Mi nauliza huyu mtu anajiita Lemutuz, kwanza kabisa umri wake, elimu yake na kazi amayofanya. Mana vitu anavyofanya, ninavyokadiria umri wake, elimu anayodai anayo, exposure anayodai anayo haviendani kabisa na mambo anayoyafanya.
Nachoshangaa anajilinganisha na watu ambao haendani nao hata kwa kitu kimoja, anadai ana Degree 3, sasa degree ni inputs you have to ultilize it to produce outputs unless otherwise ni useless, labda mi simjui vizuri kuna mtu anaweza kunisaidia huyu mtu kafanya nini tangible na kina manufaa gani kwa jamii mpaka ajilinganishe na vijana ambao kweli tunajua wanachokifanya na hata wanatoa ajira kwa vijana wengine wengi tu au ndio ameajiri mpiga picha anampiga picha za kuweka kwenye social media?
Niliona eti anauliza maswali kisha anatoa zawadi za vigauni kwa watoto wa kike. Huwa naona anapiga picha na watu kama Joseph Kusaga, Erick Shigongo, Yusuph Bhakresa, Salum Lussasi, na wengineo eti ansema ndege wa rangi moja huruka pamoja. watu hawa wamefanya vitu ambavyo vimeonekana na jamii na wamesaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana kisha huyu mtu anajiita Lemutuz anajilinganisha nao sijui anafanya nini mpaka anajiilinganisha na hawa watu au ni hivyo vigauni anavyotoa zawadi, Si bora Diamond anaimba kutuburudisha na kuitangaza nchi yetu.
Kwanza anafanya kazi gani mana hayuko busy muda wote hupiga picha na watu especially watoto wa kike na watu anaotudanganya ni rafiki zake (lakini nazani wengine huomba tu kupiga nao picha mana hawaendani hata kidogo) kwenye tafrija mbalimbali zingine nazani huwa hajaalikwa pia, mana mtu huwezi kuwa na marafiki wote hawa labda huna misimamo na ni mnafiki.
Ukiongea nae sana atakuambia oooh mi baba yangu alikua balozi, alikua waziri wa mambo nje, ooh nakaa see view ambako pia nazani ni kwa baba yake hivi kweli mtu wa umri wake anapaswa kuongea hayo, niliona siku moja kapiga picha na Wema Sepetu eti anasema baba zetu walikua mabalozi tumekula wote bata osterbay sasa sijui mtu wa umri wake bado ana haja ya kujisifia kupitia baba yake badala watoto wake kujisifia kupitia jina lake, mbona baba yake kwa umri wake tayari alikua kiongozi wa nchi hii, kwa kweli huyu mtu ananishangaza sana haya mambo ni ya watoto wa miaka 16.
Sasa hivi anasema nafatilia vyeti vya Sitti Mtemvu ili avuliwe taji mi nazani kwanza tufatilie hivyo vyeti anavyodai ana degree tatu.
NAOMBENI MNISAIDIE LABDA MI SIMJUI VIZURI HUYI MTU ILA ANANISHANGAZA SANA!
1. The King of All Bongo Social Media Network Le Mutuz Nation, nina Degree 3 1. Marine Engineering niliisomea at Angtwerpen/Belgium 2. Ciriminology niliisomea at Westchester College/USA 3. Political Science niliisomea at Lehman College USA.
2. Nimeishi Belgium Miaka 6 ambayo nilikuwa ninasoma na kufanya Field Melini kwa katika kipindi hicho cha Miaka 6 nimefanikiwa kutembelea nchi zaidi ya 85% ya Dunia, na baada ya kumaliza masomo nikarudi bongo na kuhamia New York City/USA.
3. Nimeishi USA I mean New York City Miaka 25, nikaamua kurudi nyumbani moja kwa moja miaka 3 iliyopita, nilipofika tu niligombea ubunge wa East Africa, kura hazikutosha lakini nikagombea nafasi zingine ndani ya chama changu CCM ambacho nikiwa New York City nilikifungulia Tawi la kwanza la CCM toka tupate uhuru ambalo lipo mpaka leo, na CCM kwa kuheshimu kazi yangu wakamtuma Katibu Muenezi Nape kuja kunisaidia kulifungua lipo mpaka leo. Ndani ya CCM Taifa nilifanikiwa kushinda vyeo 3 na vifuatavyo ambavyo ninaendelea kuwa navyo mpaka MWaka 2017:-
1. Mjumbe wa Mkutano Mkuu wa CCM Taifa unaochagua Mgombea urais wa CCM.
2. Mjumbe Baraza Kuu la Taifa Wazazi/CCM
3. Mjumbe Baraza Kuu UVCCM Taifa.
3. Nina kampuni ya Blogu ya Wananchi Media Company Limited ambayo ni registered Brela na ina wafanyakazi 4 Vijana waliomaliza Chuo Kikuu cha Mlimani, hivyo nimesaidia kupunguza tatizo la ajira kwa Taifa I hope na wewe umefanya hilo, Mimi pia ni Transportation Manager wa Chicasa ICD Mbagala Project, ndio maana kila Kampuni yangu inapokuwa na Meli nihamia bandarini kusimamia kazi za Kampuni yangu, Mimi ni Promoter wa Music na events mbali mbali ndiye ninayeratibu events za Intagram Party Tanzania Tour 2014 ambazo tulianza na Dar, Mwanza, Mbeya, juzi Dar Jumamosi ijayo Dodoma na pia sasa hivi ninatayarisha the biggest event ya music Tarehe 22/11/2014 at Escape 1 Beach Club ambayo itakuwa ni aina yake na kugharimu Mamilioni ya pesa kutoka wadhamini. Na pia mimi ni Balozi maalum wa kinywaji cha Shuda Cocktails kutoka London UK ndio maana majuzi nilikuwa na Diamond kwenye ufunguzi wa kampuni hiyo hapa bongo pale Serena.
4. Binafsi sio mwizi mali zangu zote ni za halali ndio maana huwa sina tatizo kuzitaja, Nina Shamba kubwa la Eka 5 na nyumba kubwa niliyoijenga Kinyerezi nikiwa USA, nina 3 Bedrooms Apartment Changombe na pia nina 3 Bedrooms Apartment hapa Mjini at Jamhuri Street hizi nimezipata baada ya kurudi nchini katika kipindi hiki cha miaka 3 niliyoishi hapa. Niliporudi nilishindwa kwenda kuishi Kinyerezi kwa sababu ya umbali na pofisi yangu ambayo ipo Gerezani kwa hiyo nikaamua kuishi kwenye tupu ya Baba yangu iliyopo Sea View mpaka pale nitakapopata Nyumba yangu, kwa hiyo baada ya kupata nipo kwenye nyumba yangu Jamhuri Street, sidhani kama ni ishu sana maana baada ya kurudi Tanzania after 30 years nje nilihitaji pa kuanzia na ninamshukuru sana baba yangu kwamba amekuwa na uwezo wa kuishi Dodoma akiwa na nyumba hapa mjini ambazo hazina mtu na ni mpoja ya niliyokuwa nikiishi.
5. Nina haki zote za kujisifia na kazi za Baba yangu siamini kwamba ni kuvunja sheria, ninamini na wewe una baba yako ambayo upo proud naye na kazi zake hapa Duniani. Ni kweli Baba yangu akiwa Waziri wa nje baba yake Wema Sepetu alikuwa Waziri wake mdogo, sijui kosa langu ni nini kwa kusema hivyo as a FACT!!
6. Mimi as Le Mutuz Nation ni Celebrity ninaalikwa kwa kawaida hata sehemu 10 usiku mmoja watu wanataka niseme nilikuwepo kwenye envets zao maana mimi ni The King wa Social Media, na hata ukienda kwenye my Instagram Wall utaona kwamba makampuni makubwa kama Airtel, na Vodacom watanatangaza matangazo yao ya biashara na pia ninawasaidia Wajasiriamali wadogo wadogo kwa kuwashindanisha my folowers at Instagram na kwuapa zawadi lengo ni kutangaza biashara za hao wajariamli wadogo waodogo wanaonilipa kwa kila tangazo.
7 Ni kweli nina marafiki wengi sana kwa sababu tabia zangu zinakubalika sana na wananchi wengi hapa Tanzania, ndio maana Mfayabiashara maarufu kama Omar Bahkressa huwa hakubali kupiga pichaa na mtu lakini anapiga na mimi, vyombo vyangu vya media vinatumika sana na watu wasiopenda ujinga kwa mfano majuzi mdogo wake Rais wa Jamhuri Kiwadinyo Kikwete alipfanya harusi aliruhusu vymbo vyangu tu kurusha picha zake za harusi, hii inaonyesha jinsi gani ninaheshimika sana na watu wengi muhimu katika hii jamii.
- Sasa kwa kumaliza kwanza naomba kukushukuru kwa mara nyingine tena kunipatia nafasi ya kuelimisha umma mimi ni nani, ninaamini kwa mwenye akili yoyote atakayesoma hapa atakubaliana na mimi kwamba unyemzungumzia wewe sio mimi maana ulichoandika ni majungu, chuki, wivu na fitina, soma tena hapa unijue vizuri mkuu, nezt time muwe mnauliza badala ya kurukia rukia watu msiowajua, wewe hunijui na ninasema hivi kama haya yote ninayoyafanya kwenye maisha yangu ya binafsi na jamii hayafanani na Degree 3 na umri wangu, ninaomba unipe mifano ya walio na elimu kama yangu na umri kama wangu na wanayoyafanya ndio nitajirekebisha kama ulivyotaka, otherwise kiss my left foot and mind your business ok!!
hahahahahahahaahahahahahahahahah
The King Of All Bongo Social Media Network
Le big Show