Kama kweli tunahitaji kufanyia marekebisho Katiba Mpya, tuanze na tume Huru ya Uchaguzi na kupunguza madaraka ya Rais

Kama kweli tunahitaji kufanyia marekebisho Katiba Mpya, tuanze na tume Huru ya Uchaguzi na kupunguza madaraka ya Rais

Tume huru ya uchaguzi bila katiba mpya ni sawa na kuziba mashimo ya panya kwa mikate!

Maana Tanzania uchaguzi ni mfumo sio tume tu.Nguvu ya Rais na wateule wake, polisi, TISS, Jeshi, Tume, Tamisemi na wengineo lazima viangaliwe kwa pamoja kupitia katiba mpya kwa sababu vyote hivi huwa vinahusika na chaguzi zetu.

Hiki kinachoitwa ni Tume huru ya uchaguzi ni changa la macho kwa wajinga ambao ndiyo wengi kwenye hii nchi.

ACT wazalendo ambao ndiyo vinara wa kudai tume huru ya uchaguzi badala ya katiba mpya ni chama pandikizi cha CCM kwa ajili ya kuvuruga maslahi mapana ya demokrasia kwenye nchi hii kwa maslahi ya kuhakikisha kuwa CCM inaendelea kutawala.
View attachment 2159445
Uko sahihi. Tume ya uchaguzi ni mojawapo la zao la katiba.
 
Nani kamuona dalali mkuu😀

Screenshot_20220322-150121.png
 
Hakuna cha kuwa mbali hebu tafuteni katiba ya UAE au brunei kama mfalme wao ana mafarka kiasi gani mbona nchi inasonga

ilikuwaje chademaa ilikuwa chama kikuu cha upinzani kwa miaka takribani 10 mbona hakina makao makuu ya kueleweka au ndio walikuwa wanakijenga chama kwenye mioyo ya watu acheni tiralila
Nchi za kifalme ni tofauti na nchi za kidemokrasia
Sisi tulichagua kuwa nchi ya kidemokrasia ni lazima tufanye kwa vitendo na demokrasia ni kusikiliza na kufanyia kazi matakwa ya wananchi sio kupigania matumbo ya viongozi.

Ofisi ya Chadema inahusikaje na katiba mpya?
Kwani hujui ccm walijenga ofisi zao kwa kodi za wananchi, kuna mwanaccm ameshawahi kuchanga mkajenga ofisi?
Zile ni kodi zetu mmekwapua.

Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Yaani katiba nzima mnawaza madaraka ya Rais kama vile ndio yanakwamisha maendeleo ya nchi hii kuna nchi nyingi tu madaraka ya Rais ni makubwa na bado nchi inasonga mbele na pia Rais anaheshimu anaheshimu katiba na vyombo vyake
Madaraka ya rais yanakwamisha maendeleo sana tena sana

Kwanza Rais ana kinga
Hii inamfanya kuwa Mungu mtu yani leo hii hata rais angeua mtu hadharani huna cha kumfanya anaweza kuamua kufanya ufisadi awezavyo na hamuwezi kumuuliza wala kumshtaki kokote
Hii inahamasisha ufisadi lakini pia inampumbaza mtu hawezi kusikiliza yeyote

Pili Rais anateua majaji wa mahakana
Huku ni kuingilia uhuru wa mahakama na kumfanya jaji amtumikie aliyemteua sio wanachi

Tatu rais anateuawabunge (10)
Anateua mawaziri
Anateua Mwenyekiti wa tume ya uchaguzi na mkurugeznzi halafu anakwenda kugombea
Anateua wakurugenzi amabao ndio wasimamizi wa uchaguzi
Anateua wakuu wa vyombo vya usalama
Anateua wakuu wa wilaya na mikoa

Ni punguani pekee hataweza kuona athari za kiuchumi siasa, kijamii za kumpa madaraka yote haya mtu mmoja halafu bado mnampa na kinga ya kutoshtakiwa.


Sent from my SM-M115F using JamiiForums mobile app
 
Kipengele kilichopo kwenye katiba Kinachosema Rais aliyeko madarakani akifariki maksmu wa Rais awe Rais, haraka sana Kirekebishwe.

Makamu wa Rais awe Rais kwa Muda wa mwaka mmoja then uitishwe uchaguzi mkuu.

Kipengele hicho kinamweka Rais aliyeko madarakani Katika wakati mgumu. .
Hili umelijua baada. Ya kuona Raise ni Mama au ni nn?
 
Baadhi ya maneno ya kuangaliwa ni kupunguza madaraka ya rais juu ya teuzi hasa za mawaziri.

Ili kujenga taifa la kiwajibikaji lazima mawaziri wawe na mkataba wa ajira na wakivurunda wanatimuliwa.

Tume ya uchaguzi iwe huru na matokeo ya Urais yaweze kupingwa mahakamani.

Mahakama ziwe huru na watu wawe na uhuru wa kudai haki zao bila kuwa na kikwazo cha aina yu yoyote.

Majaji wawe wanaomba kazi kama waajiriwa wengine.

"Katiba ni jambo la muda mrefu, katika kipindi cha kati tukayafanyie maboresho yote tuliyoyasema, halafu huko mbeleni tuone kuna haja ya kurekebisha katiba yetu, pengine kutakuwa na haja tu ya kurekebisha baadhi ya maeneo na si kuandika katiba mpya" Mhe. Rais
Nimepitia Katiba ya mwaka 2005, binafsi ninaona kama vile hili swala la kurekebisha katiba ni dogo sana kuliko linavyokuzwa na wanasiasa wa upinzani; wamekalia kuwa wanamlalamikia rais ila swala hili limo mikononi mwa wabunge. Kinachotakiwa kwa mujibu wa katiba hiyo ni kwa mbunge yeyote kutumia aya ya 98 ya katiba hiyo kuleta mswada wa kubadilisha katiba ama kwa kutambulisha rasimu iliyotolewa na tume ya Warioba kama katiba kamili ya Jamhuhuri ya Muungano wa Tanzania, au kwa kuandika muswada wake binafsi wa kubadilisha baadhi ya vifungu vya katiba. Bunge linapiga kura, iwapo 2/3 ya wabunge (super majority) watakubaliana na mswada huo basi, mswada utapelekwa kwa Rais, ambaye akishasaini, basi Katiba mypa inaanza. Hakuna mbunge yeyote aliyewahi kutumia kifungu hicho, lakini utakuta wanamlalamikia rais tu.

Hata Lisu mwenyewe kabla hajashambuliwa maisha yake hakuwahi kutumia kifungu hicho cha kaatiba. Rais hana mamlaka ya kubadili katiba, ni bunge tu linaloweza kufanya hivyo. Lawama zitapelekwa kwa raistu iwapo bunge limepitisha mswada, lakini Rais amektaa kuusaini. Ningekuwa mbunge ningeunganisha mswada huo na bajeti ya serikali kiasi kuwa rais asipousaini basi serikali pia inakosa hela.

Lile bunge maalum la katiba halikuwa na mamlaka ya kikatiba kujadilina kubadili katiba kwani katiba hiyo haina kifungu chochote kinachohalalisha uwepo wa bunge maalum la katiba, kile kikao kilikuwa haramu na kilipoteza hela za walipa kodi bure. Ilitakiwa rasimu ijadiliwe na Bunge lililopo kikatiba, na bunge hilo linaweza kufanya hivyo wakati wowote, siyo lazima kuwe na tume.
 
Back
Top Bottom