Kama kweli huwa mnaibiwa kura, mnadhani kulalamika kwenye mitandao ya kijamii ndio suluhu?

Kama kweli huwa mnaibiwa kura, mnadhani kulalamika kwenye mitandao ya kijamii ndio suluhu?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Kila baada ya uchaguzi mkuu imekuwa ni jambo la kawaida kusikia wapinzani wa wakilalamika kuwa wameibiwa kura. Jambo ambalo W anaCCM huwa wanakanusha. Lakini hiki kilio cha wizi wa kura ni cha muda mrefu.

Mwaka 1995 mtifuano mkali kati ya mgombea uraisa wa NCCR Mageuzi na CCM ulisababisha watu wengi kuamini kuwa huenda matokeo yalichakachuliwa. Maana ushindani ulikuwa mkali sana. Na kwa kulinganisha ushindani kipindi cha kampeni na matokeo ndio hapo watu huamini kuwa matokeo yalichakachuliwa.

Lakini nini hasa suruhu ya hili tatizo?

Kwa nini wapinzani na chama tawala wasikubaliane kufanya mabadiliko ya katiba kuwe na kipengele kinachoruhusu matokeo ya urais kuhojiwa?

Kwa nini tusiwe na mahakama ya juu itayokuwa na mamlaka kusikiliza malalamiko ya wizi wa kura au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi?

Huu ndio wakati wa wadau wote wa demokrasia kuhakikisha kero kama hizi zinafutika. Tusisubiri 2025 kusikia kilio kinachojirudia kila uchaguzi ukifanyika.
 
Mkuu chagu wa malunde at least Leo umeongea Kama mtu mwenye akili Sasa nakujibu kwa ufupi.

Mabadiliko ya katiba ndio limekuwa hitajio kuu la upinzani siku zote katiba itakayoruhusu matokeo ya urais kuhojiwa mahakamani ndio hitajio la chadema ila CCM hawataki hii kwasababu wanajua wakiruhusu tu kesho hawapo ikulu.
 
Kila baada ya uchaguzi mkuu imekuwa ni jambo la kawaida kusikia wapinzani wa wakilalamika kuwa wameibiwa kura. Jambo ambalo wanaCCM huwa wanakanusha...
Watanzania msikodai haki na kusubiria wapinzani pekee mtasubiri sana. Sasa watu wanapigwa mpaka risasi mlitaka wafanye nini wapinzani? Wakisema muandamane hamtaki sasa tatizo ni watu hawako tayari bado wapo slow sana


vyMa
 
Kila baada ya uchaguzi mkuu imekuwa ni jambo la kawaida kusikia wapinzani wa wakilalamika kuwa wameibiwa kura. Jambo ambalo wanaCCM huwa wanakanusha

Mkuu,
Kwa sayansi yoyote ni bora kulala kuliko kukaa kimya. Ndiyo maana tunasema "Ogopa anaefukuza mwizi kimya kimya", kwani hujui anawaza nini na akimpata atafanya nini? Hapo ndo utamuelewesha mwenzio ni yapi uliyonayo/unayofikiri.

Ni wapi pa kwenda kulalamika bado haina shida kwani hata hili lako umelileta huku pia. Hivyo, unajua nguvu ya hii njia uliyotumia.

Suala la mabadiliko ya katiba si la wapinzani kupitisha chochote. Bali, ni maridhiano ya Taifa zima. Wanaoteliwa kufanya hiyo kazi huwa ni wawakilishi wetu.

Kama tungekuwa na nia njema kweli, hata hao wanasiasa pengine wangewawekwa kando. Ili tupate watu wasio na mlengo wowote na watengeneze kitu neutral.

Wapatikane watu wasionufaika na katiba kwa kugombea mamlaka, waliotumikia Taifa hili kwa nidhamu na uaminifu na wenye hofu ya Muumba. Unaweza kupata watu 50, kutoka nyanja mbalimbali wakatutengenezea kitu kizuri kuliko wale ?300/?400 waliokuwepo. Huwezi kunoa kisu cha kukuchinjia.

Unafikiri ni nani anasema Katiba ya sasa haina shida na si hitaji mhimu kwa Watanzania kwa sasa?

Ni nani ananufaika zaidi na matundu yaliyoko kwenye katiba hata kwa hayo machache unayosema?

Watu wako tayari kulinda hayo matundu kwa nguvu zote ili waendelee kuburuza.

Mimi, wewe na yule tutakapoamka na kudai katiba yetu, nakuhakikishia hata mwezi hauishi. Na itatengenezwaje pia inahitaji msukumo toka kwetu. Tukikaa kando tusubiri kulia na kusaga meno.

Tukisema ni kazi ya wanasiasa, hata miaka 50 tunaweza fika bila marekebisho yoyote na yakija, yaweza kutumbukizwa wanayohitaji wao tu kuwalinda. Nadhani UMEHAMKA sasa.
 
Kama kweli mahindi ya Tanzania hayana sumu kulalamika kwenye mitandao ndiyo suluhisho?

Kama kweli mabeberu wanataka kuiangamiza dona kantri kupitia chanjo ya korona, kulalamika kwenye mitandao ndiyo suluhisho?
 
Kutolalamika pia sio suluhu,

Kulalamika kunaleta ahueni japo sio suluhu ya wizi uliokubuhu wa maCCM
 
Hekima anakata tamaa, Ujinga anaendelea kutawala mimbari yake.
 
Kila baada ya uchaguzi mkuu imekuwa ni jambo la kawaida kusikia wapinzani wa wakilalamika kuwa wameibiwa kura. Jambo ambalo wanaCCM huwa wanakanusha. Lakini hiki kilio cha wizi wa kura ni cha muda mrefu..
Waswahili husema hata kimywa ni jibu kwa mjinga.
 
Kila baada ya uchaguzi mkuu imekuwa ni jambo la kawaida kusikia wapinzani wa wakilalamika kuwa wameibiwa kura. Jambo ambalo wanaCCM huwa wanakanusha. Lakini hiki kilio cha wizi wa kura ni cha muda mrefu. Mwaka 1995 mtifuano mkali kati ya mgombea uraisa wa Nccr Mageuzi na Ccm ulisababisha watu wengi kuamini kuwa huenda matokeo yalichakachuliwa. Maana ushindani ulikuwa mkali sana. Na kwa kulinganisha ushindani kipindi cha kampeni na matokeo ndio hapo watu huamini kuwa matokeo yalichakachuliwa.

Lakini nini hasa suruhu ya hili tatizo?
Kwa nini wapinzani na chama tawala wasikubaliane kufanya mabadiliko ya katiba kuwe na kipengele kinachoruhusu matokeo ya urais kuhojiwa?

Kwa nini tusiwe na mahakama ya juu itayokuwa na mamlaka kusikiliza malalamiko ya wizi wa kura au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi?

Huu ndio wakati wa wadau wote wa demokrasia kuhakikisha kero kama hizi zinafutika. Tusisubiri 2025 kusikia kilio kinachojirudia kila uchaguzi ukifanyika.
We pimbi tuko bize na COVID 19..mambo ya kuibiwa kura yanatokea wapi muda huu
 
Watanzania msikodai haki na kusubiria wapinzani pekee mtasubiri sana. Sasa watu wanapigwa mpaka risasi mlitaka wafanye nini wapinzani? Wakisema muandamane hamtaki sasa tatizo ni watu hawako tayari bado wapo slow sana


vyMa
Umehitimisha kila kitu!!!!
 
Back
Top Bottom