Kama mshahara ni chini ya Tsh 150,000/= kwa mwezi bora useme unatangaza nafasi za utumwa kuliko useme ni nafasi za kazi

Huna njaa wewe na hujui unachokiongea. Businesses zina mambo mengi interconnected na calculated alafu wewe unaongea superficially.
Mimi pia nafanya biashara. Naongea kwa uzoefu. Pumbav
 
Ukisoma comments za wengi hapa ni kama wanaupenda umaskini na kuwatetea wanyonyaji. Kimsingi watu wengi hawajui wanataka nini kwenye haya maisha.
 
TZ hata utangaze Kwa siku unalipa 500 Tsh Bado watu kama ni PM watajaa.na simu utapigiwa...njaa ni kubwa kweli kweli asikudanye mtu.
 
Kwako lakini wengine tunaiona kubwa
Sasa 2000 unakuwa huna majukumu mkuu, kijana wa kawaida huitaji kuajiriwa ili uipate 2000 maana ukijiajiri tu hata kwa mtaji wa 5000 unapata si chini ya 3000 kila siku......mfano huu hapa sasa.

1....ukinunua karanga kilo moja shilingi 3500 dukani.
Mkaa wa jero 500, .... ukafunga kwenye vile vimfuko ukapeleka kwa wenye viduka vya mangi au ukatembeza.

unaeza jikuta umefunga si chini ya vimfuko 25. kwa mfano kwenye viduka unamuuzia 350 kila pakiti bei ya jumla..... 350 x 25 =8750
8750-4000=4750 mtaji ulitumia 4000.....
Ukitembeza faidi ni zaidi ila wewe umetarget kuuza karanga zako jumla......sasa mkuu faida ya 4750 kwa mtaji usiozidi 5000 huoni ni bora kuliko kuajiriwa kutwa ukalipwe 2000 kwa siku.....

na hii idea inawezekana kwa kijana aliyeamua kujitoa muda wake kutengeneza karanga safi......

Mifano ni mingi sana mtaji hauzidi elfu 5000 na unapata 5000 nyingine au chini ya hapo kidogo, maana yake ukiwa na shilingi 20,000 ukichangamka kupata 10000 kila siku ni jambo jepesi.

Kuna idea ya biashara ya kijiwe nongwa cha kahawa.....

Atakuja mtu hapa aseme hesabu za makaratasi wakati hii ni real.
Hii kitu nilimpatia wife akafanya tena kwa udogo kutokana na wife ni mama wa nyumbani hili linamsave kupata pesa ya maziwa ya mtoto na hata matumizi yake madogo madogo.....
 
Fikiri.

House girl analipwa 50,000 kwa mwezi, kulala bure, kula bire, umeme bure, sabuni kuanzia ya kufulia mpaka kukogea bure, matibabu bure, kwa ugfupi kila kitu bure. Na mutu anayelipwa 200,000 ambae kila kitu anajilipia mwenyewe, kuanzia kodi ya nyumba na kila mahitaji yake binafsi.

Ipi bora hapo?
 
Wote wanaomponda jamaa kwa kuwalipa wafanyakazi wake 2000 kwa siku mnaishi tanzania tofauti na hii yetu? Nendeni mkawaulize wale mabinti wa mama ntilie mtaani kuwa wanalipwa sh ngap kwa siku. Bei huwa ni hyo hiyo ikizidi sana elfu tatu. Sasa nilidhani mngempinga kwa rejea kuwa huko mtaani kwenu mnawalipa bei gani.
 
Bora 200K kwa mwezi
 
Kima cha chini day ya viwandani angalau iwe elfu 10,000 kwa siku.na hapo iwe imetolewa hela ya chakula na nssf.
Una mlipa mtu 6,500 kwa siku kweli?,huyu mtu atakuja kununua hata TV si baada ya miaka 10
 
2000 per day?? Hata kama hela Sina hii Kazi siwezi fanyaa.
 
Create jobs,don't criticise people's who create jobs,unajua faida na uwekezaji wake? Unajua analipa kiasi Gani Kodi ya pango,umeme,taka,Ulinzi,service levy,mapato,simu,Zima moto,leseni?
 
Good Idea πŸ’‘πŸ’‘πŸ’‘
 
Kwanza ukipata kazi unashauriwa kukaa karibu na kazi, wahindi wanapesa lakini hawapandi daladala wewe unakaa chamazi halafu kazi mwenge??? Mwisho wa siku hakuna pesa ndogo, Kama unabisha ajiri watu watano kila mmoja alambe Milioni kwa mwezi πŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€bado TRA na marejesho!!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…