Kama kweli Nabi kakataa Fei Toto kurudi kambini, yuko sahihi

Kama kweli Nabi kakataa Fei Toto kurudi kambini, yuko sahihi

JFMemba

Senior Member
Joined
Jun 28, 2021
Posts
134
Reaction score
247
Nimeona taarifa ya kuwa Nabi kakataa Fei Toto kurejea kambini hata baada ya mgogoro wake na club kusuluhishwa.

Kama ni kweli basi huyu kweli ni Professor haswaa.

Viongozi wa Yanga hawakupaswa kabisa kukomaa na mchezaji ambaye tayari saikolojia yake haiko kwenye timu. Nawahakikishia itasumbua sana. Wangemuacha tu kwa amani

Screenshot_20221227-211406_Lite.jpg
 
Tunajidanganya sababu ya ushindi wa Azam wa juz

Fei Bado n muhimu kikosini subiri majeruhi yaanze ndio watajua FEI mtoto au mkubwa
Mkuu hakuna anayekataa kuwa Fei Toto ni mchezaji mzuri.

Lakini pia majeruhi hata yeye anaweza kupata akiwa Yanga au Azam. Ninachoongea mimi ni kuwa mchezaji ambaye nafsi yake iko upande mwingine utamlazimisha?

Kwa vyoyote vile hawezi kuwa huru tena, fikiria tayari coach kapoteza imani nae hapo hata wachezaji wenzake usikute nao wamegawanyika. Unaweza kukuta timu inavurugika zaidi.

Ni heri akubaliwe kuhama
 
Huyu kocha naye jau tu kwani mgogoro wa Fei toto na Viongozi wake inamhusu nn?

Kocha ana uwezo wa kumuwajibisha mchezaji iwapo ataonesha utovu wa nidhamu tofauti na hapo anaingilia mambo yasiyo muhusu.
Umesoma vizuri kweli concern ya Nabi? Yeye kasema tena kiufundi kuwa kuondoka kwake ghafla kulimvurugia match plan zake na kulazimisha kufanya technical changes. Yeye habri za ugomvi haongolei. Yule yuko smart sana
 
Mpira wa bongo ni upumbavu mtupu japo sina ushabiki wa timu yoyote ila nilikua najua kwa mchezaji kama fei mkwanja wake utakua safi tu mbona wakuja wanalipwa njema iweje wazawa waminywe kimtindo ndio maana utakuta timu hazifiki mbali figisu nyingi.........
 
Mkuu hakuna anayekataa kuwa Fei Toto ni mchezaji mzuri.

Lakini pia majeruhi hata yeye anaweza kupata akiwa Yanga au Azam. Ninachoongea mimi ni kuwa mchezaji ambaye nafsi yake iko upande mwingine utamlazimisha...
BM3 aliwafanyia vituko zaidi ya Fei lkn mpo nae kambini, why Fei!!!???
 
Back
Top Bottom