Kama sio kutukimbia uwanjani siku ile, Yanga ingeambulia kipigo cha fedheha mno

Objective football

JF-Expert Member
Joined
Oct 21, 2023
Posts
1,195
Reaction score
2,771
Hawa watu naona MUNGU aliwanusuru na kichapo kikali sana, kikosi changu kilikua sawasawa haswa.

Nakumbuka siku iyo nilishiba wali maharage, satisa nanusu alasiri nikawahi siti ya mbele kucheki mechi hii Ya SIMBA vs YANGA pale kwenye banda umiza la diwani.

Michuano ilikua ya kagame na klabu za simba na yanga zilitolewa nusu fainali kwa hiyo zilikua zinagombania mshindi wa tatu wa michuano hiyo.

Ajabu bana! tumekaa vijana,watoto kwa wazee kusubiri gemu hii! haloo yanga walitukimbia ,hawakutokea kabisa nakumbuka ilikua mwka 2008 hivii.

Nanukuu maneno ya kapteni wa simba niko nyagawa" tunawaomba yanga watokee uwanjani wale tatu waondoke zao"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…