LGE2024 Kama lile ndio Daftari la kujiandikisha kupiga kura, Professor Assad yuko Sahihi kuwa hatapiga kura

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
Mwenyewe nilienda jumapili nilishangaa sana.
Niliwauliza vitu gani nahitaji kuwa navyo iliniweze kujiandikisha, nikaambiwa huhitajiki chochote zaidi ya wewe mwenyewe na majina yako.
Nikauliza utathibitisha vipi kama haya ni majina yangu wakasema sio lazima kuthibitisha muhimu niweke saini yangu.

Sijajua kwanini wameondoa kipengele cha kadi ya mpiga kura ila naona ni udhaifu au inafanyika bora liende.
 
Aliyedizaini hili daftari alaaniwe yeye na Watoto na ukoo wake na vizazi vyake
 
Ndio matokeo ya kuweka siasa kwenye kila kitu
 
Nimekuelewa vizuri, nimejiandikisha nitapiga Kura
 
Nilipo nimemsikia kiazi(mjumbe) wa eneo letu akipayuka kwa jazba akijaribu kuwatisha watu kwamba watafuatilia wale wote wasiokwenda kujiandikisha na hatimaye kupiga kura basi watakapohitaji huduma za wenyeviti wa mitaa hawatowahudumia! Binafsi naona wanazidi kuchanganyikiwa na mgomo wa watu kutokwenda kujiandikisha kwenye daftari lao la mchongo.
 
Inaumiza Sana sana
 
hata mm mtaani sijulikani naweza kujiandikisha sehemu zaidi ya moja
 
Unakwenda kupiga kura sehemu unapojulikana! Tunajuana Mtaani!
Ulitaka utumike utaratibu upi?
Njia Rahisi na uhakika ni kujipanga mbele ya mgombea unayemtaka! Kwanza hiyo, ingepunguza gharama nyingi za uchaguzi!
Wewe unawajua wote mtaani kwako? Unamjua kila mtu mtaani kwako?

Watanzania sijui nani katuloga. Tunaishi kizamani hadi mtu unashangaa. Anyways sio uzamani ni namna ya ccm kushinda.

Sijui lini tutaamka watanzania! Kila kitu kiko wazi kabisa ila tunafanyana wajinga tu
 
hata akiacha kura yake ni moja tu ,tuna watanzania miloni 60 kwahiyo hata akiwaambia na nduguzake wote wasipige kura haina shida
 
Vile vishikwambi vya sensa ilitakiwa vihifadhiwe vitumike katika mambo kama haya,katika zama hizi wanatumia daftari wakati ni suala la kuunda database na mfumo wa uandikishaji kidigitali,ni mbinu tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…