Kama mshahara ni chini ya Tsh 150,000/= kwa mwezi bora useme unatangaza nafasi za utumwa kuliko useme ni nafasi za kazi

Kama mshahara ni chini ya Tsh 150,000/= kwa mwezi bora useme unatangaza nafasi za utumwa kuliko useme ni nafasi za kazi

Ningekuwa ni mtunga sera ningehakikisha mishara ya watu hasa wahudumu wa baa na viwandani inapanda. Kuna mishahara ya baadhi ya viwanda ni midogo mno na kazi zina risk kubwa yaani inakuta mmiliki wa kiwanda au baa ana ukwasi mkubwa kwa kunyonya watumishi wake. Ningehakikisha wanaajiri watu wachache ila wanapata maslahi mazuri ili na wao waajiri wengine mashambani au kwenye biashara zao.
Ukisoma comments za wengi hapa ni kama wanaupenda umaskini na kuwatetea wanyonyaji. Kimsingi watu wengi hawajui wanataka nini kwenye haya maisha.
 
TZ hata utangaze Kwa siku unalipa 500 Tsh Bado watu kama ni PM watajaa.na simu utapigiwa...njaa ni kubwa kweli kweli asikudanye mtu.
 
Kwako lakini wengine tunaiona kubwa
Sasa 2000 unakuwa huna majukumu mkuu, kijana wa kawaida huitaji kuajiriwa ili uipate 2000 maana ukijiajiri tu hata kwa mtaji wa 5000 unapata si chini ya 3000 kila siku......mfano huu hapa sasa.

1....ukinunua karanga kilo moja shilingi 3500 dukani.
Mkaa wa jero 500, .... ukafunga kwenye vile vimfuko ukapeleka kwa wenye viduka vya mangi au ukatembeza.

unaeza jikuta umefunga si chini ya vimfuko 25. kwa mfano kwenye viduka unamuuzia 350 kila pakiti bei ya jumla..... 350 x 25 =8750
8750-4000=4750 mtaji ulitumia 4000.....
Ukitembeza faidi ni zaidi ila wewe umetarget kuuza karanga zako jumla......sasa mkuu faida ya 4750 kwa mtaji usiozidi 5000 huoni ni bora kuliko kuajiriwa kutwa ukalipwe 2000 kwa siku.....

na hii idea inawezekana kwa kijana aliyeamua kujitoa muda wake kutengeneza karanga safi......

Mifano ni mingi sana mtaji hauzidi elfu 5000 na unapata 5000 nyingine au chini ya hapo kidogo, maana yake ukiwa na shilingi 20,000 ukichangamka kupata 10000 kila siku ni jambo jepesi.

Kuna idea ya biashara ya kijiwe nongwa cha kahawa.....

Atakuja mtu hapa aseme hesabu za makaratasi wakati hii ni real.
Hii kitu nilimpatia wife akafanya tena kwa udogo kutokana na wife ni mama wa nyumbani hili linamsave kupata pesa ya maziwa ya mtoto na hata matumizi yake madogo madogo.....
 
Leo nimesikitika sana baada ya kusoma uzi wa jamaa anayetaka wahudumu wa mgahawani kwa mshahara wa Tsh 2000/= kwa siku kwa hoja kwamba watakula bure mgahawani. Watu wengi kwenye ule uzi wamempinga vikali mleta mada. Mimi pia niliandika comments za kupinga huo ujinga.

Ninawasihi waajiri binafsi watoe ujira ambao mtu anaweza hata kulipa nauli ya daladala na kubakiwa hata na Tsh 2000/= kila siku badala ya huu utumwa wanaoutangaza. Kama biashara yako haina mzunguko mzuri ni bora ukakomaa kivyako na familia yako hadi pale utakapoweza kuajiri mtu mwingine. Au akijitokeza mtu wa kujitolea ndo umlipe hizo posho kuliko kusema eti ni nafasi za kazi wakati ni utumwa mtupu.

Hata wafanyabiashara wakubwa wenye viwanda wanatuhumiwa kulipa mishahara ya chini ya Tsh 5000/= huku watu wakipigika hatari. Utetezi wao ni kwamba wakipandisha mishahara watashindwa kuendesha viwanda. Huu ni uongo mtupu. Hao matajiri ni wabinafsi wasio na utu. Kama kwenye net profit kwa mwaka tajiri anaweza kujinunulia V8 la anasa au kujijengea hekalu anawezaje kusema gharama za ku-run ni kubwa? Pia kusema kodi ni tatizo ninapinga. TRA wanachukua kodi baada ya kuangalia gharama zako za uendeshaji. Ina maana kiasi kidogo utachoongeza kama posho kwa wafanyakazi kitajumuishwa kwenye matumizi ya kampuni na kupelekwa TRA.

Watanzania tupendane na tuache kukandamizana. Kama sisi wa chini tunakandamizana kamwe hatuwezi kuwa kitu kimoja na kukataa ukandamizaji wa baadhi ya viongozi.
Fikiri.

House girl analipwa 50,000 kwa mwezi, kulala bure, kula bire, umeme bure, sabuni kuanzia ya kufulia mpaka kukogea bure, matibabu bure, kwa ugfupi kila kitu bure. Na mutu anayelipwa 200,000 ambae kila kitu anajilipia mwenyewe, kuanzia kodi ya nyumba na kila mahitaji yake binafsi.

Ipi bora hapo?
 
Wote wanaomponda jamaa kwa kuwalipa wafanyakazi wake 2000 kwa siku mnaishi tanzania tofauti na hii yetu? Nendeni mkawaulize wale mabinti wa mama ntilie mtaani kuwa wanalipwa sh ngap kwa siku. Bei huwa ni hyo hiyo ikizidi sana elfu tatu. Sasa nilidhani mngempinga kwa rejea kuwa huko mtaani kwenu mnawalipa bei gani.
 
Fikiri.

House girl analipwa 50,000 kwa mwezi, kulala bure, kula bire, umeme bure, sabuni kuanzia ya kufulia mpaka kukogea bure, matibabu bure, kwa ugfupi kila kitu bure. Na mutu anayelipwa 200,000 ambae kila kitu anajilipia mwenyewe, kuanzia kodi ya nyumba na kila mahitaji yake binafsi.

Ipi bora hapo?
Bora 200K kwa mwezi
 
Kima cha chini day ya viwandani angalau iwe elfu 10,000 kwa siku.na hapo iwe imetolewa hela ya chakula na nssf.
Una mlipa mtu 6,500 kwa siku kweli?,huyu mtu atakuja kununua hata TV si baada ya miaka 10
 
Leo nimesikitika sana baada ya kusoma uzi wa jamaa anayetaka wahudumu wa mgahawani kwa mshahara wa Tsh 2000/= kwa siku kwa hoja kwamba watakula bure mgahawani. Watu wengi kwenye ule uzi wamempinga vikali mleta mada. Mimi pia niliandika comments za kupinga huo ujinga.

Ninawasihi waajiri binafsi watoe ujira ambao mtu anaweza hata kulipa nauli ya daladala na kubakiwa hata na Tsh 2000/= kila siku badala ya huu utumwa wanaoutangaza. Kama biashara yako haina mzunguko mzuri ni bora ukakomaa kivyako na familia yako hadi pale utakapoweza kuajiri mtu mwingine. Au akijitokeza mtu wa kujitolea ndo umlipe hizo posho kuliko kusema eti ni nafasi za kazi wakati ni utumwa mtupu.

Hata wafanyabiashara wakubwa wenye viwanda wanatuhumiwa kulipa mishahara ya chini ya Tsh 5000/= huku watu wakipigika hatari. Utetezi wao ni kwamba wakipandisha mishahara watashindwa kuendesha viwanda. Huu ni uongo mtupu. Hao matajiri ni wabinafsi wasio na utu. Kama kwenye net profit kwa mwaka tajiri anaweza kujinunulia V8 la anasa au kujijengea hekalu anawezaje kusema gharama za ku-run ni kubwa? Pia kusema kodi ni tatizo ninapinga. TRA wanachukua kodi baada ya kuangalia gharama zako za uendeshaji. Ina maana kiasi kidogo utachoongeza kama posho kwa wafanyakazi kitajumuishwa kwenye matumizi ya kampuni na kupelekwa TRA.

Watanzania tupendane na tuache kukandamizana. Kama sisi wa chini tunakandamizana kamwe hatuwezi kuwa kitu kimoja na kukataa ukandamizaji wa baadhi ya viongozi.
Create jobs,don't criticise people's who create jobs,unajua faida na uwekezaji wake? Unajua analipa kiasi Gani Kodi ya pango,umeme,taka,Ulinzi,service levy,mapato,simu,Zima moto,leseni?
 
Sasa 2000 unakuwa huna majukumu mkuu, kijana wa kawaida huitaji kuajiriwa ili uipate 2000 maana ukijiajiri tu hata kwa mtaji wa 5000 unapata si chini ya 3000 kila siku......mfano huu hapa sasa.

1....ukinunua karanga kilo moja shilingi 3500 dukani.
Mkaa wa jero 500, .... ukafunga kwenye vile vimfuko ukapeleka kwa wenye viduka vya mangi au ukatembeza.

unaeza jikuta umefunga si chini ya vimfuko 25. kwa mfano kwenye viduka unamuuzia 350 kila pakiti bei ya jumla..... 350 x 25 =8750
8750-4000=4750 mtaji ulitumia 4000.....
Ukitembeza faidi ni zaidi ila wewe umetarget kuuza karanga zako jumla......sasa mkuu faida ya 4750 kwa mtaji usiozidi 5000 huoni ni bora kuliko kuajiriwa kutwa ukalipwe 2000 kwa siku.....

na hii idea inawezekana kwa kijana aliyeamua kujitoa muda wake kutengeneza karanga safi......

Mifano ni mingi sana mtaji hauzidi elfu 5000 na unapata 5000 nyingine au chini ya hapo kidogo, maana yake ukiwa na shilingi 20,000 ukichangamka kupata 10000 kila siku ni jambo jepesi.

Kuna idea ya biashara ya kijiwe nongwa cha kahawa.....

Atakuja mtu hapa aseme hesabu za makaratasi wakati hii ni real.
Hii kitu nilimpatia wife akafanya tena kwa udogo kutokana na wife ni mama wa nyumbani hili linamsave kupata pesa ya maziwa ya mtoto na hata matumizi yake madogo madogo.....
Good Idea 💡💡💡
 
Acha kutetea unyonyaji. Hakuna mtu aliyesema ulipe 3m kwa mwezi. Nimesema mshahara angalau anaoweza kumudu nauli ya daladala na kujibakizia 2000. Hujaelewa nini hapo? Kama huwezi hata kulipa 150k si ufanye hizo kazi mwenyewe au na familia yako? Kuna haja gani ya kulazimisha kuajiri watu huku huwezi kuwalipa?
Kwanza ukipata kazi unashauriwa kukaa karibu na kazi, wahindi wanapesa lakini hawapandi daladala wewe unakaa chamazi halafu kazi mwenge??? Mwisho wa siku hakuna pesa ndogo, Kama unabisha ajiri watu watano kila mmoja alambe Milioni kwa mwezi 😀😀😀bado TRA na marejesho!!!
 
Back
Top Bottom