Kama Simba iilivyoangukia pua mbele ya Mbeya City leo, ndivyo ambavyo siku ya siku, chama dola kitaanguka kutoka madarakani hata wakibebwa na dola

Nothing lasts longer
P
 
Kwanini atasubiri sana, hebu fafanua?
P
 
Kila chenye mwanzo hakikosi mwisho!
p
 
Nakuhakikishia hiyo siku yaja na hamtoamini.

Anguko la chama dola laja, tusichokijua kwa uhakika ni mazingira gani yatapelekea anguko hilo, au kwa maneno mengine, ni mazingira gani yatasababisha anguko hilo.
Naomba niendelee kuheshimu mawazo yako, kwenye game ya football kuna kitu kinaitwa unpredictability kutokana na the playing field is level, lakini kwenye siasa zetu ni very predictable due to political dynamics za siasa zetu ukijumlisha na the political landscape ya political game yetu, the playing field is not level, hivyo kama kuna mtu anamatumaini kuwa kuna siku upinzani utashinda uchaguzi, mtu huyo atasubiri sana !.

Kwa Tanzania, determinant ya ushindi ingekuwa ni votes casted, labda hilo lingewezekana kutokea, lakini the determinant ya ushindi uchaguzi wetu sio votes casted but votes counted!, hivyo anayedetermini sio anayepiga kura, bali anayehesabu kura!.

P
 
Pamoja nayote hayo mabadiliko yanawezekana🏃.
 
Hoja ya kuhusu anguko la chama cha dola ni nzuri na hata mimi naiunga mkono ila kutumia mfano wa simba mchizi ni kama kakimbia sana kasifiwa hadi kapapita na kwao
Teh teh teh teh....huu mfano umekukera aisee....haaa haaa
 
CCM ishakufa tangu 2010 sema bado mazishi yake
 
Bibi ushungi ndiyo kaja kuimalizia kabisa amejikita kuteua wapemba wenzake ambao hata huku bara hatuwajui
 
Job ameangukaje?
 
Mzee Pascal Mayalla, ulichosema ni kweli, Sisi watanzania tunaofutilia siasa ni wachache mno, tofauti na wenzetu kama Zambia, Kenya, hata Malawi tu wanatushinda. Kwa hiyo kuitoa CCM madarakani siyo kitu Rahisi hivyo tunatofauti kubwa sana na mataifa mengine ya Africa.
 
Umenifurahisha sana kwa maelezo uliyotoa, Anayehesabu ndiye anajua mshindi, sasa hapo utashindaje?
 
Hata makaburu wa SA walikuwa na kiburi cha hivyohivyo. Walikuwa na katiba ya hovyo hivyo hivyo. Wakawabana wengine hivyohivyo. Kwa hili hatukushangai wewe wala wakijani wenzio, wasomi na wasio wasomi
 
Kuiondosha ccm madarakani ni procedural.
Kuna vitu vingi vingii inabidi vifanyike na vifanyike kikamilifu!
Kimojawapo ni elimu na uelewa wa wananchi.
Pili ni hamu ya kuleta mabadiliko na kuyaishi.
Tatu ni wasomi akina pascal mayala kuacha undumilakuwili na kukoma kuwarubuni wananchi!
 
Sisi wananchi wa hii nchi tupo tofauti Sana na wananchi wa nchi nyingine za kiafrika,watu wengi Sana bado hatufikirii sawasawa...wengine siyo kwamba wanaipenda CCM Bali ndio chaguo pekee la chama Cha siasa nchini Tanzania Sasa ndo utaona jinsi watu wengi bado ni wajinga,nimeshuhudia watu wengi tu na maeneo mengi tu huwa utasikia wakisema kuwa "ndo hivyo Tena ngoja tuchague tu",inaonekana wengine hawaipendi CCM ila ndo only option iliyopo kwasababu tu ya mtaji wa ujinga uliopo vichwani mwa watu...na hii mifumo ya kiutawala ya kijamaa wakati mwingine ni ya kipumbavu,inajishikiza kila mahali Hadi kwa usiowatarajia lengo likiwa ni kulinda tu chama, chama ambacho ndiyo serikali yenyewe...ila Mimi naamini bado watanzania hawajasagwa,wakisagwa vizuri ndo wataelewa kinachotakiwa kufanywa ni kitu gani wao wenyewe bila kusukumizwa na wapinzani wa CCM,Mana hata huko upinzani napo bado ni Tia maji Tia maji...
 
Ni mpumbavu pekee anaeweza kuamini Chama chetu kitadumu milele... Na mara nyingi kauli hizi hutolewa na wasaka fursa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…