Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,170
- 6,757
Taifa letu lina katiba mbaya sana maana imemrundikia Rais madaraka makubwa mno. Sioni umuhimu wa kutaja ibara zilizompa ais mamlaka makubwa. Lakini toka ibara ya kwanza mpaka ya mwisho rais wa JMT ana mamlaka makubwa sana. Anaweza kufanya chochota anachotaka na hakuna wa kumuuliza. Na hii huwa mbaya zaidi kama rais wetu akiwa na kiburi.
Tuna katiba ambayo imetamka wazi Rais hawezi kushitakiwa kwa jinai yoyote akiwa madarakani. Sasa je kwa kutumia madaraka yake akifanya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa nini asishitakiwe?
Tumuombe Mungu Rais wa sasa asiwe na kiburi, maana kama akiwa na kiburi, hata mtu akimtongoza binti yake tunaweza kusikia alitekwa na kufungwa jiwe zito kisha kutumbukizwa baharini. Na hakuna hatua zozote za kisheria dhidi yake zitachukuliwa.
Tuna katiba ambayo imetamka wazi Rais hawezi kushitakiwa kwa jinai yoyote akiwa madarakani. Sasa je kwa kutumia madaraka yake akifanya ukiukwaji wa haki za binadamu kwa nini asishitakiwe?
Tumuombe Mungu Rais wa sasa asiwe na kiburi, maana kama akiwa na kiburi, hata mtu akimtongoza binti yake tunaweza kusikia alitekwa na kufungwa jiwe zito kisha kutumbukizwa baharini. Na hakuna hatua zozote za kisheria dhidi yake zitachukuliwa.