Kama Saudi Arabia wanasherehekea Eid Ijumaa inakuwaje BAKWATA wadai mwezi haujaonekana?

Kama Saudi Arabia wanasherehekea Eid Ijumaa inakuwaje BAKWATA wadai mwezi haujaonekana?

Uganda ni majirani zetu na wametangaza Eid ni kesho; lakini pia Uarabuni napo Eid ni kesho.

Kwanini Tanzania wamepanga iwe Jumamosi?
Wewe endelea kula sikukuu sisi wengine kesho lazima tutii viongozi wetu
 
Kwanini nchi zote zinazotuzunguka hadi Saudi Arabia leo ni sikukuu lakin Tanzania hapana
Tuna majira tofauti, mwezi ni huuhuu mmoja, wanaweza kuuona sisi tusiuone.
Ni elimu ya aina yake kama huijiu utabakia kusema unavyosema.
Ndio maana kuna mahali saa moja giza na pengine saa moja hiyohiyo bado mwanga mkubwa...
 
Kweli ndugu sio masihara. Mimi ni mdogo wako sana. Allah akuongezee Ilmu zaidi na zaidi na akubariki nayo. Akufanyie wepesi mambo yako na akupe kheri duniani na akhera. Amin.
Allahul mustaan, allah atuzidishie sote na atufanyie wepesi sote, aaamyn.
 
Kuna madhehebu mawili kwenye Uislam na miaka yote huwa na tarehe tofauti za kufungua .. Answar Suna always ndio huwahi na hii ni miaka yote
Answar sunnah si dhehebu wala pote bali ni taasisi ya kiislamu kama IPC, ISC, IF n.k yenyewe huitwa answaar muslim youth center au AMYC makao makuu yake ni tanga, tanzania.

Wanaowahi kufungua ni watu wenye msimamo wa mwezi wa kimataifa na wanaochelewa ni watu wa mwezi wa kitaifa ikiwa hawakuuona kwao, na wote wako sahihi hapana vibaya.
 
Tuna majira tofauti, mwezi ni huuhuu mmoja, wanaweza kuuona sisi tusiuone.
Ni elimu ya aina yake kama huijiu utabakia kusema unavyosema.
Ndio maana kuna mahali saa moja giza na pengine saa moja hiyohiyo bado mwanga mkubwa...
Dini ni moja na dunia ni moja. Toa porojo zako huko, peleka kwenye vilabu vya pombe za kienyeji huko kijijini kwenu
 
Mkuu Dr Matola PhD mambo ya waislamu ungewaachia tu wenyewe mkuu maana kila mtu anajua anachokifanya.

Kwa kukuhabarisha kuna misimamo ya aina mbili na yote ni sawa, kuna msimamo wa kufunga na kufungua kwa mwandamo wa mwezi wa kitaifa na hili halina ubaya.

Na pili kuna msimamo wa kufunga na kufungua kwa mwezi wa kimataifa yaani unaoandama popote na hili halina ubaya.

Bakwata wameamua kushikilia msimamo wa mwezi wa kitaifa na waumini wana uhuru wa kuwafuata au kuswali kesho, kuna ubaya gani? hapa kuna utapeli upi? sisi wengine tunaswali kesho na tuko huru kufanya hivyo.

Nashauri wakati mwingine ungeachana na haya mambo maana ni comments zako nyingi unazungumzia utapeli n.k shika kile unachokiona ni sawa na mambo ya waislamu waachie wenyewe.

Asante.
Kufunga wafunge waislam ila muandamo wa mwezi wanaulizia wasio waislam.....
 
Back
Top Bottom