assad aliulizwa kama kuna upotevu was T1.5 hadharani ili Rais afukuze watu hadharani nikumbushe jibu alilotoa .Kukurupuka na kauli za wanasiasa hauwezi kupata uhalisia wenzako wako kazini na wewe soma iyo riport ,nikikuuliza Magufuri kafanya ufisadi upi?nipatie jibu,sio kucheza na mdundo unaopita barabarani.
 
Wasalaam

Ama baada ya salam. Ni kiri kwa moyo na kuandika kwa msaada wa madole gumba haya mawili kwamba, tusichofahamu ni kwamba MAGUFULI amefariki, alikua mwema au muovu aliwaonea watu au aliwahurumia haibadilishi ukweli kwamba MAGUFULI amefariki na kuzikwa nyumbani kwao Chato.

Mama Tanzania ni lazima aendelee, ni tuwepo au tusiwepo. Kinachoniumiza ni kwamba "limeibuka kundi la wanaoogelea kufuata muelekeo wa mawimbi wamejisahaulisha hilo"

Mama Samia Suluhu Hassan kazi iliyoko mbele yako ni kubwa na inayohitaji weledi mkubwa pia.
Naokuomba mama yangu anza kuangalia namna gani unaweza kudhibiti team ya watu wanao shambulia Legacy ya Magufuli kwani wakimaliza watakugeukia wewe na mliokuwepo wote na tahamaki Uchaguzi 2025 huu hapa.

Mzee wangu Mwanakijiji wewe ni miongoni Mwa watu waungwana waliobaki katika Dunia hii na Mwenyezi Mungu akuongezee ufahamu.
 
Bunge hatuna, hivi!!
Kunakisa lipi wananchi tukiandamana kwenda kwenye jengo letu pale bungeni ili kuwaondoa wote ili turudi kwenye uchaguzi
 
Bunge hatuna, hivi!!
Kunakisa lipi wananchi tukiandamana kwenda kwenye jengo letu pale bungeni ili kuwaondoa wote ili turudi kwenye uchaguzi
Naunga mkono hoja .Iko haja wanananchi tuwaonyeshe kuwa hatuna imani na bunge lililojaa wanafiki wakiongozwa na spika Ndugai
 
Hapa ndipo elimu inapaswa kuheshimiwa Assad aliulizwa kama kuna upotevu was T1.5 hadharani ili Rais afukuze watu hadharani nikumbushe jibu alilotoa .Kukurupuka na kauli za wanasiasa hauwezi kupata uhalisia wenzako wako kazini na wewe soma iyo riport ,nikikuuliza Magufuri kafanya ufisadi upi?nipatie jibu,sio kucheza na mdundo unaopita barabarani.
Hivi Katiba hairuhusu Spika kujiuzulu..!??
Hastahili kuwepo pale bungeni hata sekunde..
 
Mtu anaepingana na Ripoti ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali ambayo kwa hakika haijaacha shaka yoyote juu ya ubadhirifu na matumizi mabaya ya fedha za umma; nathubutu kusema kwamba atakuwa sehemu ya ufisadi. Mwanakijiji unapohoji waliopo kwanini walishindwa kuchukua hatua lazima ufahamu kwamba na ujiulize swali kwamba kiongozi mkuu wa serikali aliruhusu kukosolewa? Kwa hiyo mimi sidhani kama serikali inayoendelea inakosa legitimacy as long as imeamua kuwaonyesha watanzania ukweli kwa kumruhusu CAG ''Asimung'unye Maneno'' hii ni hatua ya dhati kabisa; hasa ukizingatia kwamba hatujapata Ripoti yoyote ya Mkaguzi wa Hesabu za Serikali tangu Assad aondolewe kwenye kiti chake.
 
Anachojaribu kusema ni hiki

Kama Magufuli alikuwa nduli, fashisti na fisadi basi alikuwa mzuri. Mtu Fisadi anakwapua pesa halafu anapeleka umeme kila kijiji na Elimu bure nchi nzima na zahanati nchi nzima na miradi ya barabara nk hadi vichochoroni. Mistendi kibao hadi mingine inaitwa stendi ya Ndugai hilo fisadi na fashisti na nduli wananchi tunalikubali sababu lilikuwa linakwapua na kuwapelekea wanyonge miradi kibao.

Lingebaki liendelee kufisadi na kupelekea wanyonge

Haya tunasubiri msio nduli na mafashisti na msio mafisadi tuone kama spidi ya maendeleo kwa wanyonge ya hilo nduli,fashisti na fisadi tuone kama spidi hiyo mtaiweza.Tuone nani zaidi kati ya nduli fashisti na Fisadi Papa Magufuli na ambao sio nani zaidi .Wanyonge ndio watakuwa mahakimu kwa hili
Hao siyo wanyonge , bali ni wajinga na wanstumika kama mtaji wa wanasiasa matapeli.
 
Kama huu ufisadi mrioripoti ni kweli basi hata rais wa sasa anahusika kwa sababu alikuwa sehemu tena muhimu ya serikali wakati yanafanyika haya, kusema sijui hakuwa na kauli sijui nini ni kudanganyana. Kama hakukubaliana nayo angeachia ngazi abaki na heshima yake, kubaki madarakani ilikuwa ni kuunga mkono kila kilichofanyika. Ndugai alikuwa spika wa bunge lenye jukumu la kuisimamia serikali na hakutimiza/hawakutimiza wajibu huo ipasavyo, so nashauri tuanzie kwa kuwaburuza wote hao mahakamani sheria ipite nao. Kuendelea kushabikia wizi wakati walioshiriki wizi huo wapo na tena wanatuongoza mbele mbele katika kushangilia ni unafiki na uzandiki.
so mimi nasimama kuhesabiwa........ KAMA UFISADI HUU WOTE ULIFANYIKA WAKATI SAMIA SULUHU HASSAN AKIWa MAKAMU WA RAIS AWAJBIKE kwa sababu ndiye alikuwa msaidizi namba moja wa rais aliyekuwepo madarakani. Kusema eti kwa sababu aliyekuwa rais hayupo basi na ufisadi Huu tuachane nao ni unafiki na uzandiki wa hali ya juu.
 
Nimesoma lakini sijaelewa unataka kufikisha ujumbe gani.
Amesema hivi wanaosema tumepigwa sana na huu ufisadi wanaouonyesha kila kona walikuwa panoja na JPM MUDA WOTE LEO WAMEGEUKA KAMA.VILE ALIVYOGEUKA JOM KWA JK ni mwendo wa KARMA
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ufisadi uliofanyika wakati wa miaka mitano ya Rais Magufuli tunaambiwa ni mkubwa sana. Kwamba, mabilioni ya fedha yameliwa na wajanja na kuwa fedha hizi zimeliwa na watu walioteuliwa na kusimamiwa na Rais Magufuli. Kwa haraka haraka - kama kawaida naona siku hizi - wakosoaji wa Rais Magufuli (na hapa nawazungumzia wale wa kisiasa) wameruka ruka kwa shangwe wakisema "si tuliwaambia!". Na kinachosikitisha kidogo ni kuwa hata baadhi ya watu ambao wamejitambulisha kuwa ni wapinzani nao wamerukia kwa furaha tu na hata hawajui ni kitu gani wanaandaliwa. Sijui ni nani anayewalengesha hawa lakini kilichofanyika na kinachoandaliwa labda ni cha kutisha zaidi kuliko kilichotokea. Kuna mtu aliuliza (jamaa yangu Philemon Michael) wakati msiba ulipotangazwa maswali ambayo sidhani kama kuna mtu atakuja kuyauliza hadharani au kutaka kuyajibu yaeleweke. Na kuna mtu aliuliza tena wakati CAG amewasilisha Bungeni ripoti yake kwamba je hii ndio ile ile ripoti ambayo kama JPM angekuwa hai angekabidhiwa? Sijui jibu lake... Kama ni ile ile inawezekana hakukuwa na jinsi ripoti hii ingekutana na JPM meza moja... Kama ni nyingine... Magufuli alikuwa sahihi mara ya 1.

Hii miaka mitano tumeshuhudia miradi mikubwa ya kila namna na hata tukajisikia kuwa kuna kifu kinafanyika... lakini leo tunaambiwa lote ni changa la macho. Hizo hospitali hakuna zilizojengwa, hakuna masoko, hakuna vituo vya mabasi, hakuna shule zilizofanyiwa matengenezo makubwa, hakuna hiki wala kile na hata ndege tulizoambiwa zilinunuliwa kwa fedha taslimu kumbe hazikununuliwa... yaani, hata hii SGR na Bwawa la Umeme la Nyerere yote ni geresha tu! Kwamba kote huku watu walikuwa wanakula tu na tunachokiona hakipo na kama hili ni kweli basi Magufuli alikuwa sahihi mara 2.

Lakini kingine ni kuwa baadhi ya watu ambao waliteuliwa na Magufuli, walifanya naye kazi, na waliimba "maendeleo" "maendeleo" na hata kusifia kuwa tumeachiwa "urithi" kumbe si kweli; tumeachiwa madeni na ufisadi. Na kwa vile hakuna anayejitokeza kuwa na ujasiri wa kutetea walichokifanya kwa sababu kuna mtu anaitwa "Mwendazake" ameende na utetezi wake kumbe watu wamelia bure. Leo wengine (kina Ndugai) wanageuka wazi wazi; kumbe walikuwa wanaunga mkono uongo; walikuwa wanashangilia ulaghai, na walikuwa wanaficha ufidadi.. hapa watanyoshewa kidole wote kuanzia aliyekuwa Makamu wa Rais, Waziri Mkuu, Mawaziri wote (na wengi wamerudi au kuhamishwa) na kwa kweli inawezekana wabunge wote walioweza kuingia wakisimama nyuma ya Magufuli. Kama hili ni kweli kwamba ufisadi umetokea wakati watu wale wale ambao leo wanatufunulia ufisadi huo walikuwepo basi Magufuli alikuwa sahihi mara ya 3.

Swali kubwa ni usahihi gani ambao ninauzungumzia? Mwenye kusoma na aelewe. Kama kinachodaiwa na kushangiliwa leo ni kweli basi nchi haina kitu kingine cha kufanya bali kurudi kwenye uchaguzi mkuu mapema zaidi (labda Oktoba mwaka huu) kusafisha uchafu huu; ili wananchi wasisubiri kupigwa tena miaka mitano ijayo... Kama kina Majaliwa na wenzake wote hawakubaliani na assessment hii ya kuwa wamekuwa ni serikali ya kifisadi basi Waziri Mkuu aongoze kujiuzulu mara moja ili kumpa Rais nafasi kweli ya kuunda serikali anayoitaka ambamo ndani yake asirudi HATA MMOJA ALIYEKUWA NDANI YA SERIKALI YA MAGUFULI. Ndio maana ya KUWAJIBIKA KWA PAMOJA.

Wakitaka kuendelea bila kuwajibika ni lazima kuna kitu kingine kinaandaliwa. Ajenda ya Magufuli haijafa, haitakufa na kwa hakina haitoachwa ife. Maana, kama ufisadi huu umefanyika kwa kiasi hiki basi inawezekana Magufuli alikuwa ni genius aliyepindukia. Yaani, kama ufisadi kama huu ungefanyika wakati wa Mkapa au JK hii nchi ingekuwa mbali sana!
Kwa hiyo unataka kusema Shirika letu la Ndege lipo vizuri hamna ufusadi wowote wanamsingizia marehemu?

NIDA, Bandari, NSSF kote safi?

Pesa hizo alizokuwa anatembea nazo kwenye gari, anagawa mitaani, zilikuwa zinatoka fungu lipi, kwa idhini ya nani?

Tufahamishe mkuu.
 
Back
Top Bottom