Kama ni kweli ninapinga kwa Papi Ousmane Sakho 'Kutemwa' Simba SC

Kama ni kweli ninapinga kwa Papi Ousmane Sakho 'Kutemwa' Simba SC

Wasilogwe wamuache Sakho..... SITAIFANYIA CHOCHOTE SIMBA.. Banda hamna kitu, Duncan Nyoni hamna kitu, Wawa na Kagere umri umeenda..... SAKHO AKIACHWA SIFUATILII SIMBA TENA..... cha mwisho itakuwa hiyo hela niliyochangia ujenzi wa uwanja.
 
Kama Sako katemwa basi mimi ndoa yangu na Simba ishaisha hata mchango situmi, watu wanaendeshwa na mihemko haiwezekani unamtoa dogo kumleta babu!

Chama nampenda lakini kwa hili ilitakiwa tu move on
 
Wasilogwe wamuache Sakho..... SITAIFANYIA CHOCHOTE SIMBA.. Banda hamna kitu, Duncan Nyoni hamna kitu, Wawa na Kagere umri umeenda..... SAKHO AKIACHWA SIFUATILII SIMBA TENA..... cha mwisho itakuwa hiyo hela niliyochangia ujenzi wa uwanja.
Nikajuwa niko peke yangu mwenye hayo mawazo!

Sako Banda Duncan wote wazuri wamekosa game time tu! Tuko desperate sana haikuhitajika kusajiri kabisa hili dirisha ukizingatia robo tatu ya usajiri wetu mpaka sasa haujatumika!

Wasituletee oya oya zao
 
Naunga hoja sakho na Banda wale Ni hazina kwa Simba ,hata wanaosema atemwe Banda hawana jicho la mbali ,hao wote wawil Ni talented pia umri wao unaruhusu Sana ,wapewe muda wa kutosha watatusaidia mbelen , hata Duncan sio mchezaj wa kuachwa kizembe.

Wakutemwa hapa Ni Hawa
Wawa
Kagere
Hawa Ni kimataifa .
Kibongo bongo wakutemwa Ni
Bocco
Nyoni
Gadiel
Kakolanya

Hao ndio hawana msaada kwa Simba ya Sasa yenye malengo ya kimataifa ,wengine wote wako fresh kabisa isipokua Kibu apewe program maalum kumfanyia councelling apunguze pupa akipata mpira awe mtulivu ,hii program imhusu na Mugalu pia.

Bench la ufundi toa yule Mrundi Hitmana maana anakula pesa ya bure tu pale msimbazi.
Wahamasishaji toa Mwijaku Tena akae mbali na Simba kabisa.
Msemaji wa Timu atafutwe mwenye Busara Simba ya Sasa sio ya kuwa na msemaji dizain ya manara ,mchukueni hata Masaubwire yule bro Ana busara Sana .
Upande wa viongoz ,Mangungu apewe semina ya Nini maana ya kiongoz mkubwa kwenye club kubwa Kama Simba ,apunguze kuharisha hovyo hovyo mbele ya kamera pia aache habar za kuwawazia wapinzan pind anapofafanua Jambo.
Kwa Leo Ni hayo tu
Agiza K Vant nakuja
 
Yatakuwa ni maajabu ya Dunia Simba kumwachq yule mtoto Sakho....kaama kina ulazima, wamttoe Wawa, Mugalu au Nyoni!
Halafu Kuna watu wanamtukana Boko,mwisho wa msimu ndiye mfungaji Bora ,hebu mwachemi mwenye Ligi yake Hadi atakapo staafu
Hivi,ni kweliSimba ilikuwa inamhitaji Chama au ndiyo.kuogopa kuwa angeenda Yanga!
 
Mchezaji mzuri hasubiriwi eti kwa kupewa muda.
Sackho
Duncan
Mugalu
Hawa ni wakusitishiwa mikataba yao.
Hawana cha ajabu.
Wana rukaruka tu kiwanjani.
 
Kwanzia kwa Chikwende niliamini Simba ujinga mwingi sana acha wapambane na kunguni zao wenyewe.
 
Genta nunakuunga mkono.
Simba wasifanye makosa ya kumtema Sakho.
Viongozi kama wapo mnaopitia mada za humu, wekeni akilini juu ya mada hii na kuifanyia kazi.
Poti wangu Mshauri Mkuu wa Mwekezaji Crescetius Magori huwa ananisoma mno kama si sana tu hapa JamiiForums hivyo naamini atakuwa ameshanisoma na kufuata huu Ushauri wangu.
 
Wataje hao wachezaji wanaompiga miba ili tuwashughulikie,wasituharibie timu yetu
GENTAMYCINE sijawahi Kukosea nikimpenda na Kumkubali Mtu kwani nina Jicho la Uhakika na la Kuona mbali pamoja na Ubora wa Mtu / Kitu.

Simba SC koseeni kote ila msithubutu Kumuacha ( Kumtema ) Mchezaji Raia wa Senegal Ousmane Papi Sakho kwani mtakuja Kujuta na Kunikumbuka hadi Kumkubuka na Yeye pia.

Sakho ni Mshambuliaji na Winga aliyekamilika karibia 90% ya Mtu ambaye Simba SC inamuhitaji ila tu Majeruhi na 'Miba' anayopigwa na Wachezaji Wawili Wazawa ndiyo vinamtesa na Kumkwamisha kutupa kile ambacho Wadau na 'Scouts' tulikiona Kwake.

Chonde Chonde Uongozi wangu wa Simba SC msimteme ( msimuache ) huyu Sakho bali mpeni mwaka Mmoja zaidi wa kuwa nae na naamini mtakuja kunipigia 'Salute' GENTAMYCINE hapa JamiiForums.

Huyu Sakho ni zaidi ya Jose Luis Miquissone ndiyo maana hata wakati anakuja Simba SC 'African Football Pundits' wengi waliipongeza Simba SC kwa Kumsajili kwani tayari alikuwa njiani kuelekea nchini Ufaransa kusajiliwa na moja ya Vilabu Shindani katika Ligi Daraja la Pili huko.

Ninasisitiza Ousmane Sakho asiachwe!!!
 
Mliuza mabasi na mmesajiri magarasa sasa mnataka kuyaacha.
Wenzenu yanga wamemchukua wonder kid Denis nkane kweli yanga wako juu
 
Simba inapata wachezaji wazuri alafu wanawaweka benchi au kuwaacha.
Ibrahim Amme.
Kahata.
Shiboob"Zizou".
Fraga.
Abdullswamad.
Chikwende.
Sakho.
Simba inakosa utulivu kwa wachezaji wa kubaki na wakuacha.
Sijui kwanini Yanga tusimbebe uyu Chikwende, jamaa anajua kweli kweli huyu.
 
Nakuheshimu brother,ila kumuheshimu mwalimu ni kitu kizuri.

Hizo imani za miba sijui nini,hazina ushahidi.
Kwa nini Luis na Chama hawakupigwa miba?
Sifurahishwi na upotoshaji mkubwa unaofanywa na watu wa mitandao kutoa sifa za kijinga kwa wachezaji kama vile Banda,Sakho n.k.
Tumwache mwalimu afanye kazi yake
GENTAMYCINE sijawahi Kukosea nikimpenda na Kumkubali Mtu kwani nina Jicho la Uhakika na la Kuona mbali pamoja na Ubora wa Mtu / Kitu.

Simba SC koseeni kote ila msithubutu Kumuacha ( Kumtema ) Mchezaji Raia wa Senegal Ousmane Papi Sakho kwani mtakuja Kujuta na Kunikumbuka hadi Kumkubuka na Yeye pia.

Sakho ni Mshambuliaji na Winga aliyekamilika karibia 90% ya Mtu ambaye Simba SC inamuhitaji ila tu Majeruhi na 'Miba' anayopigwa na Wachezaji Wawili Wazawa ndiyo vinamtesa na Kumkwamisha kutupa kile ambacho Wadau na 'Scouts' tulikiona Kwake.

Chonde Chonde Uongozi wangu wa Simba SC msimteme ( msimuache ) huyu Sakho bali mpeni mwaka Mmoja zaidi wa kuwa nae na naamini mtakuja kunipigia 'Salute' GENTAMYCINE hapa JamiiForums.

Huyu Sakho ni zaidi ya Jose Luis Miquissone ndiyo maana hata wakati anakuja Simba SC 'African Football Pundits' wengi waliipongeza Simba SC kwa Kumsajili kwani tayari alikuwa njiani kuelekea nchini Ufaransa kusajiliwa na moja ya Vilabu Shindani katika Ligi Daraja la Pili huko.

Ninasisitiza Ousmane Sakho asiachwe!!!
 
Tatizo kassim dewji hana weledi wa kusajili, akiwa katibu mkuu simba alidanganya ramadhan wasso kapata timu ubelgiji kumbe kaishia airport kamuuza yanga. Baada ya kuwatoa zamalek na kuingia makundi alimsajili clement kahabuka toka uarabuni ambaye akiwa uwanjani anaishia kuanguka na hakuna cha maana alichoongeza.
 
Back
Top Bottom