Kama mzaha hoja ya Mbunge Shabibi inaweza kutungiwa Sheria kuongeza maumivu kwa wananchi

Kama mzaha hoja ya Mbunge Shabibi inaweza kutungiwa Sheria kuongeza maumivu kwa wananchi

Akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Mbunge wa #Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Tsh. 2,000 kila Mwezi kwenye laini za simu na Tsh. 10,000 kukatwa kwa Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato ya Bima ya Afya kwa wote

Shabiby amesema kuna Wamiliki wa Laini za Simu Milioni 72 Nchini ambao makato yao kwa Mwaka yataingiza Tsh. Trilioni 1.72 na zikijumlishwa za Tsh. 10,000 kwa Mwezi za Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi, Serikali itapata kwa Mwaka takriban Tsh. Trilioni 2.

Ni kama mzaha hoja za ajabu ajabu kama hivi huwa zinageuka kuwa sheria,bila wananchi kutarajia.

Tunakumbuka Mama Salma Kikwete alivyoibua hoja ya kuwalipa wenza wa viongozi wastaafu bungeni,na kama masihara bunge likainuka na hoja hiyo na kuifanya kuwa sheria.Leo hii mabilioni ya kodi za watanzania zinatumika kuwalipa watu ambao hawakuwa na majukumu yeyote ya kiseriakli mpaka kufa kwao.

Ni kwa namna kama hii ndio Mbunge wa Ilala,Mh.Mussa Azan Zungu alivyoleta hoja ya tozo ya miamala ya simu bungeni.Watu waliona ni masihara.Ghafla sheria ikatungwa na watanzania wanaendelea kuumia kila uchao.

Hivyo nina imani kwamba hata hili la mbunge Shabibi ambalo watu wanaona kama ni sanaa tu mda sio mrefu litatungiwa sheria na litapitishwa na bunge ili kuongeza majaraha kwa wananchi.

Jambo ambalo wanapaswa watanzania wafahamu ni kwamba hakuna mbunge wa CCM anaeibuka na hoja bungeni bila kuagizwa na serikali ya CCM.Huwa ni mpango ambao huwa umeshapangwa,hivyo muhusika hutolewa kafara ili kutekeleza maagizo.

Na hii ndio maana miswaada mingi ya hovyo ndio unaona bunge linakimbilia kuitungia sheria.Na kwa bahati mbaya nchi hii imekuwa na mahakama ya hovyo kiasi kwamba Bunge au Serikali huwa ndio mwamuzi wa mwisho wa jambo lolote linalohusu mustakbali wa nchi hii.

Hivyo watanzania wawe tayari kupokea sheria mpya ya tozo za laini za simu ili kuichangia NHIF.
mtafanyaje ikipitishwa? mtalipa tu, Taifa la Mazezeta
 
kuliko kuzidi kuwaminya wananchi izo trilioni 2 zinaweza kabisa kupatikana kwa serikali kubana matumizi ya anasa na kuthibiti wizi wa pesa za walipa kodi kwenye taasisi za umma,sambamba na kufuta kabisa mashirika kausha damu kama ttcl,TANOIL n,k.
Serikali inatafuna sehemu kubwa ya bajeti kuelekezwa kwenye matumizi waliyoyapa majina kama "matumizi ya kawaida" ambayo si ya lazima.

Kumbuka watumishi wengi tunaishi nao huku mtaani na tunajua namna wanajipatia fedha kwa njia haramu au ambazo si sahihi.

Kama tukiwa serious na kuja na mfumo mpya wa uendeshaji wa serikali then nina uhakika kuwa watasave zaidi ya hizo trillion mbili.

Huu upuuzi wa kuwajazia tozo za buku buku raia ni kuyatafuta mapinduzi na wote waliohusika watachezea kitanzi very soon.
 
Huyu dawa yake ni kuacha kupanda zile daladala zake za mikoani .............tuone huu upya upya atamweleza nani?
 
Akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Mbunge wa #Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Tsh. 2,000 kila Mwezi kwenye laini za simu na Tsh. 10,000 kukatwa kwa Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato ya Bima ya Afya kwa wote

Shabiby amesema kuna Wamiliki wa Laini za Simu Milioni 72 Nchini ambao makato yao kwa Mwaka yataingiza Tsh. Trilioni 1.72 na zikijumlishwa za Tsh. 10,000 kwa Mwezi za Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi, Serikali itapata kwa Mwaka takriban Tsh. Trilioni 2.

Ni kama mzaha hoja za ajabu ajabu kama hivi huwa zinageuka kuwa sheria,bila wananchi kutarajia.

Tunakumbuka Mama Salma Kikwete alivyoibua hoja ya kuwalipa wenza wa viongozi wastaafu bungeni,na kama masihara bunge likainuka na hoja hiyo na kuifanya kuwa sheria.Leo hii mabilioni ya kodi za watanzania zinatumika kuwalipa watu ambao hawakuwa na majukumu yeyote ya kiseriakli mpaka kufa kwao.

Ni kwa namna kama hii ndio Mbunge wa Ilala,Mh.Mussa Azan Zungu alivyoleta hoja ya tozo ya miamala ya simu bungeni.Watu waliona ni masihara.Ghafla sheria ikatungwa na watanzania wanaendelea kuumia kila uchao.

Hivyo nina imani kwamba hata hili la mbunge Shabibi ambalo watu wanaona kama ni sanaa tu mda sio mrefu litatungiwa sheria na litapitishwa na bunge ili kuongeza majaraha kwa wananchi.

Jambo ambalo wanapaswa watanzania wafahamu ni kwamba hakuna mbunge wa CCM anaeibuka na hoja bungeni bila kuagizwa na serikali ya CCM.Huwa ni mpango ambao huwa umeshapangwa,hivyo muhusika hutolewa kafara ili kutekeleza maagizo.

Na hii ndio maana miswaada mingi ya hovyo ndio unaona bunge linakimbilia kuitungia sheria.Na kwa bahati mbaya nchi hii imekuwa na mahakama ya hovyo kiasi kwamba Bunge au Serikali huwa ndio mwamuzi wa mwisho wa jambo lolote linalohusu mustakbali wa nchi hii.

Hivyo watanzania wawe tayari kupokea sheria mpya ya tozo za laini za simu ili kuichangia NHIF.
Adui yetu namba Moja ni CCM
 
Tupeni mbadala,yale ni mawazo yake ya hesabu na zile ni data zake,elfu 2000 kwa mwezi na nchi nzimabtutibiwe bure we inakuuma.
Hakunaga bure kwenye nchi iliyooza kwa rushwa kama hii! Imagine leo hii tu watu wamechangia bima ila still ukifika dirisha la dawa kati ya dawa 5 utapewa mbili halafu 3 zilizobakia ukajinunulie mwenyewe.
 
Ungejua watz wanakufa kwa kukosa mia tano usingeropoka nini elf mbili hata ulewi
 
Wabongo kwa ulalamishi nini elf 2 kuokoa milioni 2 za matibabu
Kukatwa buku 2 haina shida mkuu tatizo hizo hela zinaenda kweli kufanya lililokusudiwa? Ama kuna wacenge wachache fedha zikifika hazina watagawana billion 60/60 za michango na kwenda kujenga maghorofa mbweni na kununulia mabasi na malori?
 
Akichangia mapendekezo ya bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2024/2025, Mbunge wa #Gairo (CCM), Ahmed Shabiby ameishauri Serikali kukata Tsh. 2,000 kila Mwezi kwenye laini za simu na Tsh. 10,000 kukatwa kwa Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi ili fedha hizo ziwe chanzo cha mapato ya Bima ya Afya kwa wote

Shabiby amesema kuna Wamiliki wa Laini za Simu Milioni 72 Nchini ambao makato yao kwa Mwaka yataingiza Tsh. Trilioni 1.72 na zikijumlishwa za Tsh. 10,000 kwa Mwezi za Wabunge, Wafanyabiashara na Wafanyakazi, Serikali itapata kwa Mwaka takriban Tsh. Trilioni 2.

Ni kama mzaha hoja za ajabu ajabu kama hivi huwa zinageuka kuwa sheria,bila wananchi kutarajia.

Tunakumbuka Mama Salma Kikwete alivyoibua hoja ya kuwalipa wenza wa viongozi wastaafu bungeni,na kama masihara bunge likainuka na hoja hiyo na kuifanya kuwa sheria.Leo hii mabilioni ya kodi za watanzania zinatumika kuwalipa watu ambao hawakuwa na majukumu yeyote ya kiseriakli mpaka kufa kwao.

Ni kwa namna kama hii ndio Mbunge wa Ilala,Mh.Mussa Azan Zungu alivyoleta hoja ya tozo ya miamala ya simu bungeni.Watu waliona ni masihara.Ghafla sheria ikatungwa na watanzania wanaendelea kuumia kila uchao.

Hivyo nina imani kwamba hata hili la mbunge Shabibi ambalo watu wanaona kama ni sanaa tu mda sio mrefu litatungiwa sheria na litapitishwa na bunge ili kuongeza majaraha kwa wananchi.

Jambo ambalo wanapaswa watanzania wafahamu ni kwamba hakuna mbunge wa CCM anaeibuka na hoja bungeni bila kuagizwa na serikali ya CCM.Huwa ni mpango ambao huwa umeshapangwa,hivyo muhusika hutolewa kafara ili kutekeleza maagizo.

Na hii ndio maana miswaada mingi ya hovyo ndio unaona bunge linakimbilia kuitungia sheria.Na kwa bahati mbaya nchi hii imekuwa na mahakama ya hovyo kiasi kwamba Bunge au Serikali huwa ndio mwamuzi wa mwisho wa jambo lolote linalohusu mustakbali wa nchi hii.

Hivyo watanzania wawe tayari kupokea sheria mpya ya tozo za laini za simu ili kuichangia NHIF.
Hatuna shida na hilo swala la kuchangia ila tunachotaka ni accountability sio siasa baada ya michango kukusanywa. Ikiwezekana mfuko huo uwe wa raia na account iwe specific ya michango ya bima isiingiliwe na mafisadi wa CCM wala matumizi tofauti na kulipia bill na dawa za wagonjwa tu.

Hela za michango tuwe na access ya kuona zimekusanywa ngapi na matumizi yake yawe yanawekwa wazi kwa kila raia kwamba mwezi huu umechangia ngapi, jumla mfuko una bei gani in real time sio mambo ya kutuzuga kama tozo za miamala zilivyokuwa zinakatwa halafu wanaficha taarifa za makusanyo matokeo kinakuwa kichaka cha wizi.
 
Back
Top Bottom